Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
2008-09-23 11:05:05
Na Salome Kitomary, PST Moshi
Watu wasiofahamika, wamembaka hadi kufa msichana mkazi wa Majengo kwa Mtei, Manispaa ya Moshi.
Baada ya kufanya unyama huo, watu hao waliutelekeza mwili wake karibu na nyumba aliyokuwa akiishi.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Baruti Ramadhani alisema kuwa, tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita usiku eneo la Majengo kwa Mtei, Manispaa ya Moshi.
Alisema siku ya tukio, msichana huyo alikuwa akirejea nyumbani baada ya kumaliza kazi katika duka la Liberia Mini Supermarket.
Alisema akiwa njiani, alikutana na kundi la watu wanaosadikiwa kuwa ni wahalifu ambao walimkamata kwa nguvu na kisha kumfunga mdomo na kumfanyia kitendo hicho cha kinyama.
Alisema walimziba mdomo kwa kutumia vitambaa na kuanza kumbaka kwa zamu hadi alipopoteza maisha.
Alisema baada ya watu hao kubaini kuwa msichana huyo amekufa, waliubeba mwili wake hadi katika eneo karibu na nyumba yake na kuutelekeza hapo.
Kaimu Kamanda huyo aliongeza kuwa, watu hao hawakuchukua kitu chochote cha marehemu kwani simu yake ya kiganjani na viatu vyake, vilikutwa pembeni ya mwili wake na kwamba inasadikiwa walikuwa na visa naye.
Katika tukio lingine, Agnes Ndewirio (45), mkazi wa Kiborloni, Manispaa ya Moshi ameuawa kwa kupigwa
na mume wake na kisha kumtoboa jicho la upande wa kushoto kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa kimapenzi.
Kamanda Ramadhani alisema tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki wakati marehemu huyo akiwa amelala na mume wake nyumbani kwao Kiborloni.
Alisema baada ya mauaji hayo, mtuhumiwa aliulaza mwili wa marehemu pembezoni mwa kitanda.
Alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Constantino Kaswai (60), mkazi wa Kiborloni.
Alisema mtuhumiwa huyo alikuwa ametoka gerezani
kwa dhamana Septemba 19, mwaka huu kwa kosa la kupatikana na pombe haramu ya gongo.
``Baada ya mtuhumiwa kurejea nyumbani alianza ugomvi ambao chanzo chake inadaiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi wa kwa nini hakuwa anamtembelea gerezani kwa kipindi alichokaa huko, ambapo alimpiga hadi kufa,`` alisema.
Alisema katika tukio la kwanza hakuna anayeshikiliwa na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi.
Aidha, alisema mtuhumiwa anashikiliwa na polisi na kwamba baada ya upelelezi kukamilika, atafikishwa mahakamani.
My Take:
Polisi wafanya msako na kutunza kumbukumbu za DNA ili hatimaye watu watakaokamatwa wahusishwe moja kwa moja na kifo cha binti huyu na hatimaye msumemo wa sheria uwakute .
Na Salome Kitomary, PST Moshi
Watu wasiofahamika, wamembaka hadi kufa msichana mkazi wa Majengo kwa Mtei, Manispaa ya Moshi.
Baada ya kufanya unyama huo, watu hao waliutelekeza mwili wake karibu na nyumba aliyokuwa akiishi.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Baruti Ramadhani alisema kuwa, tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita usiku eneo la Majengo kwa Mtei, Manispaa ya Moshi.
Alisema siku ya tukio, msichana huyo alikuwa akirejea nyumbani baada ya kumaliza kazi katika duka la Liberia Mini Supermarket.
Alisema akiwa njiani, alikutana na kundi la watu wanaosadikiwa kuwa ni wahalifu ambao walimkamata kwa nguvu na kisha kumfunga mdomo na kumfanyia kitendo hicho cha kinyama.
Alisema walimziba mdomo kwa kutumia vitambaa na kuanza kumbaka kwa zamu hadi alipopoteza maisha.
Alisema baada ya watu hao kubaini kuwa msichana huyo amekufa, waliubeba mwili wake hadi katika eneo karibu na nyumba yake na kuutelekeza hapo.
Kaimu Kamanda huyo aliongeza kuwa, watu hao hawakuchukua kitu chochote cha marehemu kwani simu yake ya kiganjani na viatu vyake, vilikutwa pembeni ya mwili wake na kwamba inasadikiwa walikuwa na visa naye.
Katika tukio lingine, Agnes Ndewirio (45), mkazi wa Kiborloni, Manispaa ya Moshi ameuawa kwa kupigwa
na mume wake na kisha kumtoboa jicho la upande wa kushoto kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa kimapenzi.
Kamanda Ramadhani alisema tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki wakati marehemu huyo akiwa amelala na mume wake nyumbani kwao Kiborloni.
Alisema baada ya mauaji hayo, mtuhumiwa aliulaza mwili wa marehemu pembezoni mwa kitanda.
Alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Constantino Kaswai (60), mkazi wa Kiborloni.
Alisema mtuhumiwa huyo alikuwa ametoka gerezani
kwa dhamana Septemba 19, mwaka huu kwa kosa la kupatikana na pombe haramu ya gongo.
``Baada ya mtuhumiwa kurejea nyumbani alianza ugomvi ambao chanzo chake inadaiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi wa kwa nini hakuwa anamtembelea gerezani kwa kipindi alichokaa huko, ambapo alimpiga hadi kufa,`` alisema.
Alisema katika tukio la kwanza hakuna anayeshikiliwa na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi.
Aidha, alisema mtuhumiwa anashikiliwa na polisi na kwamba baada ya upelelezi kukamilika, atafikishwa mahakamani.
My Take:
Polisi wafanya msako na kutunza kumbukumbu za DNA ili hatimaye watu watakaokamatwa wahusishwe moja kwa moja na kifo cha binti huyu na hatimaye msumemo wa sheria uwakute .