"A woman of my dreams" 25years later...

Wale wakubwa wenzangu mtanielewa vizuri! wakati wetu wasichana warembo walikuwa kwa hesabu. Nilipokuwa shule ya msingi miaka ya '70 nilisoma darasa moja na msichana ambaye kwangu alikuwa a woman of Dream.
Alikuwa msichana mrembo kwa viwango vya wakati ule ambapo maumbile ndio kigezo kikubwa. Aliumbika msichana na tuliomzunguka tulikubaliana kwa hilo. Nilimpenda kweli msichana huyo lakini sikuwa na nafasi ya kuonekana kwake kwa vile alipendwa na hata waliokuwa nje ya shule. Kusema kweli niliungulika sana na mapenzi kwake. Nasisitiza kuwa nilimpenda na nilikuwa na haja naye kiasi kuwa hata ndoto zangu, mipango yangu ya baadae na furaha yangu niliihusisha na yeye. Bahati mbaya sikuweza kumtamkia na nilipomuonyesha dalili alizidharau kwani hali duni was written all over me. Kuanzia kivazi na hata matumizi kwangu ilikuwa tabu. Hata hivyo nilikuwa na sababu moja kubwa ya kuonekana pale shule nayo ni kuwa nilikuwa ni mmoja wa wanafunzi bora shuleni jambo ambalo lilisaidia kuwa na uhusiano mzuri na baadhi ya wasichana. Hata hivyo nilikuwa na sifa nyengine nayo ni DOMO ZEGE hivyo sikuwa na uwezo wa kutengeneza uhusiano na msichana yeyote pale shuleni.
Tuliingia Sekondari nikiendelea na ndoto na njozi juu ya huyu msichana lakini hapa hali ya kutonitambua ilizidi kwani tulienda sehemu iliyohitaji hali nzuri zaidi ya maisha. Bahati nzuri nilifanikiwa kuendelea na masomo ya juu na my dream girl hakufanikiwa na wenye uwezo wakatangaza ndowa wakaondoka nae.
Tuliendelea na maisha yetu na Mungu akinijaalia kazi nzuri nami nikafunga ndowa. Ni miaka karibu 25 sasa na kwa nyakati tofauti nikikutana na yule msichana ambae amekuwa mama wa familia. Kwa kuthamini cheo cha ndowa tukikutana humsalimia kwa heshima lakini bado sijasahau niliyvompenda hapo nyuma.
Kipindi cha miezi 6 nyuma nimekutana nae na amenijuulisha kuwa ameachika kwenye ndowa yake na kuanzia hapo ameanza kunionyesha hamu ya kuwa na mimi. Ama kwa upande wangu bado namuona ananivutia na ninashawishika kutibu yale majeraha ya zamani lakini nikiifikiria ndowa yangu nabaki njia panda.

Kaka umeshaoa, na mashahidi wako wapo.... jitahidi asikuvunjie ndoa!!

Kumbuka kwamba si wewe tu unayekutwa ma masahibu hayo, yawezekana hata mkeo ana "a man of her dreams" lakini kwa kukuheshimu wewe, anamwomba nguvu Mungu amsaidie amshinde na kubaki na wewe

fikiria kabla ya kutenda, takwimu zisizo rasmi zinasema zaidi ya 80% ya wanandoa hawaoi au kuolewa na wale watu wa dreams zao

ni rare!!

Jiulize kwanini ameachika?
 
Thats true love, never die! Hawajapenda hao wasingelijidai kuwa werevu mbele ya kupenda!

Ngekewa, a true love iko both sides, yeye haku-share your dreams so it was not a true love!!!! DID SHE LOVE YOU?
 
Ngekewa, a true love iko both sides, yeye haku-share your dreams so it was not a true love!!!! DID SHE LOVE YOU?

Nakubaliana nawe kuwa ndowa inahitaji true love(Yaani mpendane wote) lakini kupenda ni uhuru wa mtu binafsi. Baadhi ya wakati tunalazimika kupenda mbadala baada ya kukosa first choice ili ndowa inawiri. Lakini moyo ni moyo bado hautaacha kupenda na hii haiwi dhambi kwani kupenda sio lazima kuwe na uhusiano. Ndowa naam inahitaji vitu viwili,penzi na uhusiano.
Nilimpenda a woman of my dream na ninaendelea kumpenda lakini bado sina uhusiano nae. Kitachoendelea ndio kitandawili ambacho wenzangu mnaweza kunisaidia.
 
Mzee mzima kajipoze machungu muda haujaenda sana ila usijenge kibanda, zuga zuga kidogo kisha usepe usijemtesa bi mkubwa atakapogundua.
 
babu thikamoo! eb tulia na bibi uliyenaye acahana na huyo bibi mdogo! mwenzio kaachia nini na wewe utake kuparamia
 
Mzee mzima kajipoze machungu muda haujaenda sana ila usijenge kibanda, zuga zuga kidogo kisha usepe usijemtesa bi mkubwa atakapogundua.

Ndugu yangu mawanzo yako huwa yananipitia sana na kusema kweli sijui nguvu gani zinazonizuia mara zote ninapoweka lengo hilo.
 
babu thikamoo! eb tulia na bibi uliyenaye acahana na huyo bibi mdogo! mwenzio kaachia nini na wewe utake kuparamia
Mjukuu wangu marahaba na ushauri wako ni mzuri lakini usidanganyike mjukuu wangu kuwa watu wazima hatusalitiki.
 
Zee zima linafikiria kutumia kichwa cha chini? Tumia kichwa chako cha juu mzee wewe la sivyo utachapika na maisha!
 
Zee zima linafikiria kutumia kichwa cha chini? Tumia kichwa chako cha juu mzee wewe la sivyo utachapika na maisha!


Kwani ulishasikia zee anapunguziwa kokwa moja ya korodani zake? Unafikiri wewe toto tu ndio unaruhusa ya kutumia vichwa viwili na mimi zee nitumie kimoja?
Sikuelewi unakusudia nini? Hebu jiweke wazi!
 
Kwani ulishasikia zee anapunguziwa kokwa moja ya korodani zake? Unafikiri wewe toto tu ndio unaruhusa ya kutumia vichwa viwili na mimi zee nitumie kimoja?
Sikuelewi unakusudia nini? Hebu jiweke wazi!
Yaani unafikiria huku ukiwa ume..dindi..sh.'* hivyo badala ya kutumia kichwa chako cha juu unakuwa unaongozwa na hicho cha chini sasa, na ndiyo wanaume wengi tunavyofanya, ndiyo maana nikakushauri tumia brain yako ya juu kufikiri kabla ya kutenda! Mara nyingi utakuja na majibu sahihi zaidi.
 
Yaani unafikiria huku ukiwa ume..dindi..sh.'* hivyo badala ya kutumia kichwa chako cha juu unakuwa unaongozwa na hicho cha chini sasa, na ndiyo wanaume wengi tunavyofanya, ndiyo maana nikakushauri tumia brain yako ya juu kufikiri kabla ya kutenda! Mara nyingi utakuja na majibu sahihi zaidi.

Kama ulikusudia kunishauri basi pengine ungenipa sababu na sio kutumia lugha ya ugomvi au kumuona mwenzako mjinga. Ushauri unatolewa ili kumuongoza mtu lakini unapotowa kitu kama karipio anaeshauriwa hatoona hivyo!
La pili ni kuwa bado natumia kichwa changu cha juu kwa kutaka kupata ushauri kutoka kwa wajuzi, wenye busara na ningekuwa naongozwa na hicho cha pili basi ushauri wa nini wakati kiongozi wangu ameshaniamuru?
La tatu ni kuwa hata hicho kichwa cha juu nacho kinataka utafakari kabla ya kusema, jee kuna dalili yeyote inayoonyesha kuwa niliongozwa na kichwa cha chini? Tatizo lenu ni kuchanganya mapenzi na tendo la kujamiiana. Kama hamu ya kujamiana basi mbona ningekwenda Jolly au Kinondoni nikatekeleza hiyo amri ya kichwa cha chini.
 
Kama ulikusudia kunishauri basi pengine ungenipa sababu na sio kutumia lugha ya ugomvi au kumuona mwenzako mjinga. Ushauri unatolewa ili kumuongoza mtu lakini unapotowa kitu kama karipio anaeshauriwa hatoona hivyo!
La pili ni kuwa bado natumia kichwa changu cha juu kwa kutaka kupata ushauri kutoka kwa wajuzi, wenye busara na ningekuwa naongozwa na hicho cha pili basi ushauri wa nini wakati kiongozi wangu ameshaniamuru?
La tatu ni kuwa hata hicho kichwa cha juu nacho kinataka utafakari kabla ya kusema, jee kuna dalili yeyote inayoonyesha kuwa niliongozwa na kichwa cha chini? Tatizo lenu ni kuchanganya mapenzi na tendo la kujamiiana. Kama hamu ya kujamiana basi mbona ningekwenda Jolly au Kinondoni nikatekeleza hiyo amri ya kichwa cha chini.
Yaani umenichekesha kinoma, kumbe unajua matatizo ya kichwa cha chini!!! hahahah!! basi ulikuwa ushauri tu, wala si ugomvi mkuu. Sema wanaume wengi yanapofika maswala ya mapenzi hufanya maamuzi kutumia kichwa cha chini na ndilo tatizo kubwa sana kwa ndoa nyingi.
 
Miaka ya 70 mpaka sasa thats make over 40yrs! Hivyo ndio kusema bado unamapenzi na mtu ambaye miaka zaidi ya arobaini amekuwa nje ya mfumo wa maisha yako? Au mimi ndio

sielewi haya mambo ya kupenda? Na je ulikuwa unampenda mkeo? Na bado unampenda mkeo? Na upo tayari kutoka na mtu aliyeachika? Sikuelewi
 
Miaka ya 70 mpaka sasa thats make over 40yrs! Hivyo ndio kusema bado unamapenzi na mtu ambaye miaka zaidi ya arobaini amekuwa nje ya mfumo wa maisha yako? Au mimi ndio

sielewi haya mambo ya kupenda? Na je ulikuwa unampenda mkeo? Na bado unampenda mkeo? Na upo tayari kutoka na mtu aliyeachika? Sikuelewi

Hujakosea hata kidogo lakini hii ndio inayoitwa true love.
Mapenzi yangu na ndowa yangu ni vitu viwili tofauti kwani usifanye kosa kufikiri kuwa kupenda kunakuwa ndani ya uhusiano tu. Naamini umeshasoma wengi humu akieleza mapenzi ya upande mmoja yaani unaweza ukampenda mtu lakini usiwe na mahusiano nae kwa sababu mbali mbali ikiwemo kubwa kuwa yeye hakupendi.
Sitaki kuwa muongo kujidai kuwa mapenzi yangu kwake yalikufa lakini kutokana na sababu kama nilivyoeleza ilibidi nitafute mpenzi mwengine ambaya huyu tuliunda uhusiano wa mke na mume.
 
Cha msingi ni kumuepuka tu yaani usiwe na mazoea nae ya karibu..unless otherwise utaisaliti ndoa yako very soon!
 
Purple, ahsante kwa ushauri wako,nitajitahidi kusahau majeraha!
 
Hujakosea hata kidogo lakini hii ndio inayoitwa true love.
Mapenzi yangu na ndowa yangu ni vitu viwili tofauti kwani usifanye kosa kufikiri kuwa kupenda kunakuwa ndani ya uhusiano tu. Naamini umeshasoma wengi humu akieleza mapenzi ya upande mmoja yaani unaweza ukampenda mtu lakini usiwe na mahusiano nae kwa sababu mbali mbali ikiwemo kubwa kuwa yeye hakupendi.
Sitaki kuwa muongo kujidai kuwa mapenzi yangu kwake yalikufa lakini kutokana na sababu kama nilivyoeleza ilibidi nitafute mpenzi mwengine ambaya huyu tuliunda uhusiano wa mke na mume.

Ok, kwanza hongera kuwa kupenda kweli! Ila what I know huwezi ukawa unawapendwa watu wawili equally. Ninachokiona

ni wewe kujifunga katika kifungo cha ndoa kwa muda mrefu ilahali huna mapenzi ya kweli kwa unayeishi nae! Ndio maana

tunasema lazima watu waoe kwa sababu sahihi
 
Mwaka 1970.........nimeshindwa hata niseme nini...

kulikuwa na thread moja hivi ya kumpongeza member fulani kufikisha 30yrs ya ndoa nilibaki wow....nilivyokuwa namhic ni tofauti kabisa, sasa hii leo ya 70's...hahaha...hii ndio JF bana unaweza kuhic thread imeanzishwa na under age ukish2ka ni libaba/limama lizima....kha.
 
Ok, kwanza hongera kuwa kupenda kweli! Ila what I know huwezi ukawa unawapendwa watu wawili equally. Ninachokiona

ni wewe kujifunga katika kifungo cha ndoa kwa muda mrefu ilahali huna mapenzi ya kweli kwa unayeishi nae! Ndio maana

tunasema lazima watu waoe kwa sababu sahihi


Mapenzi ya kweli ni yepi na mapenzi ya uongo ni yepi, unapokuwa na mapenzi ya uongo huwa unamuongopea nani , nafsi yako? Ni nafsi yangu ndiyo inayopenda nami binafsi naungama hilo sasa ulitaka ushahidi gani zaidi?
Inaonyesha kuwa unakubali kuwa mapenzi sio sababu pekee ya kuingia katika ndowa na hapo mwanzo nilisema kuwa kuna sababu zinatufanya tusipate vile tunavyovipenda. Naam nilimpenda msichana lakini hali haikuniruhusu kuwa naye na kwa kuelewa hilo nikijuwa kuwa hakuna idadi iliyowekwa kwa kupenda nilitafuta mwengine nikampenda na nikafunga ndowa nae. Hili halinifanyi kuwa nisimpende mwengine wakati naweza kumpenda bila kuwa na uhusiano nae wa kimapenzi. Kinachonitanza hapa sasa ni kuwa pengine vile vitu vilivyonizuia nisimpate havipo tena. Bahati nzuri naendelea kujizuia na kuishi kama awali lakini vishawishi ndio tatizo. Ushauri wako unahitajika.
 
Back
Top Bottom