A whooping 43bn/= to upgrade an airstrip in Sumbawanga!

Sadly, we need to go to Kenya to learn this.


Or maybe the "great and mighty" sleeping giant aka JWTZ might wake up from it's deep slumber and shake things around a bit. Peacefully lakini. Ila jamaa yuko strategic 'cause army officials are being handed government posts like peanuts...this is not without reason. Hence nothing will happen in good ol' "peaceful" Tanzania.

And that's the sad story of our life. Our country. Disintergrating while we watch
 
mimi nakujua sumbawanga kuliko wewe
uwanja wa ndege upo na unatosha,
kinachotakiwa ni barabara au reli..
Watanzania wangapi wanapanda ndege????

Umetumia kigezo gani kwamba wewe unakujua Sumbawanga kuliko mimi?
Na hao wananchi wa Sumbawanga watapanda vipi ndege ikiwa uwanja wa uhakika haupo?Hauwezi kuamua kwamba watu wenyewe hawapandi ndege wakati huduma za ndege hamna !!
Ninaangalia picha kubwa kwamba ujenzi wa miundombinu ni muhimu kwa maendeleo, haijalishi ni wapi inajengwa, achilia mbali kwamba mkoa huu una uwezo mkubwa kiuchumi ambao bado haujachotwa.
Kuna maamuzi mabovu yamefikiwa na serikali hii, lakini sidhani kama hili ni mojawapo.
 
GT,

It is not about Ukabila, it is about priorities.

TRL/TRC is in need of almost same amount to run effectivelly, but we have declared we do not have money. The movement of good from Kigoma and Mwanza have stalled, lakini leo tuna pesa kujenga uwanja wa ndege Sumbawanga or 3 years ago pale Arusha Mjini and couple years ago kule Songwe au sijui Rungwe?
 
Mchungaji Kishoka,



Mbona unakuwa na roho ya korosho ndugu yangu? yaani uwanja wa Sumbawanga ukiimarishwa japo kwa ka-lami tu ndio inakuwa nongwa sasa unataka kila kitu kizuri kijengwe Arusha na Dom na Dar pekee?



Huo ulinganifu wa maendeleo utapatikana lini katika nchi hii? wana-Rukwa ni wachapakazi sana na wamekuwa wakiilisha Tanganyika miaka nenda rudi lakini hata barabara nzuri ya lami tu imekosekana. Saa zingine tuwe tunatoa hoja bila ya upendeleo na kuzingatia pia kuwa nchi yetu ni kubwa na kuna wananchi wengine ambao nao wanahitaji maendeleo.



Mwisho huyo Mheshimiwa Mizengo Pinda hatoki Sumbawanga ni mtu aliyezaliwa na kuishi/kusomea wilaya ya Mpanda.



Amani.



Kishoka mi nakupinga Sumbawanga kunahitaji airport nzuri yaani hizo hela ni sawa kwa kuangalia potentials za huko huo uwanja utatumika kwa faida zaidi kuliko huo wa Bagamoyo! Sumbawanga kuna ardhi nzuri ya kuruhusu kilimo cha maua na mbogamboga kama Arusha, Mbeya na Kilimanjaro! Pia tukumbuke kuna madini Sumbawanga na kuna mbuga za wanyama! nathani wanahitaji airport!
 
Kishoka mi nakupinga Sumbawanga kunahitaji airport nzuri yaani hizo hela ni sawa kwa kuangalia potentials za huko huo uwanja utatumika kwa faida zaidi kuliko huo wa Bagamoyo! Sumbawanga kuna ardhi nzuri ya kuruhusu kilimo cha maua na mbogamboga kama Arusha, Mbeya na Kilimanjaro! Pia tukumbuke kuna madini Sumbawanga na kuna mbuga za wanyama! nathani wanahitaji airport!

Swali langu kwa wote si kwa nini tunajenga uwanja Sumbawanga, bali ni kwa nini tunajenga uwanja sasa hivi Sumbawanga huku hizo fedha zinahitajika kununua mitambo ya Umeme kuhakikisha nchi inajitosheleza na umeme na hivyo kutoleta mtikisiko katika uzalishaji!
 
Wajerumani na wajapan wangekuwa na kasumba hii ya kujenga miundo mbinu ni luxury wasingekuwa wanasifika leo hii kwa miundo mbinu safi kabisa! Wao walitumia nadharia ya "jenga na maendeleo yatafuata"!
 
Kishoka mi nakupinga Sumbawanga kunahitaji airport nzuri yaani hizo hela ni sawa kwa kuangalia potentials za huko huo uwanja utatumika kwa faida zaidi kuliko huo wa Bagamoyo! Sumbawanga kuna ardhi nzuri ya kuruhusu kilimo cha maua na mbogamboga kama Arusha, Mbeya na Kilimanjaro! Pia tukumbuke kuna madini Sumbawanga na kuna mbuga za wanyama! nathani wanahitaji airport!
Geza hatupingi kwamba S'wanga hakuna potential ipo, ila kila kitu kinatakiwa kwenda ngazi kwa ngazi, na haina maana ya kuwa mahali pakiwa na airport ndio symbol ya maendeleo au kukua kwa uchumi.
Uwekezaji unaotakiwa kwa sasa katika nchi yetu hususana S'wanga na mikoa kama hiyo ni usafiri wa uhakika kwa watu wengi na vitu vya biashara navyo ni Reli na Barabara, umeme wa uhakika, elimu ndipo vitu vingine vitakuja automatically bila kelele au mikwaruzo, mfano leo hii ukitaka kujengaS'wanga utajiuliza cement utaipitishaje ili ujenge maghala, shule, nyumba bora za kuishi, hoteli nk nk, sasa huyo mwekezaji atakaye kuja kwa ndege ataka wapi atakula wapi? maana mimi s'wanga naijuia chakula au mghawa wenye hadhi ni mpaka kwa yule muhindi tu, upendo wapo wapo? au labda uende kwa masista/kwa mapadre.
nafikiri ndugu yangu utakuwa umenielewa.
kwa mimi mswahili ni rahisi saana kula kutokana na hali ninayo kuta lakini kwa mwekezaji mwingine atauliza hoteli ya kufikia ipoje? nyumba za kupanga zipoje, mazingira ya maisha ya poje, shule za watoto zipoje, ulinzi na usalama ipoje, Huduma za Afya na Umeme nk nk.
na kuongezea tu hapa Kibunguno kauliza Kilomita moja ya lami ni Shs ngapi? kwani kinacho takiwa kwa Sasa hapo S'wanga ni run way ambayo itaruhusu utuaji wa ndege bila matatizo na kuanzia ni hizi ndege zetu za abiria 50 kwenda chini, ambayo kwa kigezo changu zinaweza zisifike 43bn. kutengeneza hiyo run way kama tunataka Jengo kwa Ajili ya Waheshimiwa letu linaweza kujengwa kwa namna ya kwamba mambo yakiwa mazuri Jengo linaongezwa, lakini kwa sasa tunaweza Jengo la nafuu in Phases.
na viwanja vye kuhitaji run way za uhakika ni Kagera ambacho kwa sasa kina ndege nyingi au frequency kubwa ya kutua ndege kuliko S'wanga, lakini kweli hatuwezi kuiacha S'wanga, Mpanda, Tabora, Singida, Lindi Iringa , Songwe, Njombe, Ruvuma, wote tuna haki ni kupangilia tu ndipo kuna Gomba. haki nk nk
 
Is this a joke or prank news? We have Rubada folks matching all the way to South Korea to borrow 50 million Shillings to grow food and we are ready to sign of 43 billion to pave a tarmac for flying magic carpets of Rukwa? Kisa eti Waziri Mkuu awe na hadhi ya kushusha Gulf Stream?

Why not allocate that money to rebuild our Railway System or clean the JKNIA or KIA which are disgusting?

Yaani ukisikia Amani na Utulivu uliojaa upumbavu ni huu. Serikali ina deni kubwa kiasi haiwezi kulipa mishahara au kutoa huduma za jamii, lakini tunajenga Uwanja Rukwa?

Why not spend that money to buy 3 thermal generators that can produce a minimum total of 150mw?

When will people get angry and riot?



Pesa za uchaguzi hizo mkuu....
 
Geza hatupingi kwamba S'wanga hakuna potential ipo, ila kila kitu kinatakiwa kwenda ngazi kwa ngazi, na haina maana ya kuwa mahali pakiwa na airport ndio symbol ya maendeleo au kukua kwa uchumi.
Uwekezaji unaotakiwa kwa sasa katika nchi yetu hususana S'wanga na mikoa kama hiyo ni usafiri wa uhakika kwa watu wengi na vitu vya biashara navyo ni Reli na Barabara, umeme wa uhakika, elimu ndipo vitu vingine vitakuja automatically bila kelele au mikwaruzo, mfano leo hii ukitaka kujengaS'wanga utajiuliza cement utaipitishaje ili ujenge maghala, shule, nyumba bora za kuishi, hoteli nk nk, sasa huyo mwekezaji atakaye kuja kwa ndege ataka wapi atakula wapi? maana mimi s'wanga naijuia chakula au mghawa wenye hadhi ni mpaka kwa yule muhindi tu, upendo wapo wapo? au labda uende kwa masista/kwa mapadre.
nafikiri ndugu yangu utakuwa umenielewa.
kwa mimi mswahili ni rahisi saana kula kutokana na hali ninayo kuta lakini kwa mwekezaji mwingine atauliza hoteli ya kufikia ipoje? nyumba za kupanga zipoje, mazingira ya maisha ya poje, shule za watoto zipoje, ulinzi na usalama ipoje, Huduma za Afya na Umeme nk nk.
na kuongezea tu hapa Kibunguno kauliza Kilomita moja ya lami ni Shs ngapi? kwani kinacho takiwa kwa Sasa hapo S'wanga ni run way ambayo itaruhusu utuaji wa ndege bila matatizo na kuanzia ni hizi ndege zetu za abiria 50 kwenda chini, ambayo kwa kigezo changu zinaweza zisifike 43bn. kutengeneza hiyo run way kama tunataka Jengo kwa Ajili ya Waheshimiwa letu linaweza kujengwa kwa namna ya kwamba mambo yakiwa mazuri Jengo linaongezwa, lakini kwa sasa tunaweza Jengo la nafuu in Phases.
na viwanja vye kuhitaji run way za uhakika ni Kagera ambacho kwa sasa kina ndege nyingi au frequency kubwa ya kutua ndege kuliko S'wanga, lakini kweli hatuwezi kuiacha S'wanga, Mpanda, Tabora, Singida, Lindi Iringa , Songwe, Njombe, Ruvuma, wote tuna haki ni kupangilia tu ndipo kuna Gomba. haki nk nk

August,
Kwanza, je umeshapata jibu la kilometa moja ya lami ni kiasi gani?. Na hata kama una-suggest kuwa ka-uwanja kawekwe ka-lami kidogo mbona bado unajifunga kwa pointi yako kuwa huyo mwekezaji atakula na kulala wapi!. Mbona chakula kinachozalishwa na Mkoa wa Rukwa kwa msimu mmoja tu ni zaidi ya mara tatu ya hizo bln. 43!!!

Pili, kumbuka potential ya ka hako-ka uwanja sio tu Sumbawanga pekee ni kwa mkoa mzima wa Rukwa, unazungumzia wageni watalala wapi kwani watalii wanaokwenda mbuga za wanyama za KATAVI huwa wanalala wapi? pia usisahau mkoa una vivutio vingine vya kitalii ambavyo tumeshindwa kuviendeleza kutokana na miundo mbinu mibovu mfano mzuri ni KALAMBO FALLS (The second highest water falls in Africa). Potential nyinginezo ni za wafanyabiashara wa CONGO mashariki na ZAMBIA ambao wanakwenda kule kununua chakula kila kukicha.

Ndugu yangu Uwanja wa ndege una umuhimu wake na barabara, reli pia vina umuhimu na changamoto zake na sio vizuri kusema kwamba ni lazima kwanza barabara ijengwe ama reli ijengwe halafu uwanja wa ndege ufuate au vice versa!

Tunakumbuka kuwa wakati Mwalimu JKN anapewa taarifa ya kuwa Waziri Mkuu wa Tanganyika alikuwa ziarani Sumbawanga (Ufipa enzi hizo) ilibidi akimbizwe Zambia ili akachukue ndege ya kumuwahisha Dar kwa ajili ya shughuli hiyo sasa ebu niambie hata kama barabara ingekuwa na mkeka wa aina gani angewahi kufika kwa ajili ya maandalizi?.

Kumbukumbu zangu zinaonyesha kuwa miaka ya mwishoni mwa themanini ATC walikuwa wanapeleka ndege zao Sumbawanga mara mbili kwa wiki na zilikuwa zinajaa abiria (asilimia kubwa ilikuwa ni WAFANYABIASHARA na sio WANASIASA) na hivyo kukuza biashara, wafanyabiashara walifikia hata kupeleka SANGARA wabichi kutoka Mwanza wa-kadhalika (utility).

Nimeona kuwa Mchungaji Kishoka anapendekeza pesa hiyo ingepelekwa Kigoma kuimarisha Reli na wewe nawe unapendekeza ingepelekwa Kagera kuimarisha Uwanja wa ndege! kwangu mimi naona mawazo yenu hayana tofauti na Mkuu wa Mkoa fulani aliyechukuwa/hamisha mapipa ya lami yaliyokusudiwa kujengea barabara za mji wa Sumbawanga enzi hizoo na kuyapeleka kwao!!

All in all, pesa hiyo bado ni ndogo sana na hata huo uwanja bado utakuwa hautoshi ningeomba wa-Tanganyika wenzangu tuachane na udogo-udogo; tuanze kuwa na fikra na mawazo makubwa zaidi kama ni viwanja basi tujenge vikubwa na kama ni barabara zijengwe pana zaidi, kama ni hospitali tujenge kubwa, kama ni masoko tujenge makubwa zaidi wa-kadhalika.

BTW:
Nimepata taarifa kuwa barabara ya kuunganisha Sumbawanga na Mbeya inajengwa kwa kiwango cha lami kupitia MCC.

Amani.



 
August,
Kwanza, je umeshapata jibu la kilometa moja ya lami ni kiasi gani?. Na hata kama una-suggest kuwa ka-uwanja kawekwe ka-lami kidogo mbona bado unajifunga kwa pointi yako kuwa huyo mwekezaji atakula na kulala wapi!. Mbona chakula kinachozalishwa na Mkoa wa Rukwa kwa msimu mmoja tu ni zaidi ya mara tatu ya hizo bln. 43!!!

Pili, kumbuka potential ya ka hako-ka uwanja sio tu Sumbawanga pekee ni kwa mkoa mzima wa Rukwa, unazungumzia wageni watalala wapi kwani watalii wanaokwenda mbuga za wanyama za KATAVI huwa wanalala wapi? pia usisahau mkoa una vivutio vingine vya kitalii ambavyo tumeshindwa kuviendeleza kutokana na miundo mbinu mibovu mfano mzuri ni KALAMBO FALLS (The second highest water falls in Africa). Potential nyinginezo ni za wafanyabiashara wa CONGO mashariki na ZAMBIA ambao wanakwenda kule kununua chakula kila kukicha.

Ndugu yangu Uwanja wa ndege una umuhimu wake na barabara, reli pia vina umuhimu na changamoto zake na sio vizuri kusema kwamba ni lazima kwanza barabara ijengwe ama reli ijengwe halafu uwanja wa ndege ufuate au vice versa!

Tunakumbuka kuwa wakati Mwalimu JKN anapewa taarifa ya kuwa Waziri Mkuu wa Tanganyika alikuwa ziarani Sumbawanga (Ufipa enzi hizo) ilibidi akimbizwe Zambia ili akachukue ndege ya kumuwahisha Dar kwa ajili ya shughuli hiyo sasa ebu niambie hata kama barabara ingekuwa na mkeka wa aina gani angewahi kufika kwa ajili ya maandalizi?.

Kumbukumbu zangu zinaonyesha kuwa miaka ya mwishoni mwa themanini ATC walikuwa wanapeleka ndege zao Sumbawanga mara mbili kwa wiki na zilikuwa zinajaa abiria (asilimia kubwa ilikuwa ni WAFANYABIASHARA na sio WANASIASA) na hivyo kukuza biashara, wafanyabiashara walifikia hata kupeleka SANGARA wabichi kutoka Mwanza wa-kadhalika (utility).

Nimeona kuwa Mchungaji Kishoka anapendekeza pesa hiyo ingepelekwa Kigoma kuimarisha Reli na wewe nawe unapendekeza ingepelekwa Kagera kuimarisha Uwanja wa ndege! kwangu mimi naona mawazo yenu hayana tofauti na Mkuu wa Mkoa fulani aliyechukuwa/hamisha mapipa ya lami yaliyokusudiwa kujengea barabara za mji wa Sumbawanga enzi hizoo na kuyapeleka kwao!!

All in all, pesa hiyo bado ni ndogo sana na hata huo uwanja bado utakuwa hautoshi ningeomba wa-Tanganyika wenzangu tuachane na udogo-udogo; tuanze kuwa na fikra na mawazo makubwa zaidi kama ni viwanja basi tujenge vikubwa na kama ni barabara zijengwe pana zaidi, kama ni hospitali tujenge kubwa, kama ni masoko tujenge makubwa zaidi wa-kadhalika.

BTW:
Nimepata taarifa kuwa barabara ya kuunganisha Sumbawanga na Mbeya inajengwa kwa kiwango cha lami kupitia MCC.

Amani.
Ninavyo sema uwanja kuwekea lami atleast kwa ajili ya ndege ndogo, ni ili uwanja uwe reliable kutua ndege hata wakati wamasika na kuna hitaji hilo la ndege kusafiri.
Sasa ukija mambo ya kiuchumi na kibiashara, mahali pengi duniani hujijenga penye kutokana na economic activities, kama biashara inalipa hapo S'wanga leo hii ungekuta kuna Hoteli nyingi tu zimeisha jengwa, na ukiwa Tomaso wa suala hili angalia Mza kwa nini imejengeka? ni kutokana na kuweko kwa shughuli za kiuchumi ndio maana unaona leo hii PPf, NSSF na wengineo wanajenga Office Blocks, Nyumba za Kupangisha nk.
Na kama uwanja wa ndege ungekuwa unalipa ungeweza kukuta kampuni/mtu anaweza kuwaambia serikali kufanya mradi wa kujenga kiwanja toza kodi yako rudisha hela yako then baada ya kujilipa unarudi serikali au kwa mamlaka zinazo husika (Built own transfer).
Na kuongezea hata haya mashirika yetu ya ndege yangeweza kusema tujange uwanja ule maana ndipo tunapopatia faida yetu, lakini hilo hatulioni.
Jingine ambalo lilikuwa likiwezesha ndege kujaa wakati huo linaweza kuwa lilitokana na mashirika ya umma na wafanya kazi wa serikali kujaa huko kikazi, maana Barabara sio nzuri (NMC, NBC, RTC, CRDB, NIC na pia ilikuwa sera ya nchi chini ya CCM kwamba ile mikoa ambazo barabara sio nzuri basi serikali kupitia shirika lake ATC wafanye hivyo angalau fligt mbili kwa wiki nk nk )
Jingine unalotakiwa kulielewa na kuwa Potential za kiuchumi zinatakiwa kuwa Stimulated, sasa ukiangalia kwa sasa kinachotakiwa kwa sasa ni Barabara, pili Reli, na tatu Umeme, kumubuka Hata Muumba alianza na Siku ya kwanza ya pili na hata alipofika ya kupumzika na kuangalia nyuma aliridhika na kazi yake. na ukumbuke Muumba alimuumba Binadamu kwa mfano wake. Basi nasi tunatakiwa tufuate utaratibu huo huo,
nafikiri umenielewa ndugu yangu na mimi napenda saaana tu niomne S'wanga inayo ngara, lakini sioni kwamba inaweza kungara kwa kuwekewa uwanja wa ndege kwanza, bali barabara, na reli, na umeme wa hukika utakao wafikia wengi.
Sasa sijui wewe kwa fikra zako unaona tuanze na Uwanja wa Ndege au barabara, na nilipoweka mfano wa Kagera sio kwamba na wadharau watu wa S'wanga lakini nataka kukuonyesha kama tunapanga mipango yetu kutokana na activities basi Kagera umeonysha unazo hizo activities za ndege kuliko S'wanga, lakini kama tuna panga kutokana na kisiasa au utashi wa kibinafsi basi na huo uwanja waanzie S'wanga.
 
Ninavyo sema uwanja kuwekea lami atleast kwa ajili ya ndege ndogo, ni ili uwanja uwe reliable kutua ndege hata wakati wamasika na kuna hitaji hilo la ndege kusafiri.
Sasa ukija mambo ya kiuchumi na kibiashara, mahali pengi duniani hujijenga penye kutokana na economic activities, kama biashara inalipa hapo S'wanga leo hii ungekuta kuna Hoteli nyingi tu zimeisha jengwa, na ukiwa Tomaso wa suala hili angalia Mza kwa nini imejengeka? ni kutokana na kuweko kwa shughuli za kiuchumi ndio maana unaona leo hii PPf, NSSF na wengineo wanajenga Office Blocks, Nyumba za Kupangisha nk.
Na kama uwanja wa ndege ungekuwa unalipa ungeweza kukuta kampuni/mtu anaweza kuwaambia serikali kufanya mradi wa kujenga kiwanja toza kodi yako rudisha hela yako then baada ya kujilipa unarudi serikali au kwa mamlaka zinazo husika (Built own transfer).
Na kuongezea hata haya mashirika yetu ya ndege yangeweza kusema tujange uwanja ule maana ndipo tunapopatia faida yetu, lakini hilo hatulioni.
Jingine ambalo lilikuwa likiwezesha ndege kujaa wakati huo linaweza kuwa lilitokana na mashirika ya umma na wafanya kazi wa serikali kujaa huko kikazi, maana Barabara sio nzuri (NMC, NBC, RTC, CRDB, NIC na pia ilikuwa sera ya nchi chini ya CCM kwamba ile mikoa ambazo barabara sio nzuri basi serikali kupitia shirika lake ATC wafanye hivyo angalau fligt mbili kwa wiki nk nk )
Jingine unalotakiwa kulielewa na kuwa Potential za kiuchumi zinatakiwa kuwa Stimulated, sasa ukiangalia kwa sasa kinachotakiwa kwa sasa ni Barabara, pili Reli, na tatu Umeme, kumubuka Hata Muumba alianza na Siku ya kwanza ya pili na hata alipofika ya kupumzika na kuangalia nyuma aliridhika na kazi yake. na ukumbuke Muumba alimuumba Binadamu kwa mfano wake. Basi nasi tunatakiwa tufuate utaratibu huo huo,
nafikiri umenielewa ndugu yangu na mimi napenda saaana tu niomne S'wanga inayo ngara, lakini sioni kwamba inaweza kungara kwa kuwekewa uwanja wa ndege kwanza, bali barabara, na reli, na umeme wa hukika utakao wafikia wengi.
Sasa sijui wewe kwa fikra zako unaona tuanze na Uwanja wa Ndege au barabara, na nilipoweka mfano wa Kagera sio kwamba na wadharau watu wa S'wanga lakini nataka kukuonyesha kama tunapanga mipango yetu kutokana na activities basi Kagera umeonysha unazo hizo activities za ndege kuliko S'wanga, lakini kama tuna panga kutokana na kisiasa au utashi wa kibinafsi basi na huo uwanja waanzie S'wanga.

August,

Sawa nimekusikia, mimi nimeshasema hapo awali kuwa uwanja wa ndege, barabara na reli vyote vina umuhimu kiuchumi kwani changamoto zake ni tofauti hivyo basi huwezi sema tujenge kwanza barabara ama reli alafu uwanja wa ndege ufuate ama vice versa.

Wana-Rukwa wamesahauliwa katika mipango ya kimaendeleo ya nchi kwa muda mrefu ingawaje wamekuwa wakijitahidi kuwa waadilifu na kuchapa kazi kwa bidii na hii si kwamba hawana uwezo wa kupanda/kutumia usafiri wa ndege! mbona pesa wanazo za kutosha tu!! (angalia per capital income comparison ya Tanzania mwaka 1994 walikuwa ni 3rd ukiondoa Dar na Arusha!).

Mwisho nazidi kusisitiza kuwa Tsh bln. 43 ni pesa ndogo mno kwa mradi wowote wa maana kwa miundo mbinu ya nchi, hii ni less that USD 40 Mil. Hivi tumeshapata jibu kilometa moja ya lami ni kiasi gani??

Amani.

Attached, angalia:

1: Nimeweka kielelezo cha kuonyesha kuwa Milenium Challenge Company (MCC) wanajenga hiyo barabara kuu ya kuunganisha Mkoa wa Rukwa na wa Mbeya na;

2: Ulinganishi wa wastani wa kipato cha mwananchi wa mkoa wa Rukwa na wa mikoa mingine ya Tanzania ripoti ya mwaka 1994!
 

Attachments

  • RUKWA-BARABARA.pdf
    4.3 MB · Views: 78
  • PEER-CAPITAL.doc
    66.5 KB · Views: 26
Nashukuru kwa majibu yako , na hizo attachment, lakini kwa kuwa mimi si tomaso, ninakuamini na ninaulewa Mkoa wa Rukwa kwa hizo bidhaa walizo kuwa nazo iwe dhahabu, mahindi, Katavi National Park na hayo maporomoko ambayo kwa kweli nilikuwa nimeyasahau kidogo, na nimeelewa mantiki yako ya uwanja wa ndege vs barabara, kwani hiyo barabara ipo chini ya mradi wa MGC, kwa hiyo nayo serikali kama sehemu ya majukumu yake basi watupatie nasi Uwanja wa Ndege, lakini upingaji wangu ulikuwa unaangalia zaidi mahitaji ya nchi, kwa mfano barabara toka S'wanga mjini kwenda Mpanda , Mpanda-Tabora, na Rukwa-Kigoma, Barabara za kuunganisha Singida na mikoa inayo pakana nayo, Dodoma-Mtera-Iringa nk
na kama kuna ziada tuwekeze kwenye labda Reli tukawa na Express train S'wanga Mbeya na hata utalii wa kutumia train, train nyingine S'wanga Mjini kwenda Mpanda Tabora. na hapa sijazungumzia mahitaji ya Umeme, sasa sijui hizo Kagambo Falls zinaweza kuzalisha umeme, au njia zingine mbadala, basi kila tunapokuwa naziada natuna fanya ile mizani ya kiuchumi faida na hasara ya mradi fulani katika nchi S'wanga ikiwemo , basi utaona hapo jinsi wacongo, wazambia. wamalawi na hata mimi tutakavyo tia nanga/mguu hapo Rukwa na umuhimu wa Uwanja utaonekana dhahiri/peupe bila mikwaruzo wala mikwala, na hata mapato ya kodi kwa Manisipa/halmashauri ya mji yataongezeka na tutasema , kama serikalikuuu wanachelewesha airport yetu sisi wenyewe tunaijenga, kwani fedha si zipo? na faida inarudi kwetu. kwani airport ni biashara nayo.
Samahani sijapata bado gharama za kilomita moja na pia ni kilomita ngapi zinatakiwa ilikuwa na uwanja wa kati hapo Rukwa, bahati mbaya mimi si mtaalamu wa mambo ya ujenzi, labda baadae atatokea Engineer Moja au mtu mwenye Excess na taarifa hizo akatusaidia.
Ila nakuomba uelewe Hiyo Ardhi ni ya watanzania usije ukadhubutu kumuuzia Mtu wa Nje, labda umkodishe, na mkataba utuonyeshe usije ukapigwa kanyaboya
 
August,

Naona tunaelewana sasa, ingawaje sio sahihi kufanya socio-economic assessment kwa ajili ya huo mradi wa kilometa moja ya lami kwa kaji-uwanja ka-ndege vs Reli kwa budget ya Tsh 43 bln. siwezi kukuelewa kwani pesa hiyo ni ndogo sana kwa reli ya kuunganisha Sumbawanga-Mpanda unajua pale unazungumzia kilometa zaidi ya 200!!! sasa sijui gharama ya hiyo reli itakuwa kiasi gani itabidi wana-Rukwa wasubiri karne nyingine tena kabla hiyo pesa haijapatikana!!

Kuhusu pendekezo lako la BOT (Build Operate Transfer) nadhani ingekuwa vema basi hiyo mikoa mikubwa ionyeshe mfano kwanza! ili pesa zetu za bajeti ya maendeleo zipelekwe mikoa ya pembezoni iliyosahaulika kama Rukwa, Mtwara, Kigoma, Lindi wa-kadhalika, sioni kwanini unataka wana-Rukwa wafanye hivyo wakati mikoa mikubwa bado inabebwa kila siku kwenye bajeti?, ni ukweli usiopingika mikoa yote tunayoiona leo imeendelea ki-miundo mbinu na ki-uchumi imekuwa ikipewa upendeleo na serikali zilizopita!!. Potential za nchi hii bado hazijawa exploited kwa sababu hizo za kunga'ng'ania kuwekeza central badala ya kuangalia kwanza kwenye egde ambako ndio kuna vast resources.

Suala la kivutio cha utalii cha Kalambo Falls halina tofauti na suala la Mlima Kilimanjaro ambavyo tumekuwa tukilala na majirani zetu wakifaidika kimapato. Nimekuwekea kiunganishi hapo chini uone jinsi wenzetu wa-Zambia wanavyo changamkia hio kitu.

http://www.go2africa.com/zambia/kalambo-falls


Amani
 
<LI class=g>Nimeangalia ramani ya Rukwa na hapo unaposema naona kutakuwa na tatizo la usafiri toka airport ilipo kwenda kwenye falls, southwest of rukwa sasa unasemaje hiyo fedha za airport tujenge barabara toka itakapoishia hiyo ya MGC kwenda huko kalambo water falls.

<LI class=g>Na pia nimeona kuwa watu wa zambia wanafaidika saana kutokana na kuwepo na national park mbili karibu na sehemu hiyo hivyo economy of scales na vivutio vingine vinawafanya watu wapitie huko.

<LI class=g>Katavi nimeona ipo karibu ya mji wa mpanda North west ya Mkoa wa Rukwa , kwa hiyo kwa hali ilivyo rukwa ni wazi mtu akitaka kwenda katavi inabidi atumie njia ya kutoka Mpanda, na kama akitokea S'wanga ambako Barabara ya MGC itaishia basi ni wazi tunahitaji barabara nyingine ya kutoka S'wanga Kwenda Mpanda.

<LI class=g>

<LI class=g>[ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Kalambo_Falls"]Kalambo Falls - Wikipedia, the free encyclopedia[/ame]

Kalambo Falls on the Kalambo River is a 772ft (235m) single drop waterfall on the border of Zambia and Tanzania at the southeast end of Lake Tanganyika. ...
en.wikipedia.org/wiki/Kalambo_Falls - Cached - [ame="http://www.google.co.ug/search?hl=en&ie=UTF-8&q=related:en.wikipedia.org/wiki/Kalambo_Falls+kalambo+falls&sa=X&ei=u70bS_CgBs6C_Qa3mJHkAw&ved=0CBgQHzAH"]Similar[/ame]
<LI class=g>Kalambo Falls | Northern Province | Zambia | Go 2 Africa

Kalambo Falls , Northern Province , Zambia - a travel guide with information, accommodation and tours. Go2Africa - the African Africa Safari Experts.
www.go2africa.com › Zambia - Cached - [ame="http://www.google.co.ug/search?hl=en&ie=UTF-8&q=related:www.go2africa.com/zambia/kalambo-falls+kalambo+falls&sa=X&ei=u70bS_CgBs6C_Qa3mJHkAw&ved=0CB0QHzAI"]Similar[/ame]
<LI class=g>Kalambo Falls Prehistoric Site - Cambridge University Press

Final volume of Kalambo Falls prehistoric site, to complete a mammoth press publication • Desmond Clark, editor, and author of much of the text, ...
www.cambridge.org › Home › Catalogue - Cached - [ame="http://www.google.co.ug/search?hl=en&ie=UTF-8&q=related:www.cambridge.org/uk/catalogue/catalogue.asp%3Fisbn%3D0521200717+kalambo+falls&sa=X&ei=u70bS_CgBs6C_Qa3mJHkAw&ved=0CCMQHzAJ"]Similar[/ame]
<LI class=g>Kalambo Falls | World Waterfall Database: World's Tallest Waterfalls

1 Dec 2004 ... Located at the very southern end of Lake Tanganyika, Kalambo Falls is one of the more famous waterfalls in Africa.
www.world-waterfalls.com/waterfall.php?num=248 - Cached - [ame="http://www.google.co.ug/search?hl=en&ie=UTF-8&q=related:www.world-waterfalls.com/waterfall.php%3Fnum%3D248+kalambo+falls&sa=X&ei=u70bS_CgBs6C_Qa3mJHkAw&ved=0CCYQHzAK"]Similar[/ame]
<LI class=g>Kalambo Falls (waterfall, East Africa) -- Britannica Online ...

Britannica online encyclopedia article on Kalambo Falls (waterfall, East Africa), waterfall, the second highest uninterrupted fall in Africa (after Tugela ...
www.britannica.com/EBchecked/topic/.../Kalambo-Falls - Cached - [ame="http://www.google.co.ug/search?hl=en&ie=UTF-8&q=related:www.britannica.com/EBchecked/topic/310022/Kalambo-Falls+kalambo+falls&sa=X&ei=u70bS_CgBs6C_Qa3mJHkAw&ved=0CCkQHzAL"]Similar[/ame]
<LI class=g>Kalambo falls on Flickr - Photo Sharing!

Kalambo falls photo taken by Bryan Baker in 1966 access by road is impossible these days one way to see to beauty of this water fall is to use a water taxi ...
www.flickr.com/photos/zambia_trip/421775936/ - Cached - [ame="http://www.google.co.ug/search?hl=en&ie=UTF-8&q=related:www.flickr.com/photos/zambia_trip/421775936/+kalambo+falls&sa=X&ei=u70bS_CgBs6C_Qa3mJHkAw&ved=0CCwQHzAM"]Similar[/ame]
<LI class=g>Kalambo Falls: Zambia Travel Articles: Safari Lodges in Zambia…

Few visitors venture up to northern Zambia to its border with Tanzania, but if they do they may witness one of Africa's purest sights - the 212-metre drop ...
zambia.safari.co.za/kalambo-falls-zambia.html - Cached - [ame="http://www.google.co.ug/search?hl=en&ie=UTF-8&q=related:zambia.safari.co.za/kalambo-falls-zambia.html+kalambo+falls&sa=X&ei=u70bS_CgBs6C_Qa3mJHkAw&ved=0CC8QHzAN"]Similar[/ame]
<LI class=g>Kalambo Falls Pictures

Find your Kalambo Falls pictures at Picsearch.com! We have over a billion indexed images in our directory, and it continually expands.
www.picsearch.com/.../waterfalls/waterfalls%20d.../kalambo%20falls.html - Cached - [ame="http://www.google.co.ug/search?hl=en&ie=UTF-8&q=related:www.picsearch.com/pictures/travel/nature/waterfalls/waterfalls%2520d-k/kalambo%2520falls.html+kalambo+falls&sa=X&ei=u70bS_CgBs6C_Qa3mJHkAw&ved=0CDIQHzAO"]Similar[/ame]
<LI class=g>Kalambo falls archaeological site (prehistoric settlement site ...

The Kalambo falls prehistoric settlement is located about 30 kilometres North-West of Mbala district, Northern province. The site was excavated by professor ...
whc.unesco.org/en/tentativelists/868/ - Cached - [ame="http://www.google.co.ug/search?hl=en&ie=UTF-8&q=related:whc.unesco.org/en/tentativelists/868/+kalambo+falls&sa=X&ei=u70bS_CgBs6C_Qa3mJHkAw&ved=0CDUQHzAP"]Similar[/ame]
<LI class=g>Kalambo falls travel guide

Complete, objective information on Kalambo falls travel, including photos and reviews. Add your own wiki-style contributions.
www.world66.com/africa/zambia/kalambofalls - Cached
 
Bantugbro, August,

Shida si kujengwa uwanja wa ndege, au kwa nini kuujenga upya uwanja wa ndege, tatizo ni kipi cha kipaumbele?

Ikiwa wakulima wa Rukwa wanalalamika hawana pembejeo, maghala au njia ya kusafirisha mazao yao bila kupoteza faida, kwa nini fedha hizo zisitumike kujenga barabara za kuinganisha Rukwa na mikoa minginem kuhakikisha kuwa maghala yanajengwa, kuna umeme wa kutosha na baada ya uchumi wa Rukwa kuendelea kushamiri ndipo pajengwe uwanja wa ndege?

Nimeulizia kuhusu Reli ya Kati si kwa mantiki ya kupendelea watu wa Kigoma ila ni hali halisi kuwa Reli ya Kati ni uti wa mgongo wa usafirishaji wa bidhaa na watu Tanzania.

Watu kutoka Kagera, Mwanza, Rwanda, Burundi, Kigoma, Congo, Shinyanga, Tabpra, Singida, Dodoma, Morogoro wanategemea usafirishaji wa bidhaa zao kupitia Reli kitu ambacho ni cha unafuu kuliko kutumia malori.

Zaidi ni kuwa kukosekana kwa Reli kunasababisha barabara kuendelea kuharibika kutokana na msongamano wa malori unaotokana na udhaifu wa barabara.

So the question becomes, where are our priorities?

Nimeendelea hata kusema kwa nini basi hizo pesa wasingepewa TANESCO wanunue mitambo ya kuzalisha umeme na nchi isiingie hasara kwa kukosa umeme au kuingia ubiya na makampuni kama Richmond na IPTL?

Sometimes lack of common sense and prioritization is the great hindrance of Tanzania development!
 
August,

Bajeti ambayo imekuwa ikitengwa kila mwaka kwa ajili ya kuikarabati hiyo barabara ili iweze kupitika kipindi cha masika ni kubwa mno na inaweza kupunguzwa baada ya kuwekwa lami na pesa ingine ikaelekezwa kwenye barabara kama ya kwenda Kalambo Falls ama border ya Zambia (sio Tunduma) ili kuongeza msisimko wa maendeleo.

Barabara ya Sumbawanga-Mpanda kwa Mh.Pinda tayari nayo iko kwenye mchakato wa kujengwa kiwango cha lami nadhani unaelewa kuwa kutoka Mpanda kuelekea Tabora tayari kuna usafiri wa treni inabaki ile ya kuelekea/kutokea Kigoma ingawaje nako pia waweza tumia treni ama meli za ziwa Tanganyika!

 
Back
Top Bottom