A true MMU story with photos, happened in 2016

Hapo ni kwayule mtunga stori za uwongo a.k.a anaewadai chama chakavu
hapana mkuu.....sio hapo.

ila nalo chimbo la shigongo sio baya kufanyia maasi.....lipo vizuri...nilishawahi kulala pale mwaka jana nikiwa na kademu flan hivi ka chuo cha ustawi wa jamii-kijitonyama.
 
hii ni thread yangu ya kwanza MMU kwa mwaka huu wa 2016,mara ya mwisho kuweka mada hapa kama sikosei ilikuwa ni 2014.

hili tukio la hadithi ya kweli lililo nitokea mimi mwenyewe mwezi wa tatu mwaka 2016.
ilikuwa ni siku ya jumamosi,nikiwa maeneo ya mlimani city kwa appointment ya kukutana na dada mmoja mrembo,mwanafunzi wa mwaka wa tatu,degree ya kwanza ya sheria ya UDSM.

nilikutana nae wiki moja kabla nikiwa pale chuo kikuu kwa mizunguko ya shughuli zangu binafsi,tukabadilisha namba za simu.

baada ya mawasiliano ya hapa na pale ya njia ya simu ikiwemo na mesaji za whatsapp,hatimaye tukapanga tukutane pale mlimani city ili tufahamiane zaidi.

tulikutana arround saa tano hivi kuelekea saa sita mchana,hakika binti alipendeza sana,kama unavojua wadada wanaosoma UDSM kwa kujiweka classic kimuonekano.

kwa kuwa mimi si mgeni wa eneo la mlimani city,nikamwambia tukakae pale samaki samaki.yeye akasema tuingie kwanza nakumat kuna bidhaa anataka kwenda kucheki kama inapatikana.basi tukaingia nakumat super market.

baada ya mzunguko wa kama dakika 15 ndani ya nakumat,akasema tutoke,product aliyokuwa anaitafuta haipo.basi tukawa tunatoka.

wakati tunatoka,kabla hatujakaribia lango kuu la nakumat,nikwambia twende kwenye section inayouza vileo ambayo ipo humo humo nakumat.tulipofika pale,moja kwa moja nikaenda kachukua chupa moja la whiskey ya jack daniel,nikamwabia na yeye achague kinywaji anachopenda,akachagua chupa kubwa la wiskey ya amarula.nikalipa then tukatoka.

tulipotoka akasema yeye hana confidence ya kukaa pale samaki samaki,anahisi ni eneo wanalopenda kukaa mastaa na baadhi ya vijana maarufu wa town,yeye hapawezi.

basi nikamwambia twende takakae pale marry brown,akakubari.
tulikaa pale kama lisaa lizima tukipiga story huku tukisindikizwa na vitafunwa kadhaa laini laini vya kuchangamsha mdomo.

kama mnavojua wanaume tulivo,tukiwa katikati ya maongezi,taratibu hisia za kumtamani zilikuwa zinanijia.kwa kuwa alikuwa na mvuto sana,moyoni mwangu nilikuwa napiga calculation za kumaliza mchezo siku hiyo hiyo.

basi katikati ya maongezi nikachomekea swala la tutoke pale mlimani city,tukakae eneo lingine nje ya pale.alikubari japo kwa mapozi sana,nahisi hata yeye mwenyewe alikuwa kashazimika na mimi kadoda11.

tukaingia kwenye gari then nikawasha mchuma kuelekea maeneo ya katikati ya sinza sio mbali sana na eneo lile la mlimani city.sikutaka kwenda nae mbali.

tukaingia katika lodge moja tulivu sana eneo lile,siwezi kuitaja jina ila kwa wale wajanja wa town bila shaka kwa kuangilia picha nilizo ambatanisha watakuwa washaijua.

TUKIO RASMI
tulikuwa zetu chumbani tukila raha za dunia ambazo hupeana watu wazima waliovuka umri wa miaka 18.
hakika ilikuwa ni siku ya kipekee kwetu,kila mtu alikuwa excited na mwenzake utadhani tulifahamiana kwa mda mrefu.

stimu ya ile amarula niliyo mnunulia pale nakumat ilimlegeza kisawa sawa maana alikuwa anainywa kwa pupa.na mimi ile jacky daniel yangu ilinipa mzuka sana wa kutoa dozi nene kwa yule binti.hakika vyuma vilikuwa vimekaza.

bacdb11ee1415507a975649555dafec1.jpg

basi tukiwa tumemaliza round ya tatu ya kupeana mahaba mazito,nikaamua nifungue pazia ili nione mandhari ya nje ya ile lodge huku nikiacha vioo vile vya ku-slide vya aluminum vikiwa vimefungwa.

ghafla kwa nje hatua chache kutoka pale dirishani,nikaona njemba moja iliyovaa kaptula ya kaki,ikipiga picha kwa simu ya mkononi usawa wa mlango wetu wa chumba tulichokuwa.

machale yakanicheza,ila nilificha hisia zangu kwa yule mrembo ili asigundue kama tayari nimeshaingiwa na hofu.yeye alikuwa amekaa kwenye kochi huku akiendelea kupiga fundo kadhaa za amarula.

binafsi nilihisi yule jamaa kaja kufumania,kwamba yule mdada niliyekuwa naye mle chumbani yawezekana ni mke wake au ni mwanamke wake wa siku nyingi anayemgharamia na anayetarajia kuja kumuoa.
nilihisi nimechukua demu wa mwenyewe.kingine nilihisi yule demu kaanda jamaa wa kuja kuniharibia.

zaidi ya yote yote nilikuwa nahofia kutokea tukio ambalo lingeweza kuja kunivunjia heshim yangu na kutumika kama topic katika social media mbalimbali ikiweno ma-group ya whatsapp.

kutokana na nature ya career yangu,sikupoteza wakati,haraka sana nami nikatoa simu yangu,nikampiga picha yule jamaa kwa ndani kupitia kioo cha aluminiaum.yeye alikuwa hanioni ila mimi nilikuwa namuona.nilichukua uamuzi wa kumpiga picha ili kutunza record,nije nizitumie baadae endapo jambo lolote baya lingenitokea.nikazi-foward haraka sana kwa njia ya whatsapp kwenye nambari yangu nyingine ya simu ambayo huwa sitembei nayo.halafu nika delete zile picha.

wakati huo yule mrembo wangu nileyekuja nae alikuwa haonyeshi wasiwasi wowote yeye alikuwa anaendelea tu kufyonza amarula mdogo mdogo akisubiri tuingie ktk round ya nne ya kupeana mahaba.

yule jamaa kule nje yeye alikuwa anaendelea tu kupiga picha usawa wa kile chumba huku akibadilisha angle mbalimbali,nami niliendelea kufatilia mienendo yake kwa kupitia pale dirishani.


ghafla akaja binti mmoja mrembo wa wastani,akaungana na yule jamaa kupiga picha usawa ule ule wa chumba chetu.kwa kitendo kile,kidogo hofu ikaanza kunitoka.

nilibaini kwamba kumbe yule jamaa alikuwa pale na mpenzi wake.lakini nao pia walikodisha chumba jirani na chumba chetu.baada ya kuspend masaa kadhaa chumbani kwao,waliamua watoke nje wapate kumbukumbu ya outing yao.

baada ya hapo tukarudi zetu katika round ya nne,vyuma vilikaza barabara na mshindo wa round hii haukuwa wa kawaida,mwangwi wa sauti wa yule mrembo wangu ulivuka mpaka kuta za chumba cha tatu.

SOMO LA KUJIFUNZA KWA SISI WANAUME TUNAPOTOKA OUT KWA MARA YA KWANZA NA WASICHANA TUSIOFAHAMIANA NAO VIZURI.
siku zote hutakiwi kujiamini sana,chukua tahadhari if you see anything unusual is taking place within your surrounding.usimwani sana mtu.mjini shule chochote kinaweza kukutokea.


samahani kwa kuwachosha kwa story ndefu.

NA HIZI NDIO BAADHI YA PICHA NILIZO MPIGA YULE JAMAA NA DEMU WAKE KWA KUPITIA DIRISHANI.enjoy!

2300815be65bb179534ebaf5a12a1a1d.jpg


4e4c985669761073bfdc6115a28d6e47.jpg


c429e644e34b72aa1f118a971ded8dda.jpg
Hapo ni twistas sinza?
 
hapana mkuu.....sio hapo.

ila nalo chimbo la shigongo sio baya kufanyia maasi.....lipo vizuri...nilishawahi kulala pale mwaka jana nikiwa na kademu flan hivi ka chuo cha ustawi wa jamii-kijitonyama.
Au wista chapel ndio sehemu mabazazi wanapenda
 
Back
Top Bottom