A Lesson from Tunisia

Masanilo

Platinum Member
Oct 2, 2007
22,286
4,493
Nguvu ya umma si ya kudharau hata kidogo! Kilichotokea Tunisia ni vyema viongoi wengi wasiojali wananchi wafikiri mara mbili. Ben Ali hakuwahi kuamini kama kuna siku angeishi ughaibuni Saudia. Nimefika Tunis Ben alikuwa kama ni Mungu mtu alikuwa msikiti mkubwa sana uliokuwa ukijulikana kama Ben Ali Mosque


P3150017.jpg

Ben Ali Mosque

Ilikuwa hairuhusiwi kabisa kutaja jina la Ben Ali vinginevyo uliwea potea. Oppression in Tunis was of the first order. Inteligensia ilikuwa ya hali ya juu sana lakini nguvu ya umma imeweza mtoa bila kupenda na kukimbilia Saudia.

P3150013.jpg


Ben Ali Park

P3150010.jpg


Bara bara ya kuelekea Carthage airport ! Kama Ben Ali alikuwa akitumia basi ilifungwa kwa masaa kadhaa.

TS8thGr-03.JPG


Baadhi ya vivutio Tunisia.

Hali ya wananchi kutoiridhishwa na utawala mbovu imehamia Egypt! Hii itamwondoa Hosni Mubarak madarakani. He is a dead man walking!

Nikirudi kwetu Tanzania Mh Kikwete kitendo chake cha kuunga mkono ufisadi na kukuza rushwa wakati huo huo wanachi wakawaida maisha yakiwa magumu siwei shangaa hali ilikuwa Tunisia ikaikumba Tanzania. Kikwete utendaji wake umekuwa kisanii sana anshabikia malipo ya Dowans ajilipe anasahau kuwa nguvu ya umma ipo karibu kulipuka. Migomo ya wanafunzi elimu ya juu ni kielelezo cha uongoi wake uliooza. Kikwete lazimaufanye kitu kunusuru hii hali, htautaki kulipwa dowans kwa sababu yeyote ile. Vinginevyo aanze walisiana na King Abdulla wa Saudia kwa hifadhi

Abrams-TunisDemonstration-20110114.jpg


God bless Tanzania.

Rev Masa K
 

Attachments

  • P3150017.jpg
    P3150017.jpg
    18.6 KB · Views: 41
Hata paka ukimfukuza atakimbia lakini ole wako afike kwenye kona na hakose pa kukimbilia, utakimbia wewe...
 
Du Rev Masanilo tatizo la Tunisia ni umaskini uliotopa hata rais wa Nchi kuhamisha tani 1.5 ya dhahabu na kisa kilichoibua maandamano yote hayo na ya Misri yalianzia baada ya kijana mmoja kujilipua na moto kuonyesha hasira zake kwa walionacho bofya hapa Mohamed Bouazizi - Wikipedia, the free encyclopedia
Pia Rais wetu jana amewaelewesha umma kuwa hausiki na Dowans na haitalipwa Hotuba yake hii hapo
Miezi kadhaa baadaye, likazuka sakata la Dowans ifutiwe mkataba kwa hoja kuwa wamerithi mkataba na kampuni ambayo haikupata kihalali mkataba wake. Kamati ya Bunge ilisema hivyo na wanasheria wa TANESCO pia walishauri hivyo. TANESCO ikavunja mkataba. Dowans hawakuridhika, wakashitaki kwenye Baraza la Usuluhishi kama yalivyo masharti ya mkataba waliotiliana sahihi. Madai yamesikilizwa na TANESCO imeonekana ni mkosaji hivyo wakatozwa fidia ya Dola za Marekani 64 milioni. Taarifa hiyo imetushtua wengi. Niliuliza na kupewa ushauri mbali mbali. Wapo waliosema lazima tulipe, wapo waliosema tusilipe, wapo waliosema tusiharakishe kulipa kwani kuna uwezekano wa kutokulipa kwa kutumia sheria. Uamuzi wangu ukawa tusiharakishe kulipa, tutafute njia za kuepuka katika kulipa. Ndiyo maana ya taarifa ya Mheshimiwa Chiligati na ile ya Waziri Mkuu. Ni mzigo mkubwa mno kwa TANESCO kubeba, hivyo tufanye kila tuwezalo tuepuke kulipa. Tumewataka wanasheria wetu wasaidiane na wale wa TANESCO kuhakikisha hilo halitokei. Nataka kuwahakikishia kuwa na mie ni miongoni mwa wale wasiotaka TANESCO ilipe, hivyo kauli za kuhusika na Dowans inanishangaza maana nisingeamua hivyo katika Kamati Kuu na Kamati ya Wabunge wa CCM. Ama kweli akutukanae hakuchagulii tusi.
Kwa hiyo Rais wetu hawezi wasiliana na King Abdullah wa saudia hadi 2015 kama atapenda kwenda huko
 
Du Rev Masanilo tatizo la Tunisia ni umaskini uliotopa hata rais wa Nchi kuhamisha tani 1.5 ya dhahabu na kisa kilichoibua maandamano yote hayo na ya Misri yalianzia baada ya kijana mmoja kujilipua na moto kuonyesha hasira zake kwa walionacho bofya hapa Mohamed Bouazizi - Wikipedia, the free encyclopedia
Pia Rais wetu jana amewaelewesha umma kuwa hausiki na Dowans na haitalipwa Hotuba yake hii hapo
Miezi kadhaa baadaye, likazuka sakata la Dowans ifutiwe mkataba kwa hoja kuwa wamerithi mkataba na kampuni ambayo haikupata kihalali mkataba wake. Kamati ya Bunge ilisema hivyo na wanasheria wa TANESCO pia walishauri hivyo. TANESCO ikavunja mkataba. Dowans hawakuridhika, wakashitaki kwenye Baraza la Usuluhishi kama yalivyo masharti ya mkataba waliotiliana sahihi. Madai yamesikilizwa na TANESCO imeonekana ni mkosaji hivyo wakatozwa fidia ya Dola za Marekani 64 milioni. Taarifa hiyo imetushtua wengi. Niliuliza na kupewa ushauri mbali mbali. Wapo waliosema lazima tulipe, wapo waliosema tusilipe, wapo waliosema tusiharakishe kulipa kwani kuna uwezekano wa kutokulipa kwa kutumia sheria. Uamuzi wangu ukawa tusiharakishe kulipa, tutafute njia za kuepuka katika kulipa. Ndiyo maana ya taarifa ya Mheshimiwa Chiligati na ile ya Waziri Mkuu. Ni mzigo mkubwa mno kwa TANESCO kubeba, hivyo tufanye kila tuwezalo tuepuke kulipa. Tumewataka wanasheria wetu wasaidiane na wale wa TANESCO kuhakikisha hilo halitokei. Nataka kuwahakikishia kuwa na mie ni miongoni mwa wale wasiotaka TANESCO ilipe, hivyo kauli za kuhusika na Dowans inanishangaza maana nisingeamua hivyo katika Kamati Kuu na Kamati ya Wabunge wa CCM. Ama kweli akutukanae hakuchagulii tusi.
Kwa hiyo Rais wetu hawezi wasiliana na King Abdullah wa saudia hadi 2015 kama atapenda kwenda huko

Zile propaganda za kidumu chama chama cha.................

Zidumu fikra sahihi za mwenyeki wa C....

Hawa watu hufikiria sijui kutumia kiungo gani mwilini nina hakika si ubongo!
 
Misri naona kama wamekata tamaa ya maandamano vile! hata pale square wamebakia kidogo sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom