A country of self service-Tanzania

Che Kalizozele

JF-Expert Member
Jul 20, 2008
777
49
Nimegundua ukiwa na uchungu na maisha ya watanzania wanaotaabika na hali zao duni,utakuwa umebeba mzigo mzito sana.Kila siku uwa najiuliza,kwa nini maisha yetu yanakuwa mabaya kila siku na sipendi kukubali kuwa ufisadi ndo sababu ya haya yote.Najua kuna sehemu ya umasikini wetu umechangiwa na ufisadi lakini nina imani haya hayakuanza leo na si tatizo la tanzania peke yake.kwa mfano,uwa najiuliza ni nini kilichosababisha mabadiliko makubwa ya ukali wa maisha toka kikwete ameingia madarakani na maisha yanapanda kila siku,amekosea wapi?

Siku moja nikiwa katika kufikiri,nikahisi tatizo tulilonalo ni uongozi.Hatuna viongozi mathubuti,viongozi wenye nia thabiti ya kuwatoa watanzania katika lindi hili la umasikini.Viongozi wanaojua wajibu wao na wanao heshimu na kujua uzito wa kazi aliyopewa.Kukosekana kwa uongozi mathubuti kumesababisha nchi yetu imekuwa ni nchi ya self service,hakuna nidhamu na wala hakuna anaeangalia na kufikiri kuwa kuna vizazi vinakuja na vinawategemea katika yale wanayotengeneza sasa.Kila mtu anajiudumia ili mradi tu kapewa nafasi,sasa tatizo linakuwa kwetu tunaosubiri tuudumiwe.

Nchi hii inahitaji kufanyiwa repair ya nguvu,na ili hili lifanikiwe linahitaji kiongozi,nikimaanisha kiongozi na si mbabaishaji.Nafikiri vita dhidi ya ufisadi isipokwenda bega kwa bega na kuangalia nani anaweza kutuongoza katika kuifanyia repair nchi yetu,vita hii itakuwa kama ile ya Israel na wapalestina.

Haya ni mawazo yangu.
 
Mheshimiwa nakuunga mkono kwa sababu hatujawahi kuwa na kiongozi madhibuti bali wababaishaji hata Mwalimu alijitahidi kufanikisha umoja wa kitaifa na upendo.

kwa mfano,uwa najiuliza ni nini kilichosababisha mabadiliko makubwa ya ukali wa maisha toka kikwete ameingia madarakani na maisha yanapanda kila siku,amekosea wapi?

hiyo message hapo juu kidogo siungani na wewe!Maisha yamekuwa magumu tangu enzi za Mwalimu tena enzi hizo hali ilikuwa mbaya vibaya sana ila kuanzia enzi hizo maisha ya Mtanzania wa kawaida yamekuwa yakusikitisha sana.
Tunahitaji better policies in all spheres of the economy aimed at boosting up our economy and making lives better for the ordinary Tanzanians.
The gap between the rich and the poor is widening and people are living below the poverty line.
WE NEED SOME REPAIRING TO DO!
 
tatizo tulilonalo ni uongozi.Hatuna viongozi mathubuti,viongozi wenye nia thabiti ya kuwatoa watanzania katika lindi hili la umasikini.Viongozi wanaojua wajibu wao na wanao heshimu na kujua uzito wa kazi aliyopewa.Kukosekana kwa uongozi mathubuti kumesababisha nchi yetu imekuwa ni nchi ya self service,hakuna nidhamu na wala hakuna anaeangalia na kufikiri kuwa kuna vizazi vinakuja na vinawategemea katika yale wanayotengeneza sasa.Kila mtu anajiudumia ili mradi tu kapewa nafasi,sasa tatizo linakuwa kwetu tunaosubiri tuudumiwe.

Hilo ndio tatizo,yoyote mengineyo ni YATOKANAYO TU na hilo.
Na nadhani ,WAAFRIKA tuna athirika na kutokua na viongozi thabiti ni kutoka na Familia zetu na misingi ya makuzi katika hizo familia.

Ninachojaribu kusema hapa ni,Viongozi na wasio viongozi hujaribu kuridhisha mwembers wa familia kutokana na nafasi walizonazo haijarishi kiserikaliama kiofisi.
sasa hili on the long run,lazima lilete matatizo katika ujenzi wa taifa zima,kwanimisingi na sheria za nchi huachwa ili kuwapa nafasi wale wanao TUHUSU (familia) kupata yale wasiostahiri kuyapata.
 
Babawatu,
Nakubaliana nawe ila nataka kuongeza kuwa wananchi kutokana uduni wa elimu hataujawa makini katika kufuatilia yanayofanywa kwa niaba yetu. Aidha, wasomi wanaojua nini kinachoendelea nao aidha wamekaa kimya au wameingia katika mifumo fisadi.
Mabadiliko ya kweli yatatokana na sisi wenyewe tukiamka.
 
Back
Top Bottom