X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
(¯`·._.•In Loving Memory of My Mother™•._.·´¯)
Assalamu Alaikum
Amani iwe nanyi.
Kwanza kabisa napenda kutoa shukrani zangu kwa wote ambao walithubutu kuniandikia email na PM kutaka kujua wapi na mahala gani msiba utakuwepo, kwa bahati ghafi, nilipotoa taarifa ya msiba, sikujaaliwa tena kuingia Jf na kuwafahamisha wale ambao kwa mapenzi yao juu yangu walitaka kwenda kuzika na kuna ambao wamediriki kutaka kutoa mkono wa rambirambi. Kwa kweli mmenionyesha jambo kubwa sana katika maisha, hakika nimejifunza mengi mno katika msiba huu.
Kwa taarifa tu mazishi ya Mama mpendwa yalifanyika siku ile ile aliyofariki, jioni mida ya saa kumi. Na kufuatiliwa na Dua kwa siku tatu za msiba tangia alipo fariki...!
Nawashukuru nyote kwa kutumia wakati wenu na kuonyesha kujali, sina neno ambalo linaweza kuwakilisha shukrani zangu kwenu zaidi ya kusema Ahsanteni sana na nimefarijika sana sana, bila kifani.
Hakika Mwenyezi Mungu amesema kweli kuwa ...ameumba mauti na uhai ili kutujaribu ni yupi miongoni mwetu atakayefanya mambo mema.
"Inna-Kula-Shay-In Khalqnahu-Biqadar"
Kwa Hakika Sisi Tumekiumba Kila Kitu Kwa Kipimo.
Verily, All Things Have We Created In Proportion And Measure.
Qur'an 54:49
Du'aa
"Amani ishuke juu yenu watu waliotutangulia walio waumini, nasi apendapo Mwenyezi Mungu tutakutana nanyi, tunamuomba Mwenyezi Mungu atusamehe, sisi na nyinyi.
Na Mwenyezi Mungu awarehemu wa mwanzo na wa mwisho wetu namuomba Mwenyezi Mungu atupe sisi afya njema na siha njema."
Amin Summa Amin
Dua hii iwaendee wote walio ondokewa na wazazi wao, ndugu na jamaa wote waliotutangualia Insha'Allah Mwenyezi Mungu atuwafikishe dua hii iwanufaishe maiti wetu.
Hakika Mtu mwema ni hai hata kama atahamishwa katika makazi ya wafu.