51% ya wabunge wa JMT hawana shahada [Degree]

Naunga mkono,

Hususan kwa sababu hao wanaosemwa wanashindwa kuongoza kwa sababu hawajui kiingereza, hata Kiswahili chenyewe pia hawakijui!

Ni muhimu tukapanuka zaidi na kuangalia umuhimu wa lugha katika international relations and international development community, hasa kwa nchi kama yetu ambayo traditionally imekuwa inategemea wahisani in terms of loans, aid, trade negotiations etc; tumeshindwa kuendeleza kiswahili kufikia hatua kama kiren kwa brazil; na kati ya sababu kubwa zinazotuingiza kwenye mikataba mibovu ni ufisadi lakini pia lugha; suala la ufisadi hapa kulijadili haina haja sana kwani wengi tupo ukurasa mmoja ju ya hilo, lakini hili la lugha, kuna case studies nyingi sana ambazo zinaelezea jinsi gani viongozi wetu wanashindwa kufanikisha mambo mengi wakikutana na wenzao wa nje kwa sababu ya kutojua lugha ya kiingereza; hii haina maana kwamba lugha ya kiswahili haifai, suala la msingi hapa ni kwamba hatuitumii ipasavyo hence kutukoseshwa potential leaders in the context of the above....
 
Asalaam,
Katika tafiti nilizofanya kwenye website ya bunge, zaidi ya nusu (50+%) ya wabunge hawana degree. Hii inadhihirisha jinsi gani chombo kikuu cha kutunga sheria na kusimamia serikali hakina wataalamu.
Katika tafiti zangu nimebaini kuwa;
1. Wabunge wengi ni form four graduates na wana poccess certificates za mambo mbalimbali.
2. Wabunge wengi wasio na degree ni wale wa viti maalumu, huku wengi wao wakitokea CCM na CUF.
3. Wabunge wengi watokao visiwani hawana hata deploma.(STASHAHADA) i.e 60%.
MY CONCERN:
HIVI BUNGE LETU LINASIMAMIA SERIKALI AU LINASIMAMIWA NA SERIKALI.
Happy Ramadhan Kareem.

Ni hakika elimu ni muhimu kwa ajili ya uchambuzi makini wa hoja. Lakini nikikumbuka yaliyopo vyuoni na hizo baadhi ya degree ninapata kigugumizi. Ni lazima nikiri kuwa elimu itolewayo katika vyuo vingi hapa kwetu ni dhaifu. Na mbaya zaidi vyuo vikuu hasa vya binafsi vimejielekeza kutoa certificates na Diplama ambapo kiukweli wanajali zaidi kuwapitisha wanafunzi ili kuwapa sifa bandia za kuchukua degree ili vyuo vipate mapato. Utashangaa mtu anayechukua shahada mfano ya elimu anaogopa kwenda field sekondari badala yake wanakimbilia maofisini na hata wakimaliza masomo hawataki kufundisha sekondari. Huu ni mfano tu wapo waasibu,wanasheria nk wa aina hii. Sasa hawa hata wakiwa wabunge ni janga kwa taifa pamoja na kuwa na shahada hata mbili.
 
I didnt necessarily mean it that way; point ya msingi hapa ni kwamba lugha ya kiingereza ni muhimu kwa sababu tumeshindwa kukitumia kiswahili kwa maendeleo ya taifa kama wanavyofanya brazil na kireno, warusi na kirusi, nk; viongozi wa urusi, ureno, brazil wakienda to any summits nje, wanazungumza lugha yao na kinachoendelea ni tafsiri kwa pande ze mbili zinazohusika; sisi viongozi wetu wengi wanatuingiza kwenye mikataba mibovu au wanashindwa to negotiate better deals za AID, Loans kwa sababu ya kushindwa to master lugha ya kiingereza huku wakiweka less efforts kuhakikisha tnabadilika na kuwa kama brazil in that context;

Kama Ureno inapeta na kuwa katika mataifa i think kumi bora kiuchumi duniani (brazil also being in top 10), why not brazil wakati mataifa yote haya wanatumia kireno kwenye kila kitu, na kama kuna suala toka lugha nyingine, wanalifanyia tafsiri into kireno na kulifanyia kazi.

Ureno ninayoijua mimi inahemea tumbo sasa hivi, right up there with Greece.

Unasema ipo katika mataifa kumi bora kiuchumi kwa msingi gani?

http://www.bloomberg.com/news/2012-...aps-signaling-gain-from-pain-euro-credit.html
 
Ureno ninayoijua mimi inahemea tumbo sasa hivi, right up there with Greece.

Unasema ipo katika mataifa kumi bora kiuchumi kwa msingi gani?

Portugal Default Swaps Signaling Gain From Pain: Euro Credit - Bloomberg

Nilikosea kuhusu Portugal, maana yangu ni kwamba katika top ten performing countries in the EU, lakini upo sawa, kwani after haya matatizo, inaweza hata isiwe top ten in the EU; Lakini Brazil is top ten in the world, kama sikosei ni ya nane in terms of world's largest economies; point yangu ya msingi lakini kama tukiamua kuangalia kwa ujumla wake ni kwamba hizi jamii zimepiga hatua kubwa sana na ku maintain their status huku wakitumia lugha 'nje' ya kiingereza katika masuala yao mbali mbali ya kitaifa na kimataifa - lugha ya kireno ikiwa ndio lugha kuu; lugha and economic development, je nini kinawezekana? hiyo ndio focus yangu;
 
Nilikosea kuhusu Portugal, maana yangu ni kwamba katika top ten performing countries in the EU, lakini upo sawa, kwani after haya matatizo, inaweza hata isiwe top ten in the EU; Lakini Brazil is top ten in the world, kama sikosei ni ya nane in terms of world's largest economies; point yangu ya msingi lakini kama tukiamua kuangalia kwa ujumla wake ni kwamba hizi jamii zimepiga hatua kubwa sana na ku maintain their status huku wakitumia lugha 'nje' ya kiingereza katika masuala yao mbali mbali ya kitaifa na kimataifa - lugha ya kireno ikiwa ndio lugha kuu; lugha and economic development, je nini kinawezekana? hiyo ndio focus yangu;

Ukifuatilia kwa makini utagundua kwamba, kujitambua kusiiishie katika lugha tu, hata point ya elimu nayo itabidi tuiangalie upya.

Marekani wanathamini sana ma nuclear physicist na rocket scientists, hawa ndo watu walio katika moja ya "cutting edge sciences" kwao.

Sie inawezekana kabisa mtu aliyesoma mambo hayo asitusaidie sana, kwani hata ndoto ya kuwa na industry ya vinu vya kufua umeme kwa nyuklia hatuna. Msomi huyu atakuwa pambo tu na atabaki kukata tepe.

Kwetu bwana shamba anaweza kuwa wa maana sana kumpita huyu msomi wa nyuklia.

Kwa hiyo hata tunapoongelea elimu, tuangalie elimu kwa upana wa "itatusaidia nini".

Na ukiamgalia elimu kwa upana wa "itatusaidia nini" huwezi kui reduce to a degree.

Aung San Suu Kyi hivi karibuni aliongea kuhusu umuhimu wa elimu kwa maendeleo ya nchi yake.

Na kinyume na matarajio ya wengi, akafafanua zaidi kwamba elimu anayoongelea yeye si ya midigrii, anaongelea zaidi "vocational education" iliyo practical zaidi.

Sasa hapo unaona mtu aliye practical, ambaye kashafika kwenye ma ivory towers lakini hayajamlevya na kumfanya kuhusudu mi degree bila kuangalia practical needs za watu wake.
 
Ukifuatilia kwa makini utagundua kwamba, kujitambua kusiiishie katika lugha tu, hata point ya elimu nayo itabidi tuiangalie upya.

Marekani wanathamini sana ma nuclear physicist na rocket scientists, hawa ndo watu walio katika moja ya "cutting edge sciences" kwao.

Sie inawezekana kabisa mtu aliyesoma mambo hayo asitusaidie sana, kwani hata ndoto ya kuwa na industry ya vinu vya kufua umeme kwa nyuklia hatuna. Msomi huyu atakuwa pambo tu na atabaki kukata tepe.

Kwetu bwana shamba anaweza kuwa wa maana sana kumpita huyu msomi wa nyuklia.

Kwa hiyo hata tunapoongelea elimu, tuangalie elimu kwa upana wa "itatusaidia nini".

Na ukiamgalia elimu kwa upana wa "itatusaidia nini" huwezi kui reduce to a degree.

Aung San Suu Kyi hivi karibuni aliongea kuhusu umuhimu wa elimu kwa maendeleo ya nchi yake.

Na kinyume na matarajio ya wengi, akafafanua zaidi kwamba elimu anayoongelea yeye si ya midigrii, anaongelea zaidi "vocational education" iliyo practical zaidi.

Sasa hapo unaona mtu aliye practical, ambaye kashafika kwenye ma ivory towers lakini hayajamlevya na kumfanya kuhusudu mi degree bila kuangalia practical needs za watu wake.

Wengi wetu Tanzania tunatafuta elimu ili - tupate ajira na kukidhi haja za matumbo yetu (ikiwezekana hata ajira za siasa) au tuwe tu tofauti na wengine kwamba tumebobea katika vitu vizito sana au just ili tuonekane wa maana na bora ya wengine; ni wachache sana walioelimika au wenye nia ya kutafuta elimu kuisaidia jamii inayomzunguka, hata kama ni kwa kujihusisha na NGO au private sector ambayo mwisho wa siku itakuwa na shughuli zenye mchango kwenye jamii inayomzunguka;

Inashangaza sana katika siasa, unakuta viongozi wanapigana fitina kwamba nchi hai hitaji viongozi ma professor..., lakini wao bado ndio vinara wa kutafuta kwa nguvu zote doctorate degrees za heshima, na usipomwita Doctor before jina lake, anakuona hauna heshima kabisa...
 
hao wenye degree mbona nao hatuoni tofauti na wasio na degree hasa kutoka ccm! mfano wewe unaona tofauti ya mchango kati ya mwigulu mwenye degree first class ya uchumi na Lusinde wa darasa la saba?? AU ipo tofauti ya kimtizamo na mchango kati ya dr.Mary Nagu na Ole sendeka??

Ama joseph mbilinyi mr sugu na tendu lissu ama kasulumbayi na mnyika ama freeman mbowe na zito kabwe
 
Chadema wabunge wenye degree ni wachache sana...hawa ni baadhi ambao hawana degree mleta mada nadhani kafanya makusudi kutowataja.

1. Freeman Mbowe
2. John Mnyika
3. Joseph Mbilinyi
4. Highness Kiwia
5. Silvester Mhoja
6. John Shibuda
7. Jeremiai Opulukwa
8. Said Afri
9. Vicent Nyerere
10. Ezekia Wenye
11. Joseph Machemuli

Hapo sijazama kwa wabunge wa viti maalum kina Rose Kamili.
 
Miongoni mwa sifa za mtu kuwa mbunge kwa mujibu wa katiba ni awe mtanzania aliyefikisha umri wa miaka 21 na angalau awe amemaliza darasa la saba.

After all, kuunga mkono kwa kusema "ndiyoooo" au "siyoooo" ama kupiga makofi, kwa uelewa wangu HAIHITAJI MTU AWE NA DEGREE, nadhani hivyo vigezo ndio maana vipo kama vilivyo! nadhani huu ni wakati mzuri tutoe maoni ya katiba ili vipengele kama hivi, viboreshwe.
 

Kuwa na Shahada si lazima ni Hekima na Uongozi Bora; Wale waliokuwa Mafisadi wanawakatia Umeme wananchi Nchi Nzima

Hao wote walikuwa na Madigree hawakujali Uzalendo, Walijali ni lini Matumbo yao yatajaa makaratasi ya kijani; Green US Dollars

Wengine Wana-Degree wanaona Mimi ni Mbunge nitapata kidogo kidogo kwenye Mauzo ya Bangi... Wengine 10% za Madini

Wengine ndio hao Wasomi kabisaa wanaiuza Serengeti...

Lakini kuna ambao hawajasoma na Wanapendwa na Wananchi wao sababu Wanatekeleza Matakwa yao na pia kuwatumikia

Ipasavyo, na ni Mzalendo hakwenda kutafuta hizo 10% au kujitangaza kama wengine Mfano; SUGU yeah Elimu ndogo lakini

Dunia Imemfundisha Mengi sidhani kama Wamachinga wa Mbeya - Watu wa chini kabisa; watalalamikia Uongozi wake; au

Daktari Mbeya atalalamikia Uongozi wake... Uongozi wake hauna Matabaka; ni Mzalendo; hapo Elimu haikutakiwa kama wewe

Utakavyo...
Jamaa zako wote wenye ELIMU WANA UWALAKINI; WEZI; WATOROSHAJI UTAJIRI WA NCHI.

Tusijidanganye kwamba uongozi ni karama, uongozi unapatikana kwa kutumia mambo mbali mbali. Zamani watoto wa watemi walifundwa katika ugo wa mtemi na hivyo kuwa warithi. Muundo huu unapingwa na njia za kidemokrasia kwa hiyo lazima kupata shule kama kweli unataka tupite mapito mazuri vinginevyo tunajidanganya tutabaki nyuma tu kama tuna viongozi mbumbumbu.
 
Ni muhimu tukapanuka zaidi na kuangalia umuhimu wa lugha katika international relations and international development community, hasa kwa nchi kama yetu ambayo traditionally imekuwa inategemea wahisani in terms of loans, aid, trade negotiations etc; tumeshindwa kuendeleza kiswahili kufikia hatua kama kiren kwa brazil; na kati ya sababu kubwa zinazotuingiza kwenye mikataba mibovu ni ufisadi lakini pia lugha; suala la ufisadi hapa kulijadili haina haja sana kwani wengi tupo ukurasa mmoja ju ya hilo, lakini hili la lugha, kuna case studies nyingi sana ambazo zinaelezea jinsi gani viongozi wetu wanashindwa kufanikisha mambo mengi wakikutana na wenzao wa nje kwa sababu ya kutojua lugha ya kiingereza; hii haina maana kwamba lugha ya kiswahili haifai, suala la msingi hapa ni kwamba hatuitumii ipasavyo hence kutukoseshwa potential leaders in the context of the above....

Mchambuzi ninakubaliana na wewe kuhusu suala la lugha na maendeleo (yawe ya kijamii, kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni, kisayansi, nk.). Kwa hakika, suala la lugha linakwenda mbali zaidi ya international relations. Jiulize kama kuna nchi yo yote duniani ambayo imeendelea (kiuchumi) inayotumia lugha za watu wengine katika elimu? China ambayo sasa hivi ni tishio la Marekani wanatumia lugha gani ambayo imewafikisha hapa walipo? Sera mbovu ya lugha katika elimu (ushahidi jinsi gani ukoloni ulivyotuathiri hadi karne hii) imechangia sana kutufukisha kwenye elimu ya ukariri (yaani copy & paste) na hivyo haitoi nafasi kwa the so called 'wasomi' kujenga ubunifu, utunduutundu wa kuhoji kila kinacotuzungula, kuwa wavumbuzi, nk. Tukiisha kariri na kupata digrii za udaktari basi tumemaliza kazi. Hicho ndo chanzo cha kwa nini hatuoni tofauti kubwa kati ya waheshimiwa sana wabunge 'wasomi' na wabunge wenye 'kisomo' cha chini!! Kama nchi hii imeharibiwa, imeharibiwa na the so called "wasomi". "wasomi' wameifanyia nini nchi hii kama sio kuwa ana akili finyu za kufisadi. Matokeo ya elimu ya copy & paste!!!!
 
hao wenye degree mbona nao
hatuoni tofauti na wasio na degree hasa kutoka ccm! mfano wewe unaona
tofauti ya mchango kati ya mwigulu mwenye degree first class ya uchumi
na Lusinde wa darasa la saba?? AU ipo tofauti ya kimtizamo na mchango
kati ya dr.Mary Nagu na Ole sendeka??

mfano hauendani. linganisha wabunge kwa wabunge siyo wabunge na mawaziri
 
Chadema wabunge wenye degree
ni wachache sana...hawa ni baadhi ambao hawana degree mleta mada nadhani
kafanya makusudi kutowataja.

1. Freeman Mbowe
2. John Mnyika
3. Joseph Mbilinyi
4. Highness Kiwia
5. Silvester Mhoja
6. John Shibuda
7. Jeremiai Opulukwa
8. Said Afri
9. Vicent Nyerere
10. Ezekia Wenye
11. Joseph Machemuli

Hapo sijazama kwa wabunge wa viti maalum kina Rose Kamili.

mnyika ni graduate!
 
Kenyans have a bill,waiting the signature of the head of states which commands each MP should have atleast a degree to support his/her stay in the house of representatives. TANZANIANS WORK UP, LETS BE OURSELVES IN 2015.


Wewe naona hujipendi...hivi unawajuwa wabunge wa Tanzania kwa ushikirikina? Utarogwa wewe, ipo siku utajikuta computer yako inakupiga makofi kisa unakosoa wabunge.
 
Naona umeanzisha vita ambayo wengi watachangia negative. Ila kwasasa ni vema tukawa na viongozi walioenda shule, hivyo kuwa rahisi kutafuta ufumbuzi katika changamoto mablimbali. Sikatai kuwa kuna watu ambao hawana Degree lakini wanaufanisi wa hali ya juu kuliko hata wenye nazo, ila hii imekuwa utetezi kwa wale ambao hawajaenda shule na hawajiwezi katika kupambanua changamoto zozote.

Nafikiri tutafute njia nzuri ya kuchagua viongozi wetu, maana pia kuwa na degree siyo kuwa wewe unaweza uongozi zaidi. Bali inaondoa shaka kuwa angalau utakuwa na uwelewa wa mambo.

Naomba nikupe assignment nyingine, je hao wenye degree ndiyo wafanisi zaidi? Na je hizo Degree ni za halali/ zinatambulika??
Inatakiwa itungwe sheria,kama ilivyo kwa ajira zingine kuwepo pia na sifa maalumu za kuwa mbunge,sifa hizi ziwekwe kwa wabunge wa majimbo na pia viti maalumu kuepuka uwezekano wa kuwachagua vimada wao,alafu hii issue ya ubunge wa kuteuliwa ifutwe kabisa,ni ulaji tu.
 
Chadema wabunge wenye degree ni wachache sana...hawa ni baadhi ambao hawana degree mleta mada nadhani kafanya makusudi kutowataja.

1. Freeman Mbowe
2. John Mnyika
3. Joseph Mbilinyi
4. Highness Kiwia
5. Silvester Mhoja
6. John Shibuda
7. Jeremiai Opulukwa
8. Said Afri
9. Vicent Nyerere
10. Ezekia Wenye
11. Joseph Machemuli

Hapo sijazama kwa wabunge wa viti maalum kina Rose Kamili.
Ila si kasema wabunge wa BUNGE JMT! Ingawa katoa uwiano wa wabunge wa CUF,CCM pekee.
 
Back
Top Bottom