51% ya wabunge wa JMT hawana shahada [Degree]

JERUSALEM 2006

JF-Expert Member
Apr 23, 2012
526
583
Asalaam,
Katika tafiti nilizofanya kwenye website ya bunge, zaidi ya nusu (50+%) ya wabunge hawana degree. Hii inadhihirisha jinsi gani chombo kikuu cha kutunga sheria na kusimamia serikali hakina wataalamu.
Katika tafiti zangu nimebaini kuwa;
1. Wabunge wengi ni form four graduates na wana poccess certificates za mambo mbalimbali.
2. Wabunge wengi wasio na degree ni wale wa viti maalumu, huku wengi wao wakitokea CCM na CUF.
3. Wabunge wengi watokao visiwani hawana hata deploma.(STASHAHADA) i.e 60%.
MY CONCERN:
HIVI BUNGE LETU LINASIMAMIA SERIKALI AU LINASIMAMIWA NA SERIKALI.
Happy Ramadhan Kareem.
 
Na katika hao 40% ambao wanaonyesha wana degree karibia 30% ni degree za kuchakachua...sasa ndio uamini kwa nini tunaona vioja na vurugu bungeni siku hizi....ni kwa sababu hatuna wasomi tuna wahuni tu huko
 
Naona umeanzisha vita ambayo wengi watachangia negative. Ila kwasasa ni vema tukawa na viongozi walioenda shule, hivyo kuwa rahisi kutafuta ufumbuzi katika changamoto mablimbali. Sikatai kuwa kuna watu ambao hawana Degree lakini wanaufanisi wa hali ya juu kuliko hata wenye nazo, ila hii imekuwa utetezi kwa wale ambao hawajaenda shule na hawajiwezi katika kupambanua changamoto zozote.

Nafikiri tutafute njia nzuri ya kuchagua viongozi wetu, maana pia kuwa na degree siyo kuwa wewe unaweza uongozi zaidi. Bali inaondoa shaka kuwa angalau utakuwa na uwelewa wa mambo.

Naomba nikupe assignment nyingine, je hao wenye degree ndiyo wafanisi zaidi? Na je hizo Degree ni za halali/ zinatambulika??
 
Sifa na kujuakusoma na kuandika na mamuzi yao hupitishwa kwa kupaza sauti! “Serikali itaendelea kutumia sheria mbaya mpakazitakpobadlishwa’’ Pinda
 
Na katika hao 40% ambao wanaonyesha wana degree karibia 30% ni degree za kuchakachua...sasa ndio uamini kwa nini tunaona vioja na vurugu bungeni siku hizi....ni kwa sababu hatuna wasomi tuna wahuni tu huko
Vioja na Vurugu zenyewe bora vingekuwa ni mabishano ya hoja, worse inakuwa ni kushabikia au kuponda hoja kwa vile tu zimetolewa na fulani!
In actual fact haihitaji hata kufanya utafiti kwenye website!...you just watch the session for 30 min...u have all the data!
 
hao wenye degree mbona nao hatuoni tofauti na wasio na degree hasa kutoka ccm! mfano wewe unaona tofauti ya mchango kati ya mwigulu mwenye degree first class ya uchumi na Lusinde wa darasa la saba?? AU ipo tofauti ya kimtizamo na mchango kati ya dr.Mary Nagu na Ole sendeka??
 
Kenyans have a bill,waiting the signature of the head of states which commands each MP should have atleast a degree to support his/her stay in the house of representatives. TANZANIANS WORK UP, LETS BE OURSELVES IN 2015.
 
Asalaam,
Katika tafiti nilizofanya kwenye website ya bunge, zaidi ya nusu (50+%) ya wabunge hawana degree. Hii inadhihirisha jinsi gani chombo kikuu cha kutunga sheria na kusimamia serikali hakina wataalamu.
Katika tafiti zangu nimebaini kuwa;
1. Wabunge wengi ni form four graduates na wana poccess certificates za mambo mbalimbali.
2. Wabunge wengi wasio na degree ni wale wa viti maalumu, huku wengi wao wakitokea CCM na CUF.
3. Wabunge wengi watokao visiwani hawana hata deploma.(STASHAHADA) i.e 60%.
MY CONCERN:
HIVI BUNGE LETU LINASIMAMIA SERIKALI AU LINASIMAMIWA NA SERIKALI.
Happy Ramadhan Kareem.

Kenyans have a bill,waiting the signature of the head of states which commands each MP should have atleast a degree to support his/her stay in the house of representatives. TANZANIANS WORK UP, LETS BE OURSELVES IN 2015.

Wanaotunga hizo sheria ni wao. Hebu jaribu kufikiria kama mswaada wa namna hii ukipelekwa bungeni, utakwamishwa kwa asilima ngapi? Lazima itakuwa sawa au zaidi ya 51%. Bunge letu linahitaji wasomi wenye uelewa wa mambo mbalimbali ili tusonge mbele.
 
Asalaam,
Katika tafiti nilizofanya kwenye website ya bunge, zaidi ya nusu (50+%) ya wabunge hawana degree. Hii inadhihirisha jinsi gani chombo kikuu cha kutunga sheria na kusimamia serikali hakina wataalamu.
Katika tafiti zangu nimebaini kuwa;
1. Wabunge wengi ni form four graduates na wana poccess certificates za mambo mbalimbali.
2. Wabunge wengi wasio na degree ni wale wa viti maalumu, huku wengi wao wakitokea CCM na CUF.
3. Wabunge wengi watokao visiwani hawana hata deploma.(STASHAHADA) i.e 60%.
MY CONCERN:
HIVI BUNGE LETU LINASIMAMIA SERIKALI AU LINASIMAMIWA NA SERIKALI.
Happy Ramadhan Kareem.


ASILIMIA 99.9 YA WABUNGE WA CDM WANADEGREE MBILI,ASILIMIA 99 YA WABUNGE WA CCM HAWANA HATA DEGREE MOJA,ASILIMIA 80 YA WABUNGE WA CUF HAWANA DEGREE.

ASILIMIA 99.9 YA WABUNGE WAKRISTO WANA DEGREE ,ASILIMIA 99.9 YA WABUNGE WAISLAM HAWANA HATA DIPLOMA


ASILIMIA 99 YA WABUNGE KUTOKA ZENJI WAMEMALIZA MADRASATUL TUU HAWAJUI HAT FORM ONE nI NINI
 
sidhani kama taifa linahitaji utitiri wa shahada wakati huu lakini linahitaji watanzania wenye uthubutu wakuleta mabadiriko ya kweli kwa nchi na maisha ya watanzania wenzao
 
Asalaam,
Katika tafiti nilizofanya kwenye website ya bunge, zaidi ya nusu (50+%) ya wabunge hawana degree. Hii inadhihirisha jinsi gani chombo kikuu cha kutunga sheria na kusimamia serikali hakina wataalamu.
Katika tafiti zangu nimebaini kuwa;
1. Wabunge wengi ni form four graduates na wana poccess certificates za mambo mbalimbali.
2. Wabunge wengi wasio na degree ni wale wa viti maalumu, huku wengi wao wakitokea CCM na CUF.
3. Wabunge wengi watokao visiwani hawana hata deploma.(STASHAHADA) i.e 60%.
MY CONCERN:
HIVI BUNGE LETU LINASIMAMIA SERIKALI AU LINASIMAMIWA NA SERIKALI.
Happy Ramadhan Kareem.

Kuwa na Shahada si lazima ni Hekima na Uongozi Bora; Wale waliokuwa Mafisadi wanawakatia Umeme wananchi Nchi Nzima

Hao wote walikuwa na Madigree hawakujali Uzalendo, Walijali ni lini Matumbo yao yatajaa makaratasi ya kijani; Green US Dollars

Wengine Wana-Degree wanaona Mimi ni Mbunge nitapata kidogo kidogo kwenye Mauzo ya Bangi... Wengine 10% za Madini

Wengine ndio hao Wasomi kabisaa wanaiuza Serengeti...

Lakini kuna ambao hawajasoma na Wanapendwa na Wananchi wao sababu Wanatekeleza Matakwa yao na pia kuwatumikia

Ipasavyo, na ni Mzalendo hakwenda kutafuta hizo 10% au kujitangaza kama wengine Mfano; SUGU yeah Elimu ndogo lakini

Dunia Imemfundisha Mengi sidhani kama Wamachinga wa Mbeya - Watu wa chini kabisa; watalalamikia Uongozi wake; au

Daktari Mbeya atalalamikia Uongozi wake... Uongozi wake hauna Matabaka; ni Mzalendo; hapo Elimu haikutakiwa kama wewe

Utakavyo...
Jamaa zako wote wenye ELIMU WANA UWALAKINI; WEZI; WATOROSHAJI UTAJIRI WA NCHI.
 

Kuwa na Shahada si lazima ni Hekima na Uongozi Bora; Wale waliokuwa Mafisadi wanawakatia Umeme wananchi Nchi Nzima

Hao wote walikuwa na Madigree hawakujali Uzalendo, Walijali ni lini Matumbo yao yatajaa makaratasi ya kijani; Green US Dollars

Wengine Wana-Degree wanaona Mimi ni Mbunge nitapata kidogo kidogo kwenye Mauzo ya Bangi... Wengine 10% za Madini

Wengine ndio hao Wasomi kabisaa wanaiuza Serengeti...

Lakini kuna ambao hawajasoma na Wanapendwa na Wananchi wao sababu Wanatekeleza Matakwa yao na pia kuwatumikia

Ipasavyo, na ni Mzalendo hakwenda kutafuta hizo 10% au kujitangaza kama wengine Mfano; SUGU yeah Elimu ndogo lakini

Dunia Imemfundisha Mengi sidhani kama Wamachinga wa Mbeya - Watu wa chini kabisa; watalalamikia Uongozi wake; au

Daktari Mbeya atalalamikia Uongozi wake... Uongozi wake hauna Matabaka; ni Mzalendo; hapo Elimu haikutakiwa kama wewe

Utakavyo...
Jamaa zako wote wenye ELIMU WANA UWALAKINI; WEZI; WATOROSHAJI UTAJIRI WA NCHI.

Mkuu hii ni kwa wachache mno kama ulivyotoa mfano kwa Sugu na tena wenye exposure kubwa ya kimaisha. Lakini wengi na hasa wasiokuwa na exposure ya maisha zaidi ndo wanaotudidimiza. Tukubali kwamba msomi ananafasi kubwa zaidi ya kutumia elimu yake kujenga au kubomoa kwa umakini zaidi kuliko asiyekuwa na elimu. Kikubwa tuchague wasomi ambao watatumia elimu zao kujenga nchi.Huoni utofauti ya Dr. za ukweli na wengine?
 
chukulia mfano mtu amesoma degree ya umeme, mwingine ya muziki, mwingine ya beauty therapy, mwingine ya kilimo. Degree hizo zitawasaidia vipi katika kuamua kama mpaka wa Tanzania ni Malawi uko ziwani au nchi kavu, utawasaidia vipi kujua kwa daraja la Kigamboni siyo muhimu zaidi ya madaraja yanayounganisha wilaya mbalimbali nchini?
Hakuna uhusiano kati ya degree na ubunge. Unawakilisha mawazo na matakwa ya watu sio kuweka akili zako kwenye mahitaji yao. Sifa ya mwakilishi ni kuheshimu matakwa ya anaowawakilisha. Sasa degree ya nini hapo? Mtu anaweza asiwe na cheti chochote lakini akawa ana ujuzi mkubwa wa mambo mbalimbali. Kwa reference someni historia ya malcolm X.
 
Mkuu hii ni kwa wachache mno kama ulivyotoa mfano kwa Sugu na tena wenye exposure kubwa ya kimaisha. Lakini wengi na hasa wasiokuwa na exposure ya maisha zaidi ndo wanaotudidimiza. Tukubali kwamba msomi ananafasi kubwa zaidi ya kutumia elimu yake kujenga au kubomoa kwa umakini zaidi kuliko asiyekuwa na elimu. Kikubwa tuchague wasomi ambao watatumia elimu zao kujenga nchi.Huoni utofauti ya Dr. za ukweli na wengine?

Wametajwa Wabunge wa CUF kuwa wengi wao hawana hizo ELIMU; Lakini wabunge wa CUF ni wakali kweli kuhusu

UFISADI, CCM hawana advantage kuhusu Uzalendo Wamechota Chota kila Mahali Utajiri wa Nchi, yaani hadi Madiwani wao

Ni wachotaji kwa Baraka ya baadhi ya Wabunge kwenye Kamati za Bunge, na Wengi wao humo ndani ni Wenye Madigree

Wewe Speaker anakataza Wabunge kutoongelea mbunge gani anatoa rushwa jimboni kwake? Huyu Mama ana Degree

Kwanini anafanya hivyo? Si Maficho? it is totally crazy More Money Mongering... Hii haina sababu ya Usomi; Ni Uozo wa

Wabunge wa CCM; RADA issue mshitakiwa Mkubwa ni Mwanasheria Mkuu, Sio wabunge ambao hawajasoma...

Kwahiyo Mnatakwa Wasomi wote ili Nchi yooote iuzwe? tutakuwa kama CONGO-Kinsasha? Ubaya ni nini hamtaweza kuishi

Uingereza au Nchi yoyote ya UEROPE labda Malaysia au Thailand...
 
Miongoni mwa sifa za mtu kuwa mbunge kwa mujibu wa katiba ni awe mtanzania aliyefikisha umri wa miaka 21 na angalau awe amemaliza darasa la saba.
 
Nimekuja kuelewa katika vitu ambavyo vinawatenganisha Watanzania ni elimu. Mtu akipost thread kuhusu ELIMU anakumbana na mawazo kinzani. Lakini ukweli unabaki pale pale kwamba ELIMU tena ya UKWELI kwa ustawi wa taifa letu. Ndiyo maana unakuta watu wabunge wetu kwenye bunge la Afrika ya Mashariki toka tanzania wana waachia uwanja wenzao toka Kenya, Uganda na Rwanda. Hawajui lugha na hoja hakuna...kisa tunatanguliza c=CHAMA fulani kuliko weledi...Njia ya mwongo ni fupi...Tubadilike
 
Sitetei ujinga,

Lakini

Luiz Inácio Lula da Silva alikuwa na shahada gani? Na kaacha legacy gani amabayo wasomi zaidi yake hawakuweza?

Na shahada zenyewe mnazozungumzia ni zipi? Hizi za kina first class economist Mwigulu Nchemba na Baba Rizi Mkuu wa kaya au nyingine?

Nipe Lula mmoja asiye na shahada over any Kikwete with a Ph.D!

Naweza kuondoa standard ya degree kwa mtu kama Lula (trade unionist) Kawawa (trade unionist) Zuma (freedom fighter of sorts) kwa sababu nikiwauliza "kwa nini huna degree?" wanaweza kunipa sababu itakayonifanya nione kwamba wana sifa za uongozi kubwa kuliko degree, na pengine wamejifunza mengi zaidi ya degrees ambazo mara nyingine zinakuwa si relevant.

Kuna watu wanaanza uongozi tangu wadogo, wanatoka katika familia masikini katika nchi masikini, nchi zenyewe zetu hizi chuo kikuu kimoja mpaka juzi. Wengine ilibidi wafanye kazi kuwasomesha wengine, wengine ilibidi wapiganie uhuru ili nchi iwepo, wengine ilibidi waende kwenye chuo cha dunia ma trade unionist huko,wengine ma enterpreneurs kama kina Bill Gates wameona chuo kitawachelewesha tu.

Kwa hiyo, swala muhimu ni maelezo kwa nini mtu hana degree.

Mie mtu anayeniambia alipata nafasi ya kusoma akashindwa kwa sababu za kifamilia - yeye alikuwa anategemewa kufanya kazi na mama yake alikuwa mgonjwa, hakuweza kuacha kazi kwenda kuchukua degree- bado nampa maksi zake za kujitoa na kuwa kiongozi.

Tuangalie mambo kwa undani zaidi, na hii brainwashed education ya kupangiwa na wazungu tusii overrate.

Elimu haipimwi kwa degree.

Ingekuwa hivyo tusingeona madudu Magogoni pale ambapo mpaka leo watu wanatumia email ya yahoo at the risk of national security na wandishi wao hawajui kuandika hata sentensi moja bila kupindisha sarufi.

Tuongelee wabunge wenye mchango wa kisomi na wasio na mchango wa kisomi.

Usomi ni werevu, usambe shahada.
 
Luiz Inácio Lula da Silva alikuwa na shahada gani?

Ni kweli; nadhani wengi wetu tuna equate lugha ya kiingereza na elimu; Rais wa Brazil hakuwa na shida sana kwani lugha yao ndio lugha rasmi ya taifa na hata anapo interact na wenzake, bado anakuwa on point kwani kinachoendelea ni tafsiri; kiswahili kingekuwa katika hali hiyo, mbona wanasiasa wetu wenye hazina tosha ya misamiati wangetupeleka mbali sana;
 
Miongoni mwa sifa za mtu kuwa mbunge kwa mujibu wa katiba ni awe mtanzania aliyefikisha umri wa miaka 21 na angalau awe amemaliza darasa la saba.

Katiba mpya lazima tubadili hapo kwenye ELIMU iwe hivi angalau awe na degree moja. Hii itasaidia kuondoa wabunge incompetent na WAUZA unga kama akina Munde Tambwe.
 
Katiba mpya lazima tubadili hapo kwenye ELIMU iwe hivi angalau awe na degree moja. Hii itasaidia kuondoa wabunge incompetent na WAUZA unga kama akina Munde Tambwe.

Upo sahihi lakini tujiandae kupata upinzani mkali kweli kweli juu ya hilo kwani hata wakati wa uchaguzi, mara nyingi wenye elimu huwa wanatengenezewa fitina na zinaingia vizuri kwa wapiga kura wengi. Wenzetu wa UK kwa mfano hali yao ipo kama ifuatavyo:

 Nine in ten MPs in 2010 attended university – by far the highest proportion of any
Parliament to date. This includes just under three in ten who were educated at either
Oxford or Cambridge universities. Oxford has produced 102 MPs serving in the 2010
Parliament.


 38% of Conservative MPs were educated at Oxford or Cambridge compared with
20% of Labour MPs and 28% of Liberal Democrat MPs.


 Newly elected MPs were even more likely to be graduates – with 94% attending a
university,
including 69% who had attended a leading research university, and 28%
who had attended Oxbridge.

Source: The Educational Backgrounds of Members of Parliament in 2010 - Sutton Trust
 
Back
Top Bottom