2015.......Tujipange!

Hilo la kusema kusubiri ni kukipa ccm pumzi zaidi. Ningekushauri uwashauri wapinzani wengine kumuunga slaa mkono
 
Hilo la kusema kusubiri ni kukipa ccm pumzi zaidi. Ningekushauri uwashauri wapinzani wengine kumuunga slaa mkono

Mkuu soma thread yote vizuri. Hakuna ninapo shauri watu wasubiri 2015 na wasi fanye chochote sasa. Read it again properly. Na hilo la upinzani kumuunga mkono Slaa ushauri huo umesha tolewa sana hapa JF. Kama upinzani ni waku sikia basi wata kuwa wamesha sikia na kupokea huo ujumbe.
 
Don't compare apples and oranges. Uraisi ni cheo kimoja tu. Shuleni mtu ukiwa wa kumi haimaanisha huta endelea na masomo. Kinacho angaliwa ni maksi zako. SO sioni uwiano hapo na mada iliyopo. Mada ni maandalizi. Ina sikitisha kwamba watu hawaja fikiria ni nini kinacho takiwa kufanyika kumpa mgombea wamtakae ushindi bali wanaona moja kwa moja ata shinda. Watu lazima wajifunze kutofautisha hisia zao binafsi na mawazo ya wengine. Yes wewe una weza ukamsupport Slaa, yes mimi naweza kumsupport Slaa ila ume chunguza nini hisia za wapiga kura wa Tanzania? Je una uhakika kila mtu ana mawazo kama yakwako. Fikiria.

Mwanafalsafa focus ya sasa hivi ni uchaguzi wa mwaka huu 2010. Wanaotakiwa kujipanga na Uchaguzi wa 2015 kwa sasa ni CCJ. Vile vile sina uhakika kama kuna mtu ana mawazo kama yangu. Ndio maana tuko hapa na nakubali kutofautiana.

Hakuna sababu ya msingi ya kusema huwezi ku compare apple na oranges. Yote ni matunda labda ungesema ku compare apples na mawe.

Mimi nimekuelewa sababu pia na wewe una hisia kuwa Dk slaa atashindwa basi ni bora waajiandae na uchaguzi wa 2015. Unaweza kusema msemo huu huu kwa lugha nyingine kuwa kuwa JK atashinda lengo la kampeni za Urasi CCM liwe ni uchaguzi wa mwaka 2015.

Au sikukuelewa mkuu.
 

Slaa akifanikia na akashinda bado itabidi yeye na chama chake kiongoze serikali kwa miaka mitano. hamna anaye ongelea nini kifanyike baada ya ushindi kana kwamba kutoka kwa CCM tu ndiyo mwisho wa kazi. Wengi wenu mtasema tukazanie kuona kwanza ushindi wa upinzani lakini mimi ni mtu ninaye penda kuangalia mbele. Ni sawa sawa na kuomba visa ya kwenda kusoma ne bila kufikiria ada utailipaje. Mimi ni wale ambao siyo tu naangalia visa nitaipataje bali ada na mahitaji mengine nita yafanikishaje....kuangalia mbele
Unachoongea ni kweli, lakin tuki prioritize, kipi Bora kwa Sasa,kuangalia jinsi gani Dr Slaa atashinda au nini atafanya baada ya kushinda au vyote kwa pamoja,kitu ambacho mimi nadhan Mwana FA unakosea ni kule kutaka kutozungumzia mikakati ya nini kifanyike ilikupata Viongozi Bora,unacho stick ni kuwa hao viongozi watafanya nini,kumbuka kuwa akipatikana kiongozi bora,itakuwa ni Rahisi sana kwa hata wana nchi ku mshape katika maamuzi ambayo atayafanya (Tofauti na sasa),kama umekiri wewe ni kada wa CCM na utatetea maslahi ya CCM kwa ngyvu zote,yanini basi kuusemea upinzani,hauoni kuwa huo ni unafiki....
Me nadhani tu stick zaid katika kujenga hoja za nini tufanye kupa viongozi bora,na tuwapime kwa utendaji wao (Slaa Bungen,Jk Ikulu nk nk)...
 
MwanaFalsafa1

Unaonekana tu ni kuwa ni mmoja ya watu wanaodhani uongozi Tz unapaswa kuhodhiwa na CCM na familia zao. Hoja zako mara zingine kusema unajisikia kuwa kiongozi na blah blah haziwezi kuniaminisha kuwa unajua kiongozi mzuri ni wa namna gani. Watu tumechoka na huu mfumo wa Chama chako unachosema uliwekewa kwenye uji, ni nini wametenda kwa watanzania? Hii ni sawa na wale wanaosema wanapenda tu CCM, hoja ni kuwa wao wanaipenda tu!
 
Back
Top Bottom