2011 ni mwaka wa Mfumuko wa Bei, maisha magumu na Ujambazi juu!

watu wengi waliofanikiwa hawakupata mafanikio hayo kwa msaada wa serikali kama wapo ni wachache sana, mtu mweyewe ndiyo mwenye jukumu ka kuhakikisha kuwa anajiwekea katika mazingira ambayo yatamrahisishia kufanikiwa. Kama ni mwanafunzi, kinachotakiwa ni kusoma kwa bidii ili kuweza kufaulu mitihani yake vizuri ili mwisho wa siku apate ajira au maarifa yatakayomwezesha kutoka kimaisha. Serikali inachofanya ni kuweka mazingira fulani tu ambayo yatamsafishia njia mtu kutoka. mtu yeyote sijidanganye kucheza na maisha akidhani kuwa anaweza kufanikiwa kirahisi juhudi na maarifa ya mtu mwenyewe ndiyo njia pekee ya kufanikiwa kimaisha. Uvivu na ulegevu wa namna yoyote pamoja na kujihusisha na vitendo viovu yote hayo matokeo yake ni kukudhoofisha kimaisha na baadae mtu anabaki kusingizia serikali kuwa haikufanya chochote. Fanya shughuli yako yoyote halali kwa bidii, kuwa na nidhamu ya pesa unayopata, jiepushe na starehe pamoja na matumizi mabaya ya pesa yako, kuwa mbunifu katika kazi yako au biashara yako, lenga soko lenye wataja au huduma utaona kama hutafanikiwa!!! Kamwe usisubiri muujiza wa mafanikio, muujiza upo kichwani mwako.:confused2:
 
Serikali itafakari yafuatayo. Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini ilikataliwa bungeni, walienda kujipanga upya. Wakati waziri wa fedha anawasilisha bajeti yake alisema wameondoa ushuru kwenye mafuta ya diesel na Petrol ili kuleta unafuu kwa mtanzania.Ukweli ni kuwa bajeti ni ya mwaka mzima na hivyo tunategemea kama ni unafuu katika mafuta, basi kwa mwaka mzima bei inayotangazwa na kutumika katika kipindi cha mwaka mzima haitazidi bei iliyokuwepo awali. Kwanza kabisa, mimi ni miongoni mwa tuliona kuwa punguzo la bei ya mafuta ilikuwa kiini macho kwa mwenendo wa serikali yetu. Bei ilishushwa toka 2090 mpaka 2004 kwa petrol. Punguzo la shilingi 86. Hapa ni kuwa wenye kusafirisha abiria, hawawezi kushusha bei, wala mwenye gari la kutembelea punguzo la shilingi 86 kwa lita moja halikuwa na tija(huyu anaweza kuokoa shilingi 400 tu kwa siku fedha ambayo kwa mfumuko wa bei bado haina tija). Kwa wafanyabiashara, ambao wanakuwa na mafuta mengi, kwa wao ni kweli faida ilipungua(sio kiwa wanapata hasara). Sasa wakati muda si mrefu wananchi tumeambiwa kuwa bei ya mafuta inashushwa wauza mafuta wakagoma wengi tumeteseka sana. Kwa mfano, mimi kuna siku nilipita vituo viwili, nilikuta foleni ya magari yasiyopungua 200 na watu wenye galoni wasiopungua 300 kila kituo, sikuweza kusubiri. Bahati nzuri nilifika nyumbani. Kesho yake wakati natoka na gari, nikafika sehemu nikakwama(mafuta) yaliisha sehemu muda wa saa 2 asbh,matokeo yake ni kuwa nikapata mafuta saa tano mchana. Kwa hiyo kuanzia saa 2 mpaka saa 5 sikuweza kufanya chochote. Baada ya mvutano huo, wiki hii jumatatu, tarehe 15 August 2011, bei ya mafuta imekuwa 2114 kwa maeneo ambayo mimi naishi. Tunaambiwa EWURA wana mamlaka ya kutangaza bei mpya kila baada ya wiki mbili. Swali kuu. Je Waziri wa fedha kwa nini alitoa bajeti ambayo alisema anatoa nafaa kwa wananchi kwa mwaka 2011/2011 lakini bei ya mafuta imeshakuwa kubwa kuliko ya ile ya mwezi juni kabla ya kupewa matumaini. Kwa nini EWURA wawadanganye wanachi kwa kusema waliiamura wasambazaji/wauzaji wa mafuta washushe bei, lakini ndani ya wiki mbili wameongeza tena bei ni kubwa kuliko ile waliyokuwa wanawataka wauza mafuta washushe. Naomba serikali ijue kuwa 1. Inawahadaa wananchi 2. Inawapotezea wananchi muda wa kujadili mambo ambayo inajua yenyewe haiyasimamii. Mwisho;Wote tunafahamu kuwa bei ya vitu imekuwa mara mbili au tatu zaidi ya bei ya vitu ambazo zilikuwepo kabla ya serikali hii kuingia madarakani mwaka 2005.(wote tunajua bei za mafuta, sukali, vifaa vya ujenzi, mchele, unga nk). Je kipato cha mwananchi yule wa mwaka 2005 kimekuwa mara mbili au tatu? Kwa kuwa demokrasia inatoa miaka mitano ya kubadili yote haya, na kwa kuwa, mfumo wetu bado unawafanya walioserikalini waendelee kutoa hatima ya mwananchi wa kawaida, ushauri ni kwamba serikali iwe inafanya uungwana na kutafakari madhara ya kushindwa kupanga mikakati ambayo inalenga kuboresha maisha ya mtanzania.Wananchi hawaulizi maslai stahiki ya viongozi wetu, wanachouliza ni yale mambo ambayo tulitaraji viongozi wetu wanafanye lakini hayafanyiki. Wananchi wanalipa kodi, ili viongozi wetu wapate pesa ya kuleta maendeleo ya nchi, na kwa mantiki hii ndio maana viongozi wetu wanalipwa, wanahudumiwa malazi, chaluka, usafiri nk ili wapate muda wa kupanga mipango endelevu ya kusaidia mwananchi. Kwa Tanzania, mambo si hivyo. Tutafakari. Leo hii(Alhamisi, Agosti 18). Mhe. Wenje ameomba mwongozo bungeni kuwa serikali ijibu kwa nini wakati kabla ya bajeti ya wizara ya Nishati na Madini haijapiitishwa mgao ulipungua au kuondolewa, lakini bajeti imepita tu, mwanza siku nne hakuna umeme, Mbeya, Dar es Salaam, Kigoma na kwingineko hali ni mbaya, maji hayatoki sababu ya kukosekana kwa umeme, shughuli zote zimesimama. Spika ameomba serikali ijibu. Tunakoelekea ni hatari zaidi. Serikali, itafakari.
 
Maisha kwa kweli ni magumu sasa,
Kila kukicha ni stori tuuu huyu kaiba hiki na huyo kaingia mkataba feki.
 
Wanasiasa wanakoipeleka hii Tanzania siyo,<br />
<br />
Pazeni sauti, umeme bei ikipanda, bei ya mkate pia itakuwa juu,<br />
<br />
Kataeni Ufisadi, asiye na Kipato lazima atakuwa Kibaka.<br />
<br />
Licha ya Mvua kutonyesha,bado sisi viongozi wetu wanaendelea kuwa manyapara wa mafisadi.<br />
<br />
Kila kitu, tunampa huyo mhindi hadi PPF zetu tumemwachia.<br />
<br />
Napata hofu sana, vibaka watakuwa wengi mitaani,ujambazi utakuwa hatari sana.<br />
<br />
Jameni jameni amkeni,<br />
<br />
Nchi imekwenda
<br />
<br />
A Cassandra has only but rescient capability on foreseeing the misfortunes. On the other hand, optimistics sanguinely learns to face the quagmires and converts predicaments into opportunities i.e they see life in its positive side.
 
Mwita,
Its non sense to praise trash leaders,

Its stil unbelievable to smile to a person who has spent more 300 days visiting foregn country in within 1800 days kama kiongozi. Still akiulizwa maswali kwa nini Tanzania nia Maskini anajibu Hata yeye hajui

It is only shortsightened guys like you can praise a man who wants to invest more that Ten trilion at Kigamboni Project wakati watu hawana viwanda wala umeme na chakula.

Come back Home and repent
 
Katika kile wananchi walichotegemea kwa kiongozi wetu mkuu wa nchi,hali imekua kinyume sasa kwani hali ya maisha imekua ngumu kila inapokucha afadhali ya jana........bei ya sukari sasa imefikia 3000/= katika baadhi ya mikoa kutokana na kusafirishwa kwenda nchi jirani za kenya na uganda na serikali ikinyamaza kimya bila kutoa tamko.umeme wa luku nao sasa wapatikana kwa taabu sana na maeneo machache sana,kumeonekana foleni ndefu za watu wakisubiri huduma hiyo wengi wao wakikata tamaa kama watafanikiwa kuipata.

Wananchi wengi wamejikatia tamaa na hawajui hatma yao ya kesho kwani pesa imeshuka thamani,na vitu mhimu kama nishati,vyakula kua bei juu sana huku serikali ikikaa kimya kutoa matamko katika baadhi ya sekta.
"wanateteana tena hadharani kwa kutoa ama kupeana rushwa za mabilioni,wakisema ni kawaida huu ni u*********," alilalamika kijana mmoja aliekua na jazba.

"mimi bwana ni ccm lakini kwa staili hii jamaa nchi imemshinda sijui",alisema mzee aliekua katika foleni hiyo ya kununua umeme.

Katika hali nyingine isiyokua ya kawaida baadhi ya wananchi wamehusisha utendaji wa kiongozi huyo na kifo cha mnajimu shehe yahya,kua utendaji wake ulitegemea sana msaada wa shehe huyo na tangu afariki mambo si mambo.

Huku mtaani watu hawana tena imani na serikali yao,wamepoteza matumaini na viongozi wao,wanasubiri waone hatma ya nchi yao hasa tunapoelekea kutimiza miaka 50 tangu tupate uhuru,na wengine wakisema ni bora wakoloni wangeendelea kukaa na kututawala............
 
Huku mtaani watu hawana tena imani na serikali yao,wamepoteza matumaini na viongozi wao,wanasubiri waone hatma ya nchi yao hasa tunapoelekea kutimiza miaka 50 tangu tupate uhuru,na wengine wakisema ni bora wakoloni wangeendelea kukaa na kututawala............


Wasilalamike wao ndio walioiweka hii serikali ambayo wanasema hawana imani nayo,

Kama hawana imani wanangoja nini?

Afadhali wakati wa mkoloni watu waliamua na kutuletea uhuru, sasa hivi pamoja na elimu, ukilinganisha na enzi za TAA na ASP, tumekaa tu na kulalamika.
 
Wasilalamike wao ndio walioiweka hii serikali ambayo wanasema hawana imani nayo,

Kama hawana imani wanangoja nini?

Afadhali wakati wa mkoloni watu waliamua na kutuletea uhuru, sasa hivi pamoja na elimu, ukilinganisha na enzi za TAA na ASP, tumekaa tu na kulalamika.

Mkubwa ulichokizungumza japo hakifurahishi... ila ndo ukweli wenyewe. Tumezidi kuwa mazoba!! Kazi kulalamika tu ndo tunachokijua!! We are nothing but cowards!!!
 
Wasilalamike wao ndio walioiweka hii serikali ambayo wanasema hawana imani nayo,

Kama hawana imani wanangoja nini?

Afadhali wakati wa mkoloni watu waliamua na kutuletea uhuru, sasa hivi pamoja na elimu, ukilinganisha na enzi za TAA na ASP, tumekaa tu na kulalamika.
Huenda likawa jambo gumu sana kuthibitisha kama hii serikali kweli ilichaguliwa ama ilijichagua yenyewe.
 
kuna mama muuza matunda soko la nyuki tegeta njee barabarani,kasema leo yeye ni mwana ccm hai lakini kwa utawala wa huu mbovu ameamua kuachana na ccm, kahamia chadema!
 
Unajua nimegundua kuwa kumbe hata Obama mwenyewe hana utaratibu wa kuongea na wananchi wake kila mwezi. Nadhani JK naye ana kila sababu ya kutoendelea na huu utaratibu uliopitwa na wakati. Kinachoonekana kwa sasa ni kuwa ameamua kuwa mtendaji zaidi kuliko muongeaji, kitu ambacho kinastahili sifa sana. Si umeona bei za mafuta zilivyoshuka sasa.
 
kuna mama muuza matunda soko la nyuki tegeta njee barabarani,kasema leo yeye ni mwana ccm hai lakini kwa utawala wa huu mbovu ameamua kuachana na ccm, kahamia chadema!

Hivi watu kama hawa mnawasikiliza kwasababu zipi kama mtu hajasoma halama za nyakati toka mwaka 2005 akashindwa pia kusoma alama mwaka 2008 hadi 2010 sasa hivi anataka kusema nini eti mimi ni ccm lakini kwahili nahama embu muwena majibu marahisi kwa watu kama hao kwamba kama elimu ya awali au wanasema ya chekechea imekushinda basi ya chuo huwezi kujua kwamba ccm ilishindwa kuendesha nchi toka 2007 mbaka leo alafu unajua leo basi ukapimwe akili kikwete hana tofauti na maiti
 
Unajua nimegundua kuwa kumbe hata Obama mwenyewe hana utaratibu wa kuongea na wananchi wake kila mwezi. Nadhani JK naye ana kila sababu ya kutoendelea na huu utaratibu uliopitwa na wakati. Kinachoonekana kwa sasa ni kuwa ameamua kuwa mtendaji zaidi kuliko muongeaji, kitu ambacho kinastahili sifa sana. Si umeona bei za mafuta zilivyoshuka sasa.

Obama anaongea na watu wake kila wiki. Anayo weekly broadcast na huo ni mpangilio wa Marekani wa siku nyingi. Hiyo idea ni nzuri lakini nafikiri mtu wetu inamshinda kwa sababu amekuwa anadanganya kila mwezi na sasa conscience yake inamshitaki.
 
Wasilalamike wao ndio walioiweka hii serikali ambayo wanasema hawana imani nayo,
Kama hawana imani wanangoja nini?

Afadhali wakati wa mkoloni watu waliamua na kutuletea uhuru, sasa hivi pamoja na elimu, ukilinganisha na enzi za TAA na ASP, tumekaa tu na kulalamika.
yaan mimi binafsi nimechoka na hii serekali kwenye kampen zao wanatudanganya mpaka bungen watu wanaongea tuu ili mradi muda wa bunge uishe wanaongea mambo juu juu tufanyeje jaman tunaenda wap kama nilisikiaa wakisema kuhusu ajira wakasemma wanaoitimu vyuo vikuu watatumia vyeti vyao kupewa mipkopo ya kuanza kujiajir ili si changa la macho wakat hata wanachuo mikopo ya kusomea hali ni tete
 
Katika kile wananchi walichotegemea kwa kiongozi wetu mkuu wa nchi,hali imekua kinyume sasa kwani hali ya maisha imekua ngumu kila inapokucha afadhali ya jana........bei ya sukari sasa imefikia 3000/= katika baadhi ya mikoa kutokana na kusafirishwa kwenda nchi jirani za kenya na uganda na serikali ikinyamaza kimya bila kutoa tamko.umeme wa luku nao sasa wapatikana kwa taabu sana na maeneo machache sana,kumeonekana foleni ndefu za watu wakisubiri huduma hiyo wengi wao wakikata tamaa kama watafanikiwa kuipata.

Wananchi wengi wamejikatia tamaa na hawajui hatma yao ya kesho kwani pesa imeshuka thamani,na vitu mhimu kama nishati,vyakula kua bei juu sana huku serikali ikikaa kimya kutoa matamko katika baadhi ya sekta.
"wanateteana tena hadharani kwa kutoa ama kupeana rushwa za mabilioni,wakisema ni kawaida huu ni u*********," alilalamika kijana mmoja aliekua na jazba.

"mimi bwana ni ccm lakini kwa staili hii jamaa nchi imemshinda sijui",alisema mzee aliekua katika foleni hiyo ya kununua umeme.

Katika hali nyingine isiyokua ya kawaida baadhi ya wananchi wamehusisha utendaji wa kiongozi huyo na kifo cha mnajimu shehe yahya,kua utendaji wake ulitegemea sana msaada wa shehe huyo na tangu afariki mambo si mambo.

Huku mtaani watu hawana tena imani na serikali yao,wamepoteza matumaini na viongozi wao,wanasubiri waone hatma ya nchi yao hasa tunapoelekea kutimiza miaka 50 tangu tupate uhuru,na wengine wakisema ni bora wakoloni wangeendelea kukaa na kututawala............

Mkuu hapo umetaja machache sana,nimeingia hospital ya mkoa wa Dodoma juzi hali ni mbaya,wagonjwa wanalala wawili wawili kitandani,mashuka yale meupe yamebadilika rangi na haijulikani ni rangi gani ile,wagonjwa wanakaa bila kupewa huduma na wanachajiwa kwa kulala pale hii guest house au hospital.....umeme bado ni ndoto,tuliambiwa mambo yatakaa vizuri kuanzia mwezi huu,kumbe ilikuwa danganya toto tupitishe bajeti yao,

mafuta yanapatikana kwa manati na yakiwa bei juu,

unga wa sembe sasa ni 1000, kwa namna hii uwezi ukakaa ukamsikiliza huyu jamaa na hotuba zake zisizokuwa na kichwa wala miguu...

.........hata hotuba ya jana kwenye baraza la idd haileti matumaini kabisa, haoionyeshi kuwa raisi anajua kinachoendelea kwenye nchi yake na kwa wananchi wake.... haiwezekani hotuba ya raisi isigusie kwa undani masuala ya uchumi na hali mabaya za watanzania....ukiwauliza watakwambia "maisha bora ya mtanzania yanaletwa na mtanzania mwenyewe" sasa kama hakuna mazingira mazuri ya kutafuta hayo maisha inakuwaje?

Hakuna umeme, mafuta juu, hali ya maisha juu... watu wana vi-saloon vyao umeme unakatika, wakienda kwenye jenereta mafuta juu,unadhani hapo maisha bora yatatoka wapi...?

Tuache kudanganywa watanzania jamani, ni wakati wa kuamka na kusema hapana kwa mambo haya yanayoendelea serikalini.............
 
Back
Top Bottom