Elections 2010 2010; ni dr slaa na kikwete au wakristo na waislam?

kasyabone tall

JF-Expert Member
Sep 13, 2009
254
59
Tumekua tukiambiwa na kutadhaarishwa kila siku juu ya kuchanganya dini na siasa. Lakini mwaka huu 2010 ambao ni mwaka wa uchaguzi kwa nchi yetu inaonekana wazi maswala ya dini kutawala uchaguzi kiasi cha kutisha. Tunaweza kuona kuwa baadhi ya viongozi wa dini wamechoshwa na wasanii kuendelea kutawala kwa kutumia njia za kisani, huku wengine wakidhani wanapigwa vita wao. Hii imeleta patashika nguo kuchanika kwa wananchi hasa mpaka pale ujumbe wa simu unapotumika kueneza kuwa viongozi wa dini fulani wanataka muumini wao aendelee kutawala. Wengine wakija na hoja dhaifu kuwa kuna mgombea kawekwa na wakatoloki. Pia kuna ushaidi wa wazi kuwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kumekuwa na upendeleo wa wazi kwa baadhi ya watu wa dini fulani hasa katika uteuzi wa viongozi mbalimbali. Hapa mimi ninashindwa kupata jibu kama matokeo ya uchaguzi ya mwaka huu yataonjesha uwiano wa waumini wa dini hizi mbili au bado yataonyesha umoja na mshikamano wa taifa letu.

Hapa wengi wamekuwa waoga kusema ukweli juu ya mambo yanayoendelea kuhusu udini lakini wamekuwa wepesi wa kujidai kukemea udini ambao wao ndio wafadhili wakubwa wa udini katika taifa lisilo hata na misingi ya udini. Wamekua wakitumia dini kama mtaji kwa mazoea na pale dini ikiwa mwiba kwao wanakimbilia kukemea udini. Tukijiuliza mbona hawakusema lolote pale viongozi wa kidini hao hao waliposema Bosi ni chaguo Mungu.
Hapa lazima tukubali kuwa lazima wavune walichopanda, ukipanda uaribifu utavuna uaribifu. Ni vigumu kwa mwaka huu kudhibiti watu wasichague mtu kwa hisia za kidini wakati wametawaliwa na hisia za kidini. Kuna watu wa dini fulani wanaona wanatengwa ndani ya nchi yao na wengine wanahisi wanapendelewa.

Ni lazima tukubali pia kuwa misingi ya taifa letu imeyumba na kuyumbishwa na viongozi tunaowategea kulinda misingi hio.

Pia kuna suala la ufamilia ambao pia unaendelezwa kwa kasi bila kutathimini madhara yake kwa jamii ya watanzania, pale baba, mama na watoto wanapopiga kampeni ya kuingia ikulu. Hapa pia pana swali muhimu la kujiuliza kuwa sisi tunatawaliwa na familia na si mtu mmoja kama ilivyokuwa kwa Nyerere. Urais kufanywa kuwa jambo la kifamilia na watu kukaa kimya hii inatisha.

Kugusia tu kidogo, uchaguzi wa mwaka huu watanzania wanatarajia mabadiliko, kwani kila dalili zinaonesha kuwa kunamabadiliko yatatokea. Ukiangalia kama ilivyo kuwa kwa kikwete 2005 dalili zilionesha atashinda KWA KISHINDO NDIVYO ILIVYOTOKEA. Mwaka huu ushahidi upo kama kura za maoni zioneshavyo Dr. Slaa lazima ashinde. Sasa kama kuna watu watatarajia kubadilisha matokeo si ajabu tukashuhudia kenya ya Tanzania.
Natamini kufika Octoba 31, 2010. Nione tanzania mpya inayotarajiwa na watu wengi.
 
Utawala mbovu huzaa makundi, ubaguzi na kila aina ya takataka. Ndiyo yanayoisibu nchi yetu pendwa. Tumwombe Mungu tuvuke salama uchaguzi huu, na kupata viongozi bora watakaokuwa tayari kutusaidia kuziba nyufa zinazotaka kuzorotesha utaifa na umoja wetu.
 
Natamini kufika Octoba 31, 2010. Nione tanzania mpya inayotarajiwa na watu wengi.

Nami pia wasiwasi wangu ni hiyo Tanzania mpya ambayo wanasiasa wetu wa sasa waiwemo wafuasi, washabiki na hata wana mikakati wako tayari kuturithisha ili mradi mradi wao utimie....Ni kweli siasa za udini zimekuwepo muda mrefu chini kwa chini na zilikuwa ni dhambi dhidi ya utaifa wetu lakini sasa mambo wazi na huku zikifanywa kuwa ni kitu cha kawaida. Kama uonavyo UFISADI unapokuwa swala la kawaida ndivyo hali ya kutumia siasa na hisia za udini ndivyo ilivyo hivi sasa. Unachokiona hapa JF ni trela ila huko majimboni hasa mikoani mambo ni mabaya zaidi. Cha ajabu ni kuwa wote wanaoendekeza siasa hizi ama kwa kuzifanya, ama kuzinyamazia ama hata kizitetea wanasahau kuwa mwisho wa siku watakaofaidika na Tanzania iliyogawanyika ni MAFISADI. Kama sio mafisadi wazoefu basi DOWNLOW mafisadi ambao wanajiandaa kwa THEIR TURN TO EAT....
 
Mods msiziache thread za aina hii zinazochochea udini.


Mficha gonjwa kifo humuumbua: Ni heri mambo haya yakajadiliwa kwa uwazi kuliko kuyaficha wakati yapo, nikuulize Mzee Punch; Hivi udini hauko Tanzania? Cha msingi hapa sisi kama Great thinkers tuweke mambo hadharani na tujadiliane bila kurushiana ngumi wala maneno makali.
 
Udini na ukabila katika vyama vya upinzani haupo ila ni propaganda ianayotumiwa na CCM kuwatisha watanzania. Kutokana na uchanga wa vyama hivi huwa vinaanza vikiwa na wanachama wachache na mara nyingi huwa ni wa eneo fulani halafu vinasambaa. Udini au ukabila ndani ya CHADEMA na hata CUF ni propaganda ya CCM. Tungeweza kuamini kuwa vyama vina udini au ukabila kwa mfano kama CUF ingemchukua muislam Pemba wakampeleka kugombea Rombo au CHADEMA ikamchukua Mchaga kwenda kugombea kisarawe.

Kasyabone chagua rais anayefaa, Usichaguliwe na propaganda
 
KWA MARA YA KWANZA NAANZA KUCHANGIA KAMA "GREAT THINKER"
Great thinkers generally discuss issues.Ili tuweze kujadili issues ni lazima tuwe na premise.
My premise is watanzania wana dini lakini kwa ujumla wao si wadini.
Tofauti ya dini na udini.
1.Dini ni utaratibu wa mlengo wa ufahamu na imani iliyojengwa katika misingi inayopelekea kuamini,kufuata na kutanabaisha mapokeo na matarajio ya hatima ya ufahamu wetu wa sisi (Kama viumbe) ni nani,tunafanya nini (Dhumuni la kuwepo kwetu) hapa duniani na hatima yetu baada ya kufa.
2.Udini unamaananisha hali au mtazamo wa kuunganisha ufahamu wetu na imani yetu kama kigezo na kishawishi cha kutunasabahisha (associate) na maamuzi yetu,maingiliano yetu na mahusiano yetu katika kufanya maamuzi.yawe ya kisiasa,kijamii,kiuchumi au kihuria.
Hivyo basi premise kwamba watanzania KWA UJUMLA WAO ni wadini is false.
Tuna individuals,ambao kwa kushindwa kwao kujenga hoja zenye nguvu katika medani za siasa,uchumi au kijamii wamekimbilia katika kivuli cha udini ili kujijengea umaarufu na/au kukubalika ,kutwaa madaraka au kuendeleza mfumo (Status quo).
Kwa maoni yangu,Katika tunu ambazo Mwenyezi Mungu amezijaalia Taifa hili ni tunu ya mashirikiano,mshikamano na maingiliano kati ya watu wa dini mbalimbali.Tusijaribu kuichezea tunu hii.Ni adimu na ya thmani sana sana.Kwamba Mama yangu mzazi alizaliwa na baba mwislamu(Mjenga msikiti) na ambaye alikuwa tayari kumwoza binti yake kwa mkristo tena mtoka mbali!Kwamba mimi binafsi nimeoa mwislamu na nina mahusiano mazuri mno na wakwe zangu na ndugu za mke wangu!Kwamba my best,life long friends ni waislamu! HII NI TUNU NA SHANI BORA KABISA.
Tafadhali,tusije kuchanganya mitizamo yetu ya kisiasi na imani zetu.
Tuwapime watu kwa uwezo wao na vision zao za nini wataweza kuwafanyia watanzania.Si kwa dini zao au majina yao.
Kama alivyowahi kusema GEN.Collin Powell.The issue is not whether Obama is a Muslim,THE ISSUE IS WHAT IF HE IS?
DOES THAT DISQUALIFY HIM AS A CANDIDATE BY THE US CONSTITUTION?The answer is no!
 
KWA MARA YA KWANZA NAANZA KUCHANGIA KAMA "GREAT THINKER"
Great thinkers generally discuss issues.Ili tuweze kujadili issues ni lazima tuwe na premise.
My premise is watanzania wana dini lakini kwa ujumla wao si wadini.
Tofauti ya dini na udini.
1.Dini ni utaratibu wa mlengo wa ufahamu na imani iliyojengwa katika misingi inayopelekea kuamini,kufuata na kutanabaisha mapokeo na matarajio ya hatima ya ufahamu wetu wa sisi (Kama viumbe) ni nani,tunafanya nini (Dhumuni la kuwepo kwetu) hapa duniani na hatima yetu baada ya kufa.
2.Udini unamaananisha hali au mtazamo wa kuunganisha ufahamu wetu na imani yetu kama kigezo na kishawishi cha kutunasabahisha (associate) na maamuzi yetu,maingiliano yetu na mahusiano yetu katika kufanya maamuzi.yawe ya kisiasa,kijamii,kiuchumi au kihuria.
Hivyo basi premise kwamba watanzania KWA UJUMLA WAO ni wadini is false.
Tuna individuals,ambao kwa kushindwa kwao kujenga hoja zenye nguvu katika medani za siasa,uchumi au kijamii wamekimbilia katika kivuli cha udini ili kujijengea umaarufu na/au kukubalika ,kutwaa madaraka au kuendeleza mfumo (Status quo).
Kwa maoni yangu,Katika tunu ambazo Mwenyezi Mungu amezijaalia Taifa hili ni tunu ya mashirikiano,mshikamano na maingiliano kati ya watu wa dini mbalimbali.Tusijaribu kuichezea tunu hii.Ni adimu na ya thmani sana sana.Kwamba Mama yangu mzazi alizaliwa na baba mwislamu(Mjenga msikiti) na ambaye alikuwa tayari kumwoza binti yake kwa mkristo tena mtoka mbali!Kwamba mimi binafsi nimeoa mwislamu na nina mahusiano mazuri mno na wakwe zangu na ndugu za mke wangu!Kwamba my best,life long friends ni waislamu! HII NI TUNU NA SHANI BORA KABISA.
Tafadhali,tusije kuchanganya mitizamo yetu ya kisiasi na imani zetu.
Tuwapime watu kwa uwezo wao na vision zao za nini wataweza kuwafanyia watanzania.Si kwa dini zao au majina yao.
Kama alivyowahi kusema GEN.Collin Powell.The issue is not whether Obama is a Muslim,THE ISSUE IS WHAT IF HE IS?
DOES THAT DISQUALIFY HIM AS A CANDIDATE BY THE US CONSTITUTION?The answer is no!


Nimekupa V for victory kwa vile umekuja kifalsafa zaidi ila nasikitika umekwepa swali. Ulipashwa kudraw conclusion! Baada ya ufafanuzi wako mrefu, je unaamini Tanzania ina elements za kidini katika maisha ya watu au katika uongozi...this was the primary question!
 
Back
Top Bottom