Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Mwezi February mwaka 2008 nikiwa Jijini Mwanza nilipata habari za kushtusha na kushangaza kuhusu JF. Wakati nikiwa Arusha nilijaribu ku-access JF lakini bila mafanikio na nikadhani kuwa huenda ni matatizo ya mandao.
Jioni moja nikiwa Jijini Mwanza nikiwa nasikiliza BBC Dira ya Dunia nikapata habari kuwa Jeshi la Polisi linawashikilia Wamiliki wa mtandao wa Kompyuta wa JF! BBC kupitia Abdalla Majura walimhoji Kamanda wa Polisi Dar na akathibitisha hilo na pia alimhoji Mwanakijiji kama mdau wa JF. Naamini kabisa Polisi walitumika kama silaha ya ukandamizaji wa maoni huru na ilikuwa ni njia ya kuwatinsha ndugu zetu ambao wameifanya JF kuwa mahali pekee pa WaTZ kutoa maoni yao kwa uhuru mkubwa.
JF imekuwa ni kisima cha habari na ni Jukwaa hili ndilo liliotumika mwanzo kabisa kuanika uozo wa Kifisadi wa EPA pamoja na vitisho kutoka kwa Wakili wa Jeetu huko Uingereza. Naamini kuwa Jeshi la Polisi lilitumika Kifisadi na Mafisadi ili kuwalinda Mafisadi dhidi ya Ushahidi uliokuwa ukianikwa dhidi yao kupitia Mtandao wa JF.
Inasemekana kuwa Polisi waliwashikilia ndugu zetu hao (Wa JF) na kuwahoji kwa muda mrefu; kwa tabia ya Polisi wetu sidhani kama Wamiliki na Waendeshaji wa JF waliojikuta mikononi mwa Polisi waliepuka mateso ya kimwili ukiondoa ya kiakili maana Polisi wetu ni mahiri katika kutoa adhabu za vipigo kwa Watuhumiwa.
Kwa bahati mbaya sana Ndugu zetu hao waliopitia madhira hayo ya Polisi hawajawahi kutueleza wanachama wao juu ya madhira waliyopata wakiwa mikononi mwa Polisi na nawaomba watuleleze kinagaubaga juu ya kilichojiri walipokuwa mikononi mwa Polisi. Walihojiwa nini, na tuhuma zilikuwa nini na je, kulikuwa na mateso yoyote?
Kwa bahati mabaya mbinu waliyotumia Mafisadi ya kuwakamata ndugu zetu ilizidisha mara dufu umaarufu wa JF na kila Mtanzania aliyesikia habari ile alitaka kujua JF ni kitu gani na si ajabu kuona idadi ya Wananchama inazidi kuongezeka kila siku na namwomba Mod awe anatupa updates kila mwezi juu ya idadi ya wanachama.
Mwisho. Pamoja na jitihada zilizofanywa na Mafisadi kupitia Jeshi la Polisi kuwanyamazisha ndugu zetu bado JF inaendelea kukua kila kukicha na natoa wito kwa wnachama wote kuendelea ku-share na Watanzania wengine juu ya Jukwaa hili la JF. Pia napenda kuwaomba wanachama wote wa JF kuiunga mkono JF kwa hali na mali-tutoe michango ya fedha kwani akaunti zote zimeshawekwa kwenye Mtandao, KUMBUKENI JF ndiyo silaha yetu Watanzania tuliopata bahati ya kuangaziwa na nuru ya elimu.
Wakatabahu,
Ibrah
Jioni moja nikiwa Jijini Mwanza nikiwa nasikiliza BBC Dira ya Dunia nikapata habari kuwa Jeshi la Polisi linawashikilia Wamiliki wa mtandao wa Kompyuta wa JF! BBC kupitia Abdalla Majura walimhoji Kamanda wa Polisi Dar na akathibitisha hilo na pia alimhoji Mwanakijiji kama mdau wa JF. Naamini kabisa Polisi walitumika kama silaha ya ukandamizaji wa maoni huru na ilikuwa ni njia ya kuwatinsha ndugu zetu ambao wameifanya JF kuwa mahali pekee pa WaTZ kutoa maoni yao kwa uhuru mkubwa.
JF imekuwa ni kisima cha habari na ni Jukwaa hili ndilo liliotumika mwanzo kabisa kuanika uozo wa Kifisadi wa EPA pamoja na vitisho kutoka kwa Wakili wa Jeetu huko Uingereza. Naamini kuwa Jeshi la Polisi lilitumika Kifisadi na Mafisadi ili kuwalinda Mafisadi dhidi ya Ushahidi uliokuwa ukianikwa dhidi yao kupitia Mtandao wa JF.
Inasemekana kuwa Polisi waliwashikilia ndugu zetu hao (Wa JF) na kuwahoji kwa muda mrefu; kwa tabia ya Polisi wetu sidhani kama Wamiliki na Waendeshaji wa JF waliojikuta mikononi mwa Polisi waliepuka mateso ya kimwili ukiondoa ya kiakili maana Polisi wetu ni mahiri katika kutoa adhabu za vipigo kwa Watuhumiwa.
Kwa bahati mbaya sana Ndugu zetu hao waliopitia madhira hayo ya Polisi hawajawahi kutueleza wanachama wao juu ya madhira waliyopata wakiwa mikononi mwa Polisi na nawaomba watuleleze kinagaubaga juu ya kilichojiri walipokuwa mikononi mwa Polisi. Walihojiwa nini, na tuhuma zilikuwa nini na je, kulikuwa na mateso yoyote?
Kwa bahati mabaya mbinu waliyotumia Mafisadi ya kuwakamata ndugu zetu ilizidisha mara dufu umaarufu wa JF na kila Mtanzania aliyesikia habari ile alitaka kujua JF ni kitu gani na si ajabu kuona idadi ya Wananchama inazidi kuongezeka kila siku na namwomba Mod awe anatupa updates kila mwezi juu ya idadi ya wanachama.
Mwisho. Pamoja na jitihada zilizofanywa na Mafisadi kupitia Jeshi la Polisi kuwanyamazisha ndugu zetu bado JF inaendelea kukua kila kukicha na natoa wito kwa wnachama wote kuendelea ku-share na Watanzania wengine juu ya Jukwaa hili la JF. Pia napenda kuwaomba wanachama wote wa JF kuiunga mkono JF kwa hali na mali-tutoe michango ya fedha kwani akaunti zote zimeshawekwa kwenye Mtandao, KUMBUKENI JF ndiyo silaha yetu Watanzania tuliopata bahati ya kuangaziwa na nuru ya elimu.
Wakatabahu,
Ibrah