Kiby
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 6,897
- 4,621
Mimi binafsi sijawahi kumkuta shetani akifanya ubaya mfano, kuzini na mke wa mtu, kuiba, kuchonga sanamu ya kuabudiwa nk. Haya yote yanafanywa na watu tena kutoka katika dini zinazonadiwa sana. Sasa swali linakuja, je kuna dini inayoweza kumwokoa mtu kutoka katika kifungo chake cha tabia ya asili? Na pia tukijaribu kurudi nyuma kuangalia watu waliotukuka katika vizazi vya binadamu yaani manabii, mfano Wa Nuhu, Abraham, Musa, Isaya, yeremea,Ezekie,Eliya, Daniel,*Yohana, Paul, kina Petro nk walikuwa ni wa dini ipi. Naamini kama utaweza kutafakari kwa kina kuhusu mambo haya utakuwa umepata jibu la maswali mengi yanayokusumbua katika maisha.