Waungwana natumaini wote mko shwari,
Nina simu yangu Blackberry tourch 9800, nilikuwa somewhere kwenye vaccation na kwa bahati mbaya picha zote nilizochukuwa kama memory nilipiga kwa kutumia simu yangu.
sasa basi juzi wakati nataka kutoa sim lock ili nipige password ikawa inakataa kuverify nilijaribu mara nyingi baadaye ikaja option kama ya kujirestart ndipo simu ikajirestart na ikaja na sura nyingine na karibu settings zangu zote zikawa zimebadilika ikiwemo ringer tone.
sasa kinachoniacha mimi hoi picha zilizofutika ni zile tu ambazo nilizipiga nikiwa safarini, lakini zile picha za zamani zote zimebaki.
kwahiyo hapa naomba mautundu kama kuna namna yoyote naweza kupata msaada kama kuna backup ya photo inawezekana? maana mimi sikuzidelete bali ni lisimu lenyewe limeamuwa kunionesha The world wonders.

Reply With Quote



Follow Us Here