Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 30
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,189
      Rep Power : 19210
      Likes Received
      8141
      Likes Given
      26620

      Default Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars


      NI HATUA NZURI YA UWEZEKANO WA BINADAMU KWENDA KUISHI, DALILI ZAONYESHA KUNA VIUMBE HAI
      Leon Bahati
      WANASAYANSI wa anga kwa muda mrefu wamekuwa wakitafuta uwezekano wa maisha katika sayari nyingine, mbali na dunia.Kuna imani kuwa kwenye sayari hizo, huenda zikapatikana raslimali nyingi kwa urahisi kuliko duniani ambako binadamu wameishi mamilioni ya miaka hadi sasa.

      Wataalamu hao wa anga wamekuwa wakifanya hivyo kwa muda sasa na moja ya mambo muhimu wanayoangalia ni upatikanaji wa maji. Popote maji yanapopatikana, wanaamini maisha yanawezekana.Moja ya sayari ambayo wamekuwa wakiichunguza kwa miaka mingi sasa ni Mars, ambayo ni ya nne kutoka kwenye jua. Dunia ni ya tatu.

      Sababu kuu za kuichagua sayari hii tofauti na zingine ni kwamba, hali ya hewa inatofautiana kidogo sana na ya dunia.

      Sayari nyingine kama Mercury na Venus, zipo karibu zaidi na jua na hali ya joto iko juu kiasi kwamba hali ya maisha inaweza kuwa taabu.

      Mars ambayo wanasayansi wanaipa jina la sayari nyekundu, ipo karibu na dunia, hivyo ni rahisi kufika iwapo wanasayansi watathibitisha iwapo maisha yanawezekana huko.

      Wanaiita sayari nyekundu kwa sababu eneo kubwa la uso wake ni wa rangi nyekundu, tofauti na nyingine zilizomo kwenye mfumo wetu wa sayari.

      Hakuna mwanasayansi ambaye amethubutu kusafiri hadi kwenye sayari hiyo kutokana na ugumu wa kupata vyombo vya kuaminika, vinavyoweza kusafirisha watu kutoka duniani hadi Mars na kurudi salama.

      Hata hivyo, hilo siyo tatizo kwa sababu wakibaini mazingira mazuri, utengenezaji wa vyombo hivyo hauwezi kuwapa taabu.

      Kazi ya uchunguzi imekuwa ikifanywa kwa vyombo maalumu ambavyo havina watu lakini, vina uwezo wa kuleta mawasiliano duniani.

      Pia wanatumia viona mbali katika mchakato huo kuchunguza hali ilivyo kwenye sayari hii, ambayo kumekuwapo na hisia kwamba huenda waliwahi kuishi viumbe hai mamilioni ya miaka iliyopita lakini baadae mazingira yakabadilika na kuwa mabaya.

      Uchunguzi unaonyesha kuwa, sayari hii ina mabonde mengi ambayo yanakila dalili kuwa awali yalikuwa yanatiririsha maji kama ilivyo mito hapa duniani.

      Kwa muda mrefu, wanasayansi wamekuwa wakiichukulia sayari hiyo kuwa na mazingira ya jangwa yanayotokana na ukame wa muda mrefu.

      Wagundua maji
      Mwezi uliopita wanasayansi hao wamekuja na maelezo kwamba sayari hiyo ina kiwango kikubwa cha maji na mengi yapo mita chache kutoka uso wake.

      Mmoja wa wanasayansi wanaochunguza sayari hiyo ni Profesa Jay Melosh wa Chuo Kikuu cha Purdue, nchini Marekani.

      Yeye anasema uchunguzi huo umewapa imani kwamba siyo tu kwamba Mars ina maji bali kuna viumbe wadogo, mfano wa jamii ya bacteria ambao wanaendelea kuishi humo hadi leo hii.

      Ni uchunguzi ambao wanaamini una matumaini tofauti na taarifa za uchunguzi uilizopita na kizuri zaidi pia ni kubaini moja ya miezi yake miwili, maji yapo kwa wingi zaidi.

      Miezi inayoizunguka sayari ya Mars ni Demos na Phobos. Phobos ndio mwezi uliogundulika kuwa na kiwango kikubwa cha maji na ndio ulio karibu zaidi na sayari hiyo.

      Kwa sababu hiyo, wanaamini kwamba maisha yakianza kwenye sayari ya Mars, kuna uwezekano pia wengine wakahamia kwenye mwezi huo wa Phobos.

      Taarifa za uwepo wa maji kwenye sayari hii zilitolewa kwenye mkutano wa wanasayansi wanaochunguza anga za mbali, uliofanyika Austria Juni mwaka huu.

      Moja ya dalili za uwepo wa maji ni vimondo ambavyo vimekuwa vikianguka kwa wingi kwenye uso wa sayari hiyo.
      Mtaalamu wa Uhandisi na Mambo ya Anga, Profesa Kathleen Howell anasema picha walizopiga maeneo ambaye vimondo vimegonga uso wa Mars, zilionyesha dalili kama za mtu aliyetupa jiwe kwenye eneo lenye tope.

      “Sehemu kimondo kilipoigonga sayari ya Mars, aina ya kitu kama tope kiliruka na kusambaa pembeni,” anasema Profesa Howell.

      Hali hiyo wakaitafsiri kuwa maji yaliyokaribu na uso wa sayari hiyo yaliruka pamoja na udongo wakati, kimondo kilipozama ndani na kusambaa pembeni.

      Hali hii iko je?
      Utafiti huo unaashiria kwamba, sayari hiyo ina bahari kubwa iliyoenea chini kwa chini kwenye miamba mita chache kuingia ndani.

      Milipuko ya volkano ya miaka mingi iliyopita ni kiashirio kingene kwamba, sayari hii ina maji. Uchunguzi unaonyesha kwamba mlipuko huo uliandamana na maji.

      Ripoti ya utafiti huo ambao umechapishwa pia na jarida la Geology, inaonyesha kuwa kiwango cha maji kilichopo Mars kinakadiriwa kuwa sawa au kimezidi kile kilichopo hapa Duniani.

      “Kimsingi, kiwango cha maji tunayoyazungumzia kinalingana ama ni zaidi ya kile kilichopo kwenye uso wa dunia,” Anasema Kiongozi wa Jopo la Wanasayansi hao, Profesa Francis McCubbin, ambaye pia ni Mtaalamu wa Anga Chuo Kikuu cha Mexico.

      “Si jambo la kushangaza kwamba, kwenye sayari hii waliwahi kuishi viumbe hai miaka iliyopita,” anasema Profesa Howell na kuongeza:

      “Tatizo tutakalokabiliana nalo ni iwapo tayari muda umepita sana kiasi cha kutotambua vyema hali hiyo.

      “Lakini, hata kama hautapatikana uthibitisho wa kisayansi wa viumbe kuwahi kuishi miaka iliyopita, jambo muhimu ni uwezekano wa kiumbe kuweza kuishi kwa sasa.”

      Hatari kwenye Mars
      Hatari iliyopo ni kwamba, ni moja ya sayari ambayo imekuwa ikigongwa mara kwa mara na vimondo vinavyoanguka.

      Ni vimondo vichache sana ambavyo viliwahi kutua kwenye uso wa dunia. Vinapoanguka kuelekea uso wa dunia hukabiliwa na safari ndefu na kutokana na mwendo mkali wa mwanguko, hujikuta vinapata msuguano mkali na hewa, ambao husababisha joto kali linaloimomonyoa udongo hadi inakwisha.
      Sayari hii ambayo ipo karibu na ukanda wa vimondo, uso wake una makovu mengi yanayoashiria athari za vimondo vyenye ukubwa tofauti vilivyotua.

      Vimondo hivi ndivyo vimeweka wazi dalili za kuwapo kwa maji kwenye sayari hii ambayo uso wake unaonekana kama vile jangwa, kwa kutokuwa na miti na ishara ya ukame wa muda mrefu.

      MWISHO
      Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars
      Mbimbinho and Boflo like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. Miaka 50

    3. #2
      Jakubumba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2011
      Location : United states
      Posts : 1,153
      Rep Power : 714
      Likes Received
      301
      Likes Given
      123

      Default

      Ila sasa nauli si itakuwa kubwa sana? Imagine watakaoishi huko hawafi, aisee utakuwa mtafutano kwenda huko
      MziziMkavu likes this.

    4. #3
      RGforever's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2011
      Posts : 2,089
      Rep Power : 1131
      Likes Received
      413
      Likes Given
      105

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Kwahiyo mwisho wa Dunia ukifika inabidi Mungu awe na Kazi mbili. Ya MARS na EARTH....ahahahaha

    5. #4
      RGforever's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2011
      Posts : 2,089
      Rep Power : 1131
      Likes Received
      413
      Likes Given
      105

      Default

      Quote By Jakubumba
      Ila sasa nauli si itakuwa kubwa sana? Imagine watakaoishi huko hawafi, aisee utakuwa mtafutano kwenda huko
      SERIKALI ITAGHARAMIA.. Hasa hasa ya Marekani.. Huku kwetu lazima tufe tu
      MziziMkavu likes this.

    6. #5
      NingaR's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2012
      Location : C:\Windows\SysWOW64
      Posts : 2,491
      Rep Power : 856
      Likes Received
      384
      Likes Given
      76

      Default

      Quote By RGforever
      Kwahiyo mwisho wa Dunia ukifika inabidi Mungu awe na Kazi mbili. Ya MARS na EARTH....ahahahaha
      Umeona eeeeee
      MziziMkavu likes this.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      NingaR's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2012
      Location : C:\Windows\SysWOW64
      Posts : 2,491
      Rep Power : 856
      Likes Received
      384
      Likes Given
      76

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Mimi wacheni nifie hapahapa bongo
      MziziMkavu likes this.

    9. #7
      Nzowa Godat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th June 2011
      Posts : 1,383
      Rep Power : 678
      Likes Received
      229
      Likes Given
      12

      Default

      Quote By Jakubumba
      Ila sasa nauli si itakuwa kubwa sana? Imagine watakaoishi huko hawafi, aisee utakuwa mtafutano kwenda huko
      Binadamu yeyote
      atakayemwamini Yesu Kristo,
      ataishi milele MBINGUNI
      Anakoishi Yehova Mungu na
      Bwana wetu Yesu Kristo.
      Hakika ni kama hivo.
      Kaa la Moto and sijui nini like this.

    10. #8
      Angel Msoffe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2011
      Posts : 6,266
      Rep Power : 1826
      Likes Received
      1397
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Mk.were atakua wa 1 kukimbilia huko after 2015 election
      MziziMkavu likes this.

    11. #9
      mariti's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 7th July 2012
      Posts : 3
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default

      Hii ni habari njema inayoonyesha uwezo wa binadamu kuendelea kutathmini mazingira yanayoizunguka dunia. Lakini haaanishi kwamba viumbe waliopo huko (kama wapo) watafanana kimaumbile na walio dunia hii. Wanweza kuwa wajanja au wajinga zaidi yetu. Kumbuka UFOs ambao ni hadithi ya kufikirika na ndio maana kuna sehemu iitwayo Area 51 katika nchi fulani lakini Haipo katika ramani ya nchi hiyo wala kutambulika kimataifa. Si unajua tena mambo ya "classified" information. Tahadhari iliyopo ni kuleta duniani chembechembe hai kutoka huko kwani twaweza angamia sote. Ufahamu huo ni mzuri lakini tusiende huko. Tuchunguze dunia yetu zaidi kwani kuna mengi hatufahamu hasa misituni na baharini. Mfano mzuri ni "bermuda triangle" na mengi mengi yatusukumayo tufanye utafiti hapa duniani.
      MziziMkavu likes this.

    12. #10
      Boflo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2010
      Posts : 3,761
      Rep Power : 5459
      Likes Received
      3669
      Likes Given
      3718

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Makala imetulia sana..... MziziMkavu Mara nyingine uwe unatupa habari za sayari kama hizi
      MziziMkavu likes this.
      There are some people who could hear you speak a thousand words and still not understand you. And there are others who will understand—without you even speaking a word.

    13. #11
      Kwetu Iringa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th July 2011
      Posts : 339
      Rep Power : 466
      Likes Received
      54
      Likes Given
      595

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Wana uhakika gani kuwa kule kuna maisha kwa binadamu??

      Inawezekana viumbe vya kule hutumia hydrogen badala ya oxygen tutumiayo siye hapa duniani kwetu!!!!
      MziziMkavu likes this.

    14. #12
      simplemind's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2009
      Posts : 2,848
      Rep Power : 1155
      Likes Received
      509
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Hati miliki ya ardhi mars zimeanza kutolewa?
      MziziMkavu likes this.

    15. #13
      bigboi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th September 2010
      Posts : 134
      Rep Power : 465
      Likes Received
      31
      Likes Given
      7

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Du ngoja nifanye mchakato wa kwenda kule bongo longo longo kibao nikaanzishe tanzania ya mars haitakuwa na mafisadi ccm hairusiwi kwenda kule hatutaki shobo kule ni goood people only
      MziziMkavu likes this.

    16. #14
      BIG Banned's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2012
      Location : Banned
      Posts : 263
      Rep Power : 407
      Likes Received
      63
      Likes Given
      77

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Hawajaanza kuuza viwanja huko!!.
      MziziMkavu and sijui nini like this.
      Vua GAMBA Vaa GWANDA

    17. #15
      Zuia Sayayi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th March 2011
      Posts : 666
      Rep Power : 546
      Likes Received
      68
      Likes Given
      47

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Naskia kuna tume ya katiba inayoundwa kushugulikia mambo ya kule,
      MziziMkavu likes this.

    18. #16
      sijui nini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2010
      Location : home
      Posts : 1,748
      Rep Power : 7637
      Likes Received
      497
      Likes Given
      447

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Quote By BIG Banned
      Hawajaanza kuuza viwanja huko!!.
      pale posta karibu na feri mbona kuna madalali wwengi tu wa viwanja vya mars...?? kama unataka nenda pale kaulizie..
      MziziMkavu likes this.
      The signature you are looking at now does not exist.....

    19. #17
      BIG Banned's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2012
      Location : Banned
      Posts : 263
      Rep Power : 407
      Likes Received
      63
      Likes Given
      77

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Quote By sijui nini
      pale posta karibu na feri mbona kuna madalali wwengi tu wa viwanja vya mars...?? kama unataka nenda pale kaulizie..
      madalali hawaaminiki, wanaweza kuniuzia viwanja vilivyopo kwenye venus.
      MziziMkavu likes this.
      Vua GAMBA Vaa GWANDA

    20. #18
      elmagnifico's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th July 2011
      Location : Brussels
      Posts : 1,932
      Rep Power : 2543
      Likes Received
      539
      Likes Given
      36

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      hongera zao, dunia yenye maji tele ambayo huhitaji kuhangaika sana kuayapata imetushinda kuitunza sasa hiyo yenye maji yanayo sadikika yako chini na inawezekana si kweli na haina hali ya hewa ambayo sisi binadamu tutaweza ishi kwa raha mstarehe kama duniani ndo wanahangaika nayo. Bora wangewekeza kuboresha maeneo ya dunia yanayo geuka kuwa jangwa kwasababu ya uharibifu wa mazigiara.
      Lakini hongera zao.
      BabaDesi and MziziMkavu like this.

    21. #19
      Mbimbinho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st August 2009
      Posts : 1,834
      Rep Power : 865
      Likes Received
      470
      Likes Given
      210

      Default Re: Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars

      Itabidi Waafrica na sisi tuwahi ili ulaya ya Mars iwe yetu na wazungu wachukue Africa ya kule.
      MziziMkavu likes this.
      Mbwa ukimjua jina wala hakupi shida....

    22. #20
      Amoeba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2009
      Posts : 3,332
      Rep Power : 1176
      Likes Received
      435
      Likes Given
      725

      Default

      Quote By RGforever
      Kwahiyo mwisho wa Dunia ukifika inabidi Mungu awe na Kazi mbili. Ya MARS na EARTH....ahahahaha
      Mungu Hana mamlaka na sayari nyngne kwa Sabab hakuiumba

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...