Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 29
    1. #1
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4443
      Likes Given
      7465

      Default Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Monday, 27 December 2010
      Anthony Kayanda, Kigoma

      Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi), George Mkuchika, amepewa siku saba kuhakikisha anaitisha uchaguzi wa kumchagua Meya wa Halmashauri ya Manispaa Kigoma-Ujiji aliouahirisha, licha ya Mahakama kuamua ufanyike siku uliopangwa rasmi.


      Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe alipokuwa akihutubia Wananchi wa Kigoma mjini kuelezea mambo mbalimbali yanayohusiana na mustakabali wa kisiasa, ambapo alimshutumu Waziri huyo kwa kutumia Mamlaka yake vibaya.

      ‘Chadema tuna idadi kubwa ya madiwani zaidi ya CCM, hivyo juhudi zozote zinazofanywa na Waziri kusaidia Chama chake hazitasaidia kitu, badala yake zitaongeza hasira na chuki kwa Wakazi wa Kigoma mjini na kujikuta wakiichukia zaidi CCM na viongozi wake kwa vile anachangia kukwamisha maendeleo ya mji wetu’ alieleza Zitto.

      ‘Kutokana na hali hiyo, nampa Waziri wa Tamisemi siku saba ahakikishe anaitisha uchaguzi wa kumchagua Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ili tumpate Mwenyekiti wa baraza la madiwani na kamati zake za kudumu waanze kutuhudumia na kusimamia miradi ya maendeleo, kwa sababu kadri Waziri anavyochelewesha uchaguzi ndivyo Watendaji wanavyoweza kutumia vibaya nafasi hiyo kuharibu Halmashauri yetu” aliongeza.

      Alisema baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu, Chadema walishinda nafasi za madiwani katika Kata 10 dhidi ya tisa walizopata CCM, jambo lililofanya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoa nafasi nne za madiwani wa Viti Maalumu wakati CCM walipewa nafasi tatu za Madiwani wa Viti maalumu.

      Zitto alisema chanzo cha mgogoro huo ni idadi hiyo ya madiwani wa Viti maalumu ambapo alidai kuwa CCM walikwenda Mahakama ya Wilaya Kigoma kulalamikia mgawo huo, lakini Mahakama ilitupilia mbali shauri hilo.

      ‘Waziri Mkuchika anapaswa kujua kwamba siku ile alipoandika barua ya kusimamisha uchaguzi wa Meya (Desemba 17, 2010), Mahakama ya Wilaya Kigoma ilikuwa imetoa maamuzi ya shauri la CCM waliotaka Mahakama isimamishe uchaguzi, lakini Hakimu alilitupilia mbali shauri hilo kwa maelezo kwamba Tume ya Uchaguzi ipo sahihi katika mgawanyo wa madiwani wa viti maalumu” alifafanua Zitto.

      ‘Na hata kama Mahakama ingesema okay, CCM waongeongezewa diwani mmoja ili tulingane nao bado wasingekuwa na uwezo wa kushinda halmashauri, labda ile ndoa ya Mseto tuliyofunga nao mwaka 2005 inaonekana wameridhika nayo ndiyo maana wanataka turudiane nao, sisi tunasema kwa hilo hatupo tayari na kamwe mwaka huu hatuipotezi Manispaa ya Kigoma Ujiji’ alisisitiza.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4443
      Likes Given
      7465

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Waziri Mkuchika anapaswa kujua kwamba siku ile alipoandika barua ya kusimamisha uchaguzi wa Meya (Desemba 17, 2010), Mahakama ya Wilaya Kigoma ilikuwa imetoa maamuzi ya shauri la CCM waliotaka Mahakama isimamishe uchaguzi, lakini Hakimu alilitupilia mbali shauri hilo kwa maelezo kwamba Tume ya Uchaguzi ipo sahihi katika mgawanyo wa madiwani wa viti maalumu” alifafanua Zito.
      Hivi Mkuchika anaishi dunia ipi ambayo inapingana na nguvu ya raia waliomweka yeye hapo alipo?
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    4. #3
      Mbopo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2008
      Posts : 2,534
      Rep Power : 1084
      Likes Received
      375
      Likes Given
      13

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      These manouvres are a recipe for unnecessary chaos. We should be more sensible and let the will of the people prevail lest we plunge this contrary into chaos or violence.

    5. #4
      Uwezo Tunao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2010
      Posts : 6,916
      Rep Power : 2298
      Likes Received
      1155
      Likes Given
      1500

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Zitto, hapo imekaa sawa maana ni suala la kudaihaki ya wananchi / Umma wa Tanzania kupata uwakilishi wao stahiki.

      Kwa nafasi yako hiyo hiyo ya Naibu Katibu Mkuu CHADEMA, sogeza mkono wako kidogo ukajumuishe na halmashauri zile nyinginezo tata nchini tupate matokeo mapema.

      Nasikitika kwamba mwaka huu nilikua nalazimika kutofautiana na wewe katika maswala mengi sana sana, ila bila chuki. Na hata kesho mienendo isipokua ni ya kupigania umma na kujenga teamwork katika chama nako bado utarajie kwamba mimi na wewe bado tutakwaruzana tu licha ya urafiki wetu wa siku nyingi.

      Hata hivyo, mwakani jitahidi sana ku-Reclaim the Ziitto that we had always known to be standing out steadfast in you full stop.

      Vile vile anza kuiwekea mikakati murua ule mswada wa Mhe Mnyika kuhusu KATIBA MPYA kule bungeni Dodoma.

    6. #5
      Abraham's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 9th October 2008
      Posts : 110
      Rep Power : 564
      Likes Received
      6
      Likes Given
      45

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Quote By Uwezo Tunao
      Zitto, hapo imekaa sawa maana ni suala la kudaihaki ya wananchi / Umma wa Tanzania kupata uwakilishi wao stahiki.

      Kwa nafasi yako hiyo hiyo ya Naibu Katibu Mkuu CHADEMA, sogeza mkono wako kidogo ukajumuishe na halmashauri zile nyinginezo tata nchini tupate matokeo mapema.

      Nasikitika kwamba mwaka huu nilikua nalazimika kutofautiana na wewe katika maswala mengi sana sana, ila bila chuki. Na hata kesho mienendo isipokua ni ya kupigania umma na kujenga teamwork katika chama nako bado utarajie kwamba mimi na wewe bado tutakwaruzana tu licha ya urafiki wetu wa siku nyingi.

      Hata hivyo, mwakani jitahidi sana ku-Reclaim the Ziitto that we had always known to be standing out steadfast in you full stop.

      Vile vile anza kuiwekea mikakati murua ule mswada wa Mhe Mnyika kuhusu KATIBA MPYA kule bungeni Dodoma.
      Hapo umeongea sasa ...achana na migogoro ya chama badilika na anza kujenga chama upya usisikilize waandishi wa habari sana watakupoteza
      "Don't argue with a fool , as people might not notice the difference!"

    7. Miaka 50

    8. #6
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,098
      Rep Power : 12255
      Likes Received
      6016
      Likes Given
      6856

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Quote By Mbopo
      These manouvres are a recipe for unnecessary chaos. We should be more sensible and let the will of the people prevail lest we plunge this contrary into chaos or violence.
      yeye ametumwa tu, ni kama andengenye na chitanda arusha, kila sehemu wapo.... wanatekeleza amri ya mkuu wao na wao kama wanajeshi nadhani unaelewa huwa wanatekeleza then kuhoji badae
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    9. #7
      niweze's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2009
      Posts : 1,010
      Rep Power : 698
      Likes Received
      112
      Likes Given
      82

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Zitto Amerudi Sehemu Yake au ni Vipi?

    10. #8
      Uwezo Tunao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2010
      Posts : 6,916
      Rep Power : 2298
      Likes Received
      1155
      Likes Given
      1500

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Quote By niweze
      Zitto Amerudi Sehemu Yake au ni Vipi?
      Zitto unaona aina ya maswali ambayo vijana wenzako huwa tunajiuliza huku vijiweni. Mimi binafsi sihitaji ukaninunulie hata chupa ya fanta lakini uwe tu mtu wa kuaminika mbele ya jamii yako basi!!!!

    11. #9
      Speaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th August 2010
      Posts : 6,173
      Rep Power : 4561
      Likes Received
      2000
      Likes Given
      5037

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      mbona wabunge wengine wana zuiwa kuongea na wananchi lakini zito kila mara anaruhusiwa bila tatizo?
      Mjinga mpe cheo...

    12. #10
      Omulangi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2008
      Posts : 726
      Rep Power : 721
      Likes Received
      132
      Likes Given
      8

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Zitto, Ztto, Zitto...

    13. #11
      babayah67's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th March 2008
      Location : Makasuku
      Posts : 390
      Rep Power : 652
      Likes Received
      35
      Likes Given
      6

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Huyu huyu Mkuchika ndie aliyekuwa waziri wa habari na michezo serikali ilopita. Huyu jamaa ni mtata saana, siku zote yupo katika kulinda maslahi ya CCM. Kumbuka aliwahi kususiwa na waandishi wa habari hasa baada ya kuzua bifu nao, na waandishi wakaamua kumweka kolokoloni (kwa kutandika habari zake ) Sijui kama adhabu ile iliisha, mimi naamini huyu jamaa BADO anastahiri ile adhabu

    14. #12
      TUKUTUKU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Location : KIPALAPALA TU
      Posts : 8,379
      Rep Power : 2116
      Likes Received
      1739
      Likes Given
      682

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Hongera sana Zitto kawa sasa unanifurahisha sana,ni lazima uwe mwanasiasa mwenye msimamo.Naona CCM wanataka vurugu zisizokuwa za lazima!!!

    15. #13
      TUKUTUKU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Location : KIPALAPALA TU
      Posts : 8,379
      Rep Power : 2116
      Likes Received
      1739
      Likes Given
      682

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Quote By Speaker
      mbona wabunge wengine wana zuiwa kuongea na wananchi lakini zito kila mara anaruhusiwa bila tatizo?
      Mkuu mbona umeongea kitu kipya kabisa?ni mbunge yupi aliyekatazwa kuongea na wananchi!!

    16. #14
      GWeLa 2003's Avatar
      Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Posts : 26
      Rep Power : 432
      Likes Received
      1
      Likes Given
      2

      Post Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      viongozi wetu hawa (product ya CCM) kama alivyowahi kunukuliwa chenge kipindi cha Uspika.. inatakiwa kulinda maslahi ya chama na siyo ya wananchi..na ndio maana si shangai kuona mkuchikaakisindwa kutatua ssuala la Umeya kigoma...na kingine selikeli ilishaona ya kuwa raia wake hawana akilindio maana inafanya maamuzi tata..tukisema tz ni nchi ya kiimla nani atapinga? ... ni kigezo gani kilichotumika kuwapa madiwani wa3 ccm wa viti maalum kati ya nafasi hizo nne..yote kwa yote hali hii itaisha, tunachotaka ni katiba mpya

    17. #15
      Kunta Kinte's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th May 2009
      Posts : 2,579
      Rep Power : 2537
      Likes Received
      606
      Likes Given
      763

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Quote By Speaker
      mbona wabunge wengine wana zuiwa kuongea na wananchi lakini zito kila mara anaruhusiwa bila tatizo?

      Hauna taarifa ni Naibu Katibu Mkuu

    18. #16
      nyantella's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 604
      Rep Power : 548
      Likes Received
      72
      Likes Given
      33

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Quote By Rutashubanyuma
      Zitto atoa siku saba kwa Waziri Monday, 27 December 2010 19:59

      Anthony Kayanda, Kigoma

      Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi), George Mkuchika, amepewa siku saba kuhakikisha anaitisha uchaguzi wa kumchagua Meya wa Halmashauri ya Manispaa Kigoma-Ujiji aliouahirisha, licha ya Mahakama kuamua ufanyike siku uliopangwa rasmi.
      Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema,Zitto Kabwe alipokuwa akihutubia Wananchi wa Kigoma mjini kuelezea mambo mbalimbali yanayohusiana na mustakabali wa kisiasa, ambapo alimshutumu Waziri huyo kwa kutumia Mamlaka yake vibaya.

      ‘Chadema tuna idadi kubwa ya madiwani zaidi ya CCM, hivyo juhudi zozote zinazofanywa na Waziri kusaidia Chama chake hazitasaidia kitu, badala yake zitaongeza hasira na chuki kwa Wakazi wa Kigoma mjini na kujikuta wakiichukia zaidi CCM na viongozi wake kwa vile anachangia kukwamisha maendeleo ya mji wetu’ alieleza Zitto.

      ‘Kutokana na hali hiyo, nampa Waziri wa Tamisemi siku saba ahakikishe anaitisha uchaguzi wa kumchagua Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ili tumpate Mwenyekiti wa baraza la madiwani na kamati zake za kudumu waanze kutuhudumia na kusimamia miradi ya maendeleo, kwa sababu kadri Waziri anavyochelewesha uchaguzi ndivyo Watendaji wanavyoweza kutumia vibaya nafasi hiyo kuharibu Halmashauri yetu” aliongeza.


      Alisema baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu, Chadema walishinda nafasi za madiwani katika Kata 10 dhidi ya tisa walizopata CCM, jambo lililofanya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoa nafasi nne za madiwani wa Viti Maalumu wakati CCM walipewa nafasi tatu za Madiwani wa Viti maalumu.


      Zitto alisema chanzo cha mgogoro huo ni idadi hiyo ya madiwani wa Viti maalumu ambapo alidai kuwa CCM walikwenda Mahakama ya Wilaya Kigoma kulalamikia mgawo huo, lakini Mahakama ilitupilia mbali shauri hilo.

      ‘Waziri Mkuchika anapaswa kujua kwamba siku ile alipoandika barua ya kusimamisha uchaguzi wa Meya (Desemba 17, 2010), Mahakama ya Wilaya Kigoma ilikuwa imetoa maamuzi ya shauri la CCM waliotaka Mahakama isimamishe uchaguzi, lakini Hakimu alilitupilia mbali shauri hilo kwa maelezo kwamba Tume ya Uchaguzi ipo sahihi katika mgawanyo wa madiwani wa viti maalumu” alifafanua Zito.

      ‘Na hata kama Mahakama ingesema okay, CCM waongeongezewa diwani mmoja ili tulingane nao bado wasingekuwa na uwezo wa kushinda halmashauri, labda ile ndoa ya Mseto tuliyofunga nao mwaka 2005 inaonekana wameridhika nayo ndiyo maana wanataka turudiane nao, sisi tunasema kwa hilo hatupo tayari na kamwe mwaka huu hatuipotezi Manispaa ya Kigoma Ujiji’ alisisitiza.
      ----!!
      Asipoitisha atafanya nini? asitishie watu nyau!!!

    19. #17
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 3,614
      Rep Power : 1332
      Likes Received
      782
      Likes Given
      656

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      lakini nawewe mkuchikaaaaaaa soma alama za nyakati waziri,huu wakati tulionao ni tofauti sana na enzi zenu,watu wamebadilika na wana hasila kweli,wape haki yao,kwa hilo hatuko nawe juu ya hilo kwani tunahitaji maendeleo na wala sio longolongo


      mapinduziiiii daimaaaaaaa

    20. #18
      Penguine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th November 2009
      Posts : 512
      Rep Power : 584
      Likes Received
      121
      Likes Given
      19

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Mkuchika unataka KUKUCHIKA kila kitu eeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee katika siasa?

    21. #19
      shanature's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th November 2010
      Posts : 519
      Rep Power : 535
      Likes Received
      24
      Likes Given
      24

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Tabia ni kama ngozi ya mwili huwezi kuibadili
      kuku kuku jogoo jina

    22. #20
      LoyalTzCitizen's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th September 2010
      Location : Lashkar Gah, Helmand
      Posts : 1,539
      Rep Power : 763
      Likes Received
      157
      Likes Given
      147

      Default Re: Zitto atoa siku saba kwa Waziri

      Quote By nyantella
      ----!!
      Asipoitisha atafanya nini? asitishie watu nyau!!!
      ????????
      "A government that robs Peter to pay Paul can always depend on the support of Paul.." (GB Shaw)


    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Siku saba za dr slaa
      By nyengo in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 22
      Last Post: 26th May 2011, 16:22
    2. Afufuka Baada ya Siku Saba!
      By eRRy in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 28
      Last Post: 11th May 2011, 14:45
    3. Siku saba za kamati kuu mpya ya CCM
      By only83 in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 5
      Last Post: 17th April 2011, 16:28
    4. Bado siku saba dowans walipwe
      By WJN in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 7
      Last Post: 11th February 2011, 07:31
    5. mwanachuo atoa mimba ya miezi saba CBE DiODOMA na kutupa kichanga chooni
      By OgwaluMapesa in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 1
      Last Post: 24th May 2008, 17:19

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...