Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

    Report Post
    Page 5 of 6 FirstFirst ... 3456 LastLast
    Results 81 to 100 of 117
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,487
      Rep Power : 46707
      Likes Received
      16305
      Likes Given
      8386

      Default Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Tunataka kutetea demokrasia na utawala wa demokrasia, hivyo hatuwezi kuwa wa kwanza kupendekeza njia zisizo za kidemokrasia kushughulikia matatizo ya kidemokrasia. Tupo ambao tumechukizwa, kukerwa na kuumizwa na jinsi ambavyo matokeo ya uchaguzi mkuu katika ngazi zote yalivyotolewa na yanavyoendelea kutolewa na hasa mahali tulipofikia vijana wetu kulazimika "kulinda kura". Wapo ambao wanaona kabisa kuwa baadhi ya watu waliotangazwa au watakaotangazwa washindi wamekosa uhalali wa nafasi hizo.

      Pamoja na ukweli wa hilo siku za karibuni kuanzia mvurugano wa Tume na Matokeo ya Uchaguzi nimefuatilia wapo watu wamejiunga ghafla ghafla au wengine wa muda kidogo ambao wamekuja na siasa kali za kutaka kutumia JF kama jukwaa la kuanzishia itikadi ya nguvu dhidi ya utawala wa kisiasa (violence against public officials).

      Mimi binafsi nikiwa ni muumini wa nadharia ya nguvu ya hoja siungi mkono hoja za nguvu kwani katika kutumia hoja za nguvu kunathibitisha kuwa umeshindwa kutumia nguvu za hoja kuweza kuwashawishi watu wengine. Lakini ukweli ni kwamba, hadi hivi sasa tumeweza kwa kutumia hoja tu kujenga hoja na kuwashawishi mamilioni ya Watanzania kuchagua mabadiliko. Hatuna sababu ya kubadili mbinu hiyo sasa hata kama tunajisikia hasira kiasi gani.

      Binafsi napinga na kulaani vikali kauli zinazotolewa aidha kama entrapment ya JF au kutoka moyoni kweli yenye kuashiria kuwa ni bora kutumia nguvu kuweza kupata matokeo ya kisiasa. Tulipoanza JF miaka michache iliyopita hatukujua kuwa uongozi wa kisiasa ungekuwa ulivyo, lakini tumeweza kupita katika misukosuko mingi ya kitaifa na tumeweza kufika leo tumeshuhudia mabadiliko makubwa na ushindi usiokadirika wa upinzani Tanzania na hivyo kusababisha malango yaliyofungwa kuachia. Huu ni ushindi wa hoja si vitisho.

      Kama kundi ambalo baadhi yetu tunajiita au tunaitwa wasomi, ni lazima tuwe tayari kutetea hoja zetu nakutumia ushawishi wa hoja kuweza kupata matokeo ya kisiasa. Ninachosema ni kuwa tuwakatae kwa hoja wale wote wenye kujaribu kutushawishi au kutoa kauli za matumizi ya nguvu kama "laiti ningekuwa sniper", "tuwapige risasi"n.k ili waone kama kuna watu wataunga mkono - na inasikitisha wapo wanaounga mkono.

      Kwa kufanya hivyo, tunaweka mtandao wetu tuupendao hatarini kwani kikiwa ni chombo kilichoandikishwa na licha ya watu kutumia majina mbadala endapo jambo fulani linatokea mtandao huu una wajibu wa kushirikiana na vyombo vya kiusalama kutekeleza amri halali ya mahakama kuweza kuwapata wahusika. Sasa tusichukulie kimzaha tunapotoa kauli zenye mfanano wa vitisho, kauli hizo hazilindwi na "uhuru wa maoni" kwani ni kama ilivyosema "kupiga kelele moto, kwenye ukumbi uliojaa".

      Hivyo, kwa wale ambao tumekasirishwa sana na matokeo, tujitoe zaidi kujipanga katika vyama tunavyovitaka au kushiriki kuunga mkono au kuwasaidia wagombea waliochakachuliwa matokeo yao. Mtu akitoa kauli yenye mwelekeo wa vitisho kwa viongozi wa umma - haijalishi kama ni wa chama tawala au upinzani - nawaomba tuflag comment hiyo na kuwataarifu ma MOD mara moja. Tusidhania MODs wanasoma kila sentensi ya kila thread ya kila mtu kila siku. Tuwe walinzi wa forum yetu sisi wenyewe kwani ninaamini katika siku zijazo tutahitaji chombo hiki kuendelea kuwepo.

      Tukumbuke kuwa ufisadi bado upo, mgongano ndani ya CCM upo na changamoto mbalimbali za kitaifa bado zipo. Hivyo, ni kwa maslahi yetu sisi wenyewe wanachama, wageni, na mashabiki kuulinda mtandao huu kutoka kwa watu ambao wengine naamini ni political operatives wa baadhi ya watu ambao kazi yao ni kupandikiza hoja za kichochezi ili JF itajwe (kama mnakumbuka Feb 2008) kuwa ni mtandao wa kighaidi au kichochezi. Maana ikifanyika hivyo wengi hutimka na kukaa pembeni huku wachache vichwa vyao vikiwekwa katika kamba za wanyongaji.

      Tujiwajibishe wenyewe, tuilinde forum yetu..

      Napendekeza.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    2. FemaTV & Radio

    3. #81
      DENYO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Posts : 582
      Rep Power : 565
      Likes Received
      12
      Likes Given
      0

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      NAUNGA MKONO HOJA MWANAKIJIJI -BUT ili mabadiliko yafanyike hisia kali na ukweli lazima ziruhusiwe, ccm ndio mchezo wao wamezoea kuchakachua walianza siku nyingi -lazima tuwaambie ukweli kupitia JF. Tunataka Tume huru ya Uchaguzi na siyo Tume ya CCM, tunataka tume inayojali maslahi ya watanzania wengi, kwani mbona Ivory Cost wanatume bomba inashindikana vipi TZ, ni kwa kusema ukweli na kuandamana ndio watajua hiki ni kizazi kipya, TUME IVUNJWE HATUITAKI IMESHINDINDWA KAZI ILIYOPEWA KIKATIBA.

    4. #82
      Mujuni2's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th June 2008
      Posts : 141
      Rep Power : 586
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Every war has its casualities, hakuna mapinduzi ya kweli yanayoletwa kwa propaganda za maneno (kama unavyoita nguvu ya hoja) tukubali tuu, tutaendelea kukaa hapa mbele ya monitors miaka na miaka mambo yatakuwa yale yale Mwanakijiji, mifano michache ya nchi zilizokombolewa kutoka unyonyaji ni Marekani (kutoka England), Kenya (now they have a new constitution), Iran ( King Shah) and so many, na zote hizi nguvu za hoja hazikuleta mabadiliko mpaka watu walipoingia mitaani. Watanzania hatujawa tayari, tutakapokuwa tayari matumizi ya nguvu ( physical confrotation) hataepukika Mzee, trust me.

    5. #83
      kuti kavu's Avatar
      Member Array
      Join Date : 25th February 2009
      Location : Mtakuja
      Posts : 52
      Rep Power : 531
      Likes Received
      14
      Likes Given
      7

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Kweli kaka...ki ubinadamu haya yaliyojitokeza kwenye uchaguzi yametia vidonda katika mioyo ya wengi...ila nakubalina nawe kuwa kuna haja kutafuta namna ya kuzizinga hasira zisizae chuki...nina imani kuwa kwa kutumia hekima, busara na nguvu ya hoja mtanzania atakombelewa tu...
      [COLOR="rgb(139, 0, 0)"][/COLOR]Hope and optimism...... in-spite of the present difficulties!!!

    6. #84
      Kaa la Moto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Location : Bristol
      Posts : 6,819
      Rep Power : 1942
      Likes Received
      428
      Likes Given
      4188

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Quote By Mujuni2
      Every war has its casualities, hakuna mapinduzi ya kweli yanayoletwa kwa propaganda za maneno (kama unavyoita nguvu ya hoja) tukubali tuu, tutaendelea kukaa hapa mbele ya monitors miaka na miaka mambo yatakuwa yale yale Mwanakijiji, mifano michache ya nchi zilizokombolewa kutoka unyonyaji ni Marekani (kutoka England), Kenya (now they have a new constitution), Iran ( King Shah) and so many, na zote hizi nguvu za hoja hazikuleta mabadiliko mpaka watu walipoingia mitaani. Watanzania hatujawa tayari, tutakapokuwa tayari matumizi ya nguvu ( physical confrotation) hataepukika Mzee, trust me.
      Wewe nakuelewa lakini mwanakijiji kuna mahali hatutakubaliana na nakubali kutokubaliana na mwanakijiji. Bila kutumia nguvu hatutavuka. Ni nguvu za kiasi gani hapo ndipo kuna hoja. Lakini mazungumzo ya kwenye keyboard hayatatuvusha tusidanganyane!
      wakati Cuf wanataka kuchukua nchi mwaka 2000 CCM walikuja na single ya kusema Cuf ni waislamu na kwa sasa wanadai sisi Chadema ni chama cha wakristo sasa CCM nacho ni cha watu gani? Watu wakajibu mashetaaaaaniiiiii.!---Wana Kigoma.

      ....Pamoja na kansa ya uongozi wa CCM watu wataendelea kukichagua,au watu wanaweza wakachoka na kusema potelea mbali wakachagua chama KINGINE....Julius. Kambarage. NYERERE"

    7. #85
      X-PASTER's Avatar
      Super Moderator Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Firdaws (Paradise)
      Posts : 11,859
      Rep Power : 7686
      Likes Received
      1467
      Likes Given
      0

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Quote By The Good
      Mkuu I support you 100%.

      Kuna wakati nimekuwa nikijiuliza hivi kweli JF ni HOME OF GREAT THINKERS au la. Kuna mambo kadhaa ambayo yameanza ku-dilute nguvu ya hii forum ntatoa machache.

      1. Kutokubali mawazo m-badala.
      Kuna tabia inayokuwa ya wachangaiaji wengi kuamini yoyote mwenye mawazo tofauti na yako basi yuko katika njia potofu. kwangu hili ni kosa maana lengo moja la forum hii ni watu kutoa mawazo yao kwa uwazi (pasi kuvunja sheria). Hivyo basi ili uweze kujipima usahihi wa mawazo yako mawazo tofauti na yako ni muhimu ili kuona kama kuna eneo ambalo umelisahau katika kujenga hoja ambalo linaweza kukupa mwelekeo mzuri zaidi.

      2. Kushambulia watu zaidi kuliko hoja

      Mara kadhaa tunasahau hoja na kumchambua mtoa hoja. Hii pia inapunguza umaarufu wa forum.

      3. Kauli za jazba, vitisho na hata matusi
      Busara za mtu huanza kupimwa kwa kauli zake maana matendo hujitokeza baadae baada ya kumjua mtu husika. Mtu mwenye natusi huonyesha upungufu wa busara.

      My opinion:

      JF inapaswa iwe chungu cha kupika hoja ambazo zinaweza kutumiwa na mtu yoyote ikiwemo wawakilishi na viongozi wetu katika kusukuma mbele Taifa letu.

      Mgongano wa mawazo ni sharti la kwanza katika kujenga jamii imara. Lazima tujenge utamaduni wa kusikilizana. jamii lenye mawazo yanayofanana ni jamii mgando.

      Naomba kuwakilisha
      Well said mkuu!
      “I am the punishment of God... If you had not committed great sins, God would not have sent a punishment like me upon you.”

      'O Allah! Keep me alive as long as life is better for me, and let me die if death is better for me.

      (¯`·._.•X-Paster™•._.·´¯)


    8. Miaka 50

    9. #86
      Kaa la Moto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Location : Bristol
      Posts : 6,819
      Rep Power : 1942
      Likes Received
      428
      Likes Given
      4188

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Quote By Nguruvi3
      Kuanzisha forum hiyo inawezekana kila siku, lakini kuwa na forum ambayo ni jicho la jamii si kitu rahisi. Hatuhitaji mtu aipende JF lakini pia si vema watu kuvuka mipaka. Kumbuka uhuru wa mtu huishia pale wa mwenzake unapoanzia.
      Nguruvi3, Umenijibu baadhi ya hoja mkuu lakini kwa hili unasemaje? "Kuna post nimeuliza swali kwamba ikiwa hamjaona hatari iliyonayo JF kwa kuweka wazi nyaraka za siri za serikali! hatari nyingine kubwa itakuwa ni ipi?" Maana tusiishie tu kusema uhuru wako unaishia pale wa serikali unapoanzia wakati umechakachua uhuru wa mwenzio kwa kuingilia siri zake na kuziweka public.SAWA?
      wakati Cuf wanataka kuchukua nchi mwaka 2000 CCM walikuja na single ya kusema Cuf ni waislamu na kwa sasa wanadai sisi Chadema ni chama cha wakristo sasa CCM nacho ni cha watu gani? Watu wakajibu mashetaaaaaniiiiii.!---Wana Kigoma.

      ....Pamoja na kansa ya uongozi wa CCM watu wataendelea kukichagua,au watu wanaweza wakachoka na kusema potelea mbali wakachagua chama KINGINE....Julius. Kambarage. NYERERE"

    10. #87
      Madela Wa- Madilu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th March 2007
      Location : NORTH WEST USA
      Posts : 2,524
      Rep Power : 2441
      Likes Received
      277
      Likes Given
      286

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Swali la msingi KAA LA MOTO.

      Msimamo wangu ni kwamba, Hoja ya Nguvu, ni jambo la lazima na lisiloepukika, kwa sababu ni upande wa pili wa Nguvu ya hoja.
      Kuwaandaa Watanzania kukataa Amri zisizo za kisheria ni moja kati ya mambo ya Awali kabisa yenye kujenga Msingi wa Hoja ya Nguvu.
      Nguvu ya hoja itangulie ikisindikizwa na Hoja ya Nguvu. Hiyo ndiyo lugha sahihi ambayo CCM wataielewa hakuna Polisi, FFU.UWT na hata JWTZ wawwezao kupingana na Hoja ya Nguvu ya wananchi.
      Kiongozi na mwasisi wa South Afrika NELSON MANDELA alianzisha Military wing ya ANC ambayo hatimaye ilimpeleka Jela na kuwapa taabu sana Makaburu. Sisi hapa tunadeal na Makaburu Weusi ambao tumesha penetrate ngome yao kwa sana. Tutatumia Nguvu ya Hoja lakini wakae wakijua kwamba Hoja ya Nguvu haichezi mbali.

      Ndiyo maana somo la Siasa ya CCM High Schoo nilipata F lakini nikiwa chuo niliandika Misonge ya nguvu sana.
      MYPEOPLE PERISH FOR LACK OF KNOWLEDGE. HOSEA 4:6

    11. #88
      Nyunyu's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 9th March 2009
      Location : Here.
      Posts : 3,349
      Rep Power : 2043
      Likes Received
      465
      Likes Given
      2749

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Mkuu MKJJ,

      Toka kuanza na kufa kwa CCJ, harakati zote zilizopita, hadi hivi leo!! Bado sijawahi kukuelewa!!!
      There is no such a thing as part freedom- Nelson Mandela

      e-mail: [email protected]

    12. #89
      Mwanamageuko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2010
      Location : Baitul Lahm
      Posts : 1,175
      Rep Power : 672
      Likes Received
      81
      Likes Given
      211

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Quote By Mujuni2
      Every war has its casualities, hakuna mapinduzi ya kweli yanayoletwa kwa propaganda za maneno (kama unavyoita nguvu ya hoja) tukubali tuu, tutaendelea kukaa hapa mbele ya monitors miaka na miaka mambo yatakuwa yale yale Mwanakijiji, mifano michache ya nchi zilizokombolewa kutoka unyonyaji ni Marekani (kutoka England), Kenya (now they have a new constitution), Iran ( King Shah) and so many, na zote hizi nguvu za hoja hazikuleta mabadiliko mpaka watu walipoingia mitaani. Watanzania hatujawa tayari, tutakapokuwa tayari matumizi ya nguvu ( physical confrotation) hataepukika Mzee, trust me.
      Na usisahau kwamba kwingi ambako nguvu za kuondoa serikali zimetumika hakujafanikiwa mf. Somalia, Sudan, Uganda, Chad, Chechnya n.k. huku vilevile ukikumbuka mgogoro mkubwa wa Angola ulikwisha kwa maongezi tu. MATUMIZI YA NGUVU SI SULUHISHO LA KUDUMU NA KAMA INGELIKUWA NDIVYO BASI IVORY COAST NA NIGERIA MPAKA LEO KUNGEKUWA HAKUKALIKI, KAMA ILIVYO KWA IRAQ NA AFGHANISTAN.
      "...If crime fighters fight crime and fire fighters fight fire, what do freedom fighters fight?"

    13. #90
      Mwanamageuko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2010
      Location : Baitul Lahm
      Posts : 1,175
      Rep Power : 672
      Likes Received
      81
      Likes Given
      211

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Quote By kuti kavu
      Kweli kaka...ki ubinadamu haya yaliyojitokeza kwenye uchaguzi yametia vidonda katika mioyo ya wengi...ila nakubalina nawe kuwa kuna haja kutafuta namna ya kuzizinga hasira zisizae chuki...nina imani kuwa kwa kutumia hekima, busara na nguvu ya hoja mtanzania atakombelewa tu...
      apo chacha!
      "...If crime fighters fight crime and fire fighters fight fire, what do freedom fighters fight?"

    14. #91
      Kaa la Moto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Location : Bristol
      Posts : 6,819
      Rep Power : 1942
      Likes Received
      428
      Likes Given
      4188

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Quote By Madela Wa- Madilu
      Swali la msingi KAA LA MOTO.

      Msimamo wangu ni kwamba, Hoja ya Nguvu, ni jambo la lazima na lisiloepukika, kwa sababu ni upande wa pili wa Nguvu ya hoja.
      Kuwaandaa Watanzania kukataa Amri zisizo za kisheria ni moja kati ya mambo ya Awali kabisa yenye kujenga Msingi wa Hoja ya Nguvu.
      Nguvu ya hoja itangulie ikisindikizwa na Hoja ya Nguvu. Hiyo ndiyo lugha sahihi ambayo CCM wataielewa hakuna Polisi, FFU.UWT na hata JWTZ wawwezao kupingana na Hoja ya Nguvu ya wananchi.
      Kiongozi na mwasisi wa South Afrika NELSON MANDELA alianzisha Military wing ya ANC ambayo hatimaye ilimpeleka Jela na kuwapa taabu sana Makaburu. Sisi hapa tunadeal na Makaburu Weusi ambao tumesha penetrate ngome yao kwa sana. Tutatumia Nguvu ya Hoja lakini wakae wakijua kwamba Hoja ya Nguvu haichezi mbali.

      Ndiyo maana somo la Siasa ya CCM High Schoo nilipata F lakini nikiwa chuo niliandika Misonge ya nguvu sana.
      Ndugu yangu Madela Wa- Madilu,
      Leo asubuhi nilikuwa kwa shoe polisher mmoja na palikuwa vijana pale. Mmoja wa vijana wale wakaniuliza swali. "Mzee kaa la moto, je mbona Dr Slaa hasemi kitu?"
      Niliwajibu bado yuko katika tathimini na atakuja tu kutokea na hoja iliyo na uhakika na iliyosheheni ushahidi ambao hata ccm hawataweza kujitetea. Nikawambia ninavyomjua Dr Slaa si mtu wa kuja na bla bla za kulalamika kama walivyokuwa wanalalamika wakina Seif. Nikawambia lazima atakuja na evidence.
      Baadae kati ya wale vijana mmoja akaniuliza "Mzee kaa la moto, je kama hii njia ndiyo inatumika kuchagua viongozi wa nchi hii kwa nini tunapoteza muda wetu kupiga kura?" yeye akasema anaona si vema kupiga kura badala yake hawa viongozi tuwaache wawe viongozi wa maisha kuliko kupoteza muda wao na pesa ya serikali kwa ajili ya uchaguzi. Nilisikitishwa na kauli yake kwamba "Sintapiga tena kura katika nchi hii"
      Neno hilo lilinisikitisha sana kiasi kwamba nilianza kumshawishi kwamba hilo wazo lake ndilo haswa ccm wanachotaka. Maana kwa kutopiga kwake kura ccm wao hawatajali bali baadhi ya viongozi na familia zao watapiga kura na kurudisha maharamia hawa hawa na maisha yataendelea kama yalivyo.
      Mara akadakia mwenzie kwa kusema "mimi naona suruhu ni kuchapana tu wengine wafe na wengine watunze heshima ya wengine." Ghafla ikanirudisha kwenye mazungumzo yetu yanayoendelea hapa. Maana niliona wote wanaanza kukubaliana na hoja hiyo na nikaona mara kuwa kuna hatari kubwa mbele yetu. Nikajaribu kuwatuliza kwa kuwambia hapana zipo njia nyingi mbadala kama anavyotutuliza mwanakijiji hapa, lakini niliendelea kupata pressure toka kwa vijana hao kuwa hakuna njia mbadala ila tutumie nguvu kupata haki zetu. Niseme ukweli niliamua kuondoka kimya kimya nikiacha mzozo ukiendelea ili nisijikute nabanwa kwa maswali magumu zaidi. This is a true story na imetokea asubuhi ya leo.
      Sasa basi hoja yako Madela Wa- Madilu inanirudisha kule kule nilikokuwa asubuhi. Tutafute namna ya kupeleka nguvu ya hoja kwa watawala wetu hawa wakina Kikwete lakini ikishindikana the other option ni kutumia hoja ya nguvu kwa watawala hawa hawa.
      wakati Cuf wanataka kuchukua nchi mwaka 2000 CCM walikuja na single ya kusema Cuf ni waislamu na kwa sasa wanadai sisi Chadema ni chama cha wakristo sasa CCM nacho ni cha watu gani? Watu wakajibu mashetaaaaaniiiiii.!---Wana Kigoma.

      ....Pamoja na kansa ya uongozi wa CCM watu wataendelea kukichagua,au watu wanaweza wakachoka na kusema potelea mbali wakachagua chama KINGINE....Julius. Kambarage. NYERERE"

    15. #92
      chapaa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th February 2008
      Posts : 2,250
      Rep Power : 1029
      Likes Received
      176
      Likes Given
      11

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Mkuu,MWKJ.
      I support u.I hope tempers will b down guyz.

    16. #93
      Mapinduzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd August 2008
      Posts : 2,429
      Rep Power : 1033
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Great thinkers, JF kuna rules zinazoonyesha bayana do's and dont's. Kwa ubendera hadi upepo mzee ahubiri moral conducts, tuvume naye upande huo.

      Siku mwanakijiji atayohamia ccm......
      Usiogope kufa, ogopa kukosa pesa. Kilimo kwanza

    17. #94
      Jackob's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Posts : 52
      Rep Power : 446
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Appreciated

    18. #95
      Azimio Jipya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Location : Universal Space Station
      Posts : 3,281
      Rep Power : 5414
      Likes Received
      1006
      Likes Given
      1731

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi


      Nimeona dilema ilipo!

      Ni kwenye mantiki nzima ya namna ya kutumia nguvu kwenye kujenga na kustawisha jamii.

      Kimsingi tutambue kuwa kuna nguvu kuu mbili ambazo lazima zitumike kwenye kufanikisha ustawi wa maisha yetu kila siku. Ni lazima kutumia nguvu moja kati ya hizi mbili.

      Chuki, hasira, woga, kinyogo, kisasi, ukatili, unyama.. Ni nguvu

      Upendo , heshima , haki, ubinaadamu, ujasiri, ukweli, busara na Utu..pia ni Nguvu.

      Moja ni nguvu iliyo asili ya ustawi wa mwanadamu, ni nguvu ya kustawisha Utu na maendeleo ya mwanadamu…Ni lazima kuitumia tena kwa kiwango kikubwa ikibidi.

      Lazima kutumia nguvu sahihi ninapodai ustawi sahihi kwenye jamii yangu… hili halina mjadala. Nguvu ya Utu, Upendo, Heshima, Busara..na Ubinaadamu lazima itumike…hata ikibidi nguvu hii kubebeshwa silaha ya aina yeyote.

      Nguvu ya Utu na matawi yote inaweza kutumika kuistawisha na kuijenga jamii inapobebwa na ..silaha, elimu , mawazo, kauli, matendo nk. Ni nguvu inayovipa vitu vingine vyote thamani yake. Bila nguvu sahihi fikra, kauli , matendo havina maana yeyote..

      Nguvu ya utu lazima itumike kumhoji Rais, Serkali, yeyote anayehusiaka na NEC mienendo yote ya uchaguzi ilivyokwenda…sitatumia nguvu ya kuupinga utu wangu wala wa Rais wala watu wote wanaohusika, wala wa Watanzania lakini nitatumia nguvu sahihi Kutaka kujua ukweli wa kura yangu niliyopiga.

      Nitatumia nguvu sahihi ya Utu..kumhoji Rais..Lazima kufanya hivyo kwa nguvu sahihi tena kwa ubora wote. Sitatumia..chuki, hasira, kinyongo, ukatili na hali ya unyama katika kutekeleza adhma yangu. Nitatumia nguvu tena kwa kiwango sahihi kulingana na namna hoja itakavyokuwa inajiendesha..lakini kwa nguvu sahihi, ya Upendo, Heshima, Haki..na kuenzi Utu na Ubinnadamu.

      Ni lazima kufanya hivyo kwani Kibox cha kura kipo kuilinda na kuienzi nguvu sahihi katika kustawisha Serekali, wizara zake, taasisi mabalimbali…na Kiongozi mkuu yupo kulinda na kusimamia kuwa nguvu sahihi inatumika katika miongozo yote ya Tiafa, kwa hiyo nguvu sahihi lazima itumike tena kwa kiwango stahili kulingana na nyakati na mahitaji.

      Kushindwa kutumia nguvu stahili kuilinda na kuistwaisha jamii..ni aibu na ni kusaliti, Utu na ubinaadamu wa ulimwengu huu. Na iko wapi maana ya maisha kama hilo limetushinda? Taifa la Tanzania linahitaji nguvu na sio umaamuma katia kufikia ngazi inayofuta katika maendeleo yake.. Lakini Nguvu sahihi.. ile yenye inayoweza kuharibu silaha zote duniani..Nguvu ya UTU!

      Demokrasia itakuwa ni kama kasha tupu kama haikubeba moja kati ya nguvu hizi.

      Ikibeba nguvu ambayo sio sahihi …itakuwa ni demokrasia inayofaa wanyama wa mwituni na mafisadi walioikumbatia Tanzania kwa sasa huku ukitumia ujanja na mbinu tata kuifunga midomo na fikra zetu..huku wao waki advansi kwa kasi kufikia malengo yao.

      Demokrasia sahihi inayosimamia maendeleo ya kweli ..imejengwa na kubeba nguvu sahihi. Inajua shina la ustawi wa mwanadamu na kulienzi kwenye kila nyanja…na haioni tatizo nguvu kutumika kwani nguvu sahihi si adui wa mwanadamu kamili na chochote ila hili litapingwa na wapinga Utu na ubinaadamu. Na sisi hatutawaelewa kabisa…

      Kwenye demokrasia ya nguvu sahihi ya utu na ubinaadamu ni sahihi kutumia nguvu sahihi na kuibebesha silaha, mabomu, vifaru, majeshi…ili kuilinda jamii ya binaadamu timamu waliostaarabika. Na ninaongea hivi kwa ujasiri mkubwa usio na ujeuri, chuki, woga, ila kwa upendo na heshima kuu kwa watu wote.

      Lakini kwenye demokrasia pinzani kwa utu na ubinaadamu, nilichosema kitakuwa ni tatizo lakini wao watataka kutumia silaha za kivita, majeshi, na nguvu zote za dola ili kilinda nguvu isiyo sahihi ya ufisadi. Hili halikubaliki kamwe!!!

      Kwa hiyo tusiwe wajinga; Vita, mabomu ya nuklia, silaha mbalimbali, majeshi, usalama wa taifa na nyenzo kama hizo zenyewe sio tatizo. SHIDA NI NGUVU GANI VITABEBESHWA VYOMBO HIVYO! ..Kisu cha mkate ..kinaweza kutumika kwa ubaya au kwa uzuri..hilo lieleweke…hii ni pamoja na dhana ya kumwaga damu... Damu kumwagiga si tatizo inategemea unafanya hivyo kwa ajili ya nguvu ipi!!! Mwaka 1978 Tanazania kwa kutumia nguvu sahihi ilimwga damu kule kagera na hatimaye uganda! ...Hoja ni Nguvu gani inabeba hiyo vita na malengo yake...nk lakini tusiogopeshani juu ya kumwaga damu. Jambazi akavamia nyumba yangu usiku wa manane na kuanz akusogelea chumba cha mabinti ..wangu..ohh Nitamwaga damu!! Ili kulinda heshma na ubinnadamu na ustaarabu wa familia na dunia yote!!

      Chadema, CCM, TLP, nk…ni vyombo vya kuilinda na kuitetea nguvu stahili katika kujenga na kustawisha jamii. Kama chama chochote kitakiuka misiningi hiyo ..nguvu sahihihi itatumika kukihoji tena bila woga , hasira, chuki, na aina yeyote ya nguvu isiyo sahihi…ikibidi hata kutumia chochote, ..ili mradi chochote hicho kibebe nguvu sahihi. Chama hicho kisitegemee tutakuwa magoigoi na wanyonge..kukikabili la hasha tutakihoji. Lazima hili nilieleze kwa upendo, ujasiri na kuuheshimu utu wangu na watanzania wote kuwa..Lazima kitafuatwa kwa nguvu ..tena nguvu kabisa..na kitahojiwa ..vipi hakilindi uasili na ustawi wa mwanadam. Haitawezekana tena kututishia vita, kupoteza amani nk. Kama amani ikipotea kwa ajili ya nguvu sahihi ..hakuna tatizo lolote... kwani kusema kweli amani na utulivu huo havikuwepo!

      JF..inahaki kutumia nguvu sahihi kuhoji na kulinda utu na ubinaadamu wa jamii inayojikuta. Hili ni sahihi kwa blog na mitandao yote nchini. Technologia na watu wake sio tatizo..tatizo ni inabebeshwa nini….

      Utu na ubinaadamu sio mali ya mtu au chama chochote useme itafungiwa na kuangamizwa. Kuangamiza nguvu sahihi kwenye jamii..ina maana kuangamiza watu wote kwnye jamii hiyo na hilo haliwezekani. Hakuna anayeweza kuangamiza nguvu sahihi. Mtu asije kudanganywa na kudanganyika….

      Kama JF na wanachama wake ni watii wa Utu na ubinaadamu wao ..na wametumia nguvu sahihi katika kauli, fikra na matendo yao na JF ikafungiwa ..sawa… Ni kwa kuwa ujumbe na lengo la JF litakuwa limefika..na hakuna atakaye jinsikia mkosaji.

      Kama JF italazimika kutumia nguvu isiyo sahihi kama woga, wasiwasi, kuupinga na kuusaliti utu wa jamii yake nk ili isifungiwe ..hiyo sio sawa..bora ifungiwe kuliko itumike kustawisha nguvu isiyo sahihi kwenye jamii.

      Si kweli kuwa kuna mamlaka ya kibinaadamu inayoweza kufumgia nguvu ya utu inayotegeneza nguvu ya umma iliyosheheni nguvu sahihi..nguvu ya umma. Hamuoni ..viti 22 mjengoni…Hamuoni..toka 80% mwaka 2005 hadi 61% mwaka 2010..Ni bilioni ngapi zilitumika kuhonga na kuyumbisha matokeo..? Hakuna!! Ni mwanzo wa nguvu sahihi kuiteka na kuirudisha Tanzania ile ya waasisi wake!! Peoples power.

      Mamlaka yenye ufinyu wa kufikiri kuwa nguvu sahihi ya umma unafungika au kuangamizwa..malaka hiyo itakuwa imepofuka na ni dhaifu ..itaangamia.

      Tuamke tutumie nguvu sahihi..kulijenga Taifa letu! Ikibidi hata kulifia kwenye misingi sahihi kwani huo ndio uzalendo..na utanzania wenyewe..

      Na tunamuomba Mungu atubariki katika ujenzi wa Taifa hili!!
      Last edited by Azimio Jipya; 9th November 2010 at 16:23.
      Never Get Angry; Never Make Threat; Reason With People;
      "Napenda the logic of the words because in some ways it says about individual-not to use emotions-when scrutinizing something, whether it involves you or not" ...-by AshaDiii @ Jamiiforums 26th July 2011.


    19. #96
      Kamakabuzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2007
      Posts : 1,064
      Rep Power : 797
      Likes Received
      142
      Likes Given
      257

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Dawa ya moto ni moto ingawa kuna wakati mwingine dawa ya moto ni maji. Kwa sasa nakubaliana na wewe kuwa tutumie maji kama dawa ya moto, lakini ikiwa upande mwingine hautakuwa tayari kuelewa kuwa maji ndiyo dawa, basi dawa mbadala itatumika.
      Hata Yesu kuna wakati aliingia kanisani akakuta watu wanaitumia nyumba hiyo tofauti na makusudio - alitengeneza mjeledi wa kamba na kuzipindua meza zao.
      Mwanakijiji nakuelewa unachozungumzia, lakini nahisi ccm hawako tayari kwa mazungumzo. Si umeona pemba? - baada ya bakora sasa muafaka - shwariiiii!. Tuwape muda lakini wajue pia kuwa uvumilivu una mwisho na hili gunia la amani wanalotumia kufichia maovu yao iko siku litatoboka maana limekwishazeeka

    20. #97
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,244
      Rep Power : 3038
      Likes Received
      3030
      Likes Given
      4109

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Quote By Nguruvi3
      Msemo maarufu hapa JF ni '' let us call a spade the spade not a big spoon''. Tafadhali rejea mada ya MMKJ na hasa aya za mwisho. Ukweli unabaki pale pale watu waseme kwa lugha yenye hoja. Tunaposema lugha za vitisho ni kama zilizotumika ''sniper'' n.k. Watu wanataka kujenga hoja zenye nguvu,hoja zilizotufikisha mahali ambapo Chama tawala kimehofia matokeo, hoja zitakazotufikisha mahali tunapata 2/3 majority, hoja zitakazotuwezesha kuwa na mabaraza ya madiwani kama karatu. Tunahitaji hoja zitakazojibu matatizo ya wananchi. kusema nitampiga au kumdhuru fulani si hoja zenye mashiko, matatizo yetu ni mengi kiasi kwamba tunahitaji umma utuelewe na uelewe.
      Kutisha mtu ni silaha iliyotumiwa na CCM kuwadhalilisha wapinzani, hatuhitaji kuwatisha watu, tuwaambie wa morogoro wamechagua nini na wategemee nini, tujenge hoja itakayowasukuma waelewe hatima ya nchi yao kimaendeleo kama walivyoelewa kigoma,mwanza, Tanga, Lindi, Kilimanjaro, mbeya, Arusha, Singida,n.k.
      Kuanzisha forum hiyo inawezekana kila siku, lakini kuwa na forum ambayo ni jicho la jamii si kitu rahisi. Hatuhitaji mtu aipende JF lakini pia si vema watu kuvuka mipaka. Kumbuka uhuru wa mtu huishia pale wa mwenzake unapoanzia.
      Nitaita spade the spade na si big spoon hata kama kufanya hivyo kutakuwa na mtazamo tofauti. Bado naunga hoja ya MMKJ.
      Kabla hujaendelea na kushabikia anayosema MMKj, muulize aliita CCJ spade au big spoon?
      Huyu ni bingwa wa spinning, atabakia kuwa hivyo mpaka pale atakapotueleza aliingizwa chaka on CCJ issue au la. Watu wanaomwamini kama wewe na wengine ninauhakika wangehama vyama vyao vilivokuwa na dira na kuhamia kwenye hoax - CCJ. Ushindi uliopatikana sasa hivi kwa kupitia vyama vya upinzani ungepatikana?

      THINK.
      * LOVE COMES NATURALLY; HATE IS TAUGHT.....by nngu007 wa JF

    21. #98
      Azimio Jipya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Location : Universal Space Station
      Posts : 3,281
      Rep Power : 5414
      Likes Received
      1006
      Likes Given
      1731

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Kweli kaka...ki ubinadamu haya yaliyojitokeza kwenye uchaguzi yametia vidonda katika mioyo ya wengi...ila nakubalina nawe kuwa kuna haja kutafuta namna ya kuzizinga hasira zisizae chuki...nina imani kuwa kwa kutumia hekima, busara na nguvu ya hoja mtanzania atakombelewa tu...




      Quote By Mwanamageuko
      apo chacha!
      Ndio... soma post namba 97
      Never Get Angry; Never Make Threat; Reason With People;
      "Napenda the logic of the words because in some ways it says about individual-not to use emotions-when scrutinizing something, whether it involves you or not" ...-by AshaDiii @ Jamiiforums 26th July 2011.


    22. #99
      Kaa la Moto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Location : Bristol
      Posts : 6,819
      Rep Power : 1942
      Likes Received
      428
      Likes Given
      4188

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Quote By Azimio Jipya
      Nimeona dilema ilipo!

      Ni kwenye mantiki nzima ya namna ya kutumia nguvu kwenye kujenga na kustawisha jamii.

      Kimsingi tutambue kuwa kuna nguvu kuu mbili ambazo lazima zitumike kwenye kufanikisha ustawi wa maisha yetu kila siku. Ni lazima kutumia nguvu moja kati ya hizi mbili.

      Chuki, hasira, woga, kinyogo, kisasi, ukatili, unyama.. Ni nguvu

      Upendo , heshima , haki, ubinaadamu, ujasiri, ukweli, busara na Utu..pia ni Nguvu.

      Moja ni nguvu iliyo asili ya ustawi wa mwanadamu, ni nguvu ya kustawisha Utu na maendeleo ya mwanadamu…Ni lazima kuitumia tena kwa kiwango kikubwa ikibidi.

      Lazima kutumia nguvu sahihi ninapodai ustawi sahihi kwenye jamii yangu… hili halina mjadala. Nguvu ya Utu, Upendo, Heshima, Busara..na Ubinaadamu lazima itumike…hata ikibidi nguvu hii kubebeshwa silaha ya aina yeyote.

      Nguvu ya Utu na matawi yote inaweza kutumika kuistawisha na kuijenga jamii inapobebwa na ..silaha, elimu , mawazo, kauli, matendo nk. Ni nguvu inayovipa vitu vingine vyote thamani yake. Bila nguvu sahihi fikra, kauli , matendo havina maana yeyote..

      Nguvu ya utu lazima itumike kumhoji Rais, Serkali, yeyote anayehusiaka na NEC mienendo yote ya uchaguzi ilivyokwenda…sitatumia nguvu ya kuupinga utu wangu wala wa Rais wala watu wote wanaohusika, wala wa Watanzania lakini nitatumia nguvu sahihi Kutaka kujua ukweli wa kura yangu niliyopiga.

      Nitatumia nguvu sahihi ya Utu..kumhoji Rais..Lazima kufanya hivyo kwa nguvu sahihi tena kwa ubora wote. Sitatumia..chuki, hasira, kinyongo, ukatili na hali ya unyama katika kutekeleza adhma yangu. Nitatumia nguvu tena kwa kiwango sahihi kulingana na namna hoja itakavyokuwa inajiendesha..lakini kwa nguvu sahihi, ya Upendo, Heshima, Haki..na kuenzi Utu na Ubinnadamu.

      Ni lazima kufanya hivyo kwani Kibox cha kura kipo kuilinda na kuienzi nguvu sahihi katika kustawisha Serekali, wizara zake, taasisi mabalimbali…na Kiongozi mkuu yupo kulinda na kusimamia kuwa nguvu sahihi inatumika katika miongozo yote ya Tiafa, kwa hiyo nguvu sahihi lazima itumike tena kwa kiwango stahili kulingana na nyakati na mahitaji.

      Kushindwa kutumia nguvu stahili kuilinda na kuistwaisha jamii..ni aibu na ni kusaliti, Utu na ubinaadamu wa ulimwengu huu. Na iko wapi maana ya maisha kama hilo limetushinda? Taifa la Tanzania linahitaji nguvu na sio umaamuma katia kufikia ngazi inayofuta katika maendeleo yake.. Lakini Nguvu sahihi.. ile yenye inayoweza kuharibu silaha zote duniani..Nguvu ya UTU!

      Demokrasia itakuwa ni kama kasha tupu kama haikubeba moja kati ya nguvu hizi.

      Ikibeba nguvu ambayo sio sahihi …itakuwa ni demokrasia inayofaa wanyama wa mwituni na mafisadi walioikumbatia Tanzania kwa sasa huku ukitumia ujanja na mbinu tata kuifunga midomo na fikra zetu..huku wao waki advansi kwa kasi kufikia malengo yao.

      Demokrasia sahihi inayosimamia maendeleo ya kweli ..imejengwa na kubeba nguvu sahihi. Inajua shina la ustawi wa mwanadamu na kulienzi kwenye kila nyanja…na haioni tatizo nguvu kutumika kwani nguvu sahihi si adui wa mwanadamu kamili na chochote ila hili litapingwa na wapinga Utu na ubinaadamu. Na sisi hatutawaelewa kabisa…

      Kwenye demokrasia ya nguvu sahihi ya utu na ubinaadamu ni sahihi kutumia nguvu sahihi na kuibebesha silaha, mabomu, vifaru, majeshi…ili kuilinda jamii ya binaadamu timamu waliostaarabika. Na ninaongea hivi kwa ujasiri mkubwa usio na ujeuri, chuki, woga, ila kwa upendo na heshima kuu kwa watu wote.

      Lakini kwenye demokrasia pinzani kwa utu na ubinaadamu, nilichosema kitakuwa ni tatizo lakini wao watataka kutumia silaha za kivita, majeshi, na nguvu zote za dola ili kilinda nguvu isiyo sahihi ya ufisadi. Hili halikubaliki kamwe!!!

      Kwa hiyo tusiwe wajinga; Vita, mabomu ya nuklia, silaha mbalimbali, majeshi, usalama wa taifa na nyenzo kama hizo zenyewe sio tatizo. SHIDA NI NGUVU GANI VITABEBESHWA VYOMBO HIVYO! ..Kisu cha mkate ..kinaweza kutumika kwa ubaya au kwa uzuri..hilo lieleweke…hii ni pamoja na dhana ya kumwaga damu... Damu kumwagiga si tatizo inategemea unafanya hivyo kwa ajili ya nguvu ipi!!! Mwaka 1978 Tanazania kwa kutumia nguvu sahihi ilimwga damu kule kagera na hatimaye uganda! ...Hoja ni Nguvu gani inabeba hiyo vita na malengo yake...nk lakini tusiogopeshani juu ya kumwaga damu. Jambazi akavamia nyumba yangu usiku wa manane na kuanz akusogelea chumba cha mabinti ..wangu..ohh Nitamwaga damu!! Ili kulinda heshma na ubinnadamu na ustaarabu wa familia na dunia yote!!

      Chadema, CCM, TLP, nk…ni vyombo vya kuilinda na kuitetea nguvu stahili katika kujenga na kustawisha jamii. Kama chama chochote kitakiuka misiningi hiyo ..nguvu sahihihi itatumika kukihoji tena bila woga , hasira, chuki, na aina yeyote ya nguvu isiyo sahihi…ikibidi hata kutumia chochote, ..ili mradi chochote hicho kibebe nguvu sahihi. Chama hicho kisitegemee tutakuwa magoigoi na wanyonge..kukikabili la hasha tutakihoji. Lazima hili nilieleze kwa upendo, ujasiri na kuuheshimu utu wangu na watanzania wote kuwa..Lazima kitafuatwa kwa nguvu ..tena nguvu kabisa..na kitahojiwa ..vipi hakilindi uasili na ustawi wa mwanadam. Haitawezekana tena kututishia vita, kupoteza amani nk. Kama amani ikipotea kwa ajili ya nguvu sahihi ..hakuna tatizo lolote... kwani kusema kweli amani na utulivu huo havikuwepo!

      JF..inahaki kutumia nguvu sahihi kuhoji na kulinda utu na ubinaadamu wa jamii inayojikuta. Hili ni sahihi kwa blog na mitandao yote nchini. Technologia na watu wake sio tatizo..tatizo ni inabebeshwa nini….

      Utu na ubinaadamu sio mali ya mtu au chama chochote useme itafungiwa na kuangamizwa. Kuangamiza nguvu sahihi kwenye jamii..ina maana kuangamiza watu wote kwnye jamii hiyo na hilo haliwezekani. Hakuna anayeweza kuangamiza nguvu sahihi. Mtu asije kudanganywa na kudanganyika….

      Kama JF na wanachama wake ni watii wa Utu na ubinaadamu wao ..na wametumia nguvu sahihi katika kauli, fikra na matendo yao na JF ikafungiwa ..sawa… Ni kwa kuwa ujumbe na lengo la JF litakuwa limefika..na hakuna atakaye jinsikia mkosaji.

      Kama JF italazimika kutumia nguvu isiyo sahihi kama woga, wasiwasi, kuupinga na kuusaliti utu wa jamii yake nk ili isifungiwe ..hiyo sio sawa..bora ifungiwe kuliko itumike kustawisha nguvu isiyo sahihi kwenye jamii.

      Si kweli kuwa kuna mamlaka ya kibinaadamu inayoweza kufumgia nguvu ya utu inayotegeneza nguvu ya umma iliyosheheni nguvu sahihi..nguvu ya umma. Hamuoni ..viti 22 mjengoni…Hamuoni..toka 80% mwaka 2005 hadi 61% mwaka 2010..Ni bilioni ngapi zilitumika kuhonga na kuyumbisha matokeo..? Hakuna!! Ni mwanzo wa nguvu sahihi kuiteka na kuirudisha Tanzania ile ya waasisi wake!! Peoples power.

      Mamlaka yenye ufinyu wa kufikiri kuwa nguvu sahihi ya umma unafungika au kuangamizwa..malaka hiyo itakuwa imepofuka na ni dhaifu ..itaangamia.

      Tuamke tutumie nguvu sahihi..kulijenga Taifa letu! Ikibidi hata kulifia kwenye misingi sahihi kwani huo ndio uzalendo..na utanzania wenyewe..

      Na tunamuomba Mungu atubariki katika ujenzi wa Taifa hili!!
      Nimekukubali mkuu wangu. Thanks again.
      wakati Cuf wanataka kuchukua nchi mwaka 2000 CCM walikuja na single ya kusema Cuf ni waislamu na kwa sasa wanadai sisi Chadema ni chama cha wakristo sasa CCM nacho ni cha watu gani? Watu wakajibu mashetaaaaaniiiiii.!---Wana Kigoma.

      ....Pamoja na kansa ya uongozi wa CCM watu wataendelea kukichagua,au watu wanaweza wakachoka na kusema potelea mbali wakachagua chama KINGINE....Julius. Kambarage. NYERERE"

    23. #100
      The Investor's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 6
      Rep Power : 434
      Likes Received
      0
      Likes Given
      3

      Default Re: Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      ...Kwa kufanya hivyo, tunaweka mtandao wetu tuupendao hatarini kwani kikiwa ni chombo kilichoandikishwa na licha ya watu kutumia majina mbadala endapo jambo fulani linatokea mtandao huu una wajibu wa kushirikiana na vyombo vya kiusalama kutekeleza amri halali ya mahakama kuweza kuwapata wahusika. Sasa tusichukulie kimzaha tunapotoa kauli zenye mfanano wa vitisho, kauli hizo hazilindwi na "uhuru wa maoni" kwani ni kama ilivyosema "kupiga kelele moto, kwenye ukumbi uliojaa" ....
      Ni kweli kabisa, japo mi ni member mgeni wa kujiunga ila nimekuwa nikiitembelea hii forum muda mrefu, nimeona watu wengi wanapoona wanatumia majina mbadala wanatumia hoja za nguvu na kauli ambazo kwa mtazamo wangu ni hatarishi na zinawaweka ma mods pabaya.

      Hivyo nina shukuru Mkuu kwa kutujuza na kutukumbusha wanaJF kwa ujumla kuwa tuwe makini kwenye kutoa hoja tukijua kuwa uhuru wa kuoa maoni si uhuru wa kuvunja sheria, na kwa technolojia ya sasa we can easily be traced no matter tunatumia majina mbadala.

      Tusikubali JF iharibiwe na wasio itakia mema, kwani JF ime na ina endelea kutusaidia wengi, walio nchini na wasio nchini.

      Umesikika na kueleweka!

    24. Study Abroad
    Page 5 of 6 FirstFirst ... 3456 LastLast

    Similar Topics

    1. Kizazi cha sasa na matumizi ya lugha
      By Ngomo in forum Jukwaa la Lugha
      Replies: 5
      Last Post: 6th February 2011, 13:53
    2. Palipo na demokrasia nguvu ya umma haina nafasi
      By GeniusBrain in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 29
      Last Post: 31st January 2011, 18:18
    3. Matumizi sahihi ya lugha
      By Dingswayo in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 3
      Last Post: 21st June 2010, 13:15
    4. Matumizi ya lugha.
      By Ekitarangwe in forum Jukwaa la Lugha
      Replies: 1
      Last Post: 22nd April 2009, 11:57

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...