Nimeona dilema ilipo!
Ni kwenye mantiki nzima ya namna ya kutumia nguvu kwenye kujenga na kustawisha jamii.
Kimsingi tutambue kuwa kuna nguvu kuu mbili ambazo lazima zitumike kwenye kufanikisha ustawi wa maisha yetu kila siku. Ni lazima kutumia nguvu moja kati ya hizi mbili.
Chuki, hasira, woga, kinyogo, kisasi, ukatili, unyama.. Ni nguvu
Upendo , heshima , haki, ubinaadamu, ujasiri, ukweli, busara na Utu..pia ni Nguvu.
Moja ni nguvu iliyo asili ya ustawi wa mwanadamu, ni nguvu ya kustawisha Utu na maendeleo ya mwanadamu…Ni lazima kuitumia tena kwa kiwango kikubwa ikibidi.
Lazima kutumia nguvu sahihi ninapodai ustawi sahihi kwenye jamii yangu… hili halina mjadala. Nguvu ya Utu, Upendo, Heshima, Busara..na Ubinaadamu lazima itumike…hata ikibidi nguvu hii kubebeshwa silaha ya aina yeyote.
Nguvu ya Utu na matawi yote inaweza kutumika kuistawisha na kuijenga jamii inapobebwa na ..silaha, elimu , mawazo, kauli, matendo nk. Ni nguvu inayovipa vitu vingine vyote thamani yake. Bila nguvu sahihi fikra, kauli , matendo havina maana yeyote..
Nguvu ya utu lazima itumike kumhoji Rais, Serkali, yeyote anayehusiaka na NEC mienendo yote ya uchaguzi ilivyokwenda…sitatumia nguvu ya kuupinga utu wangu wala wa Rais wala watu wote wanaohusika, wala wa Watanzania lakini nitatumia nguvu sahihi Kutaka kujua ukweli wa kura yangu niliyopiga.
Nitatumia nguvu sahihi ya Utu..kumhoji Rais..Lazima kufanya hivyo kwa nguvu sahihi tena kwa ubora wote. Sitatumia..chuki, hasira, kinyongo, ukatili na hali ya unyama katika kutekeleza adhma yangu. Nitatumia nguvu tena kwa kiwango sahihi kulingana na namna hoja itakavyokuwa inajiendesha..lakini kwa nguvu sahihi, ya Upendo, Heshima, Haki..na kuenzi Utu na Ubinnadamu.
Ni lazima kufanya hivyo kwani Kibox cha kura kipo kuilinda na kuienzi nguvu sahihi katika kustawisha Serekali, wizara zake, taasisi mabalimbali…na Kiongozi mkuu yupo kulinda na kusimamia kuwa nguvu sahihi inatumika katika miongozo yote ya Tiafa, kwa hiyo nguvu sahihi lazima itumike tena kwa kiwango stahili kulingana na nyakati na mahitaji.
Kushindwa kutumia nguvu stahili kuilinda na kuistwaisha jamii..ni aibu na ni kusaliti, Utu na ubinaadamu wa ulimwengu huu. Na iko wapi maana ya maisha kama hilo limetushinda? Taifa la Tanzania linahitaji nguvu na sio umaamuma katia kufikia ngazi inayofuta katika maendeleo yake.. Lakini Nguvu sahihi.. ile yenye inayoweza kuharibu silaha zote duniani..Nguvu ya UTU!
Demokrasia itakuwa ni kama kasha tupu kama haikubeba moja kati ya nguvu hizi.
Ikibeba nguvu ambayo sio sahihi …itakuwa ni demokrasia inayofaa wanyama wa mwituni na mafisadi walioikumbatia Tanzania kwa sasa huku ukitumia ujanja na mbinu tata kuifunga midomo na fikra zetu..huku wao waki advansi kwa kasi kufikia malengo yao.
Demokrasia sahihi inayosimamia maendeleo ya kweli ..imejengwa na kubeba nguvu sahihi. Inajua shina la ustawi wa mwanadamu na kulienzi kwenye kila nyanja…na haioni tatizo nguvu kutumika kwani nguvu sahihi si adui wa mwanadamu kamili na chochote ila hili litapingwa na wapinga Utu na ubinaadamu. Na sisi hatutawaelewa kabisa…
Kwenye demokrasia ya nguvu sahihi ya utu na ubinaadamu ni sahihi kutumia nguvu sahihi na kuibebesha silaha, mabomu, vifaru, majeshi…ili kuilinda jamii ya binaadamu timamu waliostaarabika. Na ninaongea hivi kwa ujasiri mkubwa usio na ujeuri, chuki, woga, ila kwa upendo na heshima kuu kwa watu wote.
Lakini kwenye demokrasia pinzani kwa utu na ubinaadamu, nilichosema kitakuwa ni tatizo lakini wao watataka kutumia silaha za kivita, majeshi, na nguvu zote za dola ili kilinda nguvu isiyo sahihi ya ufisadi. Hili halikubaliki kamwe!!!
Kwa hiyo tusiwe wajinga; Vita, mabomu ya nuklia, silaha mbalimbali, majeshi, usalama wa taifa na nyenzo kama hizo zenyewe sio tatizo. SHIDA NI NGUVU GANI VITABEBESHWA VYOMBO HIVYO! ..Kisu cha mkate ..kinaweza kutumika kwa ubaya au kwa uzuri..hilo lieleweke…hii ni pamoja na dhana ya kumwaga damu... Damu kumwagiga si tatizo inategemea unafanya hivyo kwa ajili ya nguvu ipi!!! Mwaka 1978 Tanazania kwa kutumia nguvu sahihi ilimwga damu kule kagera na hatimaye uganda! ...Hoja ni Nguvu gani inabeba hiyo vita na malengo yake...nk lakini tusiogopeshani juu ya kumwaga damu. Jambazi akavamia nyumba yangu usiku wa manane na kuanz akusogelea chumba cha mabinti ..wangu..ohh Nitamwaga damu!! Ili kulinda heshma na ubinnadamu na ustaarabu wa familia na dunia yote!!
Chadema, CCM, TLP, nk…ni vyombo vya kuilinda na kuitetea nguvu stahili katika kujenga na kustawisha jamii. Kama chama chochote kitakiuka misiningi hiyo ..nguvu sahihihi itatumika kukihoji tena bila woga , hasira, chuki, na aina yeyote ya nguvu isiyo sahihi…ikibidi hata kutumia chochote, ..ili mradi chochote hicho kibebe nguvu sahihi. Chama hicho kisitegemee tutakuwa magoigoi na wanyonge..kukikabili la hasha tutakihoji. Lazima hili nilieleze kwa upendo, ujasiri na kuuheshimu utu wangu na watanzania wote kuwa..Lazima kitafuatwa kwa nguvu ..tena nguvu kabisa..na kitahojiwa ..vipi hakilindi uasili na ustawi wa mwanadam. Haitawezekana tena kututishia vita, kupoteza amani nk. Kama amani ikipotea kwa ajili ya nguvu sahihi ..hakuna tatizo lolote... kwani kusema kweli amani na utulivu huo havikuwepo!
JF..inahaki kutumia nguvu sahihi kuhoji na kulinda utu na ubinaadamu wa jamii inayojikuta. Hili ni sahihi kwa blog na mitandao yote nchini. Technologia na watu wake sio tatizo..tatizo ni inabebeshwa nini….
Utu na ubinaadamu sio mali ya mtu au chama chochote useme itafungiwa na kuangamizwa. Kuangamiza nguvu sahihi kwenye jamii..ina maana kuangamiza watu wote kwnye jamii hiyo na hilo haliwezekani. Hakuna anayeweza kuangamiza nguvu sahihi. Mtu asije kudanganywa na kudanganyika….
Kama JF na wanachama wake ni watii wa Utu na ubinaadamu wao ..na wametumia nguvu sahihi katika kauli, fikra na matendo yao na JF ikafungiwa ..sawa… Ni kwa kuwa ujumbe na lengo la JF litakuwa limefika..na hakuna atakaye jinsikia mkosaji.
Kama JF italazimika kutumia nguvu isiyo sahihi kama woga, wasiwasi, kuupinga na kuusaliti utu wa jamii yake nk ili isifungiwe ..hiyo sio sawa..bora ifungiwe kuliko itumike kustawisha nguvu isiyo sahihi kwenye jamii.
Si kweli kuwa kuna mamlaka ya kibinaadamu inayoweza kufumgia nguvu ya utu inayotegeneza nguvu ya umma iliyosheheni nguvu sahihi..nguvu ya umma. Hamuoni ..viti 22 mjengoni…Hamuoni..toka 80% mwaka 2005 hadi 61% mwaka 2010..Ni bilioni ngapi zilitumika kuhonga na kuyumbisha matokeo..? Hakuna!! Ni mwanzo wa nguvu sahihi kuiteka na kuirudisha Tanzania ile ya waasisi wake!! Peoples power.
Mamlaka yenye ufinyu wa kufikiri kuwa nguvu sahihi ya umma unafungika au kuangamizwa..malaka hiyo itakuwa imepofuka na ni dhaifu ..itaangamia.
Tuamke tutumie nguvu sahihi..kulijenga Taifa letu! Ikibidi hata kulifia kwenye misingi sahihi kwani huo ndio uzalendo..na utanzania wenyewe..
Na tunamuomba Mungu atubariki katika ujenzi wa Taifa hili!!
Follow Us Here