Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kikwete: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar

    Report Post
    Results 1 to 15 of 15
    1. #1
      Zawadi Ngoda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th August 2009
      Posts : 1,792
      Rep Power : 855
      Likes Received
      98
      Likes Given
      98

      Default Kikwete: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar

      Mbio za muungano zilifikia kilele chake pale JK alipoamua kuuvulia njugaMuungano, na kuahidi kuupatia ufumbuzi wa kisiasa. Muungano ulijengwa na JK(Kambarage) na kusua sua bila mafanikio, na ukatafutiwa ufumbuzi na JK (Kikwete). Maraisi wote waliopita hawakuisha kuwaita wadai haki zao kuwa ni wahuni.

      Mwaka 2000 mara baada ya uchaguzi mkuu Wazanzibari zaidi ya 200 waliuliwa na bunduki na helkopta zilizonunuliwa kwa fedha ya walipa kodi, kwa amri ya Mkapa. Na wote waliouwawa aliwaita wahuni, huku akimtafuta muhuni mkuu, Sheikh Sharif na Prof Lipumba. Na baada ya muda si mrefu nao wakashikwa na kutiwa ndani. Kwa upande wangu huo ndio ulikuwa mwisho wa demokrasia, na mwanzo wa udikteta. Hata wale aliyewauwa Mwebechai nao walikuwa wahuni tu, na sheikh ponda ndio kiongozi wa wahuni. Ilionekana kana kwamba Mkapa alikuwa Rais wa wananchi wahuni nchi nzima.

      JK wakati huo akiwa katika serikali ya Mkapa, na kwa ujumla alikuwepo ktk serikali zote zilizopita, aliyaona mapungufu yaliyosababisha matatizo hususan, Zanzibar. Na ndio maana alipoingia madarakani miaka mitano iliyopita alikuwa ni Raisi wa kwanza kukiri kuwa Zanzibar kuna mpasuko wa kisiasa. Kauli hii ilifurahiwa na wengi, na kuandikwa karibu katika magazeti yote TZ. Kwani kuutatua mgogoro wa zaidi ya miaka 40, si lelemama.

      Baada ya miaka takriban mitano toka aingia madarakani, yaonyesha dalili nzuri ya kutimizwa kwa ahadi yake. Siri kubwa ya kufanikiwa katika kutatua tatizo hilo, ni kuwaachia Wazanzibar wenyewe kuwa wachezaji wakuu, naye ni kam,a mtazamaji na mshauri. Viongozi wa Zanzibar wakaamua Serikali ya mseto, na baadae suala likatupwa kwa wananchi kupitia kura ya maoni, 66% wakapitisha pendekezo. Na baada ya hapo ikahitajika kufanyiwa marekebisho katika katiba, nayo yakapitishwa kwa kishindo na Baraza la wawakilishi. Kwa kipindi hiki chote hakuuwawa hata mtu mmoja, kana kwamba wahuni waliondoka alipostaafu Mkapa.

      Kilichonishangaza mimi ni kuwaona wasomi, wanasheria, magazeti na hata hapa JamiiForums, kupiga kelele sana hasa pale Katiba ilipoguswa. Na wengine kukiita kitendi hicho kama ni cha Kihaini, na hoja hiyo ikaungwa mkono na Watanganyika wengi tu. Sasa najiuliza wataundaje serikali ya mseto bila kugusa katiba? Au JK alipoonyesha dhamira ya kutatua mgogoro wa kisiasa Zanzibar walielewa nini? Au kulikuwa na mpaka katika ufumbuzi huo? Kama kulikuwa na mpaka ni nani aliouweka huo mpaka? N i maswali ambayo kila siku najiuliza toka kura ya maoni ipigwe na katiba kupitishwa bila majibu. Na ninapokaribia kupata jibu, basi ni jibu gumu sana, kuwa hawa watu ni watu wa shari hawataki amani.

      Na kama hivyo ndivyo, basi kundi hili liwe NGO au la kidini ndilo lililokuwa likifaidika na Muungano kwa njia moja au nyingine. Ninasikitika kusema kuwa kundi hili halina nafasi katika Tanzania ya sasa, na si tu kuwa limepotea njia bali litakufa kifo kibaya. Sioni haja yeyote ile ya kuulinda Muungano au kipengele cha katiba hata kwa kuuwa wananchi kwa kutumia madaraka vibaya. Vikundi kama hivi havifai kabisa katika jamii, na popote tunapokutana navyo ni lazima tuvionye na kuvitokomeza.

      Ninapigwa na bumbuwazi zaidi pale ambapo hoja zinazotolewa ni za kulaumu tu. Ningefurahi kama wangekuja na maelezo makini juu ya mapendekezo ya utatuaji wa mgogoro huo. Bado mnayonafasi ya kutoa hoja zenu, ni vipi mlihitaji mgogoro huo utatuliwe ili wananchi wa pande zote mbili zinazohusika huko Zanzibar wakarithika nazo. Msipoweza kutoa hoja basi malalamiko yenu hayana msingi kabisa.

      Lazima ikumbukwe kuwa polisi waliokuwa wanatumwa Zanzibar, ni makomandoo wa jeshi waliokuwa mafunzoni wakvishwa mavazi ya polisi. Watu hawa hawakujifunza kutuliza ghasia, bali kuuwa na hivyo ndivyo walivyofanya huko Zanzibar. Si hivyo tu bali vile vile wali wabaka watoto wa kike mbele ya wazazi wao. Kweli tuko tayari kuulunda muungano kwa dhamani hii? Hapana hii si Tanzania bali ni SOWETO. Hata mkinukuu maneno ya mwalimu ya mwaka 1964, bado si tiketi ya kuulinda muungano kwa dhamani hii.

      Hapa alipofikia Kikwete anahitaji pongezi, kwa hali yeyote ile si rahisi kuutatua mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 40 kwa amani kama tulivyoshuhudia. Hii ni sawa kama Rais Obama akafanikiwa kuutatua mgogoro wa Israel- Palestina. Ni nini anachoweza kupewa zaidi ya zawadi ya Nobel. Tumsifu JK kwa hapa alipotufikisha, na tuelewe kuwa ukuzaji wa uchumi unategemea sana amani ya nchi. Hongera Kikwete!!

    2. Miaka 50

    3. #2
      takashi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2009
      Posts : 787
      Rep Power : 673
      Likes Received
      139
      Likes Given
      779

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      @Zawadi NGODA Asante sana kwa kutuwekea "article " hii nzuri.

      Kwa muda mrefu hapa katika JF kumekuwa na mawazo ya wengi kuiona Zanzibar ni kama kitu kinacho kera au kero. Watu wengi wanashindwa kuelewa historia ya Zanzibar na Muungano. Mawazo ya wengi hapa ni kuiona Zanzibar kama sehemu ya Tanzania kwa maana ya Tanganyika. Kwahiyo ,wanashangaa kuano Wazanzibari kulalamika na kuujadili Muungano. Kwa mtazamo wangu mimi tatizo la MAPASUKO wa kisiasa Zanzibar limesababishwa na CCM. kwa kuwanyima wazanzibari demkrasia ya kweli. kuwanyima haki ya kuchagua viongozi wanao wataka wenyewe.

      Hii imesababisha wengi wa Wazanzibari kuanza kuuchukia Muungano kwasababu ya kuona ni kama kipingamizi cha maendeleo yao. CUF ilishinda chaguzi zote zilizofanyika tokea kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa. Kwanini CUF hawakupewa nafasi ya kuongoza? hofu ya CCM ilikua ni kwamba CUF walionekana kama ni chama cha kupinga Muungano. Kwanini watu waupinge Muungano? Sasa hapa ndio linakuja suala zima la utata wa siasa ndani ya Zanzibar.

      Kila Mtanzania anaamini au anakubali kuwa Muungano una kasoro, lakini wengi wetu hatuko tayari kukaa na kujadili kasoro na kutafutiwa ufumbuzi. Tuko tayari kulaumu na kuwaona wanaolalamika kama wanaleta kero,hata kama sababu wanayo.

      Utulivu wa kisiasa uliopa Zanzibar ni mchango mkubwa wa MH, Rais Kikwete.

    4. #3
      Solomon David's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st March 2009
      Posts : 1,146
      Rep Power : 755
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      Hongera sana Mheshimiwa Kikwete

      Tanzania inaongozwa na raisi dikteta..... Kikwete ameiba kura ili kuitawala Tanzania kimabavu

    5. #4
      Boramaisha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2009
      Posts : 826
      Rep Power : 681
      Likes Received
      5
      Likes Given
      0

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      Si kweli! Pelekeni credit kunakohusika. Mwenyekiti wa CCM alishindwa kabisa kushughulikia suala la Zanzibar hadi Karume na Seif Shariff walipoamua kuketi na kukubaliana uwepo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Hilo halikutokana na vikao vya CCM vilivyokuwa vikiongozwa na JK.

    6. #5
      Mtu wa Pwani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th December 2006
      Posts : 4,250
      Rep Power : 1491
      Likes Received
      159
      Likes Given
      147

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      jee wakati wa mkapa aliweza kuwa karibu na wapinzani kama mwere? huyu jamaa kwa kweli mie nna mpa salute

      nnamkubali
      Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      LeopoldByongje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th April 2008
      Posts : 374
      Rep Power : 639
      Likes Received
      8
      Likes Given
      9

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      Sana sana kilichofanyika ni mafuta yanayochemka kuyatia maji. Mnategemea nini zaidi ya moto kulipuka na kuwaunguza wenyewe. Mie si Shekhe Yahaya Husein, Lakini mtu mwenye akili zake ahitaji manabii au waganguzi kuliona hilo. Katiba ya JMT imevunjwa ni ukweli.

    9. #7
      Msanii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th July 2007
      Posts : 6,207
      Rep Power : 1926
      Likes Received
      210
      Likes Given
      249

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      Aliye ndani ya box haoni nje mpaka atoke
      " If you hear a voice within you say "you cannot paint", then by all means paint, and that voice will be silenced"
      [email protected]

    10. #8
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,820
      Rep Power : 2967
      Likes Received
      2425
      Likes Given
      3501

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      ..matatizo ya kisiasa Zenj yanawahusu wa-Zenj wenyewe.

      ..hakuna Mtanganyika mwenye "muarubaini" wa kuyatatua matatizo hayo.

      ..nawapongeza wa-Zenj,kupitia viongozi wao, Karume na Maalim Seif,kwa kuachana na ile dhana kwamba Tanganyika itawafanyia kila kitu, ikiwemo kuwasuluhisha ktk migogoro yao ya kisiasa.

      ..wa-Zenj wajiandae kuhakikisha kwamba serikali ya mseto waliyoazimia kuiunda inafanya kazi bila matatizo kwa manufaa ya wananchi wa visiwa hivyo.

    11. #9
      Mtu wa Pwani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th December 2006
      Posts : 4,250
      Rep Power : 1491
      Likes Received
      159
      Likes Given
      147

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar

      Mie nilidhani kuwa hivi sasa kuna mgogoro baada ya maridhiano na tegemeo la kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa GNU

      Nnaamini kwa sasa wazanzibari wako makini sana na wamejipanga. nnataraji baada ya uchaguzi tanzania kutakuwa na mambo mazito.

      Nnataraji muundo wa muungano utabadilika, maana wazanzibari kwa ujumla sasa wameelekeza macho yao kwenye muungano, wanaamini kuwa wamepoteza dola yao na kuwa wilaya na wao hawako tayari kwa hilo

      Zanzibar inahitaji nguvu zake kamili na hawakao tayari kuona hali hii inayoendelea ya kugandamizwa na kuonewa au kufananishwa na mkoa au wilaya inakoma.

      Wao wako tayari kwa mazungumzo tena ya wazi juu ya muund wa muungano na hata ikibidi tanganyika wawe na serikali yao au muuungano uwe basi

      Japo la muuungano kuwa basi mimi siliungi mkono maaana nna mtoto wa kinyamwezi na tushazaa sasa sitaki damu yangu ipotee
      Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown

    12. #10
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Re: Kikwete: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar

      Inachekesha sana naposikia watu wakitumia CCM kama ni chama cha Bara na CUF ni chama cha visiwani. Ni aibu iliyoje kwa Mzanzibar kusema kwamba Zanzibar hawana uwezo wa kuchagua viongozi wao hali viongozi wote wanaoshiriki ktk bunge, serikali na utawala wa Zanzibar ni Wazanzibar wenyewe. Yawezekana kuwa hawakuchaguliwa na wananchi lakini bado ni Wazanzibar wakiongozwa na baraza la Mapinduzi..

      Wachezaji wakuu wa serikali ya Zanzibar ni Wazanzibar wenyewe, hilo lifahamike kwani baraza la Mapinduzi sio baraza liloundwa na bara wala watu wenye asili ya Bara isipokuwa ni Wazanzibar (watawala). Kwa jambo lolote lile linalotokea Zanzibar limetokana na baraza la Mapinduzi ambao muda wote wamekuwa wakifikiria maslahi ya Zaanzibar kwa manufaa ya baraza hilo.

      Hawa ndio waisopenda kuona CUF wakishika madaraka ya kuongoza Zanzibar lakini kwa ujinga wa baadhi wachache, lawama zote zinawafuata Bara hali ukitazama kwa makini tatizo lopo visiwani kwenyewe. Huwezi kumweka Salmin Amoor na Seif Shariff Hamad meza moja wakajadiliana kwa usalama na kwa manufaa ya Wazanzibar. Na ndio maana halisi ya maneno ya JK kwamba - Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      Huo mpasuiko hauhusiani na Bara kisiasa hata kidogo isipokuwa wananchi wamepandikizwa hofu ya bara kutoa maamuzi yanayohusiana na Visiwani pasipo kufahamishwa ukweli kwamba ni baraza la Mapinduzi ndilo linaloweka masharti ya maamuzi yote ya kitaifa kuhusiana na Zanzibar.

      Hata huu mufaka uliopita baina ya CUF na CCM umepitia hatua za suluhu kwa kuwahusisha Wazanzibar wenyewe. yaani ni Wazanzibzr wenyewe wamefikia maamuzi ya kuweka kando tofauti zao na kuunda umoja wao..Kwa mara ya kwanza Karume (CCM) na Seif wa (CUF) wamekaa meza moja na kufikia maamuzi ambayo hawakuwahi kuyafanya miaka ya nyuma, hatua ambayo inatakiwa kupongezwa wahusika wake yaani Karume na Seif na sii Kikwete au serikali ya Muungano.

      Bara hawakuhusika na wala haikuwepo sababu ya wao kuhusika isipokuwa tu ktk maamuzi yaliyofikiwa ambayo ni kinyume cha katiba ya nchi Zanzibar na serikali ya Muungano. Kama wananchi WaZanzibar watakichagua chama cha CUF kuongoza nchi yao basi hakuna sababu ya kuwa na serikali ya Mseto. CUF wameshinda wameshinda wapewe Uongozi wa nchi na sio kuwahadaa wananchi na hili neno - Serikali ya Mseto ambalo linawahakikishia CCM visiwani (baraza la Mapinduzi) kuendelea kuongozi Zanzibar hata kama wameshindwa uchaguzi mkuu.

      Kilichofanyika ni kwamba Wananchi wa Zanzibar wamepigwa changa la macho, ktk kuwahakikishia WaZanzibar kwamba CUF haitaweza kuongoza nchi hiyo hata siku moja pasipo kuangaliwa na baraza la Mapinduzi. Yawezekana ni njia bora zaidi kwa leo lakini tofauti na maamuzi kama haya, chama Chadema kinapendekeza zaidi utawala wa Zanzibar kuendeshwa na chama kilichoshinda. Chama kilichochaguliwa na wananchi wake kwa ushindi wa kura nyingi ndicho kitakacho ongoza Zanzibar na sii kuunda serikali ya mseto kabla hata ya uchaguzi mkuu kufanyika huku kukiwa na dalili kubwa ya CCM kushindwa vibaya uchaguzi huu. Maamuzi haya ya kuunda serikali ya mseto ni kuwahahakikishia CCM kuendelea kuongoza hata kama wameshindwa uchaguzi...
      Exploration of reality

    13. #11
      Nyunyu's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 9th March 2009
      Location : Here.
      Posts : 3,349
      Rep Power : 2044
      Likes Received
      465
      Likes Given
      2749

      Default Re: Kikwete: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar

      Ya Ngoswe ataachiwa Ngoswe daima!!
      There is no such a thing as part freedom- Nelson Mandela

      e-mail: [email protected]

    14. #12
      Masanilo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2007
      Location : Swat valley, Keta Keta
      Posts : 19,059
      Rep Power : 5467
      Likes Received
      3486
      Likes Given
      1900

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      Quote By Mtu wa Pwani
      jee wakati wa mkapa aliweza kuwa karibu na wapinzani kama mwere? huyu jamaa kwa kweli mie nna mpa salute

      nnamkubali
      Nenda kanywe naye chai na yale mambo yenu mengine!

      Kindness is the language which the deaf can hear and the blind can see - Mark Twain
      CCM is enemy of GOD

    15. #13
      Mtu wa Pwani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th December 2006
      Posts : 4,250
      Rep Power : 1491
      Likes Received
      159
      Likes Given
      147

      Default Re: Kikwete: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar

      Quote By Mkandara
      Inachekesha sana naposikia watu wakitumia CCM kama ni chama cha Bara na CUF ni chama cha visiwani. Ni aibu iliyoje kwa Mzanzibar kusema kwamba Zanzibar hawana uwezo wa kuchagua viongozi wao hali viongozi wote wanaoshiriki ktk bunge, serikali na utawala wa Zanzibar ni Wazanzibar wenyewe. Yawezekana kuwa hawakuchaguliwa na wananchi lakini bado ni Wazanzibar wakiongozwa na baraza la Mapinduzi..

      Wachezaji wakuu wa serikali ya Zanzibar ni Wazanzibar wenyewe, hilo lifahamike kwani baraza la Mapinduzi sio baraza liloundwa na bara wala watu wenye asili ya Bara isipokuwa ni Wazanzibar (watawala). Kwa jambo lolote lile linalotokea Zanzibar limetokana na baraza la Mapinduzi ambao muda wote wamekuwa wakifikiria maslahi ya Zaanzibar kwa manufaa ya baraza hilo.

      Hawa ndio waisopenda kuona CUF wakishika madaraka ya kuongoza Zanzibar lakini kwa ujinga wa baadhi wachache, lawama zote zinawafuata Bara hali ukitazama kwa makini tatizo lopo visiwani kwenyewe. Huwezi kumweka Salmin Amoor na Seif Shariff Hamad meza moja wakajadiliana kwa usalama na kwa manufaa ya Wazanzibar. Na ndio maana halisi ya maneno ya JK kwamba - Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      Huo mpasuiko hauhusiani na Bara kisiasa hata kidogo isipokuwa wananchi wamepandikizwa hofu ya bara kutoa maamuzi yanayohusiana na Visiwani pasipo kufahamishwa ukweli kwamba ni baraza la Mapinduzi ndilo linaloweka masharti ya maamuzi yote ya kitaifa kuhusiana na Zanzibar.

      Hata huu mufaka uliopita baina ya CUF na CCM umepitia hatua za suluhu kwa kuwahusisha Wazanzibar wenyewe. yaani ni Wazanzibzr wenyewe wamefikia maamuzi ya kuweka kando tofauti zao na kuunda umoja wao..Kwa mara ya kwanza Karume (CCM) na Seif wa (CUF) wamekaa meza moja na kufikia maamuzi ambayo hawakuwahi kuyafanya miaka ya nyuma, hatua ambayo inatakiwa kupongezwa wahusika wake yaani Karume na Seif na sii Kikwete au serikali ya Muungano.

      Bara hawakuhusika na wala haikuwepo sababu ya wao kuhusika isipokuwa tu ktk maamuzi yaliyofikiwa ambayo ni kinyume cha katiba ya nchi Zanzibar na serikali ya Muungano. Kama wananchi WaZanzibar watakichagua chama cha CUF kuongoza nchi yao basi hakuna sababu ya kuwa na serikali ya Mseto. CUF wameshinda wameshinda wapewe Uongozi wa nchi na sio kuwahadaa wananchi na hili neno - Serikali ya Mseto ambalo linawahakikishia CCM visiwani (baraza la Mapinduzi) kuendelea kuongozi Zanzibar hata kama wameshindwa uchaguzi mkuu.

      Kilichofanyika ni kwamba Wananchi wa Zanzibar wamepigwa changa la macho, ktk kuwahakikishia WaZanzibar kwamba CUF haitaweza kuongoza nchi hiyo hata siku moja pasipo kuangaliwa na baraza la Mapinduzi. Yawezekana ni njia bora zaidi kwa leo lakini tofauti na maamuzi kama haya, chama Chadema kinapendekeza zaidi utawala wa Zanzibar kuendeshwa na chama kilichoshinda. Chama kilichochaguliwa na wananchi wake kwa ushindi wa kura nyingi ndicho kitakacho ongoza Zanzibar na sii kuunda serikali ya mseto kabla hata ya uchaguzi mkuu kufanyika huku kukiwa na dalili kubwa ya CCM kushindwa vibaya uchaguzi huu. Maamuzi haya ya kuunda serikali ya mseto ni kuwahahakikishia CCM kuendelea kuongoza hata kama wameshindwa uchaguzi...

      ww mjanja sana, hivi unataka kutufanya sisi hatuelewi kuwa bara ndio wanaosababisha migogoro kule zanzibar?

      wao si ndio wako nyuma ya baraza la mapinduzi? wao si ndio wanaolazimisha nani na nani awemo ndani ya baraza la mapinduzi, na nini kiamuliwe?

      wazanzibari chini ya rais Jumbe walipotaka serikali tatu waliopinga walikuwa wazanzibari? waliomuondosha madarakani kwenye kikao kilichafanyika CBE dodoma walikuwa wazanzibari?

      wanaowasaidia CCM zanzibar kuiba kura kwa kuleta mamluki walikuwa ni wazanzibari?

      mm naaamini hata huku wazanzibar kukamatana kwao, wabara wakiona itakuwa hatari sana watajiotahidi kupenya kufitinisha.


      nnachokiamini wazanzibari wakikamatana na kushikana wabara hawatakuwa na pa kupenyea, maana walikuwa wakitumia migogoro na kutokuwepo maelewano baina ya wazanzibari kama njia ya kuimeza na kuimaliza zanzibar


      sasa kumekucha tujiandae kumuona mzanzibar akiamka kutoka usingizini na kudai haki zake bila ya kumuonea mtanganyika

      nataka ile tu daraja yangu

      sitaki nyengine kama wenzangu

      siiinui mikono kushika mbingu
      Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown

    16. #14
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Re: Kikwete: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar

      Quote By Mtu wa Pwani
      ww mjanja sana, hivi unataka kutufanya sisi hatuelewi kuwa bara ndio wanaosababisha migogoro kule zanzibar?

      wao si ndio wako nyuma ya baraza la mapinduzi? wao si ndio wanaolazimisha nani na nani awemo ndani ya baraza la mapinduzi, na nini kiamuliwe?

      wazanzibari chini ya rais Jumbe walipotaka serikali tatu waliopinga walikuwa wazanzibari? waliomuondosha madarakani kwenye kikao kilichafanyika CBE dodoma walikuwa wazanzibari?

      wanaowasaidia CCM zanzibar kuiba kura kwa kuleta mamluki walikuwa ni wazanzibari?

      mm naaamini hata huku wazanzibar kukamatana kwao, wabara wakiona itakuwa hatari sana watajiotahidi kupenya kufitinisha.


      nnachokiamini wazanzibari wakikamatana na kushikana wabara hawatakuwa na pa kupenyea, maana walikuwa wakitumia migogoro na kutokuwepo maelewano baina ya wazanzibari kama njia ya kuimeza na kuimaliza zanzibar


      sasa kumekucha tujiandae kumuona mzanzibar akiamka kutoka usingizini na kudai haki zake bila ya kumuonea mtanganyika

      nataka ile tu daraja yangu

      sitaki nyengine kama wenzangu

      siiinui mikono kushika mbingu
      Hapana mkuu wangu mimi siii mjanja kwa aina yeyote ile isipokuwa nazungumzia historia ya na Ukweli usopenda kuukubali.
      Umezungumzia wakati Jumbe akitaka serikali tatu kama ni Wazanzibar waliopinga.. Jibu ni Wazanzibar ndio kwani ktk kina cha mwisho wa matatizo haya rais aliyekuwa madarakani sii alikuwa Mwinyi? Na Mwinyi ndiye alimfuata Nyerere na kumwomba msaada wake kuhusiana na hoja ya serikali Tatu. Na nani aliyekwenda kuwatonya CCM kuhusu Jumbe kama sii mwingine ila huyo Seif Shariff Hamad - Mzanzibar! Kwa hiyo ukweli unabakia kwamba hizi habari za bara kuhusika ni mazingaombwe tu mnayolishwa ili viongozi hao wa Mapinduzi wabakie madarakani lakini pamoja na yote hayo hamjachelewa.

      La kufanya jaribuni kuwaondoa hao viongozi toka baraza la Mapinduzi ktk uongozi wa Zanzibar (kwa kura zenu) kisha utanambia mbaya wako nani! Au umesahau majuzi tu Karume alitaka kuwarudisha Wangazija woote warudi Comoro kwa sababu ndio wapinzani wa hili baraza la Mapinduzi na wengi wao ni wanachama wa CUF.

      Huu ndio ukweli mkuu wangu pamoja na matatizo yoote ya Bara, hata siku moja Bara haiwezi kuingilia maslahi ya Visiwani pasipo baraka la baraza hilo ambalo ndilo lilimkataa Salim A. Salim kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano.. Na ombi lao likatimia, Nyerere asifanye kitu.
      Last edited by Mkandara; 3rd September 2010 at 05:24.
      Exploration of reality

    17. #15
      takashi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2009
      Posts : 787
      Rep Power : 673
      Likes Received
      139
      Likes Given
      779

      Default Re: JK: Kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

      Quote By Boramaisha
      Si kweli! Pelekeni credit kunakohusika. Mwenyekiti wa CCM alishindwa kabisa kushughulikia suala la Zanzibar hadi Karume na Seif Shariff walipoamua kuketi na kukubaliana uwepo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Hilo halikutokana na vikao vya CCM vilivyokuwa vikiongozwa na JK.
      wewe uliyowasikia hewani ni hao watu wawili....Maalim Seif na MH,Karume. Lakini kwa maelezo ya Maalim mwenyewe makubaliano yalianza mabali kabla ya hao watu wawili kukutana ikulu Zanzibar. Mkutano wa Ikulu Zanzibar ulikua ni kuhitimisha tu kilicho afikiwa. Karume alipewa go ahead na JK na hii haikutokana na vikao vya CCM. Kwani hiyo ilikua ni adhma ya JK kuhakikisha amani na utulivu inapatikana Zanzibar. Ndani ya CCM kuna watu ambao hawajapendezwa na maridhiano yaliyo fikiwa...Mh,Kikwete anastahili pengezi .

    Similar Topics

    1. Isingekuwa ni muungano, hali ya kiuchumi na kisiasa zanzibar ingekuwaje?
      By Gosbertgoodluck in forum Business & Economic Forum
      Replies: 71
      Last Post: 22nd February 2011, 23:26
    2. Askofu Kulola: Kuna mtandao wa kisiasa makanisani
      By MziziMkavu in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 145
      Last Post: 24th October 2010, 12:15
    3. Kikwete ahaha kunusuru mpasuko CCM
      By Smiles in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 13
      Last Post: 26th August 2010, 11:31
    4. Kura ya maoni zanzibar na muelekeo mpya wa kisiasa tanzania
      By Fungu la kukosa in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 2nd August 2010, 14:20
    5. Sera ya Majimbo, Dawa ya Mpasuko wa Zanzibar-Mbowe
      By Asha Abdala in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 10
      Last Post: 11th June 2008, 09:03

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...