Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ilani ya CHADEMA 2010-2015

    Report Post
    Page 1 of 9 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 169
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,518
      Rep Power : 46714
      Likes Received
      16434
      Likes Given
      8469

      Default Ilani ya CHADEMA 2010-2015

      Huwa sishtuliwi na mambo mengi ya kisiasa; lakini kama nilichokiona kwa macho yangu ndicho kitakachokuwepo kwenye Ilani ya Chadema basi naweza kusema tu kuwa ni ya "kuthubutu, inatisha na inawaweka CCM pabaya". Kama ndiyo hiyo, basi itabidi CCM warudi darasani kuandika Ilani yao upya maana kama watu watapigia kura Ilani.. basi mtanange huu wa demokrasia 'UNOGILE".

      Mwaka huu watu watapigia kura sura au watapigia sera!


      UPDATE:

      Download ILANI YA CHADEMA 2010 - 2015 kwa kubonyeza hapa
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Junius's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th March 2009
      Posts : 3,117
      Rep Power : 1143
      Likes Received
      47
      Likes Given
      12

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      ...kama watu watapigia kura Ilani..
      Shida yenyewe ipo hapa!
      HAKI SAWA KWA WOTE

      If you don't up set at least one person, you are not doing it right (whatever "it" might be).

      [email protected]

    4. #3
      Nyani Ngabu's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 15th May 2006
      Location : Ikungulyabashashi
      Posts : 39,263
      Rep Power : 36770
      Likes Received
      9630
      Likes Given
      686

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Aaah Mwanakijiji umeanza ku ballyhoo kama ilivyo kawaida yako.....
      Miafrika Ndivyo Tulivyo.

    5. #4
      X-PASTER's Avatar
      Super Moderator Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Firdaws (Paradise)
      Posts : 11,861
      Rep Power : 7688
      Likes Received
      1467
      Likes Given
      0

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      “I am the punishment of God... If you had not committed great sins, God would not have sent a punishment like me upon you.”

      'O Allah! Keep me alive as long as life is better for me, and let me die if death is better for me.

      (¯`·._.•X-Paster™•._.·´¯)


    6. #5
      Lukolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Location : Iringa
      Posts : 3,881
      Rep Power : 7038
      Likes Received
      2047
      Likes Given
      1573

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Changamoto kubwa ipo kwenye uelewa wa watanzania walio wengi juu ya hayo mambo ya ilani na sera za chama. Wananchi wengi hawajui hizi habari, wanachojali wamepata tshirt, khanga na kofia za kijani basi hicho ndo cha maana kwao. Pamoja na ilani hizo nzuri, hakikisheni kwamba na nyie mwaka huu mnawekeza vya kutosha kwenye mabango, tshirt, kofia na khanga. Hayo ndo mambo ya msingi zaidi kwa wananchi wa vijijini.

      Kwa namna moja au nyingine ni vema mkatambua ukweli kwamba mtaji mkubwa wa CCM ni umaskini na ujinga wa watanzania. Ndiyo maana CCM haitakaa ifanye jitihada ya kumaliza umaskini nchini wala jitihada za kupunguza umaskini kwa kuwa hali hiyo ndiyo inayowafanya wao waendelee kutawala. Wanatumia ujinga wa watanzania kuelekeza chuki kwa vyama vya upinzani kwamba ni vyama vya kuleta vita. Wananchi wa kawaida wanaohofia vita hawawezi kukubali kuchagua chama kitakacholeta vita. Kunahitajika elimu na strategy zaidi kuliko sera pekee. Take care.
      Godlisten shoo likes this.
      Mtaji mkubwa kabisa wa CCM katika chaguzi zake ni umaskini na ujinga wa watanzania. CCM haitafanya kosa la kuyamaliza matatizo hayo kwa kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wamehatarisha nafasi yao ya kuendelea kutawala

    7. Miaka 50

    8. #6
      WA MAMNDENII's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th June 2010
      Location : mamndeni
      Posts : 245
      Rep Power : 504
      Likes Received
      16
      Likes Given
      8

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      chadema oyee! sisiemu ziiii!

    9. #7
      Anfaal's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2010
      Posts : 1,157
      Rep Power : 723
      Likes Received
      102
      Likes Given
      35

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Huwa sishtuliwi na mambo mengi ya kisiasa; lakini kama nilichokiona kwa macho yangu ndicho kitakachokuwepo kwenye Ilani ya Chadema basi naweza kusema tu kuwa ni ya "kuthubutu, inatisha na inawaweka CCM pabaya". Kama ndiyo hiyo, basi itabidi CCM warudi darasani kuandika Ilani yao upya maana kama watu watapigia kura Ilani.. basi mtanange huu wa demokrasia 'UNOGILE".

      Mwaka huu watu watapigia kura sura au watapigia sera!
      Mwanakijiji unaenda mbali saana kwa kuwaza Ilani.

      Kamwe nchi hii, ilani haitaiangusha CCM. Leo hii tuulizane hapa hata kabla yakufika kule vijijini, ni nani aliisoma Ilani ya CCM ya 2005 na nani anaweza kuizungumzia utekelezaji wake! Jibu ni kuwa utashangaa saana. Wengi kati yetu tunapenda kusoma mistari miwili na kufunika na hao ndio tunajiita wasomi. Sasa, vipi kuhusu wanakijiji?

      Matatizo ni makubwa saana katika kujisomea kwa Taifa letu na ndio maana hata umakini hakuna. Tena basi si kusoma tu hata kuandika. Jipe fursa upitie hata magazeti yetu utashangaa.

      Kwahiyo binafsi naona CCM itaondoka madarakani kwa njia za kupayuka tu na kuzungumza na wananchi zaidi juu ya haki zao bila hata ya kuwaeleza ilani inasema nini!

    10. #8
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,625
      Rep Power : 2894
      Likes Received
      3845
      Likes Given
      12250

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      It is about time. Nchi inahitaji mtikisiko! Nafurahi pia Cheche zinarudi mtaani.

    11. #9
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7663
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Quote By Anfaal
      Mwanakijiji unaenda mbali saana kwa kuwaza Ilani.

      Kamwe nchi hii, ilani haitaiangusha CCM. Leo hii tuulizane hapa hata kabla yakufika kule vijijini, ni nani aliisoma Ilani ya CCM ya 2005 na nani anaweza kuizungumzia utekelezaji wake! Jibu ni kuwa utashangaa saana. Wengi kati yetu tunapenda kusoma mistari miwili na kufunika na hao ndio tunajiita wasomi. Sasa, vipi kuhusu wanakijiji?

      Matatizo ni makubwa saana katika kujisomea kwa Taifa letu na ndio maana hata umakini hakuna. Tena basi si kusoma tu hata kuandika. Jipe fursa upitie hata magazeti yetu utashangaa.

      Kwahiyo binafsi naona CCM itaondoka madarakani kwa njia za kupayuka tu na kuzungumza na wananchi zaidi juu ya haki zao bila hata ya kuwaeleza ilani inasema nini!
      Mkuu Ilani ndio sababu, nia na kuonyesha uwezo wa kutaka kushika madaraka ya kuongoza nchi..

      Hata kama watu wanachagua vichwa safari hii Chadema hawako nyuma sana hivyo ushindani utabakia ktk Ilani za chama. Na kama ujuavyo wananchi wana CHUKI!

      Naogopa tu hiyo chuki ya hawa waitwao Wajinga waliolala, isije kuwa ni zaidi ya kura zao ikawa za Wanyamulembe..
      Exploration of reality

    12. #10
      Kichuguu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th October 2006
      Location : Popote Porini
      Posts : 6,836
      Rep Power : 3272
      Likes Received
      1316
      Likes Given
      919

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Nina wasiwasi kuwa Tanzania haina tofauti yoyote na Kenya au Zimbabwe linapokuja swala la uchaguzi. Ni bora kuhakikisha kuwa vyama vyote vinajiimarisha vya kutosha kulinda na kudhibiti na upigaji na uhesabuji wa kura kwa karibu sana.
      Kichuguuu: Nyumba inayohifadhi mchwa na nguchiro kwa pamoja bila mkwaruzo

    13. #11
      RedDevil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th April 2009
      Location : Hapa Hapa
      Posts : 1,456
      Rep Power : 804
      Likes Received
      271
      Likes Given
      513

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      WanaJF, mimi niko nje lakini najitahidi kukaa karibu na mikoa yote ya Tanzania kupitia mitandao mbali mbali kama hii, najaribu kuifutilia breaking news toka kwenu na vyanzo vingine vya habari. karibu wiki nzima nimejaribu kuhoji watu mbali mbali katika mikoa ya mbeya(kuna marafiki), Dodoma(kuna marafiki), Shinyanga [Kahama na Kishapu(Home)], mwanza(Nilisoma), Tabora (nilisoma), Dar es salaam ( ninakofanya kazi), Arusha (nimefanya kazi), na Manyara( nimefanya kazi). Watanzania wengi ni wavivu wa kujisomea ndo maana wenye vijarida vyenye vituko wanauza, haviitaji kufikiria sana ni kucheka tu na kusisimuka basi.

      Kote huko nilikuwa naulizia jinsi Chadema ilivyojipanga au upinzani ulivyo nanguvu, cha kusikitisha mkoa wangu (Shinyanga) wanasema wanataka chama cha Nyerere. Iliniuma sana lakini nitafanyeje! nikabaki kutafuta sababu tu, ambayo nimeona niiweke hapa! CCM imefanikiwa kukaa muda mrefu kwa kuwanyima watu elimu bora, inawapa watu elimu ya kuendeleza umasikini badala ya kuwaondelea umaskini.

      Inauma sana kuona mkoa kama shinyanga unakuwa ni kama jimbo la CCM vile. kwa hiyo chadema au vyama vya upinzani tuna kazi, ilani najua itasaidia kwa wajanja wachache, lakini kwenye mikoa kama shinyanga nadhani kuna haja ya kuwafanyia utafiti kabla ya kampeni ili kuweza kuwapa upeo.

      Hiyo ni shinyanga, lakini kuna maeneo kibao,mikoa mingi ya namna ambayo ni kama majimbo ya ccm watu hawaelewei, wanatishiwa vita kama vya rwanda, wanaohongwa, wanaokamatwa na kubambikwa kesi yaani ni uonevu kwenda mbele. Lakini yanawezekana, maisha bila ccm yanawezekana kabisa. TWENDE KAZI chadema.
      "Never argue with stupid people, they will drag you down to their level and then beat you with experience" Mark Twain

    14. #12
      Mwanamayu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2010
      Location : Manzese
      Posts : 3,049
      Rep Power : 1069
      Likes Received
      240
      Likes Given
      112

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      The late J. K. Nyerere commended Chadema to lead the country and now it is a high time to do it!

    15. #13
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,518
      Rep Power : 46714
      Likes Received
      16434
      Likes Given
      8469

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Wananiudhi kweli watu wanaodharau "wanakijiji" wenzangu.. wakati wabunge 60 wa CCM na wengine wamebwaga na wanakijiji hao hao; ni wanakijiji hadi hivi sasa ndio wanaongoza Tanzania kwa kuchagua upinzani! Walio mjini ndio wa kulaumiwa kwa kuendelea kwa utawala wa CCM hivi sasa. Msitushakizie.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    16. #14
      mfianchi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Location : Likulufusi
      Posts : 3,574
      Rep Power : 1222
      Likes Received
      580
      Likes Given
      1209

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Quote By RedDevil
      WanaJF, mimi niko nje lakini najitahidi kukaa karibu na mikoa yote ya Tanzania kupitia mitandao mbali mbali kama hii, najaribu kuifutilia breaking news toka kwenu na vyanzo vingine vya habari. karibu wiki nzima nimejaribu kuhoji watu mbali mbali katika mikoa ya mbeya(kuna marafiki), Dodoma(kuna marafiki), Shinyanga [Kahama na Kishapu(Home)], mwanza(Nilisoma), Tabora (nilisoma), Dar es salaam ( ninakofanya kazi), Arusha (nimefanya kazi), na Manyara( nimefanya kazi). Watanzania wengi ni wavivu wa kujisomea ndo maana wenye vijarida vyenye vituko wanauza, haviitaji kufikiria sana ni kucheka tu na kusisimuka basi.

      Kote huko nilikuwa naulizia jinsi Chadema ilivyojipanga au upinzani ulivyo nanguvu, cha kusikitisha mkoa wangu (Shinyanga) wanasema wanataka chama cha Nyerere. Iliniuma sana lakini nitafanyeje! nikabaki kutafuta sababu tu, ambayo nimeona niiweke hapa! CCM imefanikiwa kukaa muda mrefu kwa kuwanyima watu elimu bora, inawapa watu elimu ya kuendeleza umasikini badala ya kuwaondelea umaskini.

      Inauma sana kuona mkoa kama shinyanga unakuwa ni kama jimbo la CCM vile. kwa hiyo chadema au vyama vya upinzani tuna kazi, ilani najua itasaidia kwa wajanja wachache, lakini kwenye mikoa kama shinyanga nadhani kuna haja ya kuwafanyia utafiti kabla ya kampeni ili kuweza kuwapa upeo.

      Hiyo ni shinyanga, lakini kuna maeneo kibao,mikoa mingi ya namna ambayo ni kama majimbo ya ccm watu hawaelewei, wanatishiwa vita kama vya rwanda, wanaohongwa, wanaokamatwa na kubambikwa kesi yaani ni uonevu kwenda mbele. Lakini yanawezekana, maisha bila ccm yanawezekana kabisa. TWENDE KAZI chadema.
      Mama yangu anamiaka 75 na kajiandikisha kupiga kura yeye naye anadai hata iweje hakuna chama kama CCM anadai je wewe mwanagu unaweza kunikataa mimi kuwa si mamako, kwake yeye CCM ndiye mama wa siasa na vyama vyote kwa hiyo vyama vingine havina nguvu au ubavu wa kushindana na chama mama.

      Loh nikaishiwa hamu,nikajaribu kumueleza maovu yote yanayofanywa na CCM kwani hata muda wa kunisikiliza hakuwa nao akaniambia we mwanangu lakini kwa hilo la kuisema CCM unaenda mbali akafunga mazungumzo, kwa hiyo ni kweli hata Chadema wangekuja na ilani ya uchaguzi nzuri kiasi gani bado kuna safari ndefu kwa wananchi walio wengi kujua ilani kwanza nini au ina manufaa gani.

      Tukumbuke enzi za Mkapa alisema ilani ya CCM haitekelezeki na bado tukamchagua mgomnea wa CCM kwa kishindo, ingekuwa ni nchi zingine zenye uelewa juu ya Ilani, CCM ingekuwa ishazikwa zamani kwenye kaburi futi sita ardhini.

    17. #15
      Lekanjobe Kubinika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2006
      Location : Tanzania
      Posts : 2,399
      Rep Power : 1656
      Likes Received
      313
      Likes Given
      578

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Kama kuna watu wanaofikiria kwamba watanzania ni wajinga milele, wasubiri masaa 12 ya tarehe 31 October 2010. Ikiwa refer (Tume ya usimamizi) atakuwa mkweli wa haki sawa kwa wote na atadhibiti itikadi ya kichama ya kuiba kura ili kishindo kionekane, na ikiwa hatamwangalia nyani usoni katika kupiga filimbi, safari hii Tanzania inayo matumaini makubwa kuwaonyesha wanaofkiri wanayo hati miliki ya kuiongoza nchikwamba hawasemi kweli daima.

      Ofcourse huwezi kumdhibiti mwizi 100%, kwani inadaiwa mwizi akifika nyumbani kwako kuiba akakosa ufanikisha zoezi hilo ni lazima afanye uharibifu japo kidogo, ataiba hata kandambili iliyochoka sana iliyosahauliwa mlangoni. Tukiongea sana tunadhaniwa ni mashabiki, so let us wait and see. Time will confirm and tell it all.

    18. #16
      kilemi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th March 2009
      Location : Dar es Salaam, Tanzania
      Posts : 496
      Rep Power : 619
      Likes Received
      51
      Likes Given
      0

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Kama ndiyo hiyo, basi itabidi CCM warudi darasani kuandika Ilani yao upya maana kama watu watapigia kura Ilani.. basi mtanange huu wa demokrasia 'UNOGILE".
      Kama watu hawatapigia kura pilau na pombe za kienyeji, na sh 5000 za kununulia kilo ya nyama

    19. #17
      Raia Fulani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2009
      Posts : 9,261
      Rep Power : 2625
      Likes Received
      1294
      Likes Given
      835

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Babu karibu sana kyadema
      Beware of a sucker punch

    20. #18
      ICHONDI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2008
      Posts : 286
      Rep Power : 591
      Likes Received
      29
      Likes Given
      2

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Quote By Anfaal
      Mwanakijiji unaenda mbali saana kwa kuwaza Ilani.

      Kamwe nchi hii, ilani haitaiangusha CCM. Leo hii tuulizane hapa hata kabla yakufika kule vijijini, ni nani aliisoma Ilani ya CCM ya 2005 na nani anaweza kuizungumzia utekelezaji wake! Jibu ni kuwa utashangaa saana. Wengi kati yetu tunapenda kusoma mistari miwili na kufunika na hao ndio tunajiita wasomi. Sasa, vipi kuhusu wanakijiji?

      Matatizo ni makubwa saana katika kujisomea kwa Taifa letu na ndio maana hata umakini hakuna. Tena basi si kusoma tu hata kuandika. Jipe fursa upitie hata magazeti yetu utashangaa.

      Kwahiyo binafsi naona CCM itaondoka madarakani kwa njia za kupayuka tu na kuzungumza na wananchi zaidi juu ya haki zao bila hata ya kuwaeleza ilani inasema nini!
      Nakubaliana na wewe kuwa kweli tunasoma kurasa chache halafu tunafunika.

      Sidhani kama hilo linasababishwana uvivu wetu hapana, ni kwa sababu hizo kurasa mbili zote ni pumba, na ni aya zile zile za toka Uhuru na ambazo tumezizoea, kama hivi "mkakati unafanywa ili kuboresha huduma za afya na maji vijijini" Sasa hapo unaniambia nini, what is tangible thing hapo ambacho mimi msomajiwa ilani nitaondoka nacho ili kesho na keshokutwa nikubane wewe mgombea kama ulideliver.

      Na ni aina hiyo hiyo ya staili ya kujibu maswali bungeni, mfano "mchakato unafanywa ili kubaini ni madai gani ya walimu halali na si halali" Seriously, what is that? So ilani ya CCM haina kitu kipya, ina vision ya 2015 na 2025, come one, kama huwezi kuwaondolea wananchi kero leo, utawezaje kuiondoa kero miaka 20 ijayo wakati anayeomba kura hatakuwepo madarakani.

      I can assure you, ilani ya Chadema ikitoka kila mwenye kuipenda na kuitakia tanzania mema atasoma, mbona wengi waliusoma ule waraka wa wakatoliki isipokuwa Kingunge? Kama first two pages zitakuwa pumba kama za CCM then hata hiyo ya Chadema wataifunika tu.

      USIWADHARAU WATANZANIA, WANA AKILI ZA KUTOSHA NDUGU LOL

    21. #19
      Shalom's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th June 2007
      Location : texas
      Posts : 1,372
      Rep Power : 895
      Likes Received
      78
      Likes Given
      49

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      Quote By mfianchi
      Mama yangu anamiaka 75 na kajiandikisha kupiga kura yeye naye anadai hata iweje hakuna chama kama CCM anadai je wewe mwanagu unaweza kunikataa mimi kuwa si mamako, kwake yeye CCM ndiye mama wa siasa na vyama vyote kwa hiyo vyama vingine havina nguvu au ubavu wa kushindana na chama mama.

      Loh nikaishiwa hamu,nikajaribu kumueleza maovu yote yanayofanywa na CCM kwani hata muda wa kunisikiliza hakuwa nao akaniambia we mwanangu lakini kwa hilo la kuisema CCM unaenda mbali akafunga mazungumzo, kwa hiyo ni kweli hata Chadema wangekuja na ilani ya uchaguzi nzuri kiasi gani bado kuna safari ndefu kwa wananchi walio wengi kujua ilani kwanza nini au ina manufaa gani.

      Tukumbuke enzi za Mkapa alisema ilani ya CCM haitekelezeki na bado tukamchagua mgomnea wa CCM kwa kishindo, ingekuwa ni nchi zingine zenye uelewa juu ya Ilani, CCM ingekuwa ishazikwa zamani kwenye kaburi futi sita ardhini.
      Sio kweli Mimi mama yangu aliyepiga kura siku zote CCM amesema mwaka huu atapiga Chadema na anajuta miaka yote hiyo alipokuwa mwalimu na kusimamia uchaguzi na kuwasaidia watu wapige CCM. kwa hiyo unategemea una mama wa aina gani na yuko eneo gani

    22. #20
      mwita ke mwita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th August 2010
      Posts : 671
      Rep Power : 0
      Likes Received
      59
      Likes Given
      112

      Default Re: Ilani ya Chadema inatisha!!! - itashtua taifa

      ilani inataka utekelezaji hivyo kama inatekelezeka tuikaribisha kwa hamu saana

    Page 1 of 9 123 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Fedha za RUZUKU ya CHADEMA 2010 - 2015
      By Bado Niponipo in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 27
      Last Post: 10th November 2010, 23:59
    2. Ijue Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010 - 2015
      By Luteni in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 59
      Last Post: 8th September 2010, 16:52
    3. Ilani 2010-2015 chadema vs ccm
      By Njowepo in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 1
      Last Post: 4th September 2010, 10:51
    4. Ilani ya Chadema 2010-2015 (Ilani ya Uchaguzi)
      By Chapakazi in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 0
      Last Post: 2nd September 2010, 13:43

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...