Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Rahma Al Kharoos anatafuta Ubunge?

    Report Post
    Page 5 of 5 FirstFirst ... 345
    Results 81 to 87 of 87
    1. #1
      Mchokonozi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th November 2009
      Posts : 15
      Rep Power : 487
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Unhappy Rahma Al Kharoos anatafuta Ubunge?

      Waungwana, mtaniwia radhi kwa kutoonekana ukumbini kwa muda mrefu. Nimekuwa nikisoma alama za nyakati ili niweze kuja hapa na mada iliyosheheni hoja za nguvu, si nguvu za hoja.

      Naanza kwa hili la Mke Mdogo wa Mkuu wa Kaya – nadhani wote mnamtambua, sihitaji kumtaja jina lake – ambaye hivi karibuni ameanza kampeni za wazi wazi, ikionekana dhahiri kwamba si kwamba anajinadi ili kuweza kupata umaarufu wa haraka haraka, lakini lengo lake haswa likiwa kuupata Ubunge wa Viti Maalum kupitia Chama Tawala.

      Habari za ndani kutoka kwa wadau walio karibu naye zinadai kwamba mwanamama huyu machachari na mkorodi, ambaye inasemekana kwamba “haambiliki” hata kwa Mkuu wa Kaya mwenyewe, amepania naye kuukwaa Ubunge huo ili naye aingie “mjengoni” mwaka 2010, lakini kisichojulikana ni kwa malengo gani haswa yanayomsukuma kufanya hivyo. Licha ya kwamba mwanamama huyu ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa kifedha – jambo ambalo amelidhihirisha wazi wazi – haieleweki ni kipi haswa anachokifuata “mjengoni” humo.

      Duru za kisiasa zinasema harakati za mwanamama huyu zinaweza kuleta athari hasi kwa Mkuu wa Kaya, kwani zitasomeka kuwa harakati za kuigeuza hali ya kisiasa nchini hapa kuwa ya “kisultani”, kwani, minong’ono inasikikika kwamba mwana wa Mkuu wa Kaya, ambaye ni Mjumbe wa NEC kupitia Wilaya ya Bagamoyo, naye pia yumo mbioni kujiandaa kugombea kuingia “mjengoni”, ingawa hajatangaza rasmi nia yake hiyo.

      Mwanamama huyu alianza kishindo cha kampeni zake siku chache zilizopita baada ya kumwaga kitita cha fedha taslim shilingi milioni 10, ambazo alihakikisha zinaonekana kwenye taarifa ya habari ya kituo cha luninga cha Channel Ten, ambacho ndicho kimekuwa karibu naye kwa wakati wote huu. Kitita hicho kilimwagwa kama “msaada” kwa timu ya soka ya wanawake, Twiga Stars, RK akitambulishwa kama “mdau wa soka ya wanawake”, na kutambulishwa kwamba amekuwa akiichangia timu hiyo mara kwa mara. Jambo la kushangaza ni kwamba, ni zaidi ya mara moja timu hiyo imekuwa ikitembeza bakuli kwa wafadhili mbalimbali, lakini haikuwahi kusikika hata mara moja kwa mwanamama huyo – ambaye anaishi nchini Oman – kujitokeza kuisaidia, licha ya uwezo wake mkubwa wa kifedha.

      Jitihada za mwanamama huyu kujinadi wazi wazi hazikuishia hapo, kwani, ni Jumapili ya wiki iliyoisha, alijitokeza kufadhili kinyanganyiro cha kuwasaka walimbwende wanaoshiriki kupitia shindano la Miss Inter College, ambao washindi wake watapata nafasi ya kuingia moja kwa moja kwenye shindano la Miss Tanzania 2010. Safari hii, dau la mwanamama huyu limeongezeka kufikia Shilingi milioni 12, akijinadi kupitia kampuni ya RBS Oil and Technology.

      Tathmini yangu ni kama ifuatavyo.

      Iwapo mwanamama huyu ataachwa kuendelea kufanya ayatakayo, huenda kambi ya Mkuu wa Kaya ikapata athari hasi, kwani harakati hizi zitaweza kuwa “mtaji wa kisiasa” (political capital) kwa kambi ya upinzani, wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2010, jambo ambalo linaweza kuathiri vibaya matokeo ya kura zitakazovunwa na Mkuu wa Kaya
      Duru za kisiasa zimezidi kudodosa na kusema kwamba, harakati za mwanamama huyu zinaweza kutafsiriwa kuwa ukandamizaji kwa wanawake kutokana na nafasi kubwa aliyonayo kama Mke Mdogo wa Mkuu wa Kaya, nafasi ambayo anaweza kuitumia ipasavyo kwani hakuna atakayeweza kumpinga wakati wa kinyang’anyiro hicho cha Ubunge kupitia Viti Maalum. Kampeni ya kusaka umaarufu kwa kutoa michango lukuki inasadikiwa kuwa ni kutaka kumwiga Mke wa Rais, ambaye tayari amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na mchango wake mkubwa kwa maendeleo ya wanawake na watoto, japokuwa Mke huyo hajaonesha nia ya kutaka kugombea nafasi ya kuingia “mjengoni”


      Wadau wa masuala ya kisiasa wamemshauri Mkuu wa Kaya kumwita mwanamama huyo na kumkalisha, kasha kumpa karipio kali na amri ya kusitisha mara moja harakati zake hizo, kwani harakati hizo za kuutaka umaarufu zinaelekea kumwaga “mtama” na kuweka wazi mambo ya ndani ya “familia” yasiyopaswa kujulikana, jambo ambalo litaweza kuiweka kambi ya Mkuu wa Kaya kwenye wakati mgumu mara tu kipenga cha kampeni za Uchaguzi Mkuu kitakapopulizwa rasmi.

      “Sio kwamba Mkuu wa Kaya anapendwa sana na wananchi wake, la hasha; sio kwamba wananchi wake wote watafurahi akirejea ulingoni, la hasha; itakuwa ni aibu akishindwa kurejea kwa sababu ya kukuru-kakara za mke wake mdogo”, alishauri mdau mmoja wa kisiasa.

      Nimepewa ujumbe niufikishe kwa Mkuu wa Kaya. Natumai utafika.



      >>> Mchokonozi, Shujaa wa Kuchokonoa!


    2. Miaka 50

    3. #81
      Game Theory's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th September 2006
      Posts : 10,054
      Rep Power : 3352
      Likes Received
      240
      Likes Given
      0

      Default Re: Rahma Al Kharoos anatafuta Ubunge?

      at least she is hustling sio kama wanawake wengine ma Goal keepers

    4. #82
      KING COBRA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th November 2011
      Posts : 518
      Rep Power : 679
      Likes Received
      127
      Likes Given
      0

      Default Re: Rahma Al Kharoos anatafuta Ubunge?

      Hii imefikia wapi???? UWT ????

    5. #83
      George Smiley's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th October 2011
      Posts : 374
      Rep Power : 457
      Likes Received
      184
      Likes Given
      108

      Default Re: Rahma Al Kharoos anatafuta Ubunge?

      kimyaaaa

    6. #84
      Ulimakafu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2011
      Location : Itabanya Balasi
      Posts : 10,933
      Rep Power : 2600
      Likes Received
      690
      Likes Given
      1615

      Default Re: Rahma Al Kharoos anatafuta Ubunge?

      Quote By Mchokonozi
      Waungwana, mtaniwia radhi kwa kutoonekana ukumbini kwa muda mrefu. Nimekuwa nikisoma alama za nyakati ili niweze kuja hapa na mada iliyosheheni hoja za nguvu, si nguvu za hoja.

      Naanza kwa hili la Mke Mdogo wa Mkuu wa Kaya – nadhani wote mnamtambua, sihitaji kumtaja jina lake – ambaye hivi karibuni ameanza kampeni za wazi wazi, ikionekana dhahiri kwamba si kwamba anajinadi ili kuweza kupata umaarufu wa haraka haraka, lakini lengo lake haswa likiwa kuupata Ubunge wa Viti Maalum kupitia Chama Tawala.

      Habari za ndani kutoka kwa wadau walio karibu naye zinadai kwamba mwanamama huyu machachari na mkorodi, ambaye inasemekana kwamba “haambiliki” hata kwa Mkuu wa Kaya mwenyewe, amepania naye kuukwaa Ubunge huo ili naye aingie “mjengoni” mwaka 2010, lakini kisichojulikana ni kwa malengo gani haswa yanayomsukuma kufanya hivyo. Licha ya kwamba mwanamama huyu ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa kifedha – jambo ambalo amelidhihirisha wazi wazi – haieleweki ni kipi haswa anachokifuata “mjengoni” humo.

      Duru za kisiasa zinasema harakati za mwanamama huyu zinaweza kuleta athari hasi kwa Mkuu wa Kaya, kwani zitasomeka kuwa harakati za kuigeuza hali ya kisiasa nchini hapa kuwa ya “kisultani”, kwani, minong’ono inasikikika kwamba mwana wa Mkuu wa Kaya, ambaye ni Mjumbe wa NEC kupitia Wilaya ya Bagamoyo, naye pia yumo mbioni kujiandaa kugombea kuingia “mjengoni”, ingawa hajatangaza rasmi nia yake hiyo.

      Mwanamama huyu alianza kishindo cha kampeni zake siku chache zilizopita baada ya kumwaga kitita cha fedha taslim shilingi milioni 10, ambazo alihakikisha zinaonekana kwenye taarifa ya habari ya kituo cha luninga cha Channel Ten, ambacho ndicho kimekuwa karibu naye kwa wakati wote huu. Kitita hicho kilimwagwa kama “msaada” kwa timu ya soka ya wanawake, Twiga Stars, RK akitambulishwa kama “mdau wa soka ya wanawake”, na kutambulishwa kwamba amekuwa akiichangia timu hiyo mara kwa mara. Jambo la kushangaza ni kwamba, ni zaidi ya mara moja timu hiyo imekuwa ikitembeza bakuli kwa wafadhili mbalimbali, lakini haikuwahi kusikika hata mara moja kwa mwanamama huyo – ambaye anaishi nchini Oman – kujitokeza kuisaidia, licha ya uwezo wake mkubwa wa kifedha.

      Jitihada za mwanamama huyu kujinadi wazi wazi hazikuishia hapo, kwani, ni Jumapili ya wiki iliyoisha, alijitokeza kufadhili kinyanganyiro cha kuwasaka walimbwende wanaoshiriki kupitia shindano la Miss Inter College, ambao washindi wake watapata nafasi ya kuingia moja kwa moja kwenye shindano la Miss Tanzania 2010. Safari hii, dau la mwanamama huyu limeongezeka kufikia Shilingi milioni 12, akijinadi kupitia kampuni ya RBS Oil and Technology.

      Tathmini yangu ni kama ifuatavyo.

      Iwapo mwanamama huyu ataachwa kuendelea kufanya ayatakayo, huenda kambi ya Mkuu wa Kaya ikapata athari hasi, kwani harakati hizi zitaweza kuwa “mtaji wa kisiasa” (political capital) kwa kambi ya upinzani, wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2010, jambo ambalo linaweza kuathiri vibaya matokeo ya kura zitakazovunwa na Mkuu wa Kaya
      Duru za kisiasa zimezidi kudodosa na kusema kwamba, harakati za mwanamama huyu zinaweza kutafsiriwa kuwa ukandamizaji kwa wanawake kutokana na nafasi kubwa aliyonayo kama Mke Mdogo wa Mkuu wa Kaya, nafasi ambayo anaweza kuitumia ipasavyo kwani hakuna atakayeweza kumpinga wakati wa kinyang’anyiro hicho cha Ubunge kupitia Viti Maalum. Kampeni ya kusaka umaarufu kwa kutoa michango lukuki inasadikiwa kuwa ni kutaka kumwiga Mke wa Rais, ambaye tayari amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na mchango wake mkubwa kwa maendeleo ya wanawake na watoto, japokuwa Mke huyo hajaonesha nia ya kutaka kugombea nafasi ya kuingia “mjengoni”


      Wadau wa masuala ya kisiasa wamemshauri Mkuu wa Kaya kumwita mwanamama huyo na kumkalisha, kasha kumpa karipio kali na amri ya kusitisha mara moja harakati zake hizo, kwani harakati hizo za kuutaka umaarufu zinaelekea kumwaga “mtama” na kuweka wazi mambo ya ndani ya “familia” yasiyopaswa kujulikana, jambo ambalo litaweza kuiweka kambi ya Mkuu wa Kaya kwenye wakati mgumu mara tu kipenga cha kampeni za Uchaguzi Mkuu kitakapopulizwa rasmi.

      “Sio kwamba Mkuu wa Kaya anapendwa sana na wananchi wake, la hasha; sio kwamba wananchi wake wote watafurahi akirejea ulingoni, la hasha; itakuwa ni aibu akishindwa kurejea kwa sababu ya kukuru-kakara za mke wake mdogo”, alishauri mdau mmoja wa kisiasa.

      Nimepewa ujumbe niufikishe kwa Mkuu wa Kaya. Natumai utafika.



      >>> Mchokonozi, Shujaa wa Kuchokonoa!

      Mchokonozi mchokonozi...!!!!!!!

    7. #85
      morphine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th January 2012
      Location : Gotham City, 666 Blue Lodge
      Posts : 382
      Rep Power : 515
      Likes Received
      65
      Likes Given
      109

      Default Re: Rahma Al Kharoos anatafuta Ubunge?

      kumbe mweeee
      The only antidote of pain is honesty.

    8. FemaTV & Radio

    9. #86
      Obby's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 31st August 2011
      Posts : 5
      Rep Power : 391
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Rahma Al Kharoos anatafuta Ubunge?

      Dats y nililalamika sana nilipopoteza password ya jamii forum,wish nitafaidi sana.
      Makala ilikua poa sana bt kiukweli huyu mwandishi hakuwa nahaja ya kuficha jina kwa ajili ya kumrida ilhali watu wengi wanamfahamu mwanamama huyu.

    10. #87
      sun wu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 1,970
      Rep Power : 7747
      Likes Received
      1087
      Likes Given
      256

      Default Re: Rahma Al Kharoos anatafuta Ubunge?

      Unyumba ndogo wake usimfanye ndio achaguliwe... LAKINI,

      Sio kwamba aache kuchaguliwa sababu ni nyumba ndogo.., cha kujiuliza ni Je anaweza Kazi ?
      Opportunities Multiply as they are Seized Sun Tzu

    Page 5 of 5 FirstFirst ... 345

    Similar Topics

    1. Mtangazaji wa CTN Rahma Aziz
      By Mwana Mpotevu in forum Celebrities Forum
      Replies: 26
      Last Post: 24th December 2011, 17:25
    2. Huyu Kasiga ni dada yake Rahma Kharoos Kasiga wa Jakaya?
      By mpayukaji in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 3
      Last Post: 7th December 2011, 10:23
    3. RIP Rahma Swai - Miss Mtwara 2011/12
      By Stany in forum Celebrities Forum
      Replies: 64
      Last Post: 1st November 2011, 19:11
    4. Replies: 7
      Last Post: 21st October 2010, 20:03

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...