Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

    Report Post
    Results 1 to 18 of 18
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,242
      Rep Power : 3563
      Likes Received
      3062
      Likes Given
      463

      Default Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM





      Na Said Njuki, Arusha

      MGOGORO ndani ya CCM Mkoa wa Arusha umeshika kasi mpya baada ya Kamati ya Usalama na Maadili na Kamati ya Siasa za chama hicho mkoa kudaiwa kumvua
      uanachama Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) Mkoa, Bw. James Ole Millya.

      Pia vijana wengine watano wa umoja huo wanaodaiwa kuwa vinara wa mgogoro nao watakumbwa na rungu hilo baada ya kamati hizo kutoa mapendekezo ya kufukuzwa uanachama kwa kitendo chao cha kushadadia kuondoka kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Bi. Mary Chatanda.

      Habari kutoka ndani ya vikao hivyo ambazo zimethibithswa na baadhi ya viongozi wa chama hicho kwa sharti la kutotajwa majina, zimedai Kamati hiyo iliyoketi mwishoni mwa
      wiki ilitoa mapendekezo yake kuwa Mwenyekiti huyo anayedaiwa kuwa kinara wa mgogoro huo pamoja na vijana hao avuliwe madaraka.

      Vyanzo hivyo vilidai kuwa kikao cha kamati hiyo pia kilihudhuriwa pia na wajumbe kutoka Kamati ya Maadili ya Taifa ikiongozwa na Kanali Mhando na wajumbe wawili kutoka UVCCM Taifa ambao ni Bw. Seif Malinda na Mzee Mipoko kilichokaa kuanzia asubuhi hadi usiku wa manane.

      Mapendekezo hayo baada ya kuridhiwa na wajumbe hao yalifikishwa katika Kikao cha Kamati ya Siasa ya Mkoa, kilichofanyika siku moja baadaye na kuridhia mapendekezo hayo, hivyo kusubiri kikao cha Halmashauri Kuu ya Mkoa kinachotarajiwa kukutana Jumamosi wiki hii kwa ajili ya maamuzi zaidi.

      Vyanzo hivyo vimewataja majina ya vijana watano kati ya 11 waliohojiwa siku hiyo, kufuatina mgogoro unaotokana na falsafa mpya ya CCM ya kujivua gamba ambapo makada waandamizi wa chama hicho, aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa, Mbunge wa Igunga, Bw. Rostam Aziz na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Bw. Andrew Chenge wanashinikizwa kuachia ngazi zao.

      Baadhi ya sababu zilizoelezwa za kuwajibika kwa Bw. Milly
      Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Bi. Mary Chatanda.

      Wadadisi wa mambo ya siasa mkoani hapa wameeleza ya kuwa iwapo hatua hiyo ya kuwavua uwanachama vijana hao itatekelezwa itazidi kuchochea na kupanua mgogoro huo ambao ungeweza kutatuliwa kwa njia za kidiplomasia na kupunguza ufa ndani ya chama hicho.

      Lakini kundi lingine linatoa matamshi mazito dhidi ya makada hao na kueleza kuwa wanapaswa kuwajibika kwa tuhuma zinazowakabili na kwenda mbali zaidi na kumtaja Bi. Chatanda ni lulu ya chama mkoani hapa na hapaswi kuondoka.

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,874
      Rep Power : 1977
      Likes Received
      2353
      Likes Given
      3038

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Wacha wafu wazike wafu wenzao.
      Mungi and WISDOM SEEDS like this.

    4. #3
      van victor's Avatar
      Member Array
      Join Date : 10th February 2011
      Posts : 38
      Rep Power : 427
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Wakishapambana wao kwa wao kazi kwetu chadema itakuwa rahisi....

    5. #4
      WISDOM SEEDS's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2011
      Location : Sweden
      Posts : 609
      Rep Power : 525
      Likes Received
      113
      Likes Given
      66

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Vita hiyo ni sawa na vita ya wachawi wanaouliana watoto.
      Let them kill each other

    6. #5
      lemberwa's Avatar
      Member Array
      Join Date : 30th March 2011
      Posts : 21
      Rep Power : 417
      Likes Received
      0
      Likes Given
      1

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      yaani hiyo safi sana wanatupa nafasi sisi chadema kazi rahisi ya kulichukua jiji letu milele

    7. Miaka 50

    8. #6
      Sir R's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2009
      Location : Moshi
      Posts : 1,139
      Rep Power : 714
      Likes Received
      99
      Likes Given
      24

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Dhambi ya kuua inawala.
      Umaskini wa Tanzania ni Matokeo ya Akili ndogo kuongoza Nchi

    9. #7
      Marytina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2011
      Posts : 4,870
      Rep Power : 1430
      Likes Received
      888
      Likes Given
      274

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Wamalizane

    10. #8
      bushman's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 1,443
      Rep Power : 722
      Likes Received
      309
      Likes Given
      84

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Mambo ya uvccm chatanda na uvccm millya hayo

    11. #9
      Pukudu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : Maskani.
      Posts : 1,172
      Rep Power : 1385
      Likes Received
      335
      Likes Given
      82

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      kumuondoa millya ni ndoto ya mchana hawawezi ana mizizi mirefu saaana hebu jiulizeni alipataje huo uenyekiti afu ndo tujadili mengine

    12. #10
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,084
      Rep Power : 12251
      Likes Received
      6015
      Likes Given
      6851

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      madhara ya siasa topetope
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    13. #11
      Nduka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2008
      Posts : 5,591
      Rep Power : 1636
      Likes Received
      382
      Likes Given
      553

      Default

      Quote By lemberwa
      yaani hiyo safi sana wanatupa nafasi sisi chadema kazi rahisi ya kulichukua jiji letu milele
      Huyo ole millya ndio aliwazuia kuchukua jiji?

    14. #12
      TUKUTUKU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Location : KIPALAPALA TU
      Posts : 8,370
      Rep Power : 2115
      Likes Received
      1731
      Likes Given
      676

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Tusubiri na kuona kitakachotokea!!!

    15. #13
      Makupa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 2,175
      Rep Power : 810
      Likes Received
      249
      Likes Given
      0

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      cdm jiandaeni kumpokea kama kawaida yenu

    16. #14
      sblandes's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th April 2010
      Location : SINGAPORE
      Posts : 521
      Rep Power : 620
      Likes Received
      31
      Likes Given
      63

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Sio habari

    17. #15
      mgodi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2010
      Posts : 994
      Rep Power : 631
      Likes Received
      114
      Likes Given
      81

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Vita vya Panzi.

    18. #16
      MAYOO's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th February 2011
      Posts : 175
      Rep Power : 454
      Likes Received
      20
      Likes Given
      15

      Default

      Quote By Makupa
      cdm jiandaeni kumpokea kama kawaida yenu
      cdm chama makini, anakaribishwa sharti atubu dhambi zake na asitegemee kupewa cheo chochote. Akubali kuwatumikia watz na sio mtu kama anavyofanya huko kwenye magamba. Uko hapo? Umeridhika? Kachukue ujira wako kwa leo, tuonane kesho tena.

    19. #17
      Black Bat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Abbottabad
      Posts : 2,479
      Rep Power : 9581
      Likes Received
      682
      Likes Given
      575

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      Quote By Nduka
      Huyo ole millya ndio aliwazuia kuchukua jiji?
      kaamua ajiondokee mwenyewe ..mchawi wanamjua wenyewe
      ukipenda niite double biiiiiii!! tchao

    20. #18
      Mathias Byabato's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2010
      Posts : 578
      Rep Power : 546
      Likes Received
      160
      Likes Given
      85

      Default Re: Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM

      kumbe sakata lilianza zamani?
      Kama Wewe ni Mwandishi kweli,unaamini ,una uhakika na uliandikalo basi Onesha Jina,Sura yako- Jeneral Ulimwengu

    Similar Topics

    1. Millya 'amchana' Ridhiwani Kikwete
      By Godlisten Masawe in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 68
      Last Post: 16th April 2012, 14:53
    2. NCCR yameiva: Kafulila kuvuliwa uanachama Jumamosi!
      By TUNTEMEKE in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 95
      Last Post: 17th December 2011, 07:50
    3. Millya na wenzake kuhojiwa tena
      By nngu007 in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 31st October 2011, 13:13
    4. Ole Millya kuvuliwa uanachama CCM
      By Buruburu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 9th June 2011, 02:04
    5. Olle milly kuvuliwa uanachama ccm
      By kibakwe in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 12
      Last Post: 8th June 2011, 10:48

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...