Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kina nani wanaomtumia mzee akilimali ndani ya yanga ?

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      Innobrown's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 28th February 2011
      Posts : 9
      Rep Power : 417
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default Kina nani wanaomtumia mzee akilimali ndani ya yanga ?



      Hi Mr. Shaffih, JUzi usiku nilikuwa nasikiliza kipindi chenu cha Michezo Sports Extra na Sports Bar, vilivyorushwa kwa wakati mmoja kupitia Clouds Fm na Clouds Tv. Nilisikiliza kipande ambacho kuna Mzee Anayeitwa Akilimali, ambaye hujiita katibu wa Baraza la Wazee Wa Yanga. Sina uhakika na hiyo nafasi kwenye Katiba ya Yanga kama ipo.

      Amekuwa akitumika sana, nashukuiru kwa kulitambuahilo jana. Waandishi mmempa sana airtime ya kutosha huyu Mzee mpaka imekuwa kero. Amekuwa Msemaji Mkuu wa Yanga kinyume na utaratibu. Wakati wachezaji wetu wamempiga refa Mechi ya Yanga na Azam alilumbana na TFF na kuongea mambo ya ajabu.

      Kwenye birthday ya Yanga aliwasifia akina Nchunga na akawageuka baadaye. Jana tu Anasema uchaguzi wa Yanga ukiisha atamfukuza Mwanachama Abedi Falcon uanachama kisa ameweka pingamizi kwa
      wagombea kuhusu uchaguzi. Kwani hajui ni haki ya mwanachama kuweka pingamizi? alisema ana milioni 750 za usajili, azitoe wapi?

      Mzee yule na wenzake wasioitakia Yanga Mema ndio hao wamewaponza wachezaji wetu wa Yanga leo hii wamekosa fursa muhimu ya kutumikia timu ya Taifa kutokana na kuwatumia mechi zetu za mwisho wacheze maigizo ili kumkomoa Nchunga. Kiko Wapi leo? Menyekiti hayupo Yanga na Yanga itaendelea kuwepo. Timu yetu ilipoteza muelekeo mwishoni mwa ligi kwa hujuma za hao wazee dhidi ya Uongozi halali.

      Leo wachezaji wanasajiliwa na watu binafsi kwa gharama kubwa, kwa akili ya kawaida wanayanga wanachekelea tu bila kutafakari. Mchezaji anasajiliwa kwa Milioni 30 na Mshahara M 1 kwa chanzo gani cha mapato klabuni? hao wanaowatumia akina Akilimali wakigombana na viongozi halali si ndio wanagoma kutoa mishahara, na kupigwa zile tano?

      Tuna safari ndefu Kaka. Nahitimisha na kusema yule Mzeee alikuwa anatumika tangu mwanzo wa mgogoro wa Yanga, na ameendelea kuwa Msemaji Mkuu, Sekretarieti ya Yanga inamuchia, Nyie waandishi wa Michezo mnampa nafasi bila sababu. Ni bora mmemgundua. Mimi ni Mshabiki wa Yanga wa Kawaida, huyo Mzee hana Mamlaka ya kunivua ushabiki ndio maana nimefunguka.

      Mr. Faraja Emmanuel Mkazi wa Kurasini.

      0717 079727


    2. Miaka 50

    3. #2
      Anselm's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th November 2010
      Location : Dar-es-salaam
      Posts : 1,471
      Rep Power : 725
      Likes Received
      181
      Likes Given
      138

      Default Re: Kina nani wanaomtumia mzee akilimali ndani ya yanga ?

      Huyu Mzee kwakweli ana matatizo lkn Shaffih Dauda na yeye ana matatizo makubwa.

    4. #3
      yahoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2011
      Location : Tanzania
      Posts : 626
      Rep Power : 393
      Likes Received
      107
      Likes Given
      23

      Default Re: Kina nani wanaomtumia mzee akilimali ndani ya yanga ?

      Mnashangaa nn? Mbona hata shafi anatumiwa na rage!

    5. FemaTV & Radio

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...