Ndugu wana JF ambao ni wapenzi wa timu ya Yanga mnaombwa kujitokeza katika kusaidia kutoa maoni na ushauri kwa ajili ya mchakato mzima wa kuanzisha tovuti ya klabu yetu ya Yanga..Wazo la kuanzisha Tovuti hii limeanzia kule kwenye blog ya Yanga Yanga ambapo baadhi ya wapenzi wenye nia njema walishauri ianzishwe Tovuti ambayo itakuwa ni chanzo kizuri cha habari ya klabu yetu kwa kushirikiana na blog yetu hiyo.....So ni matumaini ya walio wengi kwamba mtajitokeza na kutoa maoni yenu ya nini kifanyike katika kuianzisha Tovuti hiyo...Yanga Daima mbele,Nyuma mwiko
Kupaka rangi jengo lao tu ni utata wameshindwa...
Je lufungua web wataweza?
Tumeweza kushinda mechi 11 mfullulizo tutashindwa kufungua website...
kufungua website siyo issue kivile labda quality ya website ndiyo issue..
Nobody can give you freedom. Nobody can give you equality or justice or anything. If you're a man, you take it.... Malcolm X Nasubiri 'breaking news... '
Tumeweza kushinda mechi 11 mfullulizo tutashindwa kufungua website...
kufungua website siyo issue kivile labda quality ya website ndiyo issue..
Sawa mmeshinda mechi kumi na moja well, lakini kuna mambo ya msingi mnatakiwa muyafanye ili muweze kung'ara zaidi.
Kwanza mnatakiwa mpake rangi jengo lenu pale msimbazi. Pili mnatakiwa muweke vyoo jengo lenu, sio watu wanajisaidia vichochoroni na kwenye korido, pia mtafute sehemu ili mnunue na kuufanya uwanja wenu wa mazoezi na si kutanga tanga.
Na pia muachane na mfumo wa kutembeza bakuli pindi mnapohitaji pesa, mnatakiwa mjijengee mirija ya fedha zitakazowasaidia kuwafanikishia mambo yenu ya msingi.
Igeni mfano wa Yanga...ukiwa kagera ama pale usalama unaliona jengo lao linalong'aa huku madirisha yake yakiwa ya kisasa zaidi...yanga jana, leo,, daima
"...Abasi Gulamali raisi wa yanga....Yanga Afrika, Yanga Afrika mabingwa wa soka Afrika Mashariki na kati eeeeh heeee!!"
Hiyo ni sehemu tu ya lile dude....kuna mjinga mmoja wakati wa high school ilikuwa Yanga ikishinda lazima bweni likeshe, yeye Pepe Kale mie Bileku Mpasi tunawatumbuiza na "Yanga Afrika"!! Hahahahaha....
Kumbe Gulamali alikuwa Rais wa Yanga!!!! Ehe! Ama kweli umaskini m-baya.
Sawa mmeshinda mechi kumi na moja well, lakini kuna mambo ya msingi mnatakiwa muyafanye ili muweze kung'ara zaidi.
Kwanza mnatakiwa mpake rangi jengo lenu pale msimbazi. Pili mnatakiwa muweke vyoo jengo lenu, sio watu wanajisaidia vichochoroni na kwenye korido, pia mtafute sehemu ili mnunue na kuufanya uwanja wenu wa mazoezi na si kutanga tanga.
Na pia muachane na mfumo wa kutembeza bakuli pindi mnapohitaji pesa, mnatakiwa mjijengee mirija ya fedha zitakazowasaidia kuwafanikishia mambo yenu ya msingi.
Igeni mfano wa Yanga...ukiwa kagera ama pale usalama unaliona jengo lao linalong'aa huku madirisha yake yakiwa ya kisasa zaidi...yanga jana, leo,, daima
Uwe na uwanja usiwe na uwanja kama mpira unaujua utashinda tu!
Tatizi la mpira Tanzania sio la Yanga tu bali ni timu zote ikiwemo simba. Muako na mpenzi wa mpira Tanzania umeshuka sana. Kutokana na kupanuka kwa mawasiliano watanzania wanaweza kuona mipira ya mataifa mengine yaliendelea kisoka. Tunaona mipira ya ligi ya Ulaya, lingi ya Uingereza, kombe la dunia nk. Tunagundua kwamba mpira wetu ni wa cha ndimu ukilinganisha na timu za Ulaya. Matokeo yake wengi tunakuwa mashabiki wa Machesta kuliko Yanga au simba. Wakati Yanga na Simba wanancheza leo mtu haendi uwanjani wala kuwacha redio au TV aangalie mechi hiyo. Badala yake utamkuta kwenye TV anaangalia ligi za Ulaya. Mtu kama huyu unategemea atachangia nini katika soka letu.
Zamani ilikuwa mpira wa Yanga na Simba watu wako uwanjani saa nne asubuhi. Wachezaji walikuwa wanacheza kwa moyo na kujituma. Leo timu inafungwa magori matatu wachezaji wanatoka wakitabasamu. Zmani ingekuwa kilio.
Sasa mpira umekuwa na washabiki na wafadhili wasanii. Wanatumia mpira kujipatia sifa tu hali wao hawana upenzi wowote na mpira. Matokeo yake wanaweza kuwa chanzo cha migogoro.
Uongozi wa mpira njaa tupu. Mtu anataka uongozi atafune hela za timu. Timu zenyewe zina fedha gani za maana? Tunatumia fedha chungu nzima kuajili makocha toka nje kisa ni wazungu.
Wachezaji wakin'gaa kidogo katika soka kosa. Ataanza kunata na kudeka kama nini. Ataanza kuendekeza starehe na anasa aambazo haziendani na mazoezi. Matokeo yake anachuja hada miaka 23 hajatimiza. Enzi za akina Amasha, Makumbi Juma, Mziba, Omari Hussein, Athumani Chama, Hamisi Kinye, Yusufu Ismail Bana, Fred Minziro watu walikuwa wanacheza soka ya kujituma. Walidumu katika mpira kwa muda mrefu.
Ushauri wangu
1. Tuwahamasishe watu kupenda soka toka wakiwa watoto. Turudishe michezo ya soka ya shule za misingi na sekondari pamoja na kuwa na timu za watoto wadogo katika kila club.
Vipi Hii Site Dar Young Africans Ingekuwa vizuri kama watu wangeiupdate na kuifanya ya kisasa
Hiyo ni blog ya mashabiki wetu,inaendeshwa na mashabiki tu wenye mapenzi na Yanga,hii tunayoizungumzia ni Website ambayo itaendeshwa na klabu na itakuwa imejitosheleza kwa kila kitu kama ilivyo kwa klabu zilizo katika ligi za majuu....
Hiyo ni blog ya mashabiki wetu,inaendeshwa na mashabiki tu wenye mapenzi na Yanga,hii tunayoizungumzia ni Website ambayo itaendeshwa na klabu na itakuwa imejitosheleza kwa kila kitu kama ilivyo kwa klabu zilizo katika ligi za majuu....
Mkuu nimeingia kwenye website yenu, rangi inachosha macho, hamna utaratubu kwa kuibadilisha, halafu samahani imekaa kiccm sana.
Mkuu nimeingia kwenye website yenu, rangi inachosha macho, hamna utaratubu kwa kuibadilisha, halafu samahani imekaa kiccm sana.
Mkuu....
Website bado ipo kwenye majaribio na mpaka tunaanza next season itakuwa imeshakuwa bomba.......
Kuhusu rangi na kukaa ki CCM sana ni kwamba rangi rangi rasmi za timu yetu ya Yanga zinashabihiana na rangi za CCM,yaani kijani na njano so hakuna mbadala wa rangi nyingine.......Ni hizo hizo tu.....
Tuko wanne so far, na nadhani inabidi kazi ianze rasmi. Tayari tulianza discussion kidogo na Jimmy kuhusu hii kazi, na nadhani ni wakati sasa wa wajumbe wote kuanza kuchangia mawazo. Hapa chini naweka mawazo niliyonayo kuhusu hii kazi, na naomba na wengine mchangie kusudi kazi iendelee. tafadhali ipitieni na mtoe mawazo yenu, irekebishwe ili ije kuwa mwongozo wa hii kazi:
Mimi ni shabiki wa ile timu yenye makao yake pale mtaa wa Swahili, yaani Pan African SC, ila kwa wazo ili nakuunga mkono.
Pan African SC, will rise up again, as strong and well as they ever were... Will return to glory as a great Club of Africa...!
“I am the punishment of God... If you had not committed great sins, God would not have sent a punishment like me upon you.”
'O Allah! Keep me alive as long as life is better for me, and let me die if death is better for me.
This is where all administrative activities are taking place.
CLUB HIGHLIGHT
Young Africans is one of the oldest football teams in East Africa, The Club was established in the year 1935. The club won Tanzania Premier League 18 times, Tanzania Cup 4 times and CECAFA cup 4 times.
You are here: Home
YOUNG AFRICANS SPORTS CLUB
MICHUANO YA UHAI CUP 2011
Thu - 10 Nov Written by Administrator
ARTICLE HITS: 20 TIMES.
Timu 15 zinazoshiriki michuano ya mwaka huu ya Kombe la Uhai zimepangwa katika makundi matatu ambapo mechi zitachezwa katika viwanja viwili; Uwanja wa Karume na Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Mbande.
Mashindano hayo yanashirikisha timu zenye umri chini ya miaka 20 za klabu zote 14 za Ligi Kuu ya Vodacom wakati timu mwalikwa mwaka huu ni timu ya Taifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys).
Mabingwa watetezi Ruvu Shooting Stars ndiyo wanaoongoza kundi A katika michuano hiyo inayodhaminiwa na Kampuni ya Said Salim Bakhresa kupitia bidhaa yake ya maji Uhai. Timu nyingine katika kundi hilo ni Oljoro JKT, Kagera Sugar, Azam na Mtibwa Sugar.
ARTICLE HITS: 23 TIMES
Wachezaji wa kimataifa kutoka nchini Ghana, Kenneth Asamoah na Yaw Berko wameondoka jijini Dar es Salaam alfajiri ya leo kwenda nchini Ghana kwa ajili ya mapunziko ya muda mfupi. Wachezaji hao wameondoka baada ya Uongozi wa mabingwa wa soka kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati kutoa mapunziko ya wiki tatu kabla ya kuingia katika hatua nyingine ya mzunguko wa ligi kuu pamoja na michuano ya kimataifa inayoikabili Klabu ya Yanga ikiwemo mashindano ya Klabu Bingwa barani Afrika na michuano ya Kombe la Kagame. Akizungumza nawww.youngafricans.co.tz , Afisa Habari wa Klabu ya Yanga, Read more...
UHAI CUP kuanza tarehe11/11/11 katika Uwanja wa Azam FC - Mbande
Tue - 08 Nov Written by Administrator
ARTICLE HITS: 9 TIMES
Ligi ya vijana chini ya miaka 20 UHAI CUP inatazamiwa kuanza tarehe 11/11/11 katika Uwanja wa Azam FC - Mbande.
Ligi hiyo itashirikisha jumla ya timu 14 ambazo timu zao za wakubwa zinashiriki ligi kuu Tanzania Bara, timu hizo ni:
1.Young Africans B ,
2.Simba SC B,
3.Azam SC B,
4.Mtibwa Sugar B,
5.JKT Oljoro B,
6.Villa Squad B,
7.Moro United B,
8.African Lyon B,
9.Coastal Union B,
10.JKT Ruvu B, Read more...
YANGA KUIVAA POLISI DODOMA
Sat - 05 Nov Written by Administrator
Kikosi cha mabingwa wa ligi kuu Tanzania Bara leo kinatarajiwa kushuka dimbani kucheza na Police Tanzania katika mchezo wa ligi kuu ya VPL 2011/2012.
Mchezo huo utakuwa ni kumalzia mzunguko wa kwanza kwa timu zote amabapo Yanga ina point 24 ikiwa na nafasi ya pili na Police Tanzania ni ya 13 ikiwa na point 9.
from:yanga1935 - Twitter Search yanga1935: WABUNGE wanachama wa klabu ya Young Africans waliopo mjini Dodoma,wanakutana katika ukumbi wa BUNGE kujadili maendeleo ya klabu mchana huu. yanga1935: Check this video out -- YANGA vs SIMBA - VODACOM PREMIER LEAGUEhttp://t.co/Fgo918MJ via @youtube yanga1935: All the best Taifa Stars against Chad! yanga1935: I'm booking my next stay @DoubleTree by Hilton with a Facebook exclusive deal as sweet as their chocolate chip cookies!DoubleTree by Hilton | Facebook yanga1935: UHAI CUP 2011/2012 Young Africans SC (Black Stars U-20) Vs Moro United U-20 kick-off 14:00hrs @Azam FC Stadium - Mbande
...Ebana Balantanda, mie nilikuwa natafuta sana lile dude la Pepe Kalle linaitwa "Yanga Afrika" nadhani unajua jinsi linavyo flow....lakini halipatikani kwenye youtube, ukilipata liweke hapa hahahahaha nitafurahi sana chamaa! Obligado.
Follow Us Here