Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 21
    1. #1
      Mfumwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2008
      Posts : 1,470
      Rep Power : 841
      Likes Received
      14
      Likes Given
      1

      Default Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Wakati tunasuburi makabidhiano rasmi, na kama walivyoahidi kuwa watataja jina jipya leo. Nadhani jina sio muhimu sana, matunzo ndio muhimu kwa huu uwanja.

      Uwanja wa Taifa kubatizwa kesho
      na Nasra Abdallah

      HATIMAYE kitendawili cha jina la uwanja mpya wa soka uliopo Temeke, Dar es Salaam, kinatarajiwa kuteguliwa kesho, imefahamika jana jijini Dar es Salaam.

      Taarifa zilizopatikana jana kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, zinasema kwamba Serikali ya Tanzania itatangaza jina hilo kesho katika ukumbi wa wizara hiyo.

      Habari hizo zinasema kwamba, Serikali ya Tanzania pamoja na China, zimeandaa hafla ya kuzindua jina hilo ndani ya uwanja huo, uliojengwa kwa gharama ya zaidi ya sh milioni 55.

      Uwanja mpya wa Tanzania, wenye uwezo wa kubeba watazamaji wasiopungua 65,000, walioketi, ulijengwa kuanzia mapema mwa miaka 2003 na Kampuni ya China, Beijing Construction.

      Uwanja huo, umetumika kwa mechi kadhaa za kitaifa na kimataifa lakini kumbukumbu itabaki Septemba mosi, 2007 wakati ambako Stars iliifumua The Cranes ya Uganda katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa.

      Mchezaji wa kwanza kufunga bao katika uwanja huo ni Abdi Kassim Babi, aliyepiga bao hilo katika dakika ya 52 kwa shuti la umbali wa mita kama 30.

      Ulikuwa ni mchezo wa Stars wa kujipima nguvu kabla ya kuivaa Msumbiji ‘The Black Mambaz’, Septemba 8, mwaka huo ukiwa ni mchezo wa mwisho wa kundi la saba kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (CAN) 2008.

      Stars haikufuzu kwani siku hiyo ilipigwa bao 1-0 na Mamba hao. Bao hilo lilifungwa dakika ya kwanza, na mshambuliaji wa kimataifa wa Afrika Kusini, Tico Tico.
      Source: Uwanja wa Taifa kubatizwa kesho

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Invisible's Avatar
      Robot Array
      Join Date : 11th February 2006
      Location : Here...!
      Posts : 9,326
      Rep Power : 100000
      Likes Received
      4884
      Likes Given
      5616

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Wametangaza kwamba Uwanja Mpya utaitwa UWANJA WA TAIFA na wa zamani utaitwa UWANJA WA UHURU.
      Ficha Upumbavu wako; Usiifiche Hekima yako!
      24/7 Email SUPPORT: [email protected]


    4. #3
      Masanilo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2007
      Location : Swat valley, Keta Keta
      Posts : 19,059
      Rep Power : 5467
      Likes Received
      3486
      Likes Given
      1900

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Invisible
      Wametangaza kwamba Uwanja Mpya utaitwa UWANJA WA TAIFA na wa zamani utaitwa UWANJA WA UHURU.
      Heri hawajauita Benjamin Mkapa...

    5. #4
      Baba_Enock's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Location : Bunju "B"
      Posts : 5,817
      Rep Power : 1899
      Likes Received
      1161
      Likes Given
      977

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Masanilo
      Heri hawajauita Benjamin Mkapa...
      Mkuu Msanilo,


      Jina Kamili litakuwa "The Benjamin W M National Stadium"
      Ad Majorem Dei Gloriam - "For the greater glory of God"

    6. #5
      Masanilo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2007
      Location : Swat valley, Keta Keta
      Posts : 19,059
      Rep Power : 5467
      Likes Received
      3486
      Likes Given
      1900

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Baba E

      Wacha nirusha roho bana, wakati hata ile shule ya Ben Mkapa tumependekeza ibadilishwe jina kuonyesha hatuungi mkono viongozi mafisadi....


      Quote By Baba_Enock
      Mkuu Msanilo,


      Jina Kamili litakuwa "The Benjamin W M National Stadium"

      Kindness is the language which the deaf can hear and the blind can see - Mark Twain
      CCM is enemy of GOD

    7. Miaka 50

    8. #6
      Njimba Nsalilwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd March 2008
      Location : In Africa
      Posts : 253
      Rep Power : 620
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Mfumwa
      Wakati tunasuburi makabidhiano rasmi, na kama walivyoahidi kuwa watataja jina jipya leo. Nadhani jina sio muhimu sana, matunzo ndio muhimu kwa huu uwanja.

      Uwanja wa Taifa kubatizwa kesho
      na Nasra Abdallah


      Habari hizo zinasema kwamba, Serikali ya Tanzania pamoja na China, zimeandaa hafla ya kuzindua jina hilo ndani ya uwanja huo, uliojengwa kwa gharama ya zaidi ya sh milioni 55.


      Source: Uwanja wa Taifa kubatizwa kesho
      Aissee, uwanja bei nafuu sana yaani zaidi ya sh milion 55? Yaani hata nyumba yangu imenicost zaidi ya uwanja???????? kwa nini hatuna vingi????????????????? wachina njooni mtujengee vingine kama hiyo ndio bei

    9. #7
      Masanilo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2007
      Location : Swat valley, Keta Keta
      Posts : 19,059
      Rep Power : 5467
      Likes Received
      3486
      Likes Given
      1900

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Njimba Nsalilwe
      Aissee, uwanja bei nafuu sana yaani zaidi ya sh milion 55? Yaani hata nyumba yangu imenicost zaidi ya uwanja???????? kwa nini hatuna vingi????????????????? wachina njooni mtujengee vingine kama hiyo ndio bei
      Sikujua Nsajigwa Nsalilwe kama nawe ni fisadi ...55 Million tuambie umetoa wapi?
      Nadhani typo error should read 55 Mil USD...

      Kindness is the language which the deaf can hear and the blind can see - Mark Twain
      CCM is enemy of GOD

    10. #8
      Njimba Nsalilwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd March 2008
      Location : In Africa
      Posts : 253
      Rep Power : 620
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Masanilo
      Sikujua Nsajigwa Nsalilwe kama nawe ni fisadi ...55 Million tuambie umetoa wapi?
      Nadhani typo error should read 55 Mil USD...
      Nduyu yangu Masalilo si uone mwenyewe magazeti yetu yanavyokosa proof reading?

      Kwanini siyo 55 Mill Yen or 55 Mill Euro?

      Njimba

    11. #9
      Mpita Njia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 6,700
      Rep Power : 3255
      Likes Received
      980
      Likes Given
      754

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      sasa mbona majina yanayotajwa na inv na masanilo yanatofautiana?
      I assume full responsibility for my actions, except the ones that are someone else's fault.

    12. #10
      Opaque's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th October 2008
      Posts : 953
      Rep Power : 729
      Likes Received
      227
      Likes Given
      84

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Na Shamba la Bibi ndo uwanja gani?



    13. #11
      Eeka Mangi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th July 2008
      Posts : 2,687
      Rep Power : 1094
      Likes Received
      280
      Likes Given
      173

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Opaque
      Na Shamba la Bibi ndo uwanja gani?
      Shamba La bibi si shamba na uwanja ni uwanja! Au shamba ndo uwanja?

    14. #12
      Next Level's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2008
      Location : Pwani
      Posts : 3,151
      Rep Power : 1171
      Likes Received
      76
      Likes Given
      42

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Invisible
      Wametangaza kwamba Uwanja Mpya utaitwa UWANJA WA TAIFA na wa zamani utaitwa UWANJA WA UHURU.
      Vipi huko mjini, wamesha confirm kwamba hayo ndo majina mapya ya viwanja vyetu?
      “When the missionaries came to Africa they had the Bible and we had the land. They said ''Let us pray'' we closed our eyes. When we opened them we had the Bible and they had the land.
      - Rev.Bishop Desmond Tutu.

    15. #13
      Mfumwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2008
      Posts : 1,470
      Rep Power : 841
      Likes Received
      14
      Likes Given
      1

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Next Level
      Vipi huko mjini, wamesha confirm kwamba hayo ndo majina mapya ya viwanja vyetu?
      Mkuu NL, nadhani Invisible katuandikia kuwa wametangaza kuwa Uwanja mpya utaitwa UWANJA WA TAIFA na wa zamani utaitwa UWANJA WA UHURU. Sasa sijui unahitaji cofirmation gani?. Ni kuwa magazeti yaliandika leo ndio watataja jina la uwanja mpya, na Invisible kapata hiyo habari ndio akatuwekea hapa.

      Kwa kuwa naona uwanja mpya umechukua jina la uwanja wa zamani "Uwanja wa Taifa", basi ndio maana uwanja wa zamani ukapewa jina jipya "Uwanja wa Uhuru. Na hili jina la uwanja wa zamani ni zuri, manake pale ndio zilifanyika sherehe za kupata Uhuru wetu toka kwa mwingereza.

    16. #14
      Next Level's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2008
      Location : Pwani
      Posts : 3,151
      Rep Power : 1171
      Likes Received
      76
      Likes Given
      42

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Mfumwa
      Mkuu NL, nadhani Invisible katuandikia kuwa wametangaza kuwa Uwanja mpya utaitwa UWANJA WA TAIFA na wa zamani utaitwa UWANJA WA UHURU. Sasa sijui unahitaji cofirmation gani?. Ni kuwa magazeti yaliandika leo ndio watataja jina la uwanja mpya, na Invisible kapata hiyo habari ndio akatuwekea hapa.

      Kwa kuwa naona uwanja mpya umechukua jina la uwanja wa zamani "Uwanja wa Taifa", basi ndio maana uwanja wa zamani ukapewa jina jipya "Uwanja wa Uhuru. Na hili jina la uwanja wa zamani ni zuri, manake pale ndio zilifanyika sherehe za kupata Uhuru wetu toka kwa mwingereza.
      Thanks mkubwa,

      Niliona kuna mjumbe mwingine kasema eti kasikia ule mpya utaitwa BEN NKAPA NATIONAL STADIUM...so nikaona kuana confusion hapo!
      “When the missionaries came to Africa they had the Bible and we had the land. They said ''Let us pray'' we closed our eyes. When we opened them we had the Bible and they had the land.
      - Rev.Bishop Desmond Tutu.

    17. #15
      Mfumwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2008
      Posts : 1,470
      Rep Power : 841
      Likes Received
      14
      Likes Given
      1

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Next Level
      Thanks mkubwa,

      Niliona kuna mjumbe mwingine kasema eti kasikia ule mpya utaitwa BEN NKAPA NATIONAL STADIUM...so nikaona kuana confusion hapo!
      Mkuu NL, Baba Enock nadhani hajasema amesikia, bali ametoa wazo kuwa "Jina Kamili litakuwa The Benjamin W M National Stadium", nadhani anahisi baadae uwanja utabadilishwa tena jina. Sio ajabu uwanja kuwa na jina halafuukabadilishwa, ni sawa na Barabara hata shule hubadili majina.

      Haya Mkuu na wakuu wengine tusubiri kuutunza uwanja wetu.

      NB: Hivi Yanga anacheza lini na wacomoro, Amwanga nadhani una hili jibu Mkuu, ama mkuu yoyote?

    18. #16
      Next Level's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2008
      Location : Pwani
      Posts : 3,151
      Rep Power : 1171
      Likes Received
      76
      Likes Given
      42

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Mfumwa
      Mkuu NL, Baba Enock nadhani hajasema amesikia, bali ametoa wazo kuwa "Jina Kamili litakuwa The Benjamin W M National Stadium", nadhani anahisi baadae uwanja utabadilishwa tena jina. Sio ajabu uwanja kuwa na jina halafuukabadilishwa, ni sawa na Barabara hata shule hubadili majina.

      Haya Mkuu na wakuu wengine tusubiri kuutunza uwanja wetu.

      NB: Hivi Yanga anacheza lini na wacomoro, Amwanga nadhani una hili jibu Mkuu, ama mkuu yoyote?
      Nafikiri mchezo unatakiwa kurudiwa in two weeks time tangia first leg, so nafikiri itakuwa next week hivi...(sina uhakika na tarehe)!
      “When the missionaries came to Africa they had the Bible and we had the land. They said ''Let us pray'' we closed our eyes. When we opened them we had the Bible and they had the land.
      - Rev.Bishop Desmond Tutu.

    19. #17
      Cynic's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th January 2009
      Location : Around
      Posts : 2,151
      Rep Power : 967
      Likes Received
      317
      Likes Given
      185

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Invisible
      Wametangaza kwamba Uwanja Mpya utaitwa UWANJA WA TAIFA na wa zamani utaitwa UWANJA WA UHURU.
      WaTZ bwana, sasa sijui walikuwa wanangojea nini muda wote huo! Jina la uwanja lilitakiwa lijulikane hata kabla ya ujenzi. Wembley mpya, Emirates, majina yalijulikana kabla. Na hata Green Point stadium (Cape Town) bado inajengewa lakini jina lipo.
      '... Knowledge is good, but wisdom is even better ...'

    20. #18
      Next Level's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2008
      Location : Pwani
      Posts : 3,151
      Rep Power : 1171
      Likes Received
      76
      Likes Given
      42

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Quote By Cynic
      WaTZ bwana, sasa sijui walikuwa wanangojea nini muda wote huo! Jina la uwanja lilitakiwa lijulikane hata kabla ya ujenzi. Wembley mpya, Emirates, majina yalijulikana kabla. Na hata Green Point stadium (Cape Town) bado inajengewa lakini jina lipo.
      Don't worry hiyo ni staili ya kibongo mkuu!
      “When the missionaries came to Africa they had the Bible and we had the land. They said ''Let us pray'' we closed our eyes. When we opened them we had the Bible and they had the land.
      - Rev.Bishop Desmond Tutu.

    21. #19
      babertov's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th February 2009
      Posts : 34
      Rep Power : 530
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      ilani ya chama tawala imesimamiwa vyema kwa hili.

    22. #20
      Mfumwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2008
      Posts : 1,470
      Rep Power : 841
      Likes Received
      14
      Likes Given
      1

      Default Re: Uwanja Mpya Taifa na Jina Jipya

      Serikali yapitisha jina la Uwanja wa Taifa Ule wa zamani sasa kuitwa uwanja wa Uhuru Anastazia Anyimike
      Daily News; Saturday,February 14, 2009 @20:00

      Ikiwa leo uwanja mpya wa kisasa unatarajia kufunguliwa, serikali imetangaza uwanja huo utaitwa kwa jina la Uwanja wa Taifa wakati ule wa zamani utajulikana kama Uwanja wa Uhuru.

      Akizungumza jana Dar es Salaam, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo alisema kuwa: “Kuanzia leo (jana) Februari 14, uwanja mpya wa kisasa utajulikana kama Uwanja wa Taifa na ule wa zamani utaitwa uwanja wa Uhuru.

      Alisema nia ya sekali kuita uwanja wa zamani kwa jina la Uwanja wa Uhuru ni katika kutunza historia ya Taifa. “ Uwanja wa zamani ulijengwa mwaka 1961 maalumu kwa ajili ya sherehe za Uhuru wa Tanganyika. Rais wa Tanganyika na muasisi wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikabidhiwa hati za Uhuru wa Tanzania ndani ya uwanja huo Desemba 9, 1961.

      Aidha, Mkuchika alisema kuwa serikali imefikia uamuzi huu wa kuzingatia kwamba matukio muhimu ya taifa yamekuwa yakifanyika uwanjani hapo ikiwa ni pamoja na maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania na sherehe za Muungano. “ Pia tukio muhimu na la kihistoria la kuwapa fursa wananchi ya kuaga mwili wa aliyekuwa muasisi wa Taifa letu, Mwalimu Nyerere lilifanyika uwanjani hapo.

      Kwa kuzingatia sifa hizi na nia ya serikali kutunza historia ndiyo maana tumeamua kutoa majina hayo. Akijibu swali ni kwa nini uwanja huo usingepewa jina la Rais Mstaafu wa Awamu wa Tatu, Benjamini William Mkapa kama wadau wengi walivyotaka, Mkuchika alisema: “ Rais mstaafu (Mkapa) amefanya mambo mengi makubwa katika nchi hii na kama tutaenzi kila kazi aliyofanya basi majina yake yatakuwa kila mahali.

      “ Hata hivyo, tayari kuna shule ya sekondari iliyopewa jina lake, jengo la Mafuta House limeitwa kwa jina lake na pia daraja kubwa Afrika Mashariki na Kati nalo limeitwa kwa jina lake. Ninachoweza, katika kuheshimu mchango wake, kesho (leo) wakati wa ufunguzi amealikwa na amethibitisha kuhudhuria,” alisema.

      Uwanja huo ambao umejengwa na kampuni ya China ya Beijing Construction Engineering Company Limited ulianza kujengwa Januari 2005 kwa ushirikiano wa Serikali ya China na Tanzania. Gharama za ujenzi wa uwanja huo ni dola za Marekani milioni 56.4 (zaidi ya bilioni 56) ambapo Serikali ya Tanzania imetoa dola za Marekani milioni 23 na Serikali ya China imetoa dola za Marekani milioni 33.4.

      Aidha, Mkuchika alisema kuwa kwa sasa uwanja huo utaendeshwa na Kamati Maalumu iliyo chini ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Dk. Florens Turuka baada ya kushindikana kupata mtu mwenye sifa za kuendesha uwanja huo.

      “ Tulitoa tangazo kwa watu wanaotaka kuendesha uwanja huo na watu waliojitokeza wamekosa sifa za kupewa kazi hiyo, hivyo tumetangaza tena, lakini kwa sasa utakuwa chini ya usimamizi wa Kamati Maalumu inayoongozwa na Katibu Mkuu”. Uwanja huo unatarajia kufunguliwa leo na Rais wa China Hu Jintao aliyepewa mwaliko na Rais Jakaya Kikwete na kuhudhuriwa na Rais mstaafu Benjamini Mkapa na viongozi wengine wa serikali.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Uwanja mpya wa taifa: Sizitaki kura za wanasimba?
      By Phillemon Mikael in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 0
      Last Post: 3rd September 2010, 22:34
    2. Washaanza Kuuharibu Uwanja Wa Taifa Mpya
      By barabaraya18 in forum Sports
      Replies: 16
      Last Post: 12th July 2007, 18:57
    3. Maoni jina la uwanja mpya
      By Jafar in forum Sports
      Replies: 9
      Last Post: 17th January 2007, 03:00

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...