Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mwanamke afundisha timu ya soka ya wanaume.

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      Dj Khalid's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd March 2010
      Posts : 43
      Rep Power : 476
      Likes Received
      5
      Likes Given
      3

      Default Mwanamke afundisha timu ya soka ya wanaume.

      Mwanamama aitwaye Donna Powell ametengeneza historia huko nchini Uingereza ya kuwa mwanamama wa kwanza kuwa kocha wa timu ya soka, na hii yote ni baada ya kushinda shindano la kumtafuta kocha mwananama wa kwanza wa timu moja ya nchini Uingereza iitwayo Fisher Athletic. Mama Powell alipewa jukumu hilo la kuwasaidia Fisher athletic kuepuka kushuka daraja baada ya kushinda mnada ambao zawadi yake ilikuwa ni kupata nafasi ya kufundisha soka kwa siku moja katika timu ya Fisher. Inaaminika kuwa Mama Powell ndiye alikua mwanamama wa kwanza kuwa kocha wa klabu ya soka ya wanaume. Lakini hii yote ilianzaje? na ikawaje hadi mwanamke huyu akajikuta akikabidhiwa jukumu hilo zito la timu hiyo ambayo ukiachilia mbali matatizo yake ya kifedha pia ilikua hatarini kushuka daraja. Mama Powell mwenyewe alinukuliwa akisema kuwa mabosi wa timu hiyo walifanya mkutano na kufikia uamuzi wa kufanya shindano la kumtafuta kocha wa kike kwa siku moja ikiwa ni njia ya kuchangisha pesa kwa ajili ya kuinusuru klabu hiyo. Mama Powell anakubali kuwa isingekuwa hilo shindano kamwe asingeweza kupata nafasi hiyo sababu kubwa ikiwa yeye ni mwanamke. Mwanamke huyo alielezea kwamba alishawahi kuomba kazi katika nafasi hiyo mara baada ya kocha wa zamani kuondoka lakini mabosi walifikiri kuwa anatania, lakini kipindi hiki Mama Powell alijipiga mfukoni akakusanya kiasi cha pauni 500 ili aweze kushiriki katika shindano lililomuweka hapo. Mama Powell ambaye kabla ya hapo alikuwa kocha wa timu ya vijana chini ya miaka 11 iitwayo Red Lion Boys club amekabidhiwa mikoba ya kuifunga timu ya Eastleigh katika mechi yake ya kwanza akiwa katika benchi la ufundi la Fisher athletic. Tayari Mama Powell anakwambia alishafanya utafiti kuhusu timu pinzani na mpango wake wa kwanza ni kubadili mfumo wa uchezaji wa timu yake toka mfumo wa 3-5-2 na kuwa 4-4-2 sababu aliamini vijana wake wangecheza mfumo huo wangepata nafasi ya kumiliki mpira zaidi. Mwenyekiti wa klabu ya Fisher Martin Eddie alisema kwamba baada ya mwezi tu ndani ya msimu iliwalazimu kuwaachia wachezaji wote waondoke sababu walishindwa kuwalipa mishahara yao. Kocha wa zamani ilibidi aondoke na kuhamia timu nyingine wakabaki mabosi wawili akiwemo mwenyekiti na watu wachache waliojitolea kuisaidia timu hiyo. Mama Powell hakuamini kabisa kuwa Fisher wangeshuka daraja ingawa walikuwa katika nafasi ya pili toka mkiani wakiwa wamefungwa mechi 11 mfululizo!Mama Powell anajiamini sana juu ya uwezo wake na mara zote huwa yuko thabiti na msimamo wake kuwa Fisher haitoshuka daraja kamwe, anachukulia kazi yake kwa umakini mkubwa sana. Ingawa kifedha klabu hiyo haikua katika hali nzuri Mama Powell aliamini kuna njia nyingi sana za kuwahamasisha wachezaji katika vyumba vya kubadili nguo ama mazoezini. Kila mchezaji alijua baada kufungwa mechi 11 mfululizo kilichohitajika ni ushindi tu na wala si kingine. Mama Powell ambaye ana daraja la kwanza na pili la ukocha linalotambulika na chama cha soka nchini Uingereza si mgeni katika ulimwengu wa soka uliotawaliwa na wanaume, na alijua fika mikiki mikiki yote ambayo angekumbana nayo wakati akiwa katika benchi la timu ya Fisher, hii ilikua nafasi ya kung'ara kwa nyota yake. Anaelezea kwamba alishawahi kukumbana na makocha wa timu pinzani ambao waligoma kusalimiana naye mara baada ya timu yake kuwapa kichapo. Anasema wengi huwa wanakuwa wakijisikia wamedhalilishwa sababu ya kufungwa na mwanamke. Anamalizia kwa kusema kuwa anadhani ni muda umefika kwa wanawake kufundisha soka, kama wanaume wanaweza kwa nini wanawake wasiweze?

    2. Miaka 50

    3. #2
      mchapa shughuli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th May 2011
      Posts : 252
      Rep Power : 455
      Likes Received
      28
      Likes Given
      0

      Default Re: Mwanamke afundisha timu ya soka ya wanaume.

      si mchezo..safi

    4. #3
      Vin Diesel's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st March 2011
      Posts : 5,866
      Rep Power : 19946
      Likes Received
      2792
      Likes Given
      1615

      Default Re: Mwanamke afundisha timu ya soka ya wanaume.

      kumbe timu yenyewe ni ya mchangani.
      Simulated Automated Breakthroughs....

    5. Study Abroad

    Similar Topics

    1. Camacho afundisha Soka Mourhino
      By Mulongo Poteka in forum Sports
      Replies: 0
      Last Post: 30th January 2011, 21:57
    2. soka la wanawake bongo laanza kung`ara, Asha apata timu uturuki!.
      By binti ashura in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 25th January 2011, 12:59
    3. Tetesi: Waislamu Wakasirishwa na Wimbo wa Timu ya Soka ya Ujerumani
      By Bikra in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 6
      Last Post: 7th August 2009, 13:45
    4. Tanzania timu za soka ni mbili tu!!
      By MtuSomeone in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 2
      Last Post: 26th January 2009, 23:00

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...