|
Taifa Stars, Msumbiji waingiza Sh605milioni

12th September 2007, 08:20 PM
Taifa Stars, Msumbiji waingiza Sh605milioni
Na Phillip Nkini
Kutoka Gazeti la Mwananchi
BAADA ya kusita kwa siku tatu kutangaza mapato ya mechi ya kufuzu ya fainali ya Mataifa ya Afrika baina ya Taifa Stars na Msumbiji, jana Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lilitangaza kuwa Sh605milioni zilipatikana katika mechi hiyo iliyofanyika katika uwanja mpya wa kisasa jijini Dar es Salaam.
Stars ilipata kipigo cha 1-0 kutoka kwa Msumbiji katika mechi hiyo iliyochezwa Jumamosi jambo ambalo lilifanya timu zote mbili kushindwa kufuzu kwenda Ghana mwakani katika fainali za Mataifa ya Afrika ambazo zitafanyika Januari 20 hadi Februari 10.
Senegal, ndiyo imefuzu kutoka katika Kundi la Saba baada ya kuifunga Burkina Faso mabao 5-1.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Fedha wa TFF, Silas Mwakibinga alisema watazamaji 55,514 walijitokeza kuona mechi hiyo katika uwanja mpya wenye uwezo wa kubeba mashabiki 57,129.
Mwakibinga alisema Sh 605, 020,000 zilipatikana ambazo ni sawa na asilimia 94 ya uwezo wa uwanja huo katika kiingilio cha siku hiyo.
''Si kweli kuwa uwanja mpya unaingiza watu 60,000 kwani viti vilivyopo uwanjani ni 57,129 kwa hiyo idadi hiyo ndio ya tiketi zilizotengenezwa,'' alisema mkurugenzi huyo.
Alisema watazamaji 743 walikata tiketi za Sh 50,000 katika Jukwaa la VIP (A), 1,973 walikata tiketi za Sh 40,000 katika Jukwa la VIP (B) na wengine 2,242 walikata tiketi za Sh 30,000 za VIP (C).
Alisema jukwaa lenye rangi ya machungwa (orange straight) linalotazamana na VIP, waliingia watu 5,326 kwa kiingilio cha Sh 20,000 huku jukwaa kama hilo nyuma ya magoli wakiingia watu 7,300 kwa kiingilio cha Sh 10,000.
Alisema viti vya bluu mzunguko waliingia watazamaji 18,340 kwa kiingilio cha Sh 10,000 na jukwaa la kijani waliingia watu 19,590 kwa kiingilio cha Sh 3,000.
Mkurugenzi huyo alisema tiketi nyingine zote zilimazika isipokuwa za Sh 20,000 ambazo kama zingemalizika zote jumla zingepatikana Sh 644,530,000.
''Si kweli kwamba tiketi zote zilimalizika kwani tiketi za 20,000 hazikwisha," alifafanua.
Alisema mapato haya yalichelewa kutangazwa kutokana na kamati kukamilisha taratibu zake zote na walitaka kutangaza kitu cha uhakika zaidi.
Mwakibinga alisema udhibiti wa watu walioingia uwanjani ulikuwa wa kuridhisha na hakukuwa na matatizo.
Tangu kuchezwa kwa mechi hiyo kumekuwa na manung'uniko na uvumi kutoka kwa wadau wa soka ambao hawakuridhishwa na mapato ya Sh milioni 234 yaliyopatikana katika mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars na Uganda iliyofanyika Jumamosi ya wiki iliyopita.
__________________
~*~Life is Good~*~
|
Bubu Ataka Kusema
JF Premium Member
Join Date: Sun Feb 2007
Location: Mfaranyaki
Posts: 12,663
Thanks: 1,027
Thanked 1,188 Times in 690 Posts
|
|