Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna????? - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Sports & Entertainment Forum


Sports & Entertainment Forum Talk about Music, Sports, TV Shows, Movies, Entertainment & Much More


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 18th June 2008, 04:47 PM   #1
Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????
Mtu wa Pwani Mtu wa Pwani is offline 18th June 2008, 04:47 PM

haya wale magwiji wa michezo ambao mlikuwa mkifatilia kwa muda mrefu mvutano uliopo kati ya ZFA na TFF hii inatokana na kuwa ZFA ni wapenda migogoro au kuna namna.

jee huyu mwakalebela hutumia kutofahamina kati ya ZFA na SMZ ni kisingizio cha kuhalalisha ufifilishi wao kwa ZFA na zanzibar kwa ujumla?
ZFA ni wapenda migogoro - Mwakalebela
2008-06-18 09:03:14
By Somoe Ng\'itu


Shirikisho la soka nchini (TFF) limesema kuwa Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA) kinatumia muda mwingi kuanzisha malumbano na migogoro inayohusiana na safari za nje ya nchi badala ya kuandaa programu za maendeleo ya mchezo huo visiwani humo.

Akizungumza na Nipashe jana, Katibu Mkuu wa TFF, Frederick Mwakalebela alisema kuwa viongozi wa ZFA ambao hivi karibuni wametangaza rasmi kutoshirikiana na shirikisho hilo kuhusiana na timu ya taifa, Taifa Stars kila siku wamekuwa wakianzisha `hoja` zinazopingana na serikali yao na pia wakilalamikia vitu ambavyo ufafanuzi wake wanaufahamu na kuipotosha jamii.

Mwakalebela alisema kuwa katika kuonyesha kuwa chama hicho kinatumia muda mwingi `kulumbana` badala ya kufanya shughuli za maendeleo kimetangaza kutoshirikiana na TFF huku timu zao za vijana za umri chini ya miaka 17 ziko jijini Dar es Salaam na zinashiriki katika mashindano yanayojulikana zaidi kwa jina la Copa Coca Cola yanayoendelea katika viwanja mbalimbali.

``ZFA wanashindwa kujielewa mambo wanayosema na wanayofanya, kama wamevunja ndoa na TFF ni kwanini wameleta timu katika mashindano ya U-17 na mjumbe wao pia yupo,`` alisema Mwakalebela.

Aliongeza kuwa kila inapotokea safari ya viongozi wa TFF wanakwenda katika mikutano ya kimataifa kuiwakilisha nchi ndio malalamiko yanapoanza na wao wanashindwa kuwaelewa ZFA ambao wanafahamu wazi kuwa waalikwa wa mikutano hiyo ni TFF ndio wanachama wa mashirika ya soka ya kimataifa.

Alisema pia kila kinachofanywa na TFF kinatokana na maelekezo yaliyopo katika katiba na wao ZFA wana katiba yao inaowaongoza katika shughuli za kila siku za kuongoza soka hapa nchini.

Alisema kuwa ZFA mara kadhaa wameshindwa kukubali kuihudumia timu ya taifa, Taifa Stars inapotaka kwenda visiwani humo na wakati TFF imeisaidia timu yao, Zanzibar Heroes na kuinunulia vifaa ilipokuja katika mashindano ya Kombe la Chalenji mwaka jana lakini yote hayo hayasemwi.

``Umefika wakati wakaacha kuipa kipaumbele migogoro na kuangalia mambo ya msingi ya maendeleo, TFF ni wanachama wa FIFA (Shirikisho la soka la kimataifa) tutafanya kila kinachotakiwa kukuza soka hapa nchini,`` aliongeza.

Siku moja kabla ya Stars haijacheza na timu ya taifa ya Cameroon, Makamu wa Rais wa ZFA, Haji Ameir alikaririwa akisema kuwa wao wamevunja `ndoa` na TFF na kudai kuwa Stars ni timu ya Tanzania Bara.

SOURCE: Nipashe
__________________
Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown

 
Mtu wa Pwani's Avatar
Mtu wa Pwani
JF Senior Expert Member
Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Tue Dec 2006
Posts: 2,860
Thanks: 6
Thanked 8 Times in 7 Posts
Views: 638
Reply With Quote
  #2  
Old 18th June 2008, 05:08 PM
Kibunango's Avatar
Kibunango Kibunango is offline
Kibunango Mapinduzi Daima...! CCM Damu.
JF Senior Expert Member
Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100
Activity: 39% Activity: 39% Activity: 39%
 
Join Date: Tue Aug 2006
Location: Tampere
Posts: 4,870
Thanks: 351
Thanked 207 Times in 169 Posts
Rep Power: 4033
Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!
Send a message via MSN to Kibunango Send a message via Yahoo to Kibunango
Default Re: Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

Kwa wale wote ambao walikuwa wakibeza juhudi za Farouk Karim sasa watatia akili akiwepo huyo mwenyeki wa sasa wa ZFA... Mapungufu ya TFF na SMZ kuingilia mara kwa mara maamuzi ya ZFA ndio yamempa mdomo hiyo Katibu Mkuu wa TFF.
__________________
Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problems,
But, if you think again, neither does milk."
Vituko Vya Zenj
Reply With Quote
  #3  
Old 20th June 2008, 06:25 PM
Mtu wa Pwani's Avatar
Mtu wa Pwani Mtu wa Pwani is offline
Mtu wa Pwani Si Kila Kin'garacho ni dhahabu
JF Senior Expert Member
Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Dec 2006
Posts: 2,860
Thanks: 6
Thanked 8 Times in 7 Posts
Rep Power: 28
Mtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enough
Default Re: Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

farouk kariim alibezwa kivipi ?
__________________
Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown
Reply With Quote
  #4  
Old 21st June 2008, 03:01 AM
Masatu Masatu is offline
Masatu Is Magumashi
JF Senior Expert Member
Points: 733,039, Level: 100 Points: 733,039, Level: 100 Points: 733,039, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
 
Join Date: Mon Jan 2007
Location: Mbagala, Jeshini
Posts: 3,741
Thanks: 0
Thanked 88 Times in 66 Posts
Rep Power: 0
Masatu is infamous around these parts
Default Re: Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

TFF nao wamezidi safari za Taifa stars wanaenda wao tu walau wachukue mtu mmoja kutoka ZFA ile ni timu ya Taifa sio bara hawajui hata kura na kipofu! halafu wakilalamika mnasema wanapenda migogoro
__________________
Mkulima kala Mbegu......
Reply With Quote
  #5  
Old 21st June 2008, 09:50 AM
Kibunango's Avatar
Kibunango Kibunango is offline
Kibunango Mapinduzi Daima...! CCM Damu.
JF Senior Expert Member
Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100
Activity: 39% Activity: 39% Activity: 39%
 
Join Date: Tue Aug 2006
Location: Tampere
Posts: 4,870
Thanks: 351
Thanked 207 Times in 169 Posts
Rep Power: 4033
Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!
Send a message via MSN to Kibunango Send a message via Yahoo to Kibunango
Default Re: Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

Quote:
View Post
farouk kariim alibezwa kivipi ?
Kariim ndio aliye anzisha jitihada za Zenj kujulikana na FIFA na CAF, akiwa katika hatua za mwisho mwisho wakamletea za kuleta na yeye akaweka madaluga chini...
__________________
Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problems,
But, if you think again, neither does milk."
Vituko Vya Zenj
Reply With Quote
  #6  
Old 23rd June 2008, 11:13 AM
Mtu wa Pwani's Avatar
Mtu wa Pwani Mtu wa Pwani is offline
Mtu wa Pwani Si Kila Kin'garacho ni dhahabu
JF Senior Expert Member
Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Dec 2006
Posts: 2,860
Thanks: 6
Thanked 8 Times in 7 Posts
Rep Power: 28
Mtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enough
Default Re: Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

SMZ yaipinga ZFA
2008-06-23 10:32:01
By Mwinyi Sadallah,Zanzibar


Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imesema kuwa haikubaliani na tamko lililotolewa na Chama cha soka cha Zanzibar (ZFA) juu ya kujitenga na kuvunja ushirikiano na Shirikisho la mchezo huo Tanzania (TFF).

Akizungumza juzi visiwani hapa, Naibu Waziri Kiongozi na Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Ali Juma Shamhuna alisema kuwa SMZ haikuwatuma viongozi wa ZFA kutamka kauli hizo na kuongeza kuwa wao wanaitambua TFF na wataendelea kushirikiana nao katika mambo mbalimbali ya maendeleo ya soka hapa nchini.

Waziri Shamhuna alisema kwamba uamuzi uliotolewa na ZFA kupitia Makamu wake wa Rais, Haji Ameir uliishitua serikali na kuongeza kuwa chama hicho hakina mamlaka ya kuvunja ushirikiano wa kimichezo baina ya Zanzibar na Tanzania Bara.

``Ushirikiano wa TFF na ZFA uko pale pale, na hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuuvunja,`` alisema Shamhuna.

Alisema kwamba timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ni timu ya watanzania na sio timu ya TFF au ZFA, na kwa msingi huo viongozi wa ZFA hawakupaswa kutoa tamko la kumtaka kocha msaidizi wa Stars Ali Bushiri pamoja na wachezaji wa timu hiyo wanaotoka Zanzibar kurejea nyumbani kwa madai ya kuwa kuwepo kwao katika timu hiyo hakuifanyi timu hiyo kuwa na sura ya Muungano.

Alisema kwamba Serikali haitovumilia watu wanaotaka kuvuruga Muungano kwa kisingizio cha michezo na kwa kufanya hivyo wanakwenda kinyume na katiba ya nchi inayozungumzia kuwa Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aliongeza kuwa kutokana na uzito wa maneno yaliyotolewa na kiongozi huyo wa ZFA, atakutana na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Muungano, George Mkuchika ili kuzungumzia tofauti zilizojitokeza baina ya taasisi hizo zinazoongoza michezo Tanzania Bara na Visiwani baada ya vikao vya bajeti vinavyoendelea Dodoma na Zanzibar kumalizika.

Alisema ni jambo la kushangaza shutuma za ZFA zinatolewa huku baadhi ya viongozi wake wakiwa wanashiriki katika mashindano ya Copa Coca Cola yanayoshirikisha vijana wenye umri chini ya miaka 17 ambayo yanalenga kuinua vipaji vya vijana.

Alisema kwamba ZFA hivi sasa inapaswa kuwaeleza wanamichezo kuwa ina mikakati gani ya kuinua kiwango cha michezo Zanzibar hasa ikizangatiwa kuwa ni sehemu pekee inayoendelea kuendesha ligi yake katika muda wa mapumziko.

SOURCE: Nipashe
__________________
Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown
Reply With Quote
  #7  
Old 23rd June 2008, 11:15 AM
Mtu wa Pwani's Avatar
Mtu wa Pwani Mtu wa Pwani is offline
Mtu wa Pwani Si Kila Kin'garacho ni dhahabu
JF Senior Expert Member
Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Dec 2006
Posts: 2,860
Thanks: 6
Thanked 8 Times in 7 Posts
Rep Power: 28
Mtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enough
Default Re: Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

Quote:
View Post
Kariim ndio aliye anzisha jitihada za Zenj kujulikana na FIFA na CAF, akiwa katika hatua za mwisho mwisho wakamletea za kuleta na yeye akaweka madaluga chini...
vipi kuhusu Ali Tamim Fereji ? nnakumbuka yeye ndio alikuwa akienda mbio na hili?


halafu kwa nn Shamhuna na ZFA(viongozi) picha haziendi?
__________________
Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown
Reply With Quote
  #8  
Old 23rd June 2008, 11:30 AM
Kibunango's Avatar
Kibunango Kibunango is offline
Kibunango Mapinduzi Daima...! CCM Damu.
JF Senior Expert Member
Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100
Activity: 39% Activity: 39% Activity: 39%
 
Join Date: Tue Aug 2006
Location: Tampere
Posts: 4,870
Thanks: 351
Thanked 207 Times in 169 Posts
Rep Power: 4033
Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!
Send a message via MSN to Kibunango Send a message via Yahoo to Kibunango
Arrow Re: Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

Quote:
View Post
vipi kuhusu Ali Tamim Fereji ? nnakumbuka yeye ndio alikuwa akienda mbio na hili?


halafu kwa nn Shamhuna na ZFA(viongozi) picha haziendi?
Picha siku zote hazitakwenda kati ya ZFA na Wizara yao.. Kwani kumekuwewpo na mitazamo tofauti juu ya uendeshaji wa soka hapo kisiwani.. Siku zote wizara inataka watu ambao watasimamia matakwa ya wizara katika kuendesha shughuli za ZFA, wakati ZFA inatakiwa kuendeshwa kwa katiba yao na sio kwa kauli za waziri wa michezo.

Ndio maana kila waziri aingiae kwenye wizara hiyo lazima atapandikiza mtu wake.... hapo ZFA tena mwenye uwezo wa kutoa uwamuzi...
__________________
Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problems,
But, if you think again, neither does milk."
Vituko Vya Zenj
Reply With Quote
  #9  
Old 23rd June 2008, 12:16 PM
Mtu wa Pwani's Avatar
Mtu wa Pwani Mtu wa Pwani is offline
Mtu wa Pwani Si Kila Kin'garacho ni dhahabu
JF Senior Expert Member
Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100 Points: 916,995, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Dec 2006
Posts: 2,860
Thanks: 6
Thanked 8 Times in 7 Posts
Rep Power: 28
Mtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enough
Default Re: Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

Quote:
View Post
Picha siku zote hazitakwenda kati ya ZFA na Wizara yao.. Kwani kumekuwewpo na mitazamo tofauti juu ya uendeshaji wa soka hapo kisiwani.. Siku zote wizara inataka watu ambao watasimamia matakwa ya wizara katika kuendesha shughuli za ZFA, wakati ZFA inatakiwa kuendeshwa kwa katiba yao na sio kwa kauli za waziri wa michezo.


Ndio maana kila waziri aingiae kwenye wizara hiyo lazima atapandikiza mtu wake.... hapo ZFA tena mwenye uwezo wa kutoa uwamuzi...
nimekuelewa sana, sasa safari hii vipi wizara ilishindwa kuplant mtu wao au kulikoni ?


halafu kwa nini wasitafute njia yakukaa nakujadili kwa kina njia bora ya kuendesha soka visiwani.

maana mambo yakienda hivi ni aibu kwa taifa na kama mwakalibela alivyotukebehi.
__________________
Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown
Reply With Quote
  #10  
Old 23rd June 2008, 08:48 PM
Kibunango's Avatar
Kibunango Kibunango is offline
Kibunango Mapinduzi Daima...! CCM Damu.
JF Senior Expert Member
Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100
Activity: 39% Activity: 39% Activity: 39%
 
Join Date: Tue Aug 2006
Location: Tampere
Posts: 4,870
Thanks: 351
Thanked 207 Times in 169 Posts
Rep Power: 4033
Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!
Send a message via MSN to Kibunango Send a message via Yahoo to Kibunango
Default Re: Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

Quote:
View Post
nimekuelewa sana, sasa safari hii vipi wizara ilishindwa kuplant mtu wao au kulikoni ?


halafu kwa nini wasitafute njia yakukaa nakujadili kwa kina njia bora ya kuendesha soka visiwani.

maana mambo yakienda hivi ni aibu kwa taifa na kama mwakalibela alivyotukebehi.
Nahisi ZFA kiwe chombo huru... Kiwe na katiba yake ambayo haitaweza kubanwa na smz, kiwe chombo kinachojitegemea pasipo kuwa omba omba toka smz.. ila katiba yao isivunje katiba ya muungano. Katiba hiyo iweke bayana nafasi ya ZFA katika TFF na iwapo siku Zenj itakapokubalika FIFA basi mazagazaga ya TFF yawekwe pembeni.

Baraza la michezo Zenj nalo litokane na katiba mama ya ZFA.. na kiwe ni chombo cha rufaa ya faida ya soka la Zenj badala ya kusimamia matakwa ya smz katika soka la visiwa hivyo.
__________________
Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problems,
But, if you think again, neither does milk."
Vituko Vya Zenj
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
au, kuna, kweli, migogoro, namna, wapenda, zfa


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Ni wakati wa kuacha woga! Invisible Habari na Hoja mchanganyiko 6 4th June 2009 10:01 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 11:11 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com