Ombi maalumu kwa Mshana jr na Peterchoka

Kitang'wa1

JF-Expert Member
Dec 4, 2014
460
285
Hello!
Nimekusoma leo mshana jr, unajua kupangilia maandiko yako, tafadhali kukicha salama, utumalizie nini kiliendelea, japo tuweze kujifunza. Ubarikiwe sana.

Peterchoka, tafadhali imalizie ile simulizi ya 'jamaa aliyemuona mwanafunzi akilia huku akinyeshewa mvua', nimeusubiria muendelezo wake siuoni. Hadi najiuliza, sijui walivyokutukana na kuku-crash (baadhi) ya wadau humu, ndiyo umechukia ama umesusa? Wazoee hao tafadhali.

Kiufupi ninapenda simulizi zako (peterchoka na wengineo wataalamu wa hayo).

Kuhusu mshana jr, najifunza mengi sana kwa kupitia mabandiko yako (naamini nilishakuambia hili), zaidi pia napenda na kufurahi unavyojibu hoja, matusi, maswali, kashfa, tokea kwa wadau wengine.

Tafadhali msichoke, mzidi kutuelimisha.

NOTE:
SIJAWABAGUA WOTE MNAOJUA KUANDIKA, KUSIMULIA, KUJIBU HOJA, MASWALI, MATUSI, KASHFA, FEDHEHA, N.K TATIZO ID ZENU SIJAZIKARIRI.

Ahsante!
 
Back
Top Bottom