Wana-JF
Jumamosi hii katika kipindi cha Makutano kuanzia saa tisa mchana nitakuwa na Profesa Ibrahim Lipumba. Nitazungumza nae kuhusu mambo yanayogusa medani ya kisiasa, na pia mtazamo wake kuhusu hali ya nchi kwa sasa. Kama ilivyokuwa kwa vipindi vingine napenda kupata maswali toka hapa...
Wana-JF
Jumamosi hii katika Makutano nitakuwa na Mbunge wa Ubungo kupitia CHADEMA, Mheshimiwa John Mnyika. Na kama kawaida ya kipindi tutagusa kuanzia maisha yake ya kawaida mpaka kwenye siasa. Kama ada, kipindi kinaendeshwa na maswali mengi kutoka kwa wananchi hivyo napenda kuchukua fursa hii...
Wana-JF
Kama nilivyowaambia Jumamosi nilikuwa na Mhe January Makamba ambapopamoja na kuelezea maisha yake ya kawaida ya kisiasa pia alijibumaswali yenu.
Moja ya vitu alivyosema ni kuwa hana mpango wa kugombea Urais. Alisema anaamini nafasi ya urais inahitaji mtu ambaye amejiandaa...
Wana-JF
Wiki chache zilizopita nilipata udhuru sikuweza kuendesha kipindi na kukusanya maswali toka hapa JF, na sasa nimerejea.
Katika Makutano Jumamosi hii natarajia kuwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mheshimiwa January Makamba tukijadili maisha yake ya kawaida na...
Jumamosi katika kipindi cha Makutano nitakuwa na Mbunge wa Nachingwea ambaye pia ni Waziri wa Sheria na Katiba Mheshimiwa Mathias Chikawe tukiongea mambo mbalimbali ikiwemo suala la Katiba mpya.
Mheshimiwa Waziri anataka kupokea maswali na maoni toka JF, unakaribishwa kuuliza na yatamfikia. Pia...
Wana-JF
Kwenye Makutano Jumamosi hii atakuwepo katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Nape Nnauye na baadae mkurugenzi wa Clouds Media Group Ruge Mutahaba.
Moja ya vitu atakavyoiongelea Nnape ni kuhusu kauli yake ya kuwa CHADEMA ina wafadhili nje ya nchi na kuwa harambee ya M4C Jumamosi Serena...
Katika kipindi cha Makutano Jumamosi ijayo mgeni atakaeongea na Fina Mango ni mbunge wa Singida Mjini Mheshimiwa Mohammed Dewji atakaeongea masuala mbalimbali ikiwepo maisha yake binafsi, ya kisiasa na kibiashara.
Kama una swali lolote ambalo ungependa Mheshimiwa Dewji alijibu tafadhali uliza...
Ibambasi
Kwa sasa Kipanya anafanya kazi Redio nyingine si unajua mambo ya mikataba ya ajira. Nitafurahi pia kufanya nae kazi ka mara nyingine.
Asante sana kwa ushauri
Edson
Website ya Magic FM inafanyiwa matengenzo kwa sasa lakini kabla ya kipindi kingine Jumamosi itakuwa hewani na tutaiweka hapa ili wadau wote muweze kusikiliza.
Shukrani Sizinga
Kipindi ni kila Jumamosi kuanzia saa tisa hadi kumi na mbili jioni. Kuhusu live kwenye TV ondoa shaka liko ndani ya mipango itakapokuwa tayari nitakufahamisha.
Asante sana.
Wadau wa JF
Nawashukuru sana wote mliochangia katika kipindi cha kwanza cha Makutano kilichorushwa Magic FM kuanzia saa tisa mchana hadi kumi na mbili jioni kwa kumuuliza maswali Mheshimiwa Zitto Kabwe na pia kutoa maoni. Nilijaribu kadri ya uwezo wangu kumuuliza maswali yenu na aliyajibu...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.