Nendeni Kenya ndo mkaone Jeshi linafanya kazi gani.Kuanzia saa 12 jioni ni full doria na SMG ziko front.Tanzania tunachezea Amani yetu.Waislam mnamasiala sana.Mambo ya Watoto mnatuchanganya Wakristo wote na kuchafua hali ya Nchi,Shauri yenu nawaambia.
kuna Mchangiaji kutoka eneo la Jangwani anawakilisha.
Walislam wamegomea Sensa,Wamechoma Makanisa pasipokuwa na Mahakama ya Khadhi.Ikianzishwa si ndo watatumaliza?
Inanisilitisha Mpaka Muda huu,Imebaki Dakika 50 Jukwaa lifungwe,Sijamsikia Mtu mwenye MA,First Degree wala Diploma kuwasilisha Maoni.Nimesikia Wasio na Elimu,Std 7,Form 4 na Form 6,Sijui wengine wana hide CV au ni vipi...
Mkuu wa Mkoa achaguliwe na Wananchi kwani Watamchagua Mtu anaye ujua Mkoa husika.Tabia ya kupeleka Wakuu wa Mikoa wageni,inawapunguzia ufanisi katika kazi kwani hawajui vizuri Mikoa wanayo iongoza.
Mawasiliano na Tume ya Katiba
Email: maoni@katiba.go.tz
Tovuti:Tume ya Mabadiliko ya Katiba
Facebook: tumeyamabadilikoyakatiba
Barua.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba
S.L.P 1681,Dar Es Salaam
S.L.P 2775,Zanzibar
Tafadhali taja Jina Kamili,Jinsia,Mahali unapo ishi,Umri,Elimu na Kazi ndipo...
Kuna Mwakilishi anasema
Kama wimbo wa Taifa unamtaja Mungu,iweje tuseme Serikali haina Dini?,huo ni utapeli.
Katiba itamke wazi kuwa Ijumaa ni mapumziko na Jumapili.Ijumaa ya Waislam na Jumapili wa Wasabato na Wakristo.
Pia anaomba mahakama ya Khadhi.
Anaomba OIC iwekwe kwenye Katiba.
Kuna Mzee anachangia,anaomba Elimu kuanzia chekechea mpaka kidato cha sita iwe bure.Pili Mbunge anapokatiwa rufaa na kupokonywa ubunge,Mbunge wa pili ndio apewe ubunge kuepuka gharama za uchaguzi sizizo na sababu.
Kuna Mama anahoji,Kwa Nini Waislam wanataka Mahakama ya Khadhi?,kwani kama ni kesi za Ndoa,mbona Wakristo wana huwa wanatatua matatizo ya Ndoa kwa kutumia Wachungaji na Mapadri?
Kuna Siter wa RC anaombakuwe na Muda wa Kikomo Bungeni.Miaka 10 kama kwa Rais na Rais aondolewe kinga ya Mashtaka.Akifanya fyongo,ashtakiwe kama waahalifu wengine...
Kuna Mama ameomba Ijumaa iwe siku ya Mapumziko kama Jumamosi na Jumapili.Amesema wasabato ni wachache lakini wanapumzika Jumamosi,Waislam ni wengi lakini hakuna Mapumziko Ijumaa.So Ijumaa isiwe siku ya kazi...
kunagawiwa fomu.Kwa wasio taka kuongea watazitumia kujaza maoni yao.
Kwa wanao taka kutuma maoni kwa njia ya sms,Andika Jina,Kazi,Mahali unapoishi,Tuma maoni yako kwenda namba 0715 / 0787/ 0767/ 0774 081 508
Kuna kina Mama wa Kiislam nawaona Mbele yangu.Kweli wamejipanga na shughuli hii.Inapendeza.Wako na vikaratasi vina maandishi fulani wanakumbushana,Inaelekea walikuwa na Darasa Maalumu ya hili na nini waje waseme.Nasubiri watakacho kiwakilisha NIWAJUZE WANA JF.
hii kitu mimi sielewi.Zanzibar walifanya hivi na wakapata katiba yao.Leo hii Tanzania tunafanya na kuna wawakilishi kutoka Zanzibar.Mimi nilidhani hapa tunachanganyana.Zanzibar wamefanya wenyewe.Tanzania tunafanya wote,Why?.Kuna haja ya kuwa na Serikali 3 au serikali Moja hapa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.