Watu wengine bhana sasa hata kama yeye mwenyewe ndo mhusika si msaidie kwa vile ameomba msaada njia ya kuacha ushoga.Kama huna au hujui njia ya kusaidia si lazima uweke comment zisizo na msaada kaa kimya,kweli wewe cobra.
Usinikumbushe Mselem ni noma,ukipata B Plain unajiona shujaa,nasikia bado anatesa watu hadi leo. Km utakua ni miongoni mwa wanafunzi waanzilishi utakumbuka first year tulimkataa tukaletewa Juma wa Open anaeleweka lkn Mkoloni balaa.
Aiseeee...e ! Waziri hadi bastola zimejichora.Mbaya zaidi Waziri huyu,Wizara yake ndiyo yenye DHAMANA YA KUSIMAMIA UTAMADUNI,sijui ni Utamaduni gani anasimamia huyu.
Hamna kumtafuta mchawi,Private Candidates wengi wao ni vilaza.Walishindwa wakati wako shuleni na walimu full time alaf unategemea wafanye maajabu mtaani kwa kujisomea vichochoroni na vichwa vimeshaingia moshi ? Alama wanazopata ndizo wanazostahili wewe kama ulifeli ni ubongolala wako tu.
Wewe umeorodhesha maBcom mengi na unasema 1 ndiyo yenye matatizo alaf hauitaji ni ipi kati ya hizo,ni afadhali nimuamini mtoa uzi kuliko wewe maana unatoa habari nusu nusu,na hausemi kwa nini hiyo Bcom.1 ina matatizo.
Nenda polisi katoe taarifa na hizo meseji kama hujazifuta kazioneshe ili uwezi kulinda heshima yako,vinginevyo atakudhalilisha na utauza magazeti ya Shigongo.
Hoja hiyo ina mantiki na ukweli kwa vile hata ukimlaumu marehemu haisaidii kwa vile amekufa na hazisikii lawama hizo.Lawama ziende kwa aliye hai ili aweze kujirekebisha.
NB:Watu wanaweza kujifunza kupitia makosa ya marehemu ili yasijirudie na kuleta athari kwa jamii.
Acha majungu wewe,mbona huelezi anashusha vipi taaluma kazi kulialia tu.Uvivu wa kujisomea mnasingizia Mkuu wa shule.Shule ina walimu wangapi ? Kila somo lina mwalimu ? Kuna maabara na vifaa vya kutosha ? Kuna library na vitabu vya kutosha ? Acha kulialia.
Hapo wakifeli lawama lukuki kwa walimu,tena wengine wanalaumu NECTA nakumbuka matokeo ya form 4,2010 kwa vile ulikua mwaka wa uchaguzi wakasema walimu waliosahihisha walikua CHADEMA nilicheka sana,yaani watu wanasingizia siasa kila sehemu.
Hizo bilioni 8 zinaweza zisiwe au zisiwe au mchanganyiko.Ujue yule ni mfanyabiasha mkubwa na ni wa siku nyingi.Na hiyo inawezekana ni sehemu tu ya utajiri wake.Nchi hii kuna watu wanaogelea kwenye utajiri bhana.
Magamba kweli wamekwama sasa,wanachagua hadi mizimu iwaongoze !? Duuu...uh ! 2015 nafikiri watamsimamisha Hayati Mwl.Nyerere agombee urais maana ndo anaheshimika hadi leo kwa watu wa vyama vyote.
Nipokeeni wanajf,mimi ni mdau wa siku nyingi wa jf,nilikua nasoma tu bila kuchangia sasa nimeingia kwa miguu yote.Napenda sana mada za kisiasa,mimi ni ANTI-MAGAMBA.Hodi tena !
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.