Itapendeza sana kama Lulu atatoka kwani haiji akilini kwa binti huyu kufanya kosa hili. Nahisi yalikuwa ni matatizo ya kiafya kwa marehemu tu, iweje awe na uhusiano na watoto kimapenzi wakati ye mtu mzima, ameifundisha nini jamii yetu? Tukae mkao wa kula kushuhudia hukumu itakavyokuwa.
Kuna umuhimu gani kusema Visent Nyerere si ndugu wa marehemu Mwl J K? Ya nini maneno ya kuwa Dr. Slaa kafukuzwa kwa sababu ya kuiba fedha za ujio wa marehem Pope Yohane paulo wa pili-1991?
Hii ni dalili tosha kuwa ccm imeishiwa Sera za kuifanya iendelee kuwa madarakani hasa kwa kutoa ahadi...
Kukosa taarifa nzuri, hasira na maamzi yasiyo ya busara yanapelekea wengi kujiua/kujinyonga/kunywa sumu pindi tu wanaposalitiwa na kuachwa na wake/waume zao. Kwa nini uchukue uamuzi huu hatari wakati kuna mbinu kibao.
Inasikitisha kuona kuwa tunaanza semista ya pili wiki ya pili sasa (udom) bila kuwa na chochote katika akaunti zetu kwa wale tunaoitegemea serikali kupitia bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HESLB). Wanachuo wengi wanageuka kuwa ombaomba kwa ndugu, jamaa na marafiki huku idadi kubwa ikihaha kupata...
Habari; pamoja na juhudi mbalimbali za kutoa elimu juu ya utunzaji wa mazingira hususani upandaji wa miti, bado tutaendelea kuwa waharibifu wakubwa wa mazingira kwani wananchi wengi hasa wa vijijini hawana uwezo wa kutumia nishati mbadala kama vile solar power, HEP, Gio gas, nk, hata kama...
Huyu kaudanganya umma, kwani huenda alikuwa na nyaraka za serikali ambazo kuna wizi umefanyika. Ili kuua soo apitishie kwa kusema ameibiwa vitu vyake vyote. Kama serikali imekerwa na uongo huu, imfikishwe mahakamani ili aeleze kwa nini amiliki kizembe silaha ya kivita?
Hawa wachezaji waliompiga mwamzi wamekosea njia, walitakiwa kwenda kwenye Masumbwi badala ya mpira wa miguu kwani kwenye football hatuna ngumi zaidi ya mchezo wa kirafiki na kindugu (fair play). Kwa mwendo huu bongo tusahau kupata mafanikio ktk mpira wa miguu bila kuwajenga wachezaji wetu...
Hii ni Tz ya 2012 wala sina wasiwasi wowote hata kama FFU kutoka Arusha watazuiliwa kwani watakaokuja wakisimamia haki, wananchi wataiadhibu vizuri tu CCM. Police ni walewale hata wakitoka Moshi, Mara, Shy, Mtwara hawana tofauti. Mbinu hii haisaidii chochote kama wananchi wameamua kubadili...
Kiukweli kula mlo kamili inasaidia sana kuongeza nguvu za kiume, ingawa kuwa na mawazo kunapunguza sana nguvu za kiume. Chemical si nzuri kiafya, ikikulazimu sana basi tumia. Stamina ni kwa kufanya mazoezi mengi tofautitofauti kama vile pushapu nyingi kila siku, kukimbia, na kucheza michezo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.