kama walipora hayo maboksi, msimamizi wa uchaguzi alitakiwa afungue kesi ya jinai, lakini kama msimamizi aliomba msaada kwa vile hakuwa na usafiri mwingine, basi mwenyekiti wa tume ya uchaguzi alipaswa awajibishwe kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa weledi (JIPU)
Nakuunga mkono ndugu, sisi sio wa kuomba msaada, kwa hali tuliyonayo sisi ni watu wa kusaidia wasiojiweza. hebu angalia, tunayo ardhi nzuri kwa kilimo cha kila zao, Madini ya aina karibu zote yanapatikana Tanzania, Misitu ya mbao na mazao mengine, Mito na vianzo vingine vya maji, Mifugo wa kila...
Vyombo vya dola vinahujumu uchumi na kumsingizia mtu, Lema sio mkuu wa mkoa, wala sio waziri wa biashara wala sio Mkurugenzi wa jiji. Hizi hujuma zanajulikalikana sana na watu wanakubali kujitolea hadi tone la mwisho.
Haya maneno yako hayana msingi wa kuyafanya yakubalike katika jamii. Maneno mengine uliyotumia hapa ni kama uchonganishi, Huyo mtu unaemwita EL umemweka katika mazingira mabaya sana, nahofia hata usalama wake. Jinsi ulivyolitumia jina lake inaelekea humtakii mema.
Stephane Masatu Wasira wa Bunda, Esta Bulaya amemkalia kooni vibaya, CCM wakilazimisha kumpitisha kwenye kura za maoni basi CHADEMA watashinda.
Gregory George Teu wa Mpwapwa, wananchi wake bado wanasubiri barabara ya lami, Jimbo hili haliwezi kuchukuliwa na upinzani kwa miaka 15 ijayo. George...
Hakuna asieijua, hata waheshimiwa, niliwahi kumsikia Mh Lukuvi akisema "tukianza kunyosheana vidole kuhusu madawa ya kulevya, hakuna atakayesalimika humu ndani". Ndani alimaanisha bungeni. Siku nyingine nilimsikia naibu spika Mh Job Ndugai akiwalalamikia wabunge kunusa na kulamba kitu fulani...
wewe unataka wanachadema waamini fitina zako ili wamfukuze huyo muhimili wao mkuu halafu muweze kupeta. kumbuka maneno ya mwenyekiti wenu "Ni bora slaa aingie ikulu kuliko Lisu kuingia bungeni" wamekustukia, sio bure kuna jambo.
Siasa ni kamchezo ka ajabu sana, akija lipumba anagawa kadi kama kawaida, akija slaa anagawa kadi, akija mbatia vivyohivyo, watu ni wale wale. ingetokea siku ukawakagua ungekuta kila mmoja ana kadi zaidi ya moja.Yote hii inawezekana ni njaa au hawaelewi wanalolifanya.
Kuwa na mbunge wa CHADEMA mwenye cheti feki cha kidato cha nne haihalalishi matumizi ya vyeti feki Tanzania. haya ni majibu mepesi kwa maswali ya kawaida, pia ni dalili za serikali kushindwa kutimiza wajibu wake wa kisheria, kwa hiyo hapa waziri anakiri kuwa serikali anayoitumikia imechoka sana...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.