Pamoja na kupigiwa kampeni, pamoja na kuwa akina sykes walikuwa wameshaamua kumpa Nyerere urais, alishinda ushindi mwembamba tu!
Hii yote ni kujaribu kumshusha Nyerere au?
Hiyo nahamu nayo kweli. Nitatafuta hata muda wa kwenda kuisikiliza kama kweli kesi itakuwepo...Fanyeni hima mkirudishe na kile chuo cha morogoro kabla hamjafungua kesi maana hicho ni aibu tupu. Mlipewa tu kama njugu.
Ahsante sana Nyambala. Hii inazidi kuthibitisha kama tulivyosema huko mwanzo kwamba Mohamed Said anasubiri watu watangulie mbele ya haki halafu aanze kuwawekea maneno mdomoni ili kuipa uzito hoja yake.
Tujikumbushe kidogo kutoka kwa mohamed said.
Lakini baadaye tena Mohamed Said anasema...
Jamani hizi dini zitatuua...imefikia wakati tuziweke pembeni kidogo ili tuweze kufikiria vizuri mstakabali wa nchi yetu maana mambo yasipokwenda vizuri hata kuabudu kwenyewe kutakuwa na walakini...
Unaonaje ndugu yangu ukinisaidia kuielewa hiyo reference!? Hapa hakuna kuaibika, tupo kujifunza. Mimi kiu yangu ni kujua kama ni kweli hii statement aliyoisema Pengo ilichapishwa kwenye gazeti la majira kwenye tarehe na mwaka husika!?
Uchochezi ni kama tunaouona hapa chini...Kujaribu kumhusisha Nyerere/Kanisa na madhila yote wanayokumbana nayo waislam.
Au hapa...
Inaelekea hujawasoma watu vizuri au unajifanya huelewi. Soma vizuri. Siyo kila kitu watu wanampinga Mohamed Said.
Acheni porojo. Ilunga hana ushahidi wowote. Ilipoonekana wanafunzi wa kiislam wamefeli kupita kawaida kwenye somo la Islamic Knowledge, mlichunguza na mkaona hitilafu, mkapeleka NECTA/baraza la mitihani, nao wakaona hitilafu katika mfumo uliobadilishwa wa ukokotoaji. matokeo yakakokolewa upya na...
Hivi hii ligi ya kitoto mtaacha lini? Sasa kwani huu uzi kaanzisha nani? Mohamed Said au Yericko?
Mzee wenu mweyewe maji yamezidi unga, ngoma imekuwa nzito sana kwake!
Kimsingi mjadala umeshafungwa...ngoja tuwaache mkiendelea na ligi yenu ya watoto...
Mimi sizungumzii ya Mohamed Said. Nazungumzia ya huyo mwenzako kuhusu yule mtoto wa kike wa kiislam(very bright) aliyenyimwa nafasi ya kwenda form 1 kwa sababu ni muislam. Nikauliza mlipewa ushahidi au mnameza tu ngano za ustaadhi ilunga? jina lake ni nani? jina la huyu mkristu aliyechukua...
Wengine tulisemaga tangia mwanzo. Wenzetu waislam wanatafsiri vibaya uvumilivu na busara za wakristo. Kulikuwa hakuna sababu ya kwenda kwenye vyombo vya dola baada ya kula nyama ile. Ingetumika busara tu kwenye majadiliano ya pande hizi mbili. Mbona sisi tulikuwa hatulalamiki tulipokula nyama...
Hapana...Tanzania nzuri zaidi inakuja. Tukitoka kwenye hili tanuri la moto , Tanzania itang'aa kama dhahabu maana kila mmoja wetu bila kujali dini atakuwa na busara/uvumilivu. Ni lazima tufundishane hivi vitu hata kwa staili hii...
Yaleyale ya 'ngano'. Huyo mtoto aliyebebeshwa mimba hana jina? Huyo mkristo aliyependelewa hana jina?
Kwani nyie mmeshaoneshwa huo ushahidi au mnameza tu kila kitu mnachoambiwa kwa sababu kimetoka kwa shehe/ustaadh!?
Unaona ulipojikwaa? Na mzee Mohamed Said naye alijikwaa hapohapo. Kama Mohamed Said hakufanya utafiti kwa mapadre/viongozi wa dini wa kikistu , ilikuwaje akaweza kuwaweka kwenye kitabu/papers zake? alikwenda kuwauliza au amenukuu tu kutoka kutoka kwa waandishi wengine? Nyerere nae alihojiwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.