Mabadiliko ni mabadiliko. Theory of development inasema 'No change no development' hata kama mabadiliko hayo ni machungu kama shubiri. Viongozi ambao hawaoni mabadiliko yakija hujisahau na Kuwait wafalme. Hii ndivyo ilivyo Tanzania leo. Mabadiliko ni process. Hivyo Zambia wataendelea kuliko sisi...
Ni rahisi sana kwa baadhi ya watawala kutumia dini kama ngazi ya mafanikio. Sasa ni kwa nini ni lazima sheria ya TZ iitambue mahakama hii? Mbona hakuna utambuzi wa dini nyingine? Huu ndio ufa wa udini aliosema Nyerere.
Inabidi kiongozi wangu Nape arudi tena kwa waandishi wa habari atueleze. Ni kwa nini chama chetu kinataka serikali mbili wakati sisi tunanyanyasika Zanzibar? Masilahi ya chama chetu cha mapinduzi ni yapi wakati katiba ya Jamhuri ya Muungano imeshavunjwa na Zanzibar? Kati ya CCM na wananchi ni...
Wote nyinyi mnaotumia dini katika propaganda za kijinga rejeeni mafunzo ya JK Nyerere katika hotuba ya Kilimanjaro Hotel. Na kama ni kweli mnaongea kwa niaba ya CCM basi mjue kuna sisi CCM wenzenu mnatuumiza. Nawashauri acheni mara moja huu mchezo wenu mchafu.
Kwa kulifungia gazeti la Mwanahalisi serikali imesababisha CCM ichafuke kupita kiasi. Wanachama na Wapenzi wa CCM wanaumia sana ila hawana pa kusemea na wakijaribu kusema ni kama hawasikilizwi. Kwa nini viongozi msiunde tume huru ikafuatilia na kuweka hadharani kilichotokea? Woga unatokea wapi...
Inaelekea Alqaida wapo tz pia. Msikilize anayejiita malumbano. Lazima kuna kitu kinaendelea nyuma ya pazia. Mungu atawalaani wote wenye nia mbaya na nchi hii. Kwa nini kila kinachozungumzwa anarukia ukristo na uislamu? Hana ndugu zake wa damu ambao ni wakristo?
Nyerere alitupa elimu ya bure. Wa Morogoro alipelekwa kusoma Moshi wa Moshi Mtwara na kadhalika. Yote hii kwa kodi zetu. Sishangai uchumi uliyumba lakini kazi ya kuondoa udini na ukabila ilifanikiwa. Acheni udini na ukabila.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.