Kama wewe huko nyuma ulikuwa mwaminifu achana nae, ila kama nawe ulifanya hayo huko nyuma basi ujue ni mbegu ulipanda sasa vuna mazao ndohayo. Haiwezekani wewe uzini hovyo halafu uoe alie msafi. Mungu sio mnafiki anampa mtu sawa na alichopanda.
Yaonyesha hata dini yako huipendi, ndio maana unataka ushauri kwa watu. Dini ni kibebeo cha Imani kama huna Imani na unaemwamini dini si kitu kwako. Na ukibadili tu umeolewa tayari haijalishi ukiitwa mwanamume utakuwa mwanamume suruali.
Jamani kweli hivi kweli inawezekana kampuni yenye uwekezaji Mkubwa namba hii kufanya KAZI bila usajili? Hapa nahitaji msaada nami nielewe. Na mrabaha hata kama ni kidogo tulikuwa tunapokea kwa kuuandikiaje? Jamani kwani sisi madodoki? Tunameza tu.
Mnaopinga mtazamo wa Zitto tumieni basi hata akili kidogo jamani daaa mnatia aibu hata kujiuliza mara mbili hakuna? Ukiona kitu kwa kuwa cha upinzani huyo vidole vinawasha, haitawasaidia.
Kinachonishangaza ni kitu kimoja kama hawana tija na hakuna cha maana wakifanyacho bungeni hao Ukawa nyie wenye cha maana si muendelee na mambo yenu? Mbona kama nafsi zenu zinawasuta? Na kama mnakubali si muache bunge liwe fair? Halafu wengine humu wanatoa povu oooh wataona sasa wataona nn? Hivi...
Mleta mada sidhani kama umefikiri vizuri, nilipoona una nywele nyingi nikajua akili ni nywele zina faida kumbe za kwako ni bure tu. Kanyoe. Kama unafikiri kukaa wabunge wa upande mmoja ni tija mbona wakitoka wa upinzani hatuoni hoja za mashiko kutoka kwa hao watulivu? Chukua hatua "tumia akili"
Ukitaka kujua uzuri wa Arusha mtafute mfanyakazi wa ICTR aliekuwa Arusha na Muda wake ukaisha akatakiwa kuondoka ndio atakwambia uzuri au ubaya wake. Siku nyingine njoo na wako umpendae kisha uende viwanja ndo utajua ushamba wa watu wa Arusha. Hata hivyo yategemea uzuri wa mji nini katika...
Kwa hiyo kukosea kuandika Mungu na kuandika mungukunaondoa uhalali wote wa maandishi yaliyomo ndani ya hicho kitabu? Mambo mengine ni ya kitoto sana anajuaje mungualieandikwa hapo ni huyo anaemtukuza yeye yaani CCM na sio Mungu Jehova? Kuwaita wengine watoto Hilo sio neno la kuudhi? Ajiheshimu...
Kitu kingine lazima tuelewe ni kuwa shetani hajaumba kitu. na lazima tujiulize unaona taabu gani kwa wana wa Mungu wakimtukuza Muumba wao katika hali hiyo wakati huohuo unaona ni sawa kwa wana wa dunia wakifanya hivyo kwa shetani? mbona tunakuwa wanyonge wakati sie ndio wana wa mfalme na ndio...
jamani tuwe wa kweli nani alisema ukiimba bila kucheza ndio kumwabudu MUNGU YEHOVA? au tunatangaza uzuri wa dini zetu? kumbuka kama wewe hupendi sio maana kuwa jambo hilo ni kosa. na ninacho kiona hapa ni jinsi ambavyo mnawakwa na tamaa muingiapo sehemu za ibada badqla ya kumwabudu katika roho...
jamani hii imani humu jamvini mmetoa wapu? sasa kizazi kimetolewa japo sababu hasa haijatolewa nyie mnasema kwa uwezo wa Mungu atazaa hicho mnachoongea ni kweli? chukueni nafasi mngekuwa nyie mngefanya hayo mnayomwambia? ni bora angekuwa hajui. ingeeleweka sasa anajua na tena ameona. acheni...
Hata mm nakuunga mkono sijui jambo hili linatoka wapi, kama umoja wao wenyewe wameshindwa itakuwa huo wa mchanganyiko? Na siku hizi wanajipa vyeo eti Malkia wa uimbaji namba moja, mulemule jamani waimbaji wa Injili someni neno
Jamani tangu lini mchongoma ukatoa zabibu? Hayo ndio yalioko kwenye mchongoma, na ukiona mtu anaongelea sana ushoga basi ujue yeye ndo yuko hivyo, kinachonishangaza sio mwigulu bali aliemteua hivi alifikiri kweli? Na alipata ushauri kwa walioko karibu yake wakamwambia anafaa? Sasa hapa nadhani...
Kuna watu wanshangaza sana, kama CDM hakuna kitu mbona mnatumia nguvu nyingi kuisema sema? Kama haiwaumi au haitishii mambo yenu si muendelee na mambo yenu? Kila kukicha CDM, CDM hamuoni kwa maneno yenu mnaikana lakini moyoni mnaikubali? Jiangalieni vinginevyo mnatumika kuitangaza CDM.:D
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.