Yaani nyinyi wapambe wa Lowasa mmeshafanya Urais ni cheo cha kupeana kiushkaji. Kwamba mtu akiwa rais basi akitaka rafiki, ndugu au mtoto wake awe rais, lazima itokee. Kwa mtazamo wenu Kikwete alimtaka Membe awe Rais, mbona Membe hakushinda hiyo nafasi ya kugombea Urais?
Tuambieni hapa chanzo...
Toka enzi za Nyenzi, YoungAfrican, BCS, Darhotwire, Jambo mpaka Jamii Forums. Lemutuz alikuwa ni mwanajumuiya mwenye hoja zilizojaa madini na zenye mashiko pale anapoamua. Mwenyezi Mungu Ampumzishe Kwa Amani, Lemutuz.
Nilipita mitaa ya Posta ndani ya Dar Es Salaam, baadhi ya mitaa imeharibiwa kabisa na vibanda vya wamachinga. Yaani hakuna mpangilio wala sehemu ya wapita miguu. Ni kero kubwa sana, waondolewe na wapelekwe sehemu maalum ya kufanya biashara zao.
Ni aibu sana kwa Waziri Mkuu kulitangazia Taifa takwimu za UONGO ambazo hana uthibitisho nazo na hakuhakikisha anatumia vyanzo sahihi kupata ukweli. Mtu kama huyu si anaweza kuliingiza Taifa kwenye maafa makubwa kutokana na taarifa feki za mitaani.
Katika nyimbo zote alizoimba Jerry Nashon, hii ya Pesa Zanisumbua ameimba kwa hisia kali sana. Ni nyimbo ambayo naisikiliza mpaka leo hii ikiwa imejaa huzuni, huruma, na tumaini huku akinguruma na sauti yake ya Dudumizi. Mwenyezi Mungu Amlaze Mahala Pema.
Tanzania itaondolewa kwenye orodha ya "ban" ya Green Card kuingia Marekani baada ya Joe Biden kuapishwa na yeye kusaini executive order.
https://www.bongoradio.com/joe-biden-aahidi-kuiondoa-tanzania-kwenye-nchi-zilizowekewa-vikwazo-vya-kusafiri-marekani/
Hii mentality ni ya kijinga sana na inaonyesha jinsi mlivyokuwa na mavichwa makubwa huku akili hamna hata kidogo. Hivi unadhani kila mtu lazima aje na mtaji wa dola milioni 1 au zaidi? Kuna watu wengi wana uwezo wa kufungua small businesses ambazo mara nyingi hutoa ajira kwa wengi na mtaji wake...
Serikali ya Tanzania inakataa uraia pacha kwa Watanzania halisi waliozaliwa na kukulia Tanzania ambao kila siku wanatuma mamilioni ya pesa nyumbani, kufungua miradi na kusaidia ndugu, jamaa na marafiki lakini wanawakubalia raia wa Caribbean kukaa Tanzania bila ya Visa. Huu ni ujinga wa hali ya...
Ni kweli kabisa madikteta wa Afrika waanze kujiandaa kwa sababu wakati wa utawala wa Trump hakuwa na interest yeyote kushughulikia mambo yanayohusu haki za binadamu kwa Afrika. Utaona kuanzia January 20, 2021 haya mambo yanaaza kushughulikiwa kwa ukaribu kabisa na serikali ya Joe Biden.
Tahadhari bado zinatolewa na ubalozi wa Marekani, nadhani walitoa moja wiki iliyopita na unaweza kuangalia hapa Health Alert: U.S. Embassy Dar es Salaam | U.S. Embassy in Tanzania
Yaani wadini mmeshindwa kujizuia na mmetoka mafichoni baada ya kuona tu jina la Dr. Ramadhani Dau. Nakumbuka jinsi mlivyokuwa mnamuandama wakati wa uongozi wa wake pale NSSF, mbona sasa hivi wamewekwa watu wenu mnaoimba nao kwaya lakini ndio kwanza shirika linadidimia na kuingia hasara kila...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.