Ripoti ya Prof. Mruma ilituaminisha kwamba Buzwagi ni kati ya migodi yenye dhahabu nyingi sana duniani, iweje leo unafungwa kwa kuishiwa madini? Mlipoambiwa zile ripoti zilikuwa za kupikwa hamkuamini!
Ajabu ni kwamba wakati huo huo serikali inawafukuza wawekezaji kama Acacia ambao wana mchango mkubwa kwa ajira katika nchi hii - simply kwa ajili ya matakwa ya kisiasa. Tujiulize hao wafanyakazi 2000 wanaoachishwa na Acacia kwa sasa nyuma yao kuna watanzania wangapi wanaowategemea direct na...
Pia ni vema awakamate Acacia anaodai walimpelekea rushwa ya billioni 300 ya kusadikika (kwa mujibu wa Polepole). Au labda kwa hili anahitaji ushahidi upi iwapo ni yeye aliyepelekewa hiyo rushwa? Au walimpelekea akiwa hawaoni?
Mtihani mkubwa ni sisi ku-prove uhalali wa madai yetu kwa kutumia data za kupika. Cha muhimu kama uko fair ni kupendekeza sampling na analysis kwanza ya yale makontena yaliyoko bandarini. Baada ya hapo tutakuwa na uhalali wa kudai kile tunachodai.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni maajabu sana. Wakati msemaji wa serikali amekiri kuwa ndege imeshikiliwa na wanaotudai, Msukuma yeye anatoka usingizini na kudai kuwa bado iko kwenye matengenezo!! Tumuamini nani sasa???
Mkuu, madai hewa nayo ni madai ya kukaa unayafikiria? Subiri kama tutalipwa hata senti tano katika hicho kiasi unachojidandanya tunawadai Acacia. Ni mjinga peke yake na mchovu wa kushughulisha ubongo wake ndiye anaweza kuwa na matumaini na imani kuwa Acacia watatulipa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.