Mkuu Thanda jamaa anataka wanaopotoka kimaadili wawe wanarekebishwa pasipo kufukuzwa, sasa yeye mwenyewe aliyepotoka amejifukuza/amejivua uanachama mwenyewe si angewasubiri warekebishaji wa tabia mbovu waje wamrekebishe!
Mkuu, huyo Ben naona kawashika wenzake pabaya sasa kila mmoja anakuja kivyake kujitetea. Mimi naona Busara ni kwa watuhumiwa/wasaliti/masalia kukaa kimya na kila mmoja kutoa ushahidi wake au hayo malalamiko yake sehemu stahili na si hapa jukwaani.
Mkuu samahani utakuwa unachanganya habari mzee wako kushambuliwa na maneno sio mpaka awe Rais na hata wasio kanyanga baa hatuwezi kujua kwanini hawakanyangi labda yawezekana waliwatambia hapo baa watoto wao ni vichwa na wakaahidiana kuonyeshana ktk matokeo! Kikubwa mkuu hapa si kumkashifu Rais...
Mkuu ulifanya uchambuzi yakinifu kwanini mwanao alitaka kusoma PCB? Na wewe ulimpa sababu zipi za Kusoma PCM? Maoni yangu kwako mwache mtoto afanye kile kizuri kinachotoka moyoni mwake na atafanya kwa mafanikio ya juu zaidi!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.