Mambo kama haya na yanayo fanana na haya ndio yanatulazimisha wengine tupaze sauti kusema, katiba mpya iharakishwe upatikanaji wake, na katika katiba hii mpya kuwe na sheria itakayo simamia vizuri utendaji wa vyombo vya ulinzi na usalma. Vitumike kwa maslahi ya umma si kupiga propoganda za...
Mtawalaumu polisi wa watu bure, kama ilivyo kwa walalahoi wa TZ polisi nao wanamahangailko mengi kwenye maisha yao huku wakishuhudia mafisadi na viongozi vibaraka wa mafisadi wakifaidi nchi. Tusisahau ya Misri ambapo wanajeshi waliamua kuwaacha wamisri wafanye Vifaru vya jeshi kuwa viti vya...
Kwa chadema nawezasema wanawapuuza na kuwaona wanalalamika kama mtoto aliyedekezwa (a.k.a mtoto wa mama), uvccm kama hukumbuki mulize masauni atakukumbusha kilichompata.
Ukifanya udadisi kujua kuwa wazo na utaratibu huu asili yake wapi utakujagundua mtu kakopi na kupesti kutoka nchi nyingine. Kauchukua kama ulivyo bila maboresho na kuja kuutekeleza katika mazingira tofauti na yale ya asili yake. Muhimu kwake ni kufanikisha usanii tu basi.
Huko kwenye mikutano watakuwa wanaelezea kitu gani? Watawaomba wananchi wa waunge mkono maisha magumu yawe magumu zaidi, bei za bidhaa juu ziwe juu zaidi, malipo ya dowans yanacheleweshwa na mahakama mahakama ilitolee uamuzi haraka suala la dowans ili walipwe na kukodishwa haraka, wanafunzi wa...
Jambo ambalo liko wazi na hakuna ubishi ni kwamba mavazi ya mebeba ujumbe fulani. Anyway, just to be curious, hivi kama una mtu ambaye aliwahi kuwa kiongozi watu na baadhi ya watu wake aliowaongoza wakaamua kumuita baba wa taifa, huyu baba wa taifa akawa na mke wa ndoa, huyu mke wake ataitwa je...
Gauni la mama Maria linanikumbusha ule usemi wa matendo hukidhi haja kuliko maneno. Hata hivyo kila mwananchi ana utashi wake wa kisiasa, hili haliwabagui wa familia ya Nyerere aka JK original.
Kumbe hawa wameenda kwa ufadhili wa ccm nilikuwa najua ni kodi za wananchi wa tz, kama ni hivyo itabidi cdm wajitahidi kuwafadhili mawaziri vivuli wawe wanaenda.
Kwanza walio na jukumu la kumlinda rais sijui wanatuambia nini kuhusu usalama wake katika mazingira kama haya? pili ukiwaangalia rais na waziri usoni wamechoaka mbaya. Ila kwavile rais alishawahi kuwa mwanajeshi kamshinda ngeleja kwa kutumia mbinu za midani asisinzie kama mwezake anazuga kwa...
Naam! ni uzembe wa mwenye pakacha kwani mipango yote ilifanywa kwa kuweka tamaa mbele na papara bila umakini na kuna kila dalili chini ya mbingu hii kuwa mitambo itawadodea.
Kama watakuwa wamefanya hivyo na ikajulikana kuwa ni kweli, si ndio inawapa justification wale wanaowalaumu kuwa wanataka kuwang'oa isivyo halali kwenye madaraka. Kuvuja kwa pakacha.............!
Good news na mpaka hiyo tarehe mvua zitakuwa zinanyesha, hoja ya mabwawa kukauka maji haitakuwa na mashiko. Itabidi waanze kuumiza vichwa waje na hoja nyingine. Ukijua hili na wenzako wanajua jingine tz inatubidi twende kwa mtindo huu.
Hivi katiba ya tanzania inasema je juu ya rais kushindwa kazi yake? Mwenye kujua naomba anijuze kwani nafikiri hakuna kipindi kingine ambacho kifungu hicho kitahitajika kama wakati huu ambapo ni mpumbavu tu ndiye hawezi kuelewa kuwa rais wetu huyu ameshindwa kazi ya kutuongaza.
Like a candle in the wind just to add on that, your quite right we are tired of this presedent. Hatuna matumaini kabisa ya maisha yetu katika kipindi chote cha utawala wake.
Tatizo lake ni kama wewe na wengine wa aina yako mnavyotumiwa, kwa kujua au bila kujua lakini kwa maslahi pamoja ubinafsi wenu. Hili ndio tatizo lenyewe, watu wamenunuliwa kutoka sekta mbalimbali kupigia chapua dowans, sasa kwa nini iwe hivyo kama hamna tatizo, tatizo lipo ila rushwa imewatia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.