Kuuwa jambazi au gaidi siyo jambo la kujivunia labda kama mazingira yalilazimisha. Jambo la kujivunia ni kumkamata jambazi au gaidi akiwa hai ili asaidie katika kuitambua network nzima inayoendesha huo ujambazi au ugaidi. Mimi siamini kama mtu mmoja yeye kama yeye akaamua tu kuwa jambazi au...
Hapana, kwanza sidhani kama umefikia kiwango hicho cha kumchukulia kila mtanzania ni ndugu. Wataalam watanisahihisha lakini nadhani kuna UNDUGU na UDUGU. Undugu is more touching. When you miss, you real miss him or her. Ni vigumu kukaa kimya.
King Cobra
Sawa, lakini si kwa kiwango cha kukaa kimya wanapotoweka watu miongoni mwetu. Wakati mwingine ni vizuri kufikiria kwamba ingekuwa wewe ndiye ndugu, mume, mke au mtoto wa aliyetoweka ungefanya hicho unachoshauri. Anayejua maumivu ya kiatu ni mvaaji. Ninamwomba Mungu awape hekima na utu viongozi...
Kwa kifupi, Rais wetu Mhe. Magufuli hapendi watu wenye rekodi mbaya kiutendaji na mbaya zaidi ile inayotia aibu hata mbele ya umma. Kama ni kweli Mhe. Rais kafanya hivyo, ninamuunga mkono na ningemshauri huyo Dada atumie muda wake kujiuliza sababu iliyomfanya Mhe. Rais kufanya hivyo badala ya...
Nadhani hoja ya MKURUGENZI WA BANDARI ni kwamba katika hayo makontena kuna mchanga na madini mbalimbali mojawapo ikiwa ni dhahabu. Sasa ukiondoa mchanga, kinachosalia asilimia 90 yake ni dhahabu. Mimi ndivyo nilivyomwelewa and this is very possible. Nchi hii kama anavyosema Mhe. Rais imeliwa...
Labda kwa kuongeza tu ni kwamba YEYE Nape alikitumikia chama kwa kiwango hicho kinachomtia uchungu kwa sababu kwa wakati huo, alikuwa ndiye Katibu Mwenezi wa Chama. Binafsi ninathamini sana mchango wake Nape Nnauye katika CCM lakini nami ninamshauri atulie. Apunguze au aache kabisa kuongelea...
Sidhani kama Mhe. Rais hilo ndiyo lengo lake kwamba azuie kabisa mchanga kwenda nje. Ugomvi wa Mhe. Rais ni composition ya kilichomo kwenye huo mchanga. Inasemekana kuna kiwango kikubwa cha dhababu tofauti na inavyotakiwa kuwa. Hii maana yake ni kwamba kiwango kikubwa cha dhahabu inayopatikana...
Mungu akubariki sana Ndg Mwigulu na kukulinda kwa hatua hii muhimu yenye mwelekeo wa kukomesha tabia mbaya iliyoanza kuota mizizi ya askari kutumia silaha za moto kila wanapokabiliana na raia wasio na silaha yoyote.
Nina mambo mawili ya kuchangia:
Kwanza, Mwandishi wa article hii ameitoa wapi "moral authority" ya kutoa mawazo yenye mwelekeo huu!! Nina uhakika akisoma maoni yangu haya, atatambua ninamaanisha nini.
Pili, mbona kuna kigugumizi kikubwa cha Mhusika anayetetewa kuita waandishi wa habari na...
Kama una hoja za msingi kuhusu ufisadi wa huyu mtu kwa nini ujifiche humu jamvini? Kwa nini usichukue hatua madhubuti kwenda PCCB na kuwapatia vielelezo vya ufisadi unaoongelea. Vinginevyo, hapa unaonekana ni mlevi tu anayepita mtaani huku akiimba nyimbo au ni porojo za vijiwe vya kahawa.
Pasco, bajeti ikiidhinishwa na Bunge kinachofuata ni utekelezaji. Haipelekwi kwa CAG kupata idhini. Ikumbukwe kuwa hata CAG mwenyewe bajeti yake inaaidhinishwa na Bunge baada ya kuwa scrutinized na Kamati husika ya Kudumu ya Bunge. Entry point ya CAG ni baada ya matumizi kufanyika yaani mwishoni...
Mwanaume mzima unaandika lundo la maneno ya kutunga tu!!! Badala ya kufanya kazi ya maana ya kukuletea kipato halali unatumia muda kuandika stori za kitapeli ili wasomaji wakuombe hiyo program unayojifanya uliiweka kwenye simu ya mkeo!!! Acha ujinga na utapeli mwanaume mzima. Kama huna kazi...
Tunaacha kujadili mambo ya msingi tunajadili ofisi ya Mkuu wa Mkoa!! Ofisi ikiwa mbaya na chafu, kosa!! Ofisi ikiwa nzuri na safi, kosa!! Kweli unahitajika moyo wa mwendawazimu kumridhisha mswahili.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.