Mimi sina haja ya malumbano maana sijui pia malezi uliyokulia, Pengine umekulia kwenye familia ambayo inajiona kuwa wao tu ndio binaadamu. Na pia sijui upeo wa uweleo wako.
Jamani hayo sasa matusi yasivumilika. Watu wengine humu ndani utadhani wanatumia ninihii kuzungumzia badala ya mdomo. Mtu na akili zako unawezaje kukashfu kabila la mtu na kuona sio binaadamu. Pierre tall unapokosa namna ya kuchangia hoja, kukaa kimya ni busara zaidi kuliko kuharibu mfumo wote...
Jamani mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Hakuna mtu mwingine mwenye uthubutu wa kukemea maovu zaidi ya Lowasa. Kila mtu anafahamu alivyokua mchapa kazi akiwa waziri mkuu. Hii ya kujiuzulu uwaziri, hakujiuzulu kwakuwa kausika kuchukua pesa. Bali aliwajibika tuu kama waziri mkuu. Mchagueni...
Na ndio maana makampuni mengi sana inayomilikiwa na waafrika zinasuasua ama kuishia kufa kabisa sababu ya kushindwa kusimamia kikamilifu na kuruhusu uzembe makazini. Mtu kuambiwa fanya kazi sio unyanyasaji. Mtu kukatazwa kuiba sio unyanyasaji. Mtu kuambiwa tii sheria za kazi sio unyanyasaji...
Mi hapa nashangaa maana hamna hata mmoja anayesema manyanyaso gani wanapata kutoka kwa mmiliki wa Leopard. Au tatizo ni kwa rangi yate tu basi! Labda kwa faida ya wale ambao hawajui back ground Fazal & Gulam, wamezaliwa Monduli, wakakulia Monduli na kusoma Monduli. Hali yao kimaisha ikiwa ni ya...
Mimi hapa sipo kwa kumtetea mtu yeyote hapa. Nipo kwa kusema ukweli noujua mimi kupitia wadogo zangu wanaofanya kazi hapo ambao naamini kabisa kama kuna unyanyaswaji wa jinsi hiyo, wangeniambia tu. Damu nzito kuliko maji, wangeniambia tu. Mleta mada angefanya uchunguzi wa kina kuliko kukubaliana...
Huyo Fazal mwenyewe mnaye mzungumzia, nimeshuhudia mimi mwenyewe Mout meru Hospital akitoa msaada wa Magodoro kwa majeruhi waliolipukiwa na mabomu ktk kanisa la Rc lililopo Olasiti Arusha. Japo alifanya hivyo kwa nia njema kabisa lakini chama fulani cha upinzani kilitaka kuzuia msaada huo wa...
Jamani tujaribu kuwa wakweli. Penye ukweli tuzungumze ukweli. Mimi mwenyewe ninayeandika hapa nina wadogo zangu 3 wanaofanya kazi hapo Leopard wanasema maneno mengi hapo ni kutengeneza mpaka nikahisi mtoa mada amekuwa tu na chuki na kampuni ya Leopard. Isijekuwa pia ni mbinu za makampuni mengine...
Hata mimi naanza kupata wasiwasi, yaani umeguswa tu kidogo, unataka kuwarukia watu na vichwa. Swala la mapenzi yahitaji kubembelezana. Sasa kwa hali hiyo mwezangu utaweza. Mi naona tatizo lako ni ubabe, hivyo kila mmoja anataka kubaki na sura yake bila makovu, ndio maana wanakumwaga. Pole.
Pole sana Dear, Wewe nenda kama alivyokuagiza J4, Nadhani na yeye ni muelewa. Alivyokutongoza alijaribu tu. Anajua kutongoza kuna kukubaliwa au kukataliwa. Sasa inategemea ulimkatalia kwa mazingira gani. Mtu Anayekutongoza usimuone adui, mjibu tu kwa uzuri. Hata yeye angejua kama ungemkatalia...
Ni kweli ni heri kumpenda anayekupenda. Usimlaumu pia asiekupenda maana huenda wewe si chaguo lake. Kuna ambaye yeye anampenda. Unaweza ukamsii kwa kum'badilisha mawazo ila ujue hamtadumu kwakuwa hauko moyoni mwake. MPENDE AKUPENDAE, " ASIYEKUPENDA ACHANA NAYE "
Ndugu yangu pole kwa hasira amabayo hukutakiwa hata kuwa nayo. Kwanza kabisa mawasiliano na yeye invyoonekana ulilazimisha. Hukumpa na yeye kupata muda ya kufanya uamuzi. Labda ndio maana alipoendelea kuwa na wewe akagundua kuwa humfai. Na pengine alikuwa tu anatafuta namna ya kuachana na wewe...
Mengine unaweza mtu ukavumilia. Hii yakuwekewa mguu juu! hiyo siwadanganyi sintaweza. Uzalendo utanishinda. Kwa wenye uwezo huo hongereni sana. Nawapa BiG up.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.