Asante kwa kuweka andiko kuhusu Kisiwani cha ukerewe. Lakini ungerekebisha kuhusu Aya inayosema 'Ukerewe ni Kisiwa' ambapo umesema ina visiwa 38 na Kisiwa kikubwa ni ukara na kwamba visiwa vingine 'havikariwi na watu'. Mm kwetu ni Kisiwa cha Irugwa na Kuna pia visiwa vya Lyegoba, Kulazu na...
Daraja la upadri huwa halifutiki ila kama padri aliacha kutoa huduma anaweza kuomba kibali kwa askofu wake na kwa Baba Mtakatifu aruhusiwe kuoa. Hata mashemasi wa kikatoliki huomba vibali ikitokea kuacha au kuachishwa kutoa huduma ya kichungaji.
Kitila ana uzee gani wakti 45 ndo anatimiza? Bunge linatakiwa like na watu wenye uelewa tofauti na hasa bunge la Africa mashariki ambalo wawakilishi wa nakwenda kutetea sera na maslahi ya nchi zao. Kwa hiyo wasomi wanaweza kutuwakilisha vizuri. Kwani ni Tanzania tu mbao wasomi huge ukiangalia...
Enyi watu ushauri wenu ni mzuri lakini una walakini. Mnashauri mke aache kazi ili aanzishiwe biashara. Hiyo biashara isipolipa iakuaje. Mme akifa ghafla familia itaendeshwaje. Wanandoa wanatakiwa wake na kujaddili na si kushinikiza mke aache kazi. Kwani biashara hazihamishiki?
Mkuu mtoa mada nafikiri tafsiri yako kuhusu andiko hilo si sahihi. Maana halisi ni kuwa hata mwanamke aliumbwa sawa na binadamu. Biblia iliandikwa kwa lugha ya kiyahudi na neno Adam (Adamah) ili maana ha mtu mme na Eva mtu mke. Kwa maana hiyo Mungu aliumba watu wanaume ana wanawake. Waliobobea...
Sidhani kama issue ni chama. Issue ni wadhifa wa mtu. Sita alikuwa kiongozi mkuu wa moja ya mihimili ya dola (Bunge). Speaker ni mkubwa kuliko Waziri. NI sawa na Jaji Mkuu (Mkuu wa Mhimili mwingine wa dola-Mahakama).
Naona watu wameshauri sana ingawa on the negative side. Dada piga magoti na mwombe Mungu akuonyeshe. Wakti mwingine hao wachepukaji wanafanyiwa madawa na hivyo ufahamu unawatoka. Fikiria watoto wako na kama bado unaumri mdogo jiulize ni vizuri kuwa na watoto wa baba tofauti tofauti? Nikushauri...
Wewe ndg nimekushangaa mgeni hata hujamjua vizuri unamkabidhi kulala na wtt? Uko sawa ww eti huna ubaguzi du. Unajua maana ya ubaguzi? Hiyo ni kukosa umakini. Hata kama angekuwa ni ndg yako toka kijijini wanao hawatakiwi kufanyiwa hivyo.
Wewe Msalala kitendo ulichofanya si kizuri. Sasa kama umeishalipa kisasI kwa nini uendeleze kumtoa mwenzio miaka yote hiyo? Nafikiri yanatosha na muanze upya. Hakuna binadamu mkamilifu.
Tatizo lako na wengine either hamsomi au uwezo wa kuelewa ni mdogo. Mtoa mada katoa ushauri mzuri tu. Hivi ni sawa mke wa mgombea kuwaza kuwa mmewe akipata nafasi basi shopping zitakuwa makuu na kujenga ma ghorofa. Hiyo ndo mmewe alimwambia ndo sababu ya kugombea ubunge?
Tatizo ambalo linawapata viongozi wa upinzani ni jinsi ya kuwashawishi wananchi ili waapigie kura. Maneno kama atakayekipigia ccm akapimwe akili, na kwamba wasiotaka mabadiliko ni wajinga si maneno mazuri ya kutumia unapoomba kura. Huwa yanawagharimu waombaji. Lugha za matusi wananchi hawazipendi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.