Ninajizuia kufikiria nini kingetokea iwapo jeshi la Polisi lingeamua kumsafirisha Mbowe kwa gari mpaka Arusha na pengine ikatokea ajali njiani akadhurika au kutodhurika kabisa! Kwa mwenendo wa wafuasi wake .............. nini kingetokea? Inahitaji busara ya kuzaliwa sio ya .com
Tafiti kwanza ujue ukweli. Mko wengi aina yako wenye chuki zisizo sababu, kwa uzoefu wangu hata ukiwa na digrii mia mara nyingi watu wa aina yako huwa watupu ila kwa kutegemea waliolishwa na propaganda !
Inasikitisha kuona watu wakiwa na mitizamo finyu na hata uelewa! Kilichopo hapo kina uhusiano gani na mujahidina? Wangevaa kanzu za kipadre ( zenye marinda na mikanda) bwana Leonardo ungelichukuliaje, tafuta ufahamuzaidi ndugu yangu
Kila mtu akinukuu kitabu chake cha dini na hata historia ya ukandamizaji hatutafika. Mistari ya Zaburi wengine hawana hakika nayo!
Nadhani ni wakati wa Katiba mpya kusema wazi siku ya mapumziko na kwa kuwa serikali haina dini na Watanzania tujadili na kuafikiana siku ya mapumziko
Bwana Phillemon, tafadhali tafiti kwanza kuliko kuegemea historia ya mapinduzi ambayo imejaa utata mtupu. Mimi sikubaliani na mtazamo wako kumfananisha Okello na Che Guevara ni upofu! Tafuta ukweli. Nchi hii ina mashujaa wa kweli ambao wamezimwa makusudi na hawajulikani kwa kizazi cha sasa.
Ni kweli waislam tuko nyuma lakini tafuta sababu za kweli za Waislamu kuwa nyuma na wala si propaganda zilizoandikwa. Historia ya nchi imepotoshwa makusudi, sisi ndio wavaa viatu na ndio tuaoyajua maumivu yake. Usiamshe yaliyolala! Rejea kitabu " Kanisa Katoliki na Siasa za Tanzania"
Ni kukosa busara kujadili picha ambayo haina maelezo ya kina kuhusu mahali na sababu ya waandishi hao wa habari kuwa pale, vinginevyo ni kufisadi fikra za watu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.