Mimi binafsi baada ya kumsikiliza mwenyekiti akielezea mchakato mzima wa upigaji kura za kupitisha rasimu ya katiba utakavyoendeshwa nimeingiwa na wasi wasi mkubwa ya kwamba unatoa mwanya mkubwa wa kuchakachuliwa kwa matokeo ya zoezi hilo. Tuchukue madhalani upigaji wa kura za wazi; utaratibu ni...
Kabla ya kuelezea hayo ninayotaka kueleza, sina budi awali ya yote niweke wazi maslahi binafsi niliyonayo katika suala zima ninalotaka kuelezea; ambalo ni mchakato wa utungaji wa katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa maoni yangu,zoezi nzima kuanzia na uundwaji wa bunge la katiba...
Kwa mtanzania yeyote makini, mjadala unao endelea sasa juu ya utungaji wa katiba mpya siyo tu kwamba unakatisha tamaa, bali pia unaonyesha ni kwa kiwango gani unafiki umekidhili hapa nchini. Nasema hivyo kutokana na ukweli kwamba wengi wa wanaoshinikiza pande mbili asimu katika mjadala huo...
Kwangu mimi sioni kama haya mabishano yenu yana maslahi yeyote kwa taifa letu. Hata hivyo ukweli unabakia pale pale kwamba uongozi wa sasa hauja onyesha umakini wa kutosha katika kushughulikia mianya ya rushwa; Kama itakavyokumbukwa katika hotuba yake ya kwanza kwenye bunge la Tanzania JK...
Naona tatizo kubwa hapa ni "timing;" Kwa wengi wetu kuwepo kwa hizi tetesi ya kwamba baadhi ya watawara wetu wanahodhi fedha nyingi huko nje walizozipata visivyo halali kunatufanye tuamini ya kwamba huu mjadala wa uraia pacho unatokana na jitihada za mafisadi hao kutafuta njia ya kujihami ili...
Wahenga walisema unaweza ukadanganya watu kwa wakati fulani,lakini siyo wakati wote. Hayo ndiyo yametokea kwa Sitta. Tangu uko nyuma wachache wetu tulimjua Sitta kuwa mbinafsi,mbabe, mpenda makuu, mbadhirifu, ndumira kuwili, na jambazi wa siasa; lakini ilibidi tunyamaze kimya tukiamini kadri...
Anayoyasema Dr. Slaa uenda yakawa ya ukweli, lakini jambo ambalo limekuwa likinishangaza ni kwanini mpaka sasa Chadema haija iburuza tume hiyo mahakamani kutokana na wizi huo. Ni kweli, katiba ya sasa inatamka wazi ya kwamba tume ikishamtangaza yeyote kuwa ndiye mshidi wa kiti cha uraisi uamuzi...
Swali langu kwa huyo muhandishi ni nani huyo aliyefadhili hiyo safari yake ya ugunduzi na alikuwa na maslahi gani katika jambo hilo? Pili wakati alipokwenda kwenye safari yake hiyo, alifanya jitihada gani kuwasiliana na mke wa Ballali, mama Muganda, ambaye inasemekana bado anaishi huko Marekani...
Inavyoelekea kufunguliwa kwa kesi hii ni danganya toto,jambo hili baada ya kuwekwa adharani limewaumiza watu wengi na hivyo wanatafuta mbinu ya kuzuia lisiendelee kuzungumzwa kwa kisingizio cha kutoingilia madaraka ya mahakama.
Kwa maoni yangu mchakato wa kupata katiba mpya ulikwenda tenge pale ambapo sheria iliyotungwa kusimamia mchakato huo ilipoteua wabunge wasasa na wajumbe wa baraza la wawakilishi kuwa wabunge wa katiba moja kwa moja. Uamuzi huo ulikuwa ni wa makosa kwasababu wabunge hao hawakuchanguliwa na...
Hachana na propaganda tuwekee maneno halisi aliyosema Mnyika. Nani asiyejua kwamba serikali ya CCM hivi sasa inahaha kunusuru bajeti ya kuwahudumia wakubwa kwenye matanuzi yao.
watanzania tutakuwa hatujatendewa haki kama sakata alilolianzisha waziri Masele litamalizwa kwa mtindo wa; "funika kombe mwana haramu apite." Nasema hivyo kutokana na ukweli kwamba ndugu Masele kwa wadhifa wake alipashwa ajue kwamba,yeye siyo msemaji wa masuala yanayohusiana na uhusiano wa...
Kama ni kweli hii ni taarifa rasmi na imetolewa na ikulu kwa niaba ya rais,basi rais wetu atakuwa ameonyesha upendeleo, maana kuna mikasa nyingi ya aina hii iliyotokea hapa nchini na rais hajawahi kutoa tamko kali kama hilo akikemea vitendo hivyo.
Hivi majuzi, wakati akitoa mchango wake katika bunge la katiba, Mwenyekiti wa Jumuia ya wazazi alimushambulia jaji Warioba kwa madai kwamba yeye siyo mtu safi kwasababu eti aliwahi kupatikana na kosa la kutoa hongo kwenye uchaguzi, wakati anashindania ubunge na wassira.
Ukweli wa mambo, ni...
Maoni yako ni sahihi kabisa. Kama sheria za nchi zingelikuwa zinafuatwa Steven Wasira hakustahili hata kuwa mbunge; kwani kwa mujibu wa sheria, mtu aliyepatikana na kosa la jinai akahukumiwa kifungo kinachozidi miezi sita hapashwi kugombea nafasi yeyote ya uongozi. Wasira alipatikana na kosa la...
Kwa kuongezea,nashauri CDM wanapaswa wawe waangalifu sana kwa huu mchakato wa katiba unao endelea; kwa maoni yangu umetekwa nyara na CCM ili kuvifanya vyama vya upinzani, na taifa kwa ujumla kuelekeza nguvu zao zote katika zoezi hilo, na hivyo kusahau kushughulikia uwekaji wa masingira muafaka...
Kama kuna asasi ambayo imeonyesha kutokuwa na uzalendo wowote katika nchi hii, kwa miaka nenda miaka rudi, asasi hiyo ni TLS. Kama itakavyokumbukwa nchi yetu imekuwa ikishuhudia vitendo vingi vya uvunjaji wa katiba na sheria za nchi, na serikali yenyewe pamoja na vyombo vya dola lakini asasi...
Naomba niulize, na hiyo ya kutengeneza siime ni mojawapo ya shughuli zilizo ainishwa kwenye sheria iliyoanzisha bunge hilo au inatokana na kutumia vibaya kile kipengere cha sheria hiyo kinachotoa madaraka kwa bunge hilo kufanya jambo lolote ambalo kwa maoni yao litaonekana linafaa! Madhumuni ya...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.