Habari wakuu,
Nahitaji majogoo wa kisasa ili wapande kuku wa kienyeji kupata vifaranga chotara. Kwa mwenye nao hasa maeneo ya Mwanza anijulishe tafadhali ili niweze kununua kutoka kwake.
Sasa mbona hawajibishwi mkuu? Sasa kama inajulikana hivyo na hali ya umeme ni tete kiasi hiki bado tuendelee kususbiri hadi aje awajibishwe na Magufuli kweli?
Mleta mada, kwenye huo mstari wa tatu neno la mwisho kwenye hiyo tweet kuna tusi kubwa mno hapo. Nadhani kuna kosa la kiuandishi kwa huyo aliyetweet. Hili ni tatizo kubwa.
Mkuu ile orodha ya mwembeyanga ilikuwa na majina zaidi 10 na wengine ndo wenye madaraka makubwa nchini hadi hivi sasa. Kwa nini Lowassa tu ndo mwenye kusemwa vibaya zaidi kuliko hao wengine?
Hoja nyepesi sana hizo. Huwezi kumpima mtu kufaa kwenye nafasi kubwa kama ya Rais kwa kutumia vigezo hivyo unavyovisema. Kama wengi wetu tuna mawazo kama haya basi inaweza tosha kujieleza ni kwa nini nchi yetu ni masikini kiasi hiki licha ya utajiri mkubwa uliopo ndani ya milki yetu.
Haya ndo yanayosemwa na jimbo la Geita Mjini mkuu! Rogers Ruhega ambaye ndiye aliyepeperusha bendera ya Chadema mwaka 2010 na kuwapa CCM ushindani wa kutosha ameambulia nafasi ya 3 kwenye kura za maoni!! Na nimeambiwa yanayosemwa mtaani ni haya haya kwamba walioshinda wamepiga goli la mkono...
Sasa kama hii unayoisema ndo sababu na kwa vile wewe unasema umefanya kazi huko, hebu nipe maelezo kuhusiana na huu mstari ili na mimi nielewe:
''Fanya hima ni muhimu sana kinyume cha hapo watu wako hawatapiga kura''.
Ila hii ni hatari sana kwa chama cha upinzani kuwa bize kukibomoa chama kingine cha upinzani. Ingependeza sana kama mpambano huu ungekuwa ni kati ya chama cha upinzani na chama tawala.
Ni shida mkuu!! Labda wao wanajua kuhesabu zaidi kuliko wewe. Au inawezekana macho yao yanaona zaidi kuliko yako! Wanastahili kuonewa huruma tu hao na propaganda zao hizo.
Sababu zako ni nyepesi mno mkuu!! Uraisi ni zaidi ya vitu vidogo vidogo kama hivyo!! Kwa nini usifikirie kwa mfano kupata mtu ambaye atakuja kulinda rasimali ya gesi kwa maslahi mapana ya watanzania wote? Magufuli amesema nini wakati wanapitisha kwa dharula hiyo sheria ya gesi hivi karibuni...
Tatizo kuna wabunge wameifanya kazi ya ubunge ionekane ni rahisi sana na ndo maana naona kila mtu sasa anataka kuelekea huko! Sasa kama mimi natakiwa kusema ''ndiyoooo'' au ''hapanaaa" kwa kitu ambacho pengine hata sikijui undani wake kwa vile kimeletwa kwa hati ya dharula pale bungeni shida iko...
Hizi sasa nadhani labda ni chuki zako mkuu tu na hakuna kigezo kingine unachokitumia. Pointi yangu ni kwamba hata kama akiacha kutumia chopa na akapanda gari, bado nalo linaweza kupata ajali vie vile!! Naamini tutakuwa tumeelewana hapo.
Mkuu hiyo ni ajali tu kama zilivyo ajali zingine!! Hata angezungukia jimbo lake kwa gari bado angeweza kupata ajali vile vile ambayo labda hata ingemletea madhara makubwa kuliko hata hayo aliyoyapata kwenye hiyo ajali ya chopa.
Sasa mkuu watu wakiwa wameshasaini mikataba ya miaka 99 kwa kutumia sheria hiyo kama itakuwa ni mbovu itatusaidia kweli kama taifa? Hata kama itakuja kupitiwa upya? Inawezekana tukawa tunarudi kule kule kwenye asilimia 3 ya dhahabu!!
Huko aliko sidhani kama atafanya shughuli za wananchi kwa kutumia hiyo elimu yake aliyonayo na ambayo wewe imekufanya umwite kijana msomi!! Kuna maprofesa tayari wako huko lakini wanayoyatetea na kuyapitisha kwenye vikao vya bunge yanamshangaza kila mtu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.