Search results

  1. L

    Vijana si sawa kupinga kila kitu, Somo la Maadili lifundishwe toka darasa la kwanza mpaka Chuo

    Kupinga kwa hoja zenye mantiki ni sawa. Kuwafundisha vijana kukubali kila kitu ni upumpavu. Kutukana (viongozi au yeyote siyo sawa na ni kosa la jinai). Tunatakiwa kufundisha watu wetu wakubaliane na mambo ya faida kwao, jamii na taifa kwa ujumla, kupinga yale yote yaliyo kinyume chake. Huo...
  2. L

    Nchimbi anaibua Mazuri ya Serikali dhidi ya Mabaya Machache, Makonda anaibua Mabaya Mengi dhidi ya Mazuri machache kati yao nani Bingwa wa Siasa?

    Kinachotakiwa ni mabadiliko ya mfumo wa utawala kwa faida ya wengi. Iwe CCM au upinzani, itategemea nani atawahi. Mama Samia kaja na 4R, Makonda kajaribu ktatua kero kwa uwazi, Nchimbi na Mongela kutatua kero kimya kimya huku upinzani ukitoa hoja za kutatua matatizo na changamoto kwa njia zao...
  3. L

    Nimegundua matajiri wengi hapa Tanzania hawajasoma

    Kusoma ni jambo moja, akili jingine, juhudi, maarifa na utajiri (wa mali, ambao siyo lazima yawe mafanikio) ni mengine pia.
  4. L

    Rais Samia, vyeti feki kwenye taasisi za Umma bado ni tatizo

    Tatizo la vyeti siyo dogo kama ilivyoaminiwa kwenye serikali ya Magufuli. Lina uhusiano wa moja kwa moja na kura feki, serikali feki, mahakama feki, watu feki (wasiojulikana),..... Huwezi kufukia shimo kwa kuchimba jingine halafu ukajisifu umeondoa tatizo.
  5. L

    Uzalendo na utumishi waliokuwa nao akina Sokoine, Warioba haupo tena, waliopo ni wote ni wezi tu wenye wivu

    Hizi ni fikra mbaya kwa mustakabali wa jamii na taifa kwa ujumla. Wazalendo wapo na pia tunatakiwa tuwajenge wengine kifikra (wenzetu, watoto wetu na vizazi vijavyo). Kwa hiyo, unachotakiwa ni kutaja au kushawishi hatua dhidi ya wezi na mafisadi kuambatanisha na vitendo vyao. Katika idadi ya...
  6. L

    Ni lini Serikali itaondoa/ itamaliza kadhia na mateso ya usafiri wa daladala kwenye majiji makubwa?

    Usafiri bora huenda sambamba na mipango miji bora yenye miundombinu inayoendana na idadi ya watu. Ni asilimia ndogo ya majiji na miji inayopangwa (iwe rasmi au siyo rasmi), na hiyo ni changamoto kubwa ambayo haitapata suluhu kwa urahisi. Majiji yana njia mbili hadi nne za kuingilia bila...
  7. L

    Dkt. Nchimbi apinga kauli ya Mwenyekiti wa UVCCM Kagera aliyeahidi "kuwapoteza" wakosoaji wa serikali

    Vichaa hawapewi nafasi kwenye jamii ya watu wenye akili, hudhibitiwa. Wakipewa rungu inakuwaje? Wazee wa zamani walituasa.
  8. L

    Dkt. Nchimbi apinga kauli ya Mwenyekiti wa UVCCM Kagera aliyeahidi "kuwapoteza" wakosoaji wa serikali

    Ni muhimu chama kurudi kwenye mstari na utaratibu wa asili wa maadili, uungwana utu na heshima kwa wote. Tabia za unyama na kujitoa ufahamu ili kupata teuzi ni upumbavu usiokubalika na sio sawa kwa mustakabali mwema wa jamii, chamachama, serikali na taifa. CCM lazima iwe mfano wa kuigwa kwa...
  9. L

    Ndugu Amos Makalla na ndugu Nchimbi hamna mvuto mmepoa sana wananchi hawawaelewi

    Kazi ya kutatua kero na kufanya shughuli zilizopangwa kwa maendeleo ya wananchi ni ya serikali. Chama kinaenezwa kwa kufundisha itikadi na sera ili wananchi wengi wavutiwe wajiunge. Kama serikali haitekelezi sera na itikadi, itawajibishwa kwa vikao vya ndani na matokeo ya uwajibishwaji huo...
  10. L

    Malengo ya Mbio za Mwenge yabadilishwa, Sasa hivi wanauzungusha tu na kufanya Matamasha

    Aweso anapiga kazi vizuri. Hata hivyo, kwa ujumla wake, wanasiasa ni walaji (consumers) ambao hula kodi za wananchi (kwa sababu siyo wazalishaji, yaani producers kwenye jamii au taifa). Ili tupate maendeleo endelevu, kodi zetu zinatakiwa zielekezwe kwa wazalishaji (wakulima, wafugaji, watoa...
  11. L

    Serikali kutumia Tsh. Bilioni 190.57 kununua V8 mpya za Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Ujenzi wa Makazi na Utawala

    Mzalendo wetu maua yake yapo sana, Ila kwenye magari sikuona makali yake, hata mkurugenzi wa Geita ilionekana sawa tu. Huu waweza kuwa mfupa uliomshinda fisi.
  12. L

    Mufti Abubakar: Ijumaa 19/4/2024 ni siku Maalumu ya Kuliombea Taifa juu ya Mvua zinazoendelea kunyesha

    Mvua bado zinahitajika. Matendo ya binadamu kama kuingilia mtiririko wa asili wa maji (ujenzi wa mabwawa), kuishi sehemu hatarishi (kama mabondeni) na kutojenga miundombinu imara (barabara, reli, majengo,....) ndiyo chanzo cha matatizo. Kwanza kabisa tumshukuru Mungu kwa kutupa mvua nzuri...
  13. L

    Kardinali Pengo atua ofisini kwa Paul Makonda kumfanyia maombi maalumu ya baraka na kumpongeza kwa uteuzi

    Serikali ya Tanzania na taifa kwa ujumla halina dini rasmi, Ila wananchi wana Imani zao. Kwa hiyo, RC Makonda ana haki ya msingi kabisa ya kuamini na kuabudu. Je tukio la maombi ni la kiserikali au kiofisi? Hayo siyo mambo yake binafsi na Kadinali Pengo au kanisa? Kuingilia shughuli zake za...
  14. L

    Biblia zenye maudhui ya Ushoga zadaiwa kuingia nchini

    Kila raia, awe kiongozi au asiye na cheo ana wajibu wa kulinda jamii na nchi kwa ujumla. Hakuna sababu ya kuitia hofu jamii kwa kutoa taarifa kama hizi hadharani, wasambazaji na wauzaji ni maadui wa ustawi wetu, hasa kwa vizazi vijavyo, wanatakiwa washughulikiwe na kumalizwa kimya kimya. Kama...
  15. L

    ITIFAKI: Ni nani Mkubwa kati ya Waziri Mkuu na Spika wa Bunge?

    Kuongeza, spika na bunge lake waweza kumuondoa Rais madarakani. Hata hivyo, katika fikra za wabunge kuomba badala ya kuitaka serikali kufanya au kutimiza wajibu wake kwa wananchi, changamoto ni kubwa.
  16. L

    Alichokifanya leo Makonda ndo Jambo analoweza zaidi. Naionea huruma Tanzania

    Kiongozi apatikane kwa utaratibu wa kugombea zaidi kuliko kuteuliwa. Kama ikibidi kuteua, wawe watu wazima wenye uzoefu wa maisha katika nyanja mbalimbali badala ya sarakasi za siku hizi za kutafuta uteuzi.
  17. L

    Naomba Kufahamishwa. Hivi Kongamano la Kumbukizi ya Hayati Sokoine hufanyika kila mwaka au? Mbona kama limepewa uzito sana mwaka huu?

    Tafsiri ya greatness of a leader ni ka Afrika ni yule anayesumbua wananchi wenye uwezo kiuchumi warudi chini, hata kama nchi itakuwa masikini zaidi. Fikra za kimasikini (kijamaa na kijima) hutukuza sana viongozi wanaozuia juhudi za mtu mmoja mmoja kuzalisha na badala yake kuendeleza kugawana...
  18. L

    Mila na Desturi ya Watanzania ni kuwa wamoja kwenye majanga, Kata 12 Wilayani Rufiji zimezingirwa na maji, Wanahitaji msaada wa Kibinadamu

    Sijasema na siwezi kuwaza kuwa waachwe hivyo. Jitihada zinafanyika na mabadiliko kutoka hali duni kwenda bora (maendeleleo) yapo. Changamoto ni kasi ndogo kutokana na tamaduni. Jamii au nchi huendelea kwa kasi kutokana na tamaduni (fikra na vitendo) za wananchi wakazi wa eneo hilo.
  19. L

    Napendekeza TISS ivunjwe, iundwe Upya

    Wananchi ndiyo TISS namba moja. Hawa wafanyakazi wa TISS ni waajiriwa tu, hivyo kuvunja TISS ni wananchi kujielewa kwa kuwa active zaidi katika ulinzi wa nchi na uundaji wa serikali. Ni muhimu sana kwa wananchi kujua kuwa wao wana haki ya kuwa TISS namba moja, vinginevyo kizazi chao cha baadaye...
Back
Top Bottom