Kwanza niulize kwa nini anatukanwa, na pili nikuulize wewe umeenda kuyatafutia wapi matusi anayotukanwa, na tatu nikuulize matusi ya Magufuli au Lowasa uliyaona?
Kuitwa msagaji sio tusi, ni tuhuma ikiwa bado hazijathibitishwa. Sasa suala ni kwamba ni tuhuma za kweli? Kwa nini useme umetukana kuliko kusema umetuhumu basi?
Hawa watu wanamchezea tu raisi, kwa sababu wamemsoma. Kukubali kwake yale wanayofanya inaweza kuwa ni kuonyesha udhaifu kwa namna fulani. Inapaswa awakemee wao, awaambie uraisi ni ukubwa na ukubwa ni jaa. Kuna kukosolewa na hata kutukanwa, nk.
Asipofanya hivyo, inaweza kufikia akawa na...
Ukiwa na akili timamu utayapuuza maneno kama hayo badala ya kuyakuza. Kwani yanaweza kuwa kweli kwa namna yeyote ile? Ni sawa na mie kukuambia tumbili wewe. Utakasirika ikiwa unajua wewe sio tumbili? Ukasirike kama wewe ni tumbili kweli na umekuwa ukificha hilo, na sasa nimetoa siri yako hadharani
Hili suala la viongozi kujipendekeza kwa Raisi Samia sasa limeanza kupita kiasi, na lisipodhibitiwa litaleta mtafaruku nchini.
Mfano ni hili suala la Raisi Samia kutukanwa. Siamini kabisa kwamba Raisi Samia anatukanwa, kwamba maneno ya kumkosoa na kumpa majina kama Mama Tozo sijui ni jambo...
Hahaha! Kuna mwanajeshi mmoja alimpa mimba mtoto wa raisi. Akaitwa Ikulu. Akaambiwa kaa hapa subiri. Raisi alipojitokeza jamaa akasimama halafu akaanguka chini kazimia!
Raisi Samia huyu au mwingine, amtumbue Makonda? Utasubiri sana. Wenzako walishauliza maswali hivi Makonda anajiamini nini kwa Raisi Samia hadi anafikia kufanya yale anayofanya. Usione vinaelea huko ndani vilishaunganishwa siku nyingi
Payeee ni kodi ndani ya nchi, na ukifanya kazi mashirika hayo hukatwi kodi. Kwa hiyo hawakatwi Payee. Na wao wana utaratibu wao wa pension, hawawezi kusimamiwa na vikokotoo onevu kama vya Tanzania. Hivyo ni vyetu sisi, hivyo hawana mpango na NSSF
Na tunatoa demonstration:
Wanachotaka kutuambia wanasiasa ni kwamba, uwepo wa Bwawa la Nyerere hautazuia mafuriko hata miaka ya mbele. Sasa hilo si kweli. Kila itakapotokea mafuriko wakati Bwawa la Nyerere lipo ujue kuna uzembe umefanyika.
Kumbuka, masika Tanzania ni kama miezi minne, na...
Safi sana! Hatimaye Raisi Raisi Samia ameanza kutuelewa na kutupilia mbali maelezo ya kisiasa!
TUNASISITIZA
Tunapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kwamba, uongozi wa CCM umekuwa ukijaribu kutumia kila njia kuonyesha hili tatizo halijasababishwa na Bwawa la Nyerere, pamoja na kuwapa TANESCO...
Wakijua kuna watu kama wewe ndio maana wanatoa staement kama hizo. Mwaka 1974 hakukuwa na Bwawa la Nyerere, na Bwawa la Nyerere limejengwa kwa ajili pia ya kuzuia mafuriko, lakini lazima ujue namna ya kubalance maji ili kuzuia mafuriko.
Unachotaka kusema, kwa kuwa akili yako imezoea kumeza kila...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.