Unafiki na roho ya ukatili utaliingiza taifa kwenye machafuko. Amani tuliyo nayo ilitengenezwa kwa gharama kubwa ya kuhubiri upendo na kutenda haki. Tusitegemee ustawi wa nchi pasipo haki na upendo. Pia kumbukeni kuwa Mungu yupo. Asiyeamini akamuulize Herode.
Haki ni muhimu ionekane inatendeka. Kwa vile ukweli unapigwa vita, hali kadhalika maendeleo ni ndoto. Nchi ikishikamana kwa wananchi wote kujitoa kwa moyo kwa ajili ya maendeleo tutafanikiwa. Endapo ushauri utaendelea kupigwa vita na ukweli kufumbiwa macho wataumia kwenye kubeza na wasiobezwa...
Mtu unapokuwa na Udini unakuwa kipofu. Hata mambo ambayo ni wazi kabisa huyaoni. Inaelekea hata uelewa wa dini ni mdogo. Acha Udini na pia acha kujikweza. Mfuasi yeyote wa Yesu Kristo anatunza matukio yote ya Pasaka. Katiba haina uhusiano na hujuma kwa Wakatoliki wala thread yako haina mshiko...
Maana yake ni kuwa kama unaona chama hakifai basi mchague mtu unayeona anafaa japo tunajua kwa unafiki wa wabunge wa chama tawala hatuna wagombea binafsi hivyo wote watatoka kwenye chama kimojawapo. Pia sikubaliani naye kuwa wabunge wa CCM na wa CDM ni sawa. Kwanza wa CCM wanayo dola na...
Pole kwa wote ambao kwa njia moja au nyingine wameguswa na matukio haya. Mimi pia nilimsikiliza mkuu wa Mkoa wa Mara akiongea na nilichokielewa ni kuwa nia yake ilikuwa kuwatoa wananchi hofu kama kiongozi wa serikali na pia Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa. Pia alitoa ujumbe...
Huyu dada hakukutafuta ila wewe ndio ulimtafuta kwa kumpa ofa ya chakula na bado ukampa namba ya simu. Nadhani kwa kumpa namba ya simu ulitarajia kufanya mawasiliano nae. Mawasiliano ni sehemu ya kufahamiana na wakati mwingine kunasaidia kujifunza kutoka kwa wengine. Kitendo cha wewe kujitangaza...
Mume ni kichwa cha nyumba. Mume asipoimiliki nafasi yake sawasawa kunakuwa na udhaifu wa mahusiano. Chukueni nafasi zenu kama viongozi wa nyumba. Pia msisahau kuwa Mungu amewataka wanawake wawatii waume zao na wanaume wawapende wake zao. Je mnawapenda wake zenu?? Jichunguzeni kwanza ili owte...
Ukweli ni kuwa aliyetoa wazo la dawa hii ametoa tahadhari kwa wale wenye presha ya kushuka. Ameshauri awe na kahawa ili kusaidia kuipandisha pale hali hiyo itakapotokea. Tutarajie feedback kutoka kwa wale watakaotumia japo hatujajua inaponyesha baada ya muda gani.
Wakati tunasoma historia tulizoea kusoma na kusikia "RISE and FALL of.....". Sasa kwa wale waandishi mahiri wanaweza kuanza kuandika historia ya "THE RISE AND FALL OF KOVA". Hakuna ubishi kitabu kitauzwa sana kwa sababu kachumbari zipo za kutosha kunogesha kitabu.
Pamoja na umuhimu wa kumtambua huyu ni vyema mtuhumiwa akafahamika. Kumwonyesha aliyetoa taarifa kunahatarisha usalama kwa njia moja au nyingine hasa ukizingatia wimbi lililojitokeza la kuwateka watu na kuwatesa. Mbunge huyu ni makini na anastahili sifa kwa vile anatuonyesha uzalendo alio nao...
Pongezi za dhati ziwafikie viongozi na wanachama wote wa CHADEMA kwa busara za hali ya juu za kutumia nguvu ya umma hadi nchi ikatetemeka. Kampeni zilikuwa zimeenda shule na zilikuwa za kistaarabu. Sijui kale kagazeti feki ka udaku wa kisiasa kinachoitwa UHURU safari hii kitaandika nini.
Labda...
Uandishi huu unatia shaka kwani mwanzoni ulionyesha kuwa hauna upande lakini baadaye unaonyesha dalili za kuwa upande fulani. Huu ni unafiki na wahenga wanasema ni Afadhali ya mchawi kuliko mnafiki.
Nadhani CDM wamefanya kile kitu ambacho wenzao wa CCM wameshindwa kukifanya hadi wakafikia...
Huyu jamaa alimasaidia ili aweze kushuka ngazi wala sio kwa sababu alimpenda. Mtu kukusaidia kwani ni lazima akujue au umjue?? Hii ndio tafsiri duni ya kinadada wengi eti ukimpa lifti umejigonga. Hii ndio maana hatutoi lifti bila kuombwa. Na wanapodhani wanajiweza ndio wanafungua zipu za watu.
Jambo lolote la kweli huwa halina haja ya ushahidi. Jambo la uongo huhitaji ushahidi ambao mara nyingi nao ni wa uongo. Epuka ushahidi ili ubakie mkweli.
Msisahau kuna uhuru wa kutoa maoni japo wakati mwingine yanakuwa maoni butu. Maoni ya mtu mmoja ambaye ana haki zake kiraia hayawezi yakatumika kulichafua Kanisa kwa ujumla wake. Usisahau maoni mengine yanachanganyika na kujipendekeza.
Kuna jambo moja la msingi umelisahau. Katika hali tuliyo nayokwenye nchi yetu shule hizi ni zile zinaitwa za binafsi (Private Schools) Ingekuwa tuna mfumo wa elimu unaoeleweka shule hizi zingekuwa zinachukua wale watoto ambao hawakufaulu kujiunga na shule za sekondari za serikali. Kumbuka kuwa...
Upo ukweli kwamba baadhi ya watu wanafaidika na tatizo la umeme. Hivi wangethubutu vipi kuagiza majenereta yote haya kama kweli mgao ulikuwa wa mwezi mmoja tu. Sasa itabidi tuanze kufuatilia mahusiano ya hawa wafanyabiashara ya mejenereta na hawa viongozi tuliowapa dhamana. Kama ni hujuma kwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.